Waamuzi
1 Na ikawa kwamba baada ya kifo+ cha Yoshua, wana wa Israeli wakamuuliza+ Yehova, wakisema: “Ni nani kati yetu atakayepanda kwanza kwa Wakanaani ili kupigana nao?” 2 Na Yehova akasema: “Yuda atapanda.+ Tazama! Hakika nitaitia nchi hiyo mkononi mwake.” 3 Ndipo Yuda akamwambia Simeoni ndugu yake: “Panda pamoja nami kuingia katika kura yangu,+ ili tupate kupigana na Wakaanani, nami nitaenda pamoja nawe katika kura yako.”+ Basi Simeoni akaenda pamoja naye.+
4 Kwa hiyo Yuda akaenda, kisha Yehova akawatia Wakanaani na Waperizi mikononi mwao,+ nao wakawashinda katika Bezeki, watu elfu kumi. 5 Walipomkuta Adoni-bezeki kule Bezeki, ndipo wakapigana naye, wakawashinda Wakanaani+ na Waperizi.+ 6 Wakati Adoni-bezeki alipoanza kukimbia, wakamfuatilia na kumshika, wakamkata vidole gumba vya mikono yake na vidole vikubwa vya miguu yake. 7 Kwa hiyo Adoni-bezeki akasema: “Kumekuwa na wafalme 70 wakiokota chakula chini ya meza yangu, ambao vidole gumba vya mikono yao na vidole vikubwa vya miguu yao vimekatwa. Mungu amenilipa kulingana na matendo yangu.”+ Baadaye wakamleta Yerusalemu+ naye akafia huko.
8 Zaidi ya hayo, wana wa Yuda wakaendelea kupigana vita na jiji la Yerusalemu+ nao wakaliteka, wakalipiga kwa makali ya upanga, kisha wakateketeza jiji hilo kwa moto. 9 Baadaye wana wa Yuda wakashuka kupigana na Wakanaani waliokaa katika eneo lenye milima na Negebu+ na Shefela.+ 10 Basi Yuda akapiga mwendo kwenda juu ya Wakanaani waliokuwa wakikaa katika Hebroni+ (basi jina la Hebroni hapo zamani lilikuwa Kiriath-arba),+ nao wakamuua Sheshai na Ahimani na Talmai.+
11 Na kutoka hapo wakasonga mbele juu ya wakaaji wa Debiri.+ (Basi jina la Debiri hapo zamani lilikuwa Kiriath-seferi.)+ 12 Ndipo Kalebu+ akasema: “Yeyote atakayepiga Kiriath-seferi na kuliteka, nitampa Aksa+ binti yangu awe mke wake.”+ 13 Naye Othnieli+ mwana wa Kenasi,+ ndugu mdogo wa Kalebu,+ akaliteka. Kwa hiyo yeye akampa Aksa binti yake awe mke wake.+ 14 Na ikawa kwamba mwanamke huyo alipokuwa akienda nyumbani, akaendelea kumchochea aombe shamba kutoka kwa baba yake. Kisha mwanamke huyo akapiga makofi akiwa juu ya punda.+ Basi Kalebu akamwambia: “Unataka nini?” 15 Naye akamwambia: “Nipe baraka,+ kwa maana umenipa sehemu ya shamba upande wa kusini, nawe unipe Guloth-maimu.” Basi Kalebu akampa Gulothi ya Juu+ na Gulothi ya Chini.
16 Na wana wa yule Mkeni,+ ambaye Musa alikuwa mwana-mkwe wake,+ wakapanda kutoka katika lile jiji la mitende+ pamoja na wana wa Yuda, wakaingia katika nyika ya Yuda, iliyoko upande wa kusini wa Aradi.+ Ndipo wakaenda, wakaanza kukaa na watu hao.+ 17 Lakini Yuda akasonga mbele akiwa na Simeoni ndugu yake, nao wakawapiga Wakanaani waliokaa Sefathi na kuliharibu+ jiji. Basi jina la jiji hilo likaitwa Horma.+ 18 Kisha Yuda akateka Gaza+ na eneo lake na Ashkeloni+ na eneo lake na Ekroni+ na eneo lake. 19 Na Yehova akaendelea kuwa na Yuda, naye akamiliki eneo lenye milima, lakini hakuweza kuwafukuza wakaaji wa ile nchi tambarare ya chini, kwa sababu walikuwa na magari ya vita+ yenye miundu ya chuma.+ 20 Walipompa Kalebu jiji la Hebroni, kama alivyoahidi Musa,+ ndipo akawafukuza kutoka humo wale wana watatu wa Anaki.+
21 Na wana wa Benyamini hawakuwafukuza Wayebusi waliokaa Yerusalemu;+ bali Wayebusi wanaendelea kukaa pamoja na wana wa Benyamini katika Yerusalemu mpaka leo.+
22 Wakati huohuo nyumba ya Yosefu+ pia ikapanda kwenda kupigana na Betheli,+ na Yehova alikuwa pamoja nao.+ 23 Na nyumba ya Yosefu ikaanza kufanya upelelezi+ juu ya Betheli (jina la jiji hilo hapo zamani lilikuwa Luzi),+ 24 na walinzi wakaona mtu akitoka katika jiji. Kwa hiyo wakamwambia: “Tafadhali tuonyeshe njia ya kuingia ndani ya jiji, nasi hakika tutakutendea fadhili.”+ 25 Basi mtu huyo akawaonyesha njia ya kuingia ndani ya jiji; nao wakalipiga jiji kwa makali ya upanga,+ lakini wakamwachilia mtu huyo pamoja na familia yake yote.+ 26 Ndipo mtu huyo akaenda katika nchi ya Wahiti,+ akajenga jiji na kuliita jina Luzi. Hilo ndilo jina la jiji hilo mpaka leo.
27 Na Manase+ hakumiliki Beth-sheani+ na miji yake ya kandokando na Taanaki+ na miji yake ya kandokando na wakaaji wa Dori+ na miji yake ya kandokando na wakaaji wa Ibleamu+ na miji yake ya kandokando na wakaaji wa Megido+ na miji yake ya kandokando, bali Wakanaani waliendelea kukaa katika nchi hiyo.+ 28 Na ikawa kwamba Israeli walipopata nguvu,+ ndipo wakawatia Wakanaani katika kazi ya kulazimishwa,+ wala hawakuwafukuza kabisa.+
29 Wala Efraimu hakuwafukuza Wakanaani waliokuwa wakikaa Gezeri, lakini Wakanaani waliendelea kukaa kati yao katika Gezeri.+
30 Zabuloni+ hakuwafukuza wakaaji wa Kitroni na wakaaji wa Nahaloli,+ lakini Wakanaani waliendelea kukaa kati yao,+ nao wakatiwa katika kazi ya kulazimishwa.+
31 Asheri+ hakuwafukuza wakaaji wa Ako na wakaaji wa Sidoni+ na Alabu na Akzibu+ na Helba na Afiki+ na Rehobu.+ 32 Na Waasheri wakaendelea kukaa kati ya Wakanaani waliokaa katika nchi, kwa sababu hawakuwafukuza.+
33 Naftali+ hakuwafukuza wakaaji wa Beth-shemeshi na wakaaji wa Beth-anathi,+ lakini waliendelea kukaa kati ya Wakanaani waliokaa katika nchi;+ na wakaaji wa Beth-shemeshi na wale wa Beth-anathi wakawatumikia katika kazi ya kulazimishwa.+
34 Na Waamori wakaendelea kuwasukuma wana wa Dani+ mpaka ndani ya lile eneo lenye milima, kwa maana hawakuwaruhusu washuke kuja chini katika nchi tambarare ya chini.+ 35 Kwa hiyo Waamori wakaendelea kukaa katika Mlima Heresi na katika Aiyaloni+ na Shaalbimu.+ Lakini mkono wa nyumba ya Yosefu ukawa mzito sana hivi kwamba wakalazimishwa kufanya kazi ngumu.+ 36 Na eneo la Waamori lilikuwa kutoka mpando wa Akrabimu,+ kutoka Sela na juu yake.
2 Ndipo malaika+ wa Yehova akapanda kutoka Gilgali+ akaenda Bokimu+ na kusema: “Mimi niliwatoa ninyi Misri na kuwaleta katika nchi ambayo niliwaapia mababu zenu.+ Zaidi ya hayo, nikasema, ‘Sitavunja kamwe agano langu pamoja nanyi.+ 2 Nanyi kwa upande wenu, hampaswi kufanya agano na wakaaji wa nchi hii.+ Bomoeni madhabahu zao.’+ Lakini hamkuisikiliza sauti yangu.+ Kwa nini mmefanya hivi?+ 3 Basi, mimi kwa upande wangu nimesema, ‘Sitawafukuza kutoka mbele yenu, nao watakuwa mitego kwenu,+ na miungu yao itakuwa mtego kwenu.’”+
4 Na ikawa kwamba mara tu malaika wa Yehova alipokuwa amewaambia wana wote wa Israeli maneno hayo, watu wakaanza kupaaza sauti zao, wakalia.+ 5 Kwa hiyo wakaita jina la mahali pale Bokimu. Kisha wakamtolea Yehova dhabihu hapo.
6 Wakati Yoshua alipowaacha watu waende zao, ndipo wana wa Israeli wakaenda zao, kila mmoja kwa urithi wake, wapate kuimiliki nchi.+ 7 Na watu wakaendelea kumtumikia Yehova siku zote za Yoshua na siku zote za wale wanaume wazee walioendelea kuishi baada ya Yoshua na ambao walikuwa wameona kazi yote kubwa ya Yehova ambayo aliwafanyia Israeli.+ 8 Kisha Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Yehova, akafa akiwa na umri wa miaka mia moja na kumi.+ 9 Basi wakamzika katika eneo la urithi wake kule Timnath-heresi+ katika eneo lenye milima la Efraimu, upande wa kaskazini wa Mlima Gaashi.+ 10 Na kile kizazi chote pia kikakusanywa kwa baba zao,+ na kizazi kingine kikaanza kutokea baada yao ambacho hakikumjua Yehova wala ile kazi ambayo alikuwa amewafanyia Israeli.+
11 Na wana wa Israeli wakaanza kufanya yaliyo mabaya machoni pa Yehova,+ wakatumikia Mabaali.+ 12 Hivyo wakamwacha Yehova Mungu wa baba zao aliyekuwa amewatoa katika nchi ya Misri,+ wakafuata miungu mingine kutoka kati ya miungu ya watu waliowazunguka pande zote,+ wakaanza kuiinamia, hata wakamtia uchungu Yehova.+ 13 Hivyo wakamwacha Yehova, wakaanza kutumikia Baali na sanamu za Ashtorethi.+ 14 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka juu ya Israeli,+ akawatia mikononi mwa waporaji, nao wakaanza kuwapora;+ naye akawauza mkononi mwa adui zao waliowazunguka pande zote,+ wala hawakuweza tena kusimama mbele ya adui zao.+ 15 Kokote walikoenda, mkono wa Yehova ulikuwa juu yao ili kuwaletea msiba,+ kama vile Yehova alivyokuwa amesema na kama vile Yehova alivyokuwa amewaapia;+ nao wakawa katika dhiki kali sana.+ 16 Basi Yehova alikuwa akisimamisha waamuzi,+ nao walikuwa wakiwaokoa kutoka mkononi mwa waporaji wao.+
17 Nao hawakuwasikiliza hata waamuzi wao, lakini wakafanya uasherati+ na miungu mingine+ na kuiinamia. Waligeuka upesi kutoka katika njia ambayo mababu zao walikuwa wametembea kwa kutii amri za Yehova.+ Wao hawakufanya hivyo. 18 Na wakati Yehova alipowasimamishia waamuzi,+ Yehova akawa pamoja na mwamuzi huyo, naye akawaokoa kutoka mkononi mwa adui zao siku zote za mwamuzi huyo; kwa maana Yehova alikuwa akijuta+ kwa ajili ya kuugua kwao kwa sababu ya wakandamizaji+ wao na wale waliokuwa wakiwasukuma huku na huku.
19 Na ikawa kwamba mwamuzi huyo alipokufa, walikuwa wakigeuka na kutenda kwa njia ya uharibifu hata zaidi ya baba zao kwa kufuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiinamia.+ Hawakujiepusha na matendo yao na tabia yao ya ukaidi.+ 20 Mwishowe hasira ya Yehova ikawaka+ juu ya Israeli naye akasema: “Kwa sababu taifa hili wamevunja agano+ langu ambalo niliwaamuru mababu zao, nao hawakuisikiliza sauti yangu,+ 21 mimi pia, kwa upande wangu, sitafukuza tena kutoka mbele yao hata taifa moja kati ya yale mataifa ambayo Yoshua aliacha wakati alipokufa,+ 22 ili kwa njia ya hayo Israeli wajaribiwe,+ kuona kama wataishika njia ya Yehova kwa kutembea katika hiyo kama vile mababu zao walivyoishika, au hapana.” 23 Kwa hiyo Yehova akayaacha mataifa hayo yabaki kwa kutoyafukuza upesi,+ wala hakuyatia mkononi mwa Yoshua.
3 Basi haya ndiyo mataifa+ ambayo Yehova aliacha yabaki ili kupitia hayo ajaribu+ Israeli, yaani, wale wote ambao hawakuona vita vyovyote vya Kanaani;+ 2 kusudi kwamba vizazi vya wana wa Israeli vipate kufunzwa, ili kuwafundisha vita, yaani, wale tu ambao hawakuwa wameona mambo kama hayo kabla ya wakati ule: 3 Wakuu watano wa muungano+ wa Wafilisti,+ na Wakanaani+ wote, pia Wasidoni+ na Wahivi+ waliokaa katika Mlima Lebanoni+ kutoka Mlima Baal-hermoni+ mpaka maingilio ya Hamathi.+ 4 Nao wakaendelea kutumika kama vyombo vya kujaribu+ Israeli ili kujua kama wangetii amri za Yehova ambazo alikuwa ameamuru baba zao kupitia Musa.+ 5 Na wana wa Israeli wakakaa katikati ya Wakanaani,+ Wahiti na Waamori na Waperizi na Wahivi na Wayebusi.+ 6 Nao wakaanza kuoa binti zao,+ na binti zao wenyewe wakawapa wana wao,+ nao wakaanza kuitumikia miungu yao.+
7 Basi wana wa Israeli wakafanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, wakamsahau Yehova Mungu wao,+ wakatumikia Mabaali+ na miti mitakatifu.+ 8 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka juu ya Israeli,+ naye akawauza+ mkononi mwa Kushan-rishathaimu mfalme wa Mesopotamia;+ na wana wa Israeli wakaendelea kumtumikia Kushan-rishathaimu kwa miaka minane. 9 Na wana wa Israeli wakaanza kumwita Yehova awape msaada.+ Ndipo Yehova akasimamisha mwokozi+ kwa ajili ya wana wa Israeli ili apate kuwaokoa, Othnieli+ mwana wa Kenasi,+ ndugu mdogo wa Kalebu.+ 10 Basi roho+ ya Yehova ikaja juu yake, naye akawa mwamuzi wa Israeli. Alipoenda vitani, Yehova akamtia Kushan-rishathaimu mfalme wa Siria mkononi mwake na mkono wake ukamshinda nguvu+ Kushan-rishathaimu. 11 Baada ya hapo nchi haikuwa na usumbufu wowote kwa miaka 40. Mwishowe Othnieli mwana wa Kenasi akafa.
12 Kisha wana wa Israeli wakaanza tena kufanya yaliyo mabaya machoni pa Yehova.+ Ndipo Yehova akaacha Egloni mfalme wa Moabu+ apate nguvu juu ya Israeli,+ kwa sababu walifanya yaliyo mabaya machoni pa Yehova.+ 13 Zaidi ya hayo, akakusanya wana wa Amoni+ na Amaleki+ juu yao. Ndipo wakaenda, wakapiga Israeli na kulichukua jiji la mitende.+ 14 Na wana wa Israeli wakaendelea kumtumikia Egloni mfalme wa Moabu kwa miaka kumi na minane.+ 15 Na wana wa Israeli wakaanza kumwita Yehova awape msaada.+ Basi Yehova akawasimamishia mwokozi, Ehudi+ mwana wa Gera Mbenyamini,+ mwanamume mwenye kutumia mkono wa kushoto.+ Baada ya muda wana wa Israeli wakapeleka ushuru kupitia mkono wake kwa Egloni mfalme wa Moabu. 16 Wakati huohuo Ehudi akajifanyia upanga, nao ulikuwa na makali kuwili,+ urefu wake ukiwa mkono mmoja. Kisha akaufunga chini ya vazi lake kwenye paja+ lake la kuume. 17 Naye akampa Egloni mfalme wa Moabu+ ushuru huo. Basi Egloni alikuwa ni mtu mnene sana.
18 Na ikawa kwamba alipokuwa amemaliza kutoa ule ushuru,+ mara moja akawaambia watu waende zao, wale waliobeba ule ushuru. 19 Naye mwenyewe akageuka na kurudi alipofika mahali penye machimbo yaliyokuwa katika Gilgali,+ akasema: “Nina neno la siri kwako, Ee mfalme.” Basi akasema: “Nyamazeni!” Ndipo wote waliokuwa wamesimama kando yake wakatoka nje na kumwacha.+ 20 Na Ehudi akamjia alipokuwa ameketi katika chumba chake cha darini chenye baridi ambacho kilikuwa chake binafsi. Naye Ehudi akaendelea kusema: “Nina neno linalotoka kwa Mungu kwa ajili yako.” Kwa hiyo akasimama kutoka katika kiti chake cha ufalme. 21 Ndipo Ehudi akatia ndani mkono wake wa kushoto, akauchukua ule upanga kutoka kwenye paja lake la kuume na kuuingiza ndani ya tumbo lake. 22 Nao mpini pia ukazidi kuingia ndani ukiufuata upanga huo na mafuta yakaufunika upanga huo, kwa maana hakuuchomoa upanga kutoka katika tumbo lake, na mavi yakaanza kutoka nje. 23 Naye Ehudi akatoka nje kupitia tundu la hewa, lakini akaifunga kwa ufunguo milango ya chumba cha dari. 24 Naye akatoka nje.+
Na watumishi wa mfalme wakaja na kuanza kuangalia, na tazama, milango ya chumba cha dari ilikuwa imefungwa kwa ufunguo. Kwa hiyo wakasema: “Ameenda haja+ katika chumba chake cha ndani chenye baridi.” 25 Nao wakaendelea kungojea mpaka wakaona aibu, na, tazama! hakuna aliyeifungua milango ya kile chumba cha dari. Ndipo wakachukua ufunguo na kuifungua, na, tazama! bwana wao alikuwa ameanguka chini, naye amekufa!
26 Lakini Ehudi alikimbia walipokuwa bado wanakawia, naye akapita kando ya yale machimbo ya mawe,+ akakimbia, akaenda Seira. 27 Na ikawa kwamba alipofika huko akaanza kupiga baragumu+ katika eneo lenye milima la Efraimu;+ na wana wa Israeli wakaanza kushuka pamoja naye kutoka katika eneo lenye milima, yeye akiwa mbele yao. 28 Ndipo akawaambia: “Nifuateni,+ kwa maana Yehova amewatia adui zenu, Wamoabu, mkononi mwenu.”+ Nao wakamfuata, wakateka vivuko+ vya Yordani juu ya Wamoabu, wala hawakumruhusu mtu yeyote avuke. 29 Na wakati huo wakapiga Moabu, karibu wanaume elfu kumi,+ kila mmoja akiwa ni mwenye nguvu+ na kila mmoja akiwa ni mwanamume shujaa; wala hakuna hata mtu mmoja aliyepona.+ 30 Na Moabu wakatiishwa siku hiyo chini ya mkono wa Israeli; na nchi haikuwa na usumbufu wowote tena kwa miaka 80.+
31 Na baada yake kukawa na Shamgari+ mwana wa Anathi, naye akawapiga Wafilisti,+ wanaume mia sita, kwa mchokoo wa ng’ombe; naye pia akawaokoa Israeli.+
4 Ndipo wana wa Israeli wakaanza tena kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova kwa vile sasa Ehudi alikuwa amekufa.+ 2 Basi Yehova akawauza+ mkononi mwa Yabini mfalme wa Kanaani, aliyetawala katika Hasori;+ na mkuu wa jeshi lake alikuwa ni Sisera,+ naye alikuwa anakaa Haroshethi+ ya mataifa. 3 Na wana wa Israeli wakaanza kumlilia Yehova,+ kwa sababu Yabini alikuwa na magari 900 ya vita yenye miundu ya chuma,+ naye kwa miaka 20 akawakandamiza wana wa Israeli+ kwa ukali.
4 Basi Debora, nabii wa kike,+ mke wa Lapidothi, ndiye aliyekuwa akihukumu Israeli wakati huo. 5 Naye alikuwa anakaa chini ya mtende wa Debora kati ya Rama+ na Betheli+ katika eneo lenye milima la Efraimu; na wana wa Israeli wakawa wakimwendea ili awahukumu. 6 Naye akatuma ujumbe kumwita Baraka+ mwana wa Abinoamu kutoka Kedesh-naftali,+ akamwambia: “Je, Yehova Mungu wa Israeli hakutoa amri? ‘Nenda, usambae katika Mlima Tabori,+ nawe uchukue wanaume elfu kumi kutoka kwa wana wa Naftali+ na kutoka kwa wana wa Zabuloni.+ 7 Nami hakika nitamvuta kwako+ Sisera+ mkuu wa jeshi la Yabini+ na magari yake ya vita na umati wake, kwenye bonde la mto la Kishoni,+ nami hakika nitamtia yeye mkononi mwako.’”+
8 Ndipo Baraka akamwambia: “Ukienda pamoja nami, mimi pia nitaenda; lakini usipoenda pamoja nami, mimi sitaenda.” 9 Basi yule nabii akasema: “Hakika nitaenda pamoja nawe. Hata hivyo, kile kitu cha kurembesha hakitakuwa chako katika njia unayoiendea, kwa kuwa Yehova atamuuza Sisera katika mkono wa mwanamke.”+ Ndipo Debora akasimama, akaenda pamoja na Baraka mpaka Kedeshi.+ 10 Na Baraka akaanza kuita Zabuloni+ na Naftali waje Kedeshi, nao wakapanda wanaume elfu kumi wakifuata hatua zake;+ na Debora akapanda pamoja naye.
11 Lakini Heberi+ Mkeni alikuwa amejitenga na Wakeni,+ wana wa Hobabu, ambaye Musa alikuwa mwana-mkwe wake,+ naye alikuwa amelisimamisha hema lake karibu na ule mti mkubwa kule Saananimu, ambao uko katika Kedeshi.
12 Ndipo wakampasha Sisera habari kwamba Baraka mwana wa Abinoamu+ amepanda kwenda Mlima Tabori.+ 13 Mara moja Sisera akakusanya pamoja magari yake yote ya vita, yale magari mia tisa ya vita yenye miundu ya chuma,+ na watu wote waliokuwa pamoja naye, kutoka Haroshethi ya mataifa mpaka kwenye bonde la mto la Kishoni.+ 14 Ndipo Debora akamwambia Baraka: “Simama, kwa maana hii ndiyo siku ambayo Yehova hakika atamtia Sisera mkononi mwako. Je, Yehova siye ambaye ameenda mbele yako?”+ Na Baraka akashuka kutoka Mlima Tabori akiwa na wanaume elfu kumi nyuma yake. 15 Ndipo Yehova akaanza kumvuruga+ Sisera na magari yake yote ya vita na kambi yote kwa makali ya upanga mbele ya Baraka. Mwishowe Sisera akashuka kutoka garini, akaanza kukimbia kwa miguu. 16 Kisha Baraka akafuatilia+ yale magari ya vita+ na ile kambi mpaka Haroshethi ya mataifa, hivi kwamba kambi yote ya Sisera ikaanguka kwa makali ya upanga. Hakubaki hata mmoja.+
17 Lakini Sisera+ akakimbia kwa miguu mpaka kwenye hema la Yaeli+ mke wa Heberi Mkeni,+ kwa maana kulikuwa na amani kati ya Yabini mfalme wa Hasori+ na nyumba ya Heberi Mkeni. 18 Ndipo Yaeli akatoka nje kumpokea Sisera, akamwambia: “Karibia huku, bwana wangu, karibia huku kwangu. Usiogope.” Basi akakaribia kwake, akaingia katika hema. Baadaye akamfunika kwa blangeti. 19 Kisha akamwambia: “Tafadhali, nipe maji kidogo ya kunywa, kwa maana nina kiu.” Basi huyo mwanamke akafungua kiriba+ cha maziwa, akampa kinywaji,+ kisha akamfunika. 20 Naye akamwambia tena: “Simama mlangoni pa hema, na itakuwa kwamba yeyote akija na kukuuliza na kusema, ‘Je, yupo mwanamume yeyote hapa?’ ndipo useme, ‘Hapana!’”
21 Na Yaeli mke wa Heberi akachukua kigingi cha hema, akashika nyundo mkononi mwake. Kisha akaenda kwake kimyakimya, akakipigilia kile kigingi katika kipaji cha uso wake,+ akakipigilia mpaka kikaingia katika udongo, huyo akiwa amelala usingizi mzito na kuchoka. Basi akafa.+
22 Na, tazama! Baraka alikuwa anamfuatilia Sisera. Basi Yaeli akatoka nje kumpokea, akamwambia: “Njoo, nami nitakuonyesha mtu unayemtafuta.” Basi akaingia kwake ndani, na, tazama! Sisera alikuwa ameanguka na amekufa, nacho kigingi kikiwa katika kipaji cha uso wake.
23 Kwa hiyo Mungu akamtiisha+ Yabini mfalme wa Kanaani mbele ya wana wa Israeli siku hiyo. 24 Na mkono wa wana wa Israeli ukaendelea kuwa mgumu zaidi na zaidi juu ya Yabini mfalme wa Kanaani,+ mpaka walipokuwa wamemkatilia mbali Yabini mfalme+ wa Kanaani.
5 Na katika siku hiyo Debora+ pamoja na Baraka+ mwana wa Abinoamu+ wakaanza kuimba,+ wakisema:
2 “Kwa kuacha nywele zining’inie katika Israeli kwa ajili ya vita,
Kwa ajili ya watu kujitolea,+
Mbarikini Yehova.+
Ulipopiga mwendo kutoka shamba la Edomu,+
Dunia ilitikisika,+ mbingu pia zikatiririka maji,+
Mawingu pia yakatiririka maji.
5 Milima ikayeyuka kutoka mbele za uso wa Yehova,+
Mlima Sinai+ kutoka mbele za uso wa Yehova,+ Mungu wa Israeli.+
6 Katika siku za Shamgari+ mwana wa Anathi,
Katika siku za Yaeli,+ njia hazikuwa na wapitaji,
Na wasafiri wa barabarani wakawa wakisafiri kwa njia za kuzunguka.+
7 Wakaaji katika nchi iliyo wazi wakakoma, wakakoma katika Israeli,+
Mpaka mimi, Debora,+ niliposimama,
Mpaka niliposimama kama mama katika Israeli.+
8 Wakaanza kuchagua miungu mipya.+
Ndipo kukawa na vita malangoni.+
Ngao haikuonekana, wala mkuki,
Kati ya 40,000 katika Israeli.+
10 Enyi wapandaji wa punda-jike+ wenye rangi nyekundu ya kimanjano,
Enyi mnaokaa kwenye mazulia yenye thamani,
Nanyi mnaotembea barabarani,
Angalieni!+
11 Sauti za wenye kugawa maji katika mahali pa kuteka maji,+
Hapo walianza kusimulia matendo ya uadilifu ya Yehova,+
Matendo ya uadilifu ya wakaaji wake katika nchi iliyo wazi katika Israeli.
Ndipo watu wa Yehova walipoondoka na kwenda mpaka malangoni.
13 Ndipo wenye kuokoka wakashuka kwenda kwa walio mashuhuri;
Watu wa Yehova walishuka kuja kwangu ili kupigana na wanaume wenye nguvu.
14 Asili yao ilikuwa katika Efraimu katika nchi tambarare ya chini,+
Pamoja nawe, Ee Benyamini, kati ya watu wako.
Kutoka Makiri+ viongozi walishuka,
Na kutoka Zabuloni wale wanaotumia vifaa vya mwandishi.+
15 Na wakuu katika Isakari+ walikuwa pamoja na Debora,
Na kama Isakari, ndivyo alivyokuwa Baraka.+
Alipelekwa kwa miguu katika nchi tambarare ya chini.+
Katikati ya migawanyo ya Rubeni kulikuwa na uchunguzi mkubwa wa moyo.+
16 Kwa nini uliketi kati ya yale mafumba mawili ya matandiko,
Ili kusikiliza zumari zikipigiwa makundi?+
Kulikuwa na uchunguzi mkubwa wa moyo+ kwa ajili ya migawanyo ya Rubeni.
17 Gileadi alijikalia katika makao yake ng’ambo ile nyingine ya Yordani;+
Na Dani, kwa nini aliendelea kukaa wakati huo katika meli?+
Asheri aliketi kizembe kando ya bahari,
Akaendelea kukaa mahali pake pa kushukia pwani.+
19 Wafalme walikuja, wakapiga vita;
Ndipo wafalme wa Kanaani wakapiga vita+
Katika Taanaki+ kando ya maji ya Megido.+
Hawakuchukua faida yoyote ya fedha.+
21 Mto wa Kishoni ukawafagilia mbali,+
Mto wa siku za kale, mto wa Kishoni.+
Wewe ulikanyagia chini nguvu,+ ewe nafsi yangu.
23 ‘Laani+ Merozi,’ akasema malaika wa Yehova,+
‘Walaani wakaaji wake bila kukoma,
Kwa sababu hawakuja kumsaidia Yehova,
Kumsaidia Yehova pamoja na wanaume wenye nguvu.’
24 Yaeli+ mke wa Heberi Mkeni,+ atabarikiwa zaidi kati ya wanawake,
Kati ya wanawake katika mahema atabarikiwa zaidi.+
25 Aliomba maji, akampa maziwa;
Alimpa maziwa ya mgando+ katika bakuli kubwa la karamu la walio mashuhuri.
26 Akanyoosha mkono wake akashika kigingi cha hema,
Nao mkono wake wa kuume ukashika nyundo ya mti ya wafanyakazi wenye bidii.+
Akampiga Sisera kwa nyundo hiyo, akatoboa kichwa chake,+
Akapasua na kukata kipaji cha uso wake.
27 Aliporomoka katikati ya miguu yake, alianguka, akalala chini;
Aliporomoka katikati ya miguu yake, alianguka;
Hapo alipoporomoka, ndipo alipoanguka akiwa ameshindwa.+
28 Mwanamke alichungulia nje dirishani, akaendelea kumngojea,
Mama ya Sisera akiwa kwenye dirisha lenye matundu,+
‘Kwa nini gari lake la vita limechelewa kuja?+
Kwa nini vishindo vya kwato za magari yake vichelewe sana hivyo?’+
29 Wenye hekima kati ya bibi+ zake wenye vyeo walikuwa wakimjibu,
Ndiyo, yeye pia alikuwa akijibu kwa maneno yake mwenyewe,
30 ‘Je, haiwapasi wao kupata, haiwapasi wao kugawanya nyara,+
Tumbo moja la uzazi—matumbo mawili ya uzazi kwa kila mwanamume,+
Nyara za vitu vilivyotiwa rangi kwa ajili ya Sisera, nyara za vitu vilivyotiwa rangi,
Vazi lililopambwa, vitu vilivyotiwa rangi, mavazi mawili yaliyopambwa
Kwa ajili ya shingo za wanaume wa nyara?’
31 Na waangamie hivyo adui zako wote,+ Ee Yehova,
Na wanaokupenda+ wawe kama wakati jua linaposonga katika nguvu zake.”+
Na nchi ikawa bila usumbufu tena kwa miaka 40.+
6 Ndipo wana wa Israeli wakaanza kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+ Basi Yehova akawatia mkononi mwa Midiani+ kwa miaka saba. 2 Nao mkono wa Midiani ukawa na nguvu juu ya Israeli.+ Kwa sababu ya Midiani, wana wa Israeli walijifanyia maghala ya chini ya udongo yaliyokuwa katika milima, na mapango na mahali palipo pagumu kufikiwa.+ 3 Na ikatukia kwamba, Israeli wakipanda mbegu,+ Midiani na Amaleki+ na watu wa Mashariki+ walikuwa wakija, ndiyo, walikuja kupigana nao. 4 Nao wakawa wakipiga kambi juu yao na kuyaharibu mazao ya nchi mpaka Gaza, na hawakuruhusu mazao yoyote wala kondoo wala ng’ombe wala punda kubaki katika Israeli.+ 5 Kwa maana wao pamoja na mifugo yao walikuwa wakija na mahema yao. Walikuja wakiwa wengi kama nzige,+ na wao pamoja na ngamia zao hawakuwa na hesabu;+ nao walikuwa wakiingia katika nchi ili kuiharibu.+ 6 Na Israeli wakawa maskini sana kwa sababu ya Midiani; nao wana wa Israeli wakaanza kumwomba Yehova msaada.+
7 Na ikawa kwamba kwa kuwa wana wa Israeli walimwomba Yehova msaada kwa sababu ya Midiani,+ 8 Yehova akamtuma mwanamume mmoja, nabii,+ kwa wana wa Israeli, akawaambia: “Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi, ‘Mimi ndiye niliyewaleta ninyi mpande kutoka Misri,+ nikawatoa katika nyumba ya watumwa.+ 9 Kwa hiyo nikawakomboa ninyi kutoka katika mkono wa Misri na kutoka katika mkono wa wakandamizaji wenu wote, nikawafukuza kutoka mbele yenu, nikawapa ninyi nchi yao.+ 10 Zaidi ya hayo, nikawaambia ninyi: “Mimi ni Yehova Mungu wenu.+ Msiogope miungu ya Waamori+ ambao mnakaa katika nchi yao.”+ Nanyi hamkuisikiliza sauti yangu.’”+
11 Baadaye malaika wa Yehova akaja+ na kuketi chini ya mti mkubwa uliokuwa katika Ofra, mali yake Yoashi Mwabiezeri,+ wakati Gideoni+ mwana wake alipokuwa akipepeta ngano katika shinikizo la divai ili kuiondoa haraka machoni pa Midiani. 12 Ndipo malaika wa Yehova akamtokea, akamwambia: “Yehova yupo pamoja nawe,+ Ee mwanamume shujaa na mwenye nguvu.” 13 Kwa hiyo Gideoni akamwambia: “Nakuomba radhi, bwana wangu, lakini ikiwa Yehova yupo pamoja nasi, kwa nini haya yote yametupata,+ na yako wapi matendo yake yote ya ajabu+ ambayo mababu zetu walitusimulia,+ wakisema, ‘Je, Yehova siye aliyetuleta kutoka Misri?’+ Na sasa Yehova ametuacha,+ naye anatutia katika mkono wa Midiani.” 14 Ndipo Yehova akamtazama na kusema: “Nenda katika nguvu zako hizi,+ nawe hakika utawaokoa Israeli kutoka katika mkono wa Midiani.+ Je, si mimi ninayekutuma?”+ 15 Yeye naye akamwambia: “Nakuomba radhi, Yehova. Nitawaokoa Israeli na nini?+ Tazama! Elfu yangu ndiyo ndogo zaidi katika Manase, na mimi ndiye mdogo zaidi katika nyumba ya baba yangu.”+ 16 Lakini Yehova akamwambia: “Kwa sababu nitakuwa pamoja nawe,+ nawe hakika utapiga Midiani+ kama mtu mmoja.”
17 Ndipo akamwambia: “Ikiwa sasa nimepata kibali machoni pako,+ unifanyie ishara kwamba wewe ndiwe unayesema nami.+ 18 Tafadhali, usiondoke hapa mpaka nije kwako+ na kukuletea zawadi yangu na kuiweka mbele yako.”+ Basi akasema: “Mimi nitaendelea kuketi hapa mpaka utakaporudi.” 19 Na Gideoni akaingia ndani, akatayarisha mwana-mbuzi+ na efa ya unga kuwa keki zisizo na chachu.+ Akaweka nyama katika kikapu, mchuzi akauweka katika chungu cha kupikia, kisha akamletea hapo nje chini ya ule mti mkubwa, akavipakua.
20 Basi yule malaika wa Mungu wa kweli akamwambia: “Chukua nyama hiyo na keki hizo zisizo na chachu, uviweke juu ya lile jiwe kubwa pale,+ ukaumimine huu mchuzi.” Akafanya hivyo. 21 Ndipo malaika wa Yehova akainyoosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake, akaigusa ile nyama na zile keki zisizo na chachu, na moto ukaanza kupanda kutoka katika ule mwamba, ukaiteketeza ile nyama na zile keki zisizo na chachu.+ Na yule malaika wa Yehova akatoweka machoni pake. 22 Kwa hiyo Gideoni akatambua kwamba alikuwa ni malaika wa Yehova.+
Mara moja Gideoni akasema: “Ole wangu, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, kwa sababu nimeona malaika wa Yehova uso kwa uso!”+ 23 Lakini Yehova akamwambia: “Amani iwe pamoja nawe.+ Usiogope.+ Hutakufa.”+ 24 Basi Gideoni akamjengea Yehova madhabahu+ hapo, nayo inaendelea kuitwa+ jina Yehova-shalomu mpaka leo hii. Bado iko katika Ofra+ ya Waabiezeri.
25 Na ikawa usiku huo kwamba Yehova akamwambia tena: “Mchukue yule ng’ombe-dume mchanga, yule ng’ombe-dume wa baba yako, yaani, yule ng’ombe-dume mchanga wa pili mwenye miaka saba, nawe ubomoe madhabahu ya Baali+ ambayo ni ya baba yako, na ule mti mtakatifu ulio kando yake, uukate.+ 26 Nawe umjengee Yehova Mungu wako madhabahu mbele ya ngome hii, kwa mistari ya mawe, nawe umchukue ng’ombe-dume mchanga wa pili, umtoe kama toleo la kuteketezwa juu ya kuni za ule mti mtakatifu ambao utaukata.” 27 Basi Gideoni akawachukua wanaume kumi kati ya watumishi wake, akafanya kama vile Yehova alivyokuwa amemwambia;+ lakini ikawa kwamba, kwa kuwa aliogopa mno nyumba ya baba yake na watu wa jiji, hakuweza kuyafanya hayo mchana, aliyafanya usiku.+
28 Watu wa jiji walipoamka asubuhi na mapema kama kawaida, tazama! madhabahu ya Baali ilikuwa imebomolewa na ule mti mtakatifu+ uliokuwa kando yake ulikuwa umekatwa, na yule ng’ombe-dume mchanga wa pili alikuwa ametolewa juu ya madhabahu ambayo ilikuwa imejengwa. 29 Nao wakaanza kusemezana: “Ni nani ambaye amefanya jambo hili?” Wakauliza-uliza na kutafuta. Mwishowe wakasema: “Gideoni mwana wa Yoashi ndiye aliyefanya jambo hili.” 30 Kwa hiyo watu wa jiji wakamwambia Yoashi: “Mtoe nje mwana wako afe,+ kwa sababu amebomoa madhabahu ya Baali, na kwa sababu amekata mti mtakatifu uliokuwa kando yake.” 31 Ndipo Yoashi+ akawaambia wote waliosimama kumpinga:+ “Je, ninyi ndio mtakaomtetea kisheria Baali ili kuona kama ninyi wenyewe mnaweza kumwokoa? Yeyote atakayemtetea kisheria anapaswa kuuawa asubuhi hii.+ Ikiwa yeye ni Mungu,+ acheni ajitetee mwenyewe kisheria,+ kwa sababu mtu fulani amebomoa madhabahu yake.” 32 Naye akaanza kumwita jina Yerubaali+ siku hiyo, akisema: “Baali na ajitetee mwenyewe kisheria, kwa sababu mtu fulani amebomoa madhabahu yake.”+
33 Na Midiani+ wote na Amaleki+ na watu wa Mashariki+ wakakusanyika kama mtu mmoja,+ wakavuka na kupiga kambi katika nchi tambarare ya chini ya Yezreeli.+ 34 Na roho ya Yehova+ ikamfunika Gideoni naye akaanza kupiga baragumu,+ na Waabiezeri+ wakakusanywa pamoja kumfuata. 35 Naye akatuma wajumbe+ katika Manase yote, nao pia wakakusanywa pamoja kumfuata. Pia akatuma wajumbe kotekote katika Asheri na Zabuloni na Naftali, nao wakaja kukutana naye.
36 Ndipo Gideoni akamwambia Mungu wa kweli: “Ikiwa utawaokoa Israeli kupitia kwangu, kama vile ambavyo umeahidi,+ 37 tazama, ninaweka manyoya ya kondoo yakiwa wazi katika uwanja wa kupuria. Umande ukija juu ya manyoya hayo peke yake lakini nchi yote hapo iwe kavu, ndipo nitakapojua kwamba utawaokoa Israeli kupitia kwangu, kama vile ambavyo umeahidi.” 38 Na ikawa hivyo. Alipoamka mapema siku iliyofuata na kukamua manyoya hayo, akatoa katika manyoya hayo umande wa kutosha kujaza maji bakuli kubwa la karamu. 39 Hata hivyo, Gideoni akamwambia Mungu wa kweli: “Usiache hasira yako iwake juu yangu, bali acha niseme tena mara moja tu. Tafadhali, acha nifanye jaribio mara moja tu kwa manyoya hayo. Tafadhali, acha ukavu uje juu ya manyoya hayo peke yake, na umande uje juu ya nchi yote.” 40 Basi Mungu akafanya hivyo usiku huo; na ukavu ukaja kuwa juu ya manyoya peke yake, na umande ukawa juu ya nchi yote.
7 Ndipo Yerubaali,+ yaani, Gideoni,+ na watu wote waliokuwa pamoja naye, wakaondoka mapema na kupiga kambi kando ya kisima cha Harodi; na kambi ya Midiani ilikuwa upande wake wa kaskazini, kwenye kilima cha More, katika nchi tambarare ya chini. 2 Sasa Yehova akamwambia Gideoni: “Watu ulio nao ni wengi mno nisiweze kuwatia Midiani mkononi mwao.+ Labda Israeli watajivuna+ dhidi yangu, wakisema, ‘Mkono wangu ndio ulioniokoa.’+ 3 Na sasa tafadhali, ita masikioni mwa watu, ukisema, ‘Ni nani anayeogopa na kutetemeka? Na ajiondoe.’”+ Basi Gideoni akawafanyia majaribio. Ndipo watu 22,000 wakajiondoa, wakabaki watu 10,000.
4 Lakini Yehova akamwambia Gideoni: “Bado kuna watu wengi mno.+ Washushe kwenye maji ili niwajaribu kwa ajili yako pale. Na itatukia kwamba yeyote nitakayekuambia, ‘Huyu ataenda pamoja nawe,’ yeye ndiye atakayeenda pamoja nawe, lakini yeyote ambaye nitakuambia, ‘Huyu hataenda pamoja nawe,’ yeye hataenda.” 5 Basi akawashusha watu majini.+
Ndipo Yehova akamwambia Gideoni: “Kila mtu ambaye ataramba maji kwa ulimi wake kama vile mbwa anavyoramba, utamweka kando peke yake, pia kila mtu atakayepiga magoti yake anapokunywa.”+ 6 Na hesabu ya wale walioramba kwa mkono wao wakiuleta kinywani ikawa watu mia tatu. Lakini wale watu wengine wote walipiga magoti yao walipokunywa maji.
7 Yehova akamwambia Gideoni: “Kwa watu hawa mia tatu walioramba nitawaokoa ninyi, nami nitatia Midiani mkononi mwako.+ Lakini hawa watu wengine wote na waende kila mmoja mahali pake.” 8 Kwa hiyo wakachukua vyakula vya watu hao mkononi mwao, na baragumu+ zao, na watu wote wa Israeli akawaacha waende zao kila mmoja nyumbani kwake; akabaki na wale watu mia tatu. Nayo kambi ya Midiani ilikuwa chini yake katika nchi tambarare ya chini.+
9 Na ikawa kwamba usiku+ huo Yehova akamwambia hivi: “Simama, shuka juu ya kambi hiyo, kwa maana nimeitia mkononi mwako.+ 10 Lakini ikiwa unaogopa kushuka, shuka, wewe pamoja na Pura mtumishi wako, kambini.+ 11 Nawe usikilize yale watakayosema,+ na baada ya hayo mikono yako itapata nguvu,+ nawe hakika utashuka juu ya kambi hiyo.” Ndipo yeye na Pura mtumishi wake wakashuka mpaka kwenye ukingo wa wale waliokuwa wamejipanga kivita, waliokuwa katika kambi.
12 Sasa Midiani na Amaleki na watu wote wa Mashariki+ walikuwa wamejazana katika ile nchi tambarare ya chini, wengi sana kama nzige;+ na ngamia+ zao hawakuwa na hesabu, walikuwa wengi sana kama chembe za mchanga ulio kando ya bahari. 13 Basi Gideoni akaja, na, tazama! kulikuwa na mtu akimsimulia mwenzake ndoto, naye akasema: “Hii ni ndoto ambayo nimeota.+ Na, tazama! kulikuwa na keki ya mviringo ya mkate wa shayiri ikigeuka-geuka katika kambi ya Midiani. Ndipo ikaja kwenye hema na kulipiga nalo likaanguka,+ ikalipindua juu chini, na hema hilo likaanguka chini.” 14 Naye mwenzake akajibu+ na kusema: “Hiki si kitu kingine bali ni upanga wa Gideoni+ mwana wa Yoashi, mtu wa Israeli. Mungu wa kweli+ ametia Midiani na kambi yote katika mkono wake.”+
15 Na ikawa kwamba, mara tu Gideoni aliposikia masimulizi ya ndoto hiyo na maelezo yake,+ akaanza kuabudu.+ Kisha akarudi katika kambi ya Israeli na kusema: “Simameni,+ kwa kuwa Yehova ametia kambi ya Midiani katika mkono wenu.” 16 Ndipo akagawanya wale watu mia tatu katika vikosi vitatu na kuwapa wote mkononi baragumu+ na mitungi mikubwa mitupu, na mienge ndani ya mitungi hiyo mikubwa. 17 Naye akawaambia: “Jifunzeni kwa kunitazama, nanyi fanyeni vivyo hivyo. Nitakapofika kwenye ukingo wa kambi, iwe kwamba vile nitakavyofanya, fanyeni vivyo hivyo. 18 Nitakapokuwa nimekwisha kupiga baragumu, mimi na wote walio pamoja nami, ninyi pia zipigeni baragumu, kuizunguka kambi yote,+ nanyi mseme, ‘Upanga wa Yehova+ na wa Gideoni!’”
19 Baadaye Gideoni akaja na wale wanaume mia moja waliokuwa pamoja naye kwenye ukingo wa kambi mwanzoni mwa kesha la katikati ya usiku.+ Walikuwa wamemaliza tu kuweka askari-walinzi. Nao wakaanza kuzipiga zile baragumu,+ na ile mitungi mikubwa ya maji iliyokuwa mikononi mwao ikavunjwa vipande-vipande.+ 20 Ndipo vile vikosi vitatu vikapiga baragumu+ na kuivunja-vunja ile mitungi mikubwa na kuchukua tena ile mienge kwa mkono wao wa kushoto na zile baragumu katika mkono wao wa kuume ili kuzipiga, nao wakaanza kupaaza sauti: “Upanga wa Yehova+ na wa Gideoni!” 21 Nao wakaendelea kusimama kila mmoja mahali pake kuzunguka kambi pande zote, na kambi yote ikaanza kupiga mbio, wakapiga kelele na kukimbia.+ 22 Na wale mia tatu+ wakaendelea kupiga baragumu,+ na Yehova akatia upanga wa kila mmoja juu ya mwenzake katika kambi yote;+ na kambi ikaendelea kukimbia hadi Beth-shita, hadi Serera, hadi kwenye mipaka ya Abel-mehola+ kando ya Tabathi.
23 Wakati huohuo watu wa Israeli wakakusanywa pamoja kutoka Naftali+ na Asheri+ na Manase+ wote, nao wakawafuatilia+ Midiani. 24 Na Gideoni akatuma wajumbe katika eneo lote lenye milima la Efraimu,+ akisema: “Shukeni mkutane na Midiani na mshike hayo maji mbele yao mpaka Beth-bara na Yordani.” Basi watu wote wa Efraimu wakakusanywa pamoja, nao wakayashika maji+ mpaka Beth-bara na Yordani. 25 Pia wakawakamata wale wakuu wawili wa Midiani, yaani, Orebu na Zeebu;+ wakamuua Orebu+ juu ya mwamba wa Orebu, nao wakamuua Zeebu kwenye mtungi wa divai wa Zeebu. Nao wakaendelea kufuatilia Midiani,+ wakamletea Gideoni kichwa cha Orebu na kile cha Zeebu katika eneo la Yordani.+
8 Ndipo watu wa Efraimu wakamwambia: “Umetutendea jambo gani hili kwa kukosa kutuita ulipotoka kwenda kupigana na Midiani?”+ Nao wakatafuta kwa ukali kugombana naye.+ 2 Mwishowe akawaambia: “Basi mimi nimefanya nini kwa kulinganishwa nanyi?+ Je, masalio ya Efraimu+ si bora kuliko ukusanyaji wa zabibu wa Abiezeri?+ 3 Mungu aliwatia hao wakuu wa Midiani, Orebu na Zeebu+ katika mkono wenu, nami nimeweza kufanya nini kwa kulinganishwa nanyi?” Ndipo roho yao ikatulia kumwelekea aliposema neno hilo.+
4 Mwishowe Gideoni akaja Yordani, akauvuka, yeye pamoja na wale wanaume mia tatu waliokuwa pamoja naye, wakiwa wamechoka lakini wakiwa wanaendelea kufuatilia. 5 Baadaye akawaambia watu wa Sukothi:+ “Tafadhali wapeni mikate ya mviringo watu wanaofuata hatua zangu,+ kwa kuwa wamechoka nami ninawafuatilia Zeba+ na Zalmuna,+ wafalme wa Midiani.” 6 Lakini wakuu wa Sukothi wakasema: “Je, viganja vya mikono ya Zeba na Zalmuna tayari vimo mkononi mwako ili jeshi lako lipewe mkate?”+ 7 Ndipo Gideoni akasema: “Ndiyo sababu Yehova atakapowatia Zeba na Zalmuna katika mkono wangu, hakika nitaipepeta miili yenu kwa miiba ya nyikani na michongoma.”+ 8 Naye akatoka hapo na kwenda Penueli,+ akasema nao vivyo hivyo, lakini watu wa Penueli wakamjibu kama vile watu wa Sukothi walivyokuwa wamemjibu. 9 Basi akawaambia pia watu wa Penueli: “Nitakaporudi kwa amani, nitaubomoa mnara huu.”+
10 Basi Zeba na Zalmuna+ walikuwa katika Karkori, nao walikuwa pamoja na kambi zao, kukiwa na karibu watu 15,000 waliobaki kutoka katika kambi nzima ya watu wa Mashariki;+ na wale waliokuwa tayari wameanguka ni watu 120,000 waliokuwa wakitumia upanga.+ 11 Na Gideoni akaendelea kupanda kupitia njia ya wale wanaokaa katika mahema upande wa mashariki wa Noba na Yogbeha,+ naye akaanza kuishambulia kambi wakati kambi hiyo ilipokuwa haijihadhari.+ 12 Wakati Zeba na Zalmuna walipoanza kukimbia, akaanza kuwafuatilia mara moja, akawakamata hao wafalme wawili wa Midiani, Zeba na Zalmuna;+ naye akaitetemesha kambi nzima.
13 Ndipo Gideoni mwana wa Yoashi akaanza kurudi kutoka vitani kupitia ile njia nyembamba inayopanda kwenda Heresi. 14 Akiwa njiani, akamkamata kijana kutoka kwa watu wa Sukothi+ na kutafuta habari kutoka kwake.+ Basi akamwandikia majina ya wakuu+ wa Sukothi na wanaume wazee wake, watu 77. 15 Ndipo akaenda kwa watu wa Sukothi na kusema: “Tazameni, Zeba na Zalmuna ambao mlinidhihaki kuwahusu, mkisema, ‘Je, viganja vya mikono vya Zeba na Zalmuna tayari vimo mkononi mwako ili watu wako waliochoka wapewe mkate?’”+ 16 Ndipo akawachukua hao wanaume wazee wa jiji na miiba ya nyikani na michongoma, naye akaitumia kuwafundisha somo watu wa Sukothi.+ 17 Naye akabomoa mnara+ wa Penueli,+ kisha akawaua watu wa jiji hilo.
18 Kisha akawaambia Zeba na Zalmuna:+ “Wale watu mliowaua katika Tabori+ walikuwa watu wa namna gani?” Wakasema: “Kama wewe ulivyo, ndivyo wao walivyokuwa, kila mmoja wao, kama wana wa mfalme katika umbo.” 19 Kwa hiyo akasema: “Hao walikuwa ndugu zangu, wana wa mama yangu. Kama Yehova anavyoishi, ikiwa mngeliwahifadhi hai, singeliwaua ninyi.”+ 20 Ndipo akamwambia Yetheri mzaliwa wake wa kwanza: “Simama, waue.” Lakini huyo kijana hakuchomoa upanga wake, kwa sababu aliogopa, kwa maana bado alikuwa kijana tu.+ 21 Basi Zeba na Zalmuna wakasema: “Simama wewe mwenyewe utushambulie, kwa maana jinsi mwanamume alivyo, ndivyo zilivyo nguvu zake.”+ Kwa hiyo Gideoni akasimama na kuwaua+ Zeba na Zalmuna, naye akachukua yale mapambo yenye umbo la mwezi yaliyokuwa katika shingo za ngamia zao.
22 Baadaye watu wa Israeli wakamwambia Gideoni: “Tawala juu yetu,+ wewe na mwana wako na mjukuu wako vilevile, kwa maana umetuokoa kutoka katika mkono wa Midiani.”+ 23 Lakini Gideoni akawaambia: “Mimi mwenyewe sitatawala juu yenu, wala mwanangu hatatawala juu yenu.+ Yehova ndiye atakayetawala juu yenu.”+ 24 Kisha Gideoni akawaambia tena: “Acheni niwaombe jambo moja: Kila mmoja wenu anipe pete ya pua+ ya nyara yake.” (Kwa maana walikuwa na pete za pua za dhahabu, kwa sababu walikuwa Waishmaeli.)+ 25 Ndipo wakasema: “Hakika tutazitoa.” Basi wakatandika nguo ya kujitanda, na kila mmoja wao akatupa ndani yake pete ya pua ya nyara yake. 26 Na uzito wa zile pete za pua za dhahabu ambazo alikuwa ameomba ukajumlika kuwa shekeli elfu moja na mia saba za dhahabu, mbali na yale mapambo yenye umbo la mwezi+ na herini na mavazi ya sufu iliyotiwa rangi ya zambarau+ ambayo wale wafalme wa Midiani walikuwa wamevaa, na pia mbali na ile mikufu iliyokuwa katika shingo za ngamia.+
27 Naye Gideoni akavifanya kuwa efodi+ na kuiweka katika jiji lake la Ofra+ ili ionekane; na Israeli wote wakaanza kufanya uasherati nayo hapo,+ nayo ikawa mtego kwa Gideoni na kwa nyumba yake.+
28 Hivyo Midiani+ wakatiishwa mbele ya wana wa Israeli, nao hawakuinua kichwa chao tena; na nchi haikuwa na usumbufu wowote tena kwa miaka 40 katika siku za Gideoni.+
29 Na Yerubaali+ mwana wa Yoashi akaenda zake, akaendelea kukaa katika nyumba yake.
30 Naye Gideoni akaja kuwa na wana 70+ waliotoka katika viuno vyake, kwa maana alikuja kuwa na wake wengi. 31 Na yule suria wake aliyekuwa katika Shekemu, yeye pia akamzalia mwana. Basi akamwita jina lake Abimeleki.+ 32 Mwishowe Gideoni mwana wa Yoashi akafa akiwa mwenye umri mwema wa uzeeni, akazikwa katika kaburi la Yoashi baba yake katika Ofra la Waabiezeri.+
33 Na ikawa kwamba mara tu Gideoni alipokufa, wana wa Israeli wakaanza tena kufanya uasherati na Mabaali,+ nao wakamfanya Baal-berithi kuwa mungu wao.+ 34 Na wana wa Israeli hawakumkumbuka Yehova Mungu wao,+ aliyewakomboa kutoka katika mkono wa adui zao wote pande zote;+ 35 nao hawakuonyesha fadhili zenye upendo+ kwa nyumba ya Yerubaali, Gideoni, kwa kuufuata wema wote ambao aliwaonyesha Israeli.+
9 Baada ya muda Abimeleki+ mwana wa Yerubaali akaenda Shekemu+ kwa ndugu za mama yake, akaanza kusema nao na kusema na familia yote ya nyumba ya baba ya mama yake, akisema: 2 “Tafadhali, semeni masikioni mwa wenye mashamba wote wa Shekemu, ‘Ni jambo gani lililo bora kwenu, kwamba watu 70,+ wana wote wa Yerubaali, watawale juu yenu au mtu mmoja atawale juu yenu? Nanyi mkumbuke kwamba mimi ni mfupa na nyama yenu.’”+
3 Basi ndugu za mama yake wakaanza kusema maneno hayo yote kumhusu yeye masikioni mwa wenye mashamba wote wa Shekemu, na mioyo yao ikaelekea kwa Abimeleki,+ kwa maana walisema: “Yeye ni ndugu yetu.”+ 4 Ndipo wakampa vipande 70 vya fedha kutoka katika nyumba ya Baal-berithi,+ kisha Abimeleki akavitumia kukodisha watu wazembe na wenye dharau,+ ili wafuatane naye. 5 Kisha akaenda nyumbani kwa baba yake katika Ofra,+ akawaua ndugu zake,+ wana wa Yerubaali, watu 70, juu ya jiwe moja, lakini Yothamu mwana mdogo zaidi wa Yerubaali akaachwa, kwa sababu alijificha.
6 Baadaye, watu wote wenye mashamba wa Shekemu na nyumba yote ya Milo+ wakakusanyika pamoja wakaenda, wakamfanya Abimeleki atawale akiwa mfalme,+ karibu na ule mti mkubwa,+ nguzo iliyokuwa katika Shekemu.+
7 Wakati walipompasha Yothamu habari, akaenda mara moja, akasimama juu ya kilele cha Mlima Gerizimu,+ akapaaza sauti yake, akaita na kuwaambia: “Nisikilizeni, enyi wenye mashamba wa Shekemu, na acheni Mungu awasikilize ninyi:
8 “Hapo zamani za kale, miti ilienda kumtia mafuta mfalme juu yao. Basi ikauambia mzeituni,+ ‘Uwe mfalme juu yetu.’+ 9 Lakini mzeituni ukaiambia, ‘Je, niyaache mafuta yangu ambayo kwayo wao humtukuza+ Mungu na wanadamu, na je, niende kuwayawaya juu ya miti mingine?’+ 10 Ndipo miti ikauambia mtini,+ ‘Wewe njoo, uwe malkia juu yetu.’ 11 Lakini mtini ukaiambia, ‘Je, niache utamu wangu na mazao yangu mema, na je, niende kuwayawaya juu ya miti mingine?’+ 12 Kisha miti ikauambia mzabibu, ‘Wewe njoo, uwe malkia juu yetu.’ 13 Ndipo mzabibu ukaiambia, ‘Je, niiache divai yangu mpya ambayo humfurahisha Mungu na wanadamu,+ na je, niende kuwayawaya juu ya miti?’ 14 Mwishowe miti mingine yote ikauambia mkwamba,+ ‘Wewe njoo, uwe mfalme juu yetu.’ 15 Ndipo mkwamba ukaiambia miti, ‘Ikiwa kweli mnanitia mafuta niwe mfalme juu yenu, njooni, tafuteni kimbilio chini ya kivuli changu.+ Lakini kama sivyo, moto+ na utoke ndani ya mkwamba uiteketeze mierezi+ ya Lebanoni.’+
16 “Na sasa ikiwa mmetenda kwa ukweli na bila kosa, mkamfanya Abimeleki kuwa mfalme,+ na ikiwa wema ndio mmemwonyesha Yerubaali na nyumba yake, na ikiwa mmemtendea sawasawa na matendo ya mikono yake, 17 wakati baba yangu alipowapigania+ ninyi, akaihatarisha nafsi+ yake ili apate kuwakomboa ninyi kutoka katika mkono wa Midiani;+ 18 nanyi, kwa upande wenu, mmesimama juu ya nyumba ya baba yangu leo ili mpate kuwaua wanawe,+ watu 70,+ juu ya jiwe moja, na ili mpate kumfanya Abimeleki, mwana wa kijakazi wake,+ kuwa mfalme+ juu ya wenye mashamba wa Shekemu kwa sababu tu yeye ni ndugu yenu; 19 ndiyo, ikiwa mmemtendea Yerubaali na nyumba yake kwa ukweli na bila kosa leo hii, shangilieni juu ya Abimeleki naye pia ashangilie juu yenu.+ 20 Lakini kama sivyo, moto+ na utoke ndani ya Abimeleki, uwateketeze wenye mashamba wa Shekemu na nyumba ya Milo,+ kisha moto+ na utoke ndani ya wenye mashamba wa Shekemu na nyumba ya Milo, nao umteketeze Abimeleki.”+
21 Ndipo Yothamu+ akapiga mbio, akakimbia, akaenda mpaka Beeri, akaanza kukaa hapo kwa sababu ya Abimeleki ndugu yake.
22 Naye Abimeleki akaendelea kujitwalia ukuu juu ya Israeli kwa miaka mitatu.+ 23 Ndipo Mungu akaacha roho mbaya+ itokee kati ya Abimeleki na wale wenye mashamba wa Shekemu, na hao wenye mashamba wa Shekemu wakamtendea Abimeleki hila,+ 24 ili jeuri iliyotendewa wale wana 70 wa Yerubaali ije+ na kwamba apate kuweka damu yao juu ya Abimeleki ndugu yao kwa sababu aliwaua,+ na juu ya wenye mashamba wa Shekemu kwa sababu waliitia nguvu mikono+ yake ili awaue ndugu zake. 25 Basi wenye mashamba wa Shekemu wakaweka watu wamvizie juu ya vilele vya milima, nao wakawa wanamnyang’anya vitu kila mtu ambaye alipita kando yao barabarani. Baada ya muda Abimeleki akaletewa habari.
26 Ndipo Gaali+ mwana wa Ebedi na ndugu zake wakaja na kuvuka kuingia Shekemu,+ nao wenye mashamba wa Shekemu wakaanza kumtumaini.+ 27 Nao wakatoka kwenda shambani kama kawaida, wakakusanya zabibu za mashamba yao na kuzikanyaga na kusherehekea kwa furaha,+ kisha wakaingia katika nyumba ya mungu wao,+ wakala na kunywa+ na kumlaani+ Abimeleki. 28 Ndipo Gaali mwana wa Ebedi akasema: “Abimeleki+ ni nani, na Shekemu ni nani ili tumtumikie? Je, yeye si mwana wa Yerubaali,+ na je, Zebuli+ si mjumbe wake? Ninyi wengine watumikieni watu wa Hamori,+ baba ya Shekemu, lakini je, kwa nini sisi tumtumikie? 29 Laiti watu hawa wangekuwa mkononi mwangu!+ Ndipo ningemwondoa Abimeleki.” Naye akamwambia Abimeleki: “Zidisha jeshi lako kwa wingi, kisha utoke nje.”+
30 Naye Zebuli mkuu wa jiji akayasikia maneno ya Gaali mwana wa Ebedi.+ Ndipo hasira yake ikawaka. 31 Kwa hiyo akatuma wajumbe waende kwa Abimeleki kwa siri, akisema: “Tazama! Gaali mwana wa Ebedi na ndugu zake sasa wamekuja Shekemu,+ nao wanalikusanya jiji kupigana na wewe. 32 Na sasa simama wakati wa usiku,+ wewe pamoja na watu walio nawe, nanyi mvizie+ shambani. 33 Na itatukia kwamba wakati wa asubuhi mara jua linapowaka mwamke mapema, nanyi mfanye mashambulizi ya ghafula juu ya jiji; na yeye na wale watu walio pamoja naye watakapotoka nje kupigana na wewe, umtendee kadiri ya uwezo wa mkono wako.”
34 Basi Abimeleki na watu wote waliokuwa pamoja naye wakaondoka usiku, wakaanza kulivizia jiji la Shekemu wakiwa vikosi vinne. 35 Baadaye Gaali+ mwana wa Ebedi akatoka nje na kusimama penye mwingilio wa lango la jiji. Ndipo Abimeleki na watu waliokuwa pamoja naye wakasimama kutoka mahali pa kuvizia. 36 Gaali alipoona watu hao, mara moja akamwambia Zebuli: “Tazama! Watu wanashuka kutoka katika vilele vya milima.” Lakini Zebuli akamwambia: “Ni vivuli vya milima unavyoviona kana kwamba ni watu.”+
37 Baadaye Gaali akasema mara nyingine tena: “Tazama! Watu wanashuka kutoka katikati ya nchi, na kikosi kimoja kinakuja kupitia njia ya mti mkubwa wa Meonenimu.” 38 Ndipo Zebuli akamwambia: “Basi sasa yako wapi yale maneno yako uliyosema,+ ‘Abimeleki ni nani ili tumtumikie?’+ Je, hawa si wale watu ambao ulikataa?+ Tafadhali, sasa toka nje upigane nao.”
39 Basi Gaali akatoka nje mbele ya wenye mashamba wa Shekemu, akapigana na Abimeleki. 40 Na Abimeleki akamfuatilia, naye akakimbia mbele yake; na waliouawa wakazidi kuanguka kwa wingi mpaka penye mwingilio wa lango.
41 Na Abimeleki akaendelea kukaa katika Aruma, naye Zebuli+ akawafukuza Gaali+ na ndugu zake wasikae katika Shekemu.+ 42 Na ikawa kesho yake kwamba watu wakaanza kutoka nje kwenda shambani. Basi wakamwambia Abimeleki.+ 43 Kwa hiyo, akawachukua watu na kuwagawanya wawe vikosi vitatu,+ akaanza kuvizia shambani. Ndipo akaangalia, na tazama, watu walikuwa wakitoka nje ya jiji. Basi akaenda juu yao, akawapiga na kuwaua. 44 Na Abimeleki na vile vikosi vilivyokuwa pamoja naye wakaenda mbio ili wapate kusimama penye mwingilio wa lango la jiji, huku vikosi viwili vikienda mbio kuwapiga wote waliokuwa shambani, nao wakawapiga na kuwaua.+ 45 Na Abimeleki akapigana na jiji hilo siku hiyo nzima, akaliteka jiji; akawaua watu waliokuwa ndani yake,+ kisha akalibomoa jiji+ na kulitia chumvi.+
46 Wakati wenye mashamba wote wa Shekemu waliposikia habari hizo, wakaenda haraka katika ngome ya nyumba ya El-berithi.+ 47 Ndipo Abimeleki akaletewa habari kwamba wenye mashamba wote wa Shekemu wamekusanyika pamoja. 48 Kwa hiyo Abimeleki akapanda Mlima Salmoni,+ yeye na watu wote waliokuwa pamoja naye. Basi Abimeleki akachukua shoka mkononi mwake, akakata tawi la mti, akaliinua na kuliweka begani pake, akawaambia watu waliokuwa pamoja naye: “Mlivyoona nikifanya—fanyeni hivyo, haraka, kama mimi!”+ 49 Basi watu wote wakajikatia tawi kila mmoja wao, wakamfuata Abimeleki. Ndipo wakayaweka juu ya ngome ile, nao wakaitia moto ngome hiyo juu yao, hivi kwamba watu wote wa mnara wa Shekemu wakafa pia, karibu watu elfu moja, wanaume na wanawake.+
50 Na Abimeleki akaenda Thebesi,+ akapiga kambi juu ya Thebesi, akaliteka. 51 Na kwa vile kulikuwa na mnara wenye nguvu katikati ya jiji, wanaume wote na wanawake na wenye mashamba wote wa jiji walikimbilia humo, kisha wakaufunga nyuma yao na kupanda juu ya paa ya mnara huo. 52 Naye Abimeleki akaondoka akaenda kwenye mnara huo na kuanza kupigana nao, akaenda karibu na mlango wa mnara ili kuuteketeza kwa moto.+ 53 Ndipo mwanamke fulani akatupa jiwe la juu la kusagia juu ya kichwa cha Abimeleki, akalivunja fuvu la kichwa chake vipande-vipande.+ 54 Kwa hiyo, akamwita haraka mtumishi aliyechukua silaha zake na kumwambia: “Chomoa upanga wako, uniue,+ wasije wakasema juu yangu, ‘Mwanamke ndiye aliyemuua.’” Mara moja mtumishi wake akamchoma, naye akafa.+
55 Watu wa Israeli walipoona kwamba Abimeleki amekufa, basi wakaenda kila mmoja wao mahali pake. 56 Hivyo Mungu akaurudisha uovu wa Abimeleki aliomtendea baba yake kwa sababu ya kuwaua ndugu zake 70.+ 57 Na Mungu akaurudisha uovu wote wa watu wa Shekemu juu ya vichwa vyao wenyewe, ili ile laana+ ya Yothamu+ mwana wa Yerubaali+ ije juu yao.+
10 Na baada ya Abimeleki, akasimama Tola mwana wa Pua, mwana wa Dodo, mtu wa Isakari, ili kuwaokoa+ Israeli, naye alikuwa akikaa Shamiri katika eneo lenye milima la Efraimu.+ 2 Naye akaendelea kuhukumu Israeli kwa miaka 23, kisha akafa, akazikwa katika Shamiri.
3 Ndipo baada yake Yairi Mgileadi+ akasimama, naye akaendelea kuhukumu Israeli kwa miaka 22. 4 Naye akaja kuwa na wana 30 waliopanda punda 30 waliokomaa,+ nao walikuwa na majiji 30. Majiji hayo wanaendelea kuyaita Hawoth-yairi+ mpaka leo hii; yako katika nchi ya Gileadi. 5 Kisha Yairi akafa, akazikwa katika Kamoni.
6 Na wana wa Israeli wakaanza tena kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ nao wakaanza kutumikia Mabaali+ na sanamu za Ashtorethi+ na miungu ya Siria+ na miungu ya Sidoni+ na miungu ya Moabu+ na miungu ya wana wa Amoni+ na miungu ya Wafilisti.+ Basi wakamwacha Yehova wala hawakumtumikia yeye.+ 7 Hivyo hasira ya Yehova ikawaka juu ya Israeli,+ naye akawauza+ mkononi mwa Wafilisti+ na mkononi mwa wana wa Amoni.+ 8 Kwa hiyo wakawavunja-vunja na kuwakandamiza sana wana wa Israeli mwaka huo—kwa miaka kumi na minane wana wote wa Israeli waliokuwa ng’ambo ya Yordani katika nchi ya Waamori iliyokuwa katika Gileadi. 9 Na wana wa Amoni wakawa wakivuka Yordani ili kupigana na Yuda na Benyamini na nyumba ya Efraimu; na Israeli walikuwa katika taabu kubwa sana.+ 10 Na wana wa Israeli wakaanza kumwomba Yehova msaada,+ wakisema: “Tumekutendea dhambi,+ kwa sababu tumemwacha Mungu wetu nasi tunatumikia Mabaali.”+
11 Ndipo Yehova akawaambia wana wa Israeli: “Je, mimi sikuwaokoa ninyi kutoka Misri+ na kutoka mkononi mwa Waamori+ na wana wa Amoni+ na Wafilisti+ 12 na Wasidoni+ na Amaleki+ na Midiani,+ walipowakandamiza,+ nanyi mkanililia, nami nikawaokoa kutoka katika mkono wao? 13 Lakini ninyi, mliniacha,+ mkaanza kuitumikia miungu mingine.+ Ndiyo sababu sitawaokoa tena.+ 14 Nendeni mwombe msaada kutoka kwa miungu+ ambayo mmechagua.+ Hiyo na iwaokoe wakati wa taabu yenu.” 15 Lakini wana wa Israeli wakamwambia Yehova: “Tumetenda dhambi.+ Wewe mwenyewe ututendee kulingana na lolote lililo jema machoni pako.+ Lakini tafadhali, utukomboe tu leo hii.”+ 16 Nao wakaanza kuiondoa miungu ya kigeni kutoka katikati yao,+ na kumtumikia Yehova,+ hivi kwamba nafsi+ yake ikawa haina subira kwa sababu ya taabu ya Israeli.+
17 Baadaye wana wa Amoni+ wakakusanywa pamoja, wakapiga kambi katika Gileadi.+ Kwa hiyo wana wa Israeli wakajikusanya pamoja, wakapiga kambi katika Mispa.+ 18 Ndipo watu na wakuu wa Gileadi wakaanza kuambiana: “Ni nani atakayeongoza katika kupigana na wana wa Amoni?+ Huyo na awe kichwa juu ya wakaaji wote wa Gileadi.”+
11 Basi Yeftha+ Mgileadi+ akawa mwanamume mwenye nguvu na shujaa,+ naye alikuwa ni mwana wa mwanamke kahaba,+ naye Gileadi akamzaa Yeftha. 2 Na mke wa Gileadi akaendelea kumzalia wana. Wakati wana wa mke yule walipokuwa wakubwa, wakamfukuza Yeftha na kumwambia: “Usiwe na urithi wowote katika nyumba ya baba yetu,+ kwa sababu wewe ni mwana wa mwanamke mwingine.” 3 Basi Yeftha akakimbia kwa sababu ya ndugu zake, akaenda kukaa katika nchi ya Tobu.+ Kisha watu wanaozurura-zurura wakaendelea kujikusanya pamoja kwa Yeftha, nao wakawa wakienda nje pamoja naye.+
4 Na ikawa baada ya muda kwamba wana wa Amoni wakaanza kupigana na Israeli.+ 5 Ikawa kwamba wana wa Amoni walipopigana na Israeli,+ wanaume wazee wa Gileadi wakaenda mara moja kumchukua Yeftha kutoka katika nchi ya Tobu.+ 6 Nao wakamwambia Yeftha: “Njoo uwe kiongozi wetu, nasi tupigane na wana wa Amoni.” 7 Lakini Yeftha akawaambia wanaume wazee+ wa Gileadi: “Je, si ninyi mlionichukia, mkanifukuza kutoka nyumbani kwa baba yangu?+ Kwa nini basi mmenijia hivi sasa mkiwa katika taabu?”+ 8 Ndipo wanaume wazee wa Gileadi wakamwambia Yeftha: “Ndiyo sababu sasa tumerudi kwako,+ nawe uende pamoja nasi na kupigana na wana wa Amoni, nawe uwe kwetu kichwa juu ya wakaaji wote wa Gileadi.”+ 9 Basi Yeftha akawaambia wanaume wazee wa Gileadi: “Ikiwa mnanirudisha ili kupigana na wana wa Amoni, na Yehova akiwatia+ mkononi mwangu, mimi mwenyewe nitakuwa kichwa chenu!” 10 Ndipo wanaume wazee wa Gileadi wakamwambia Yeftha: “Yehova na awe msikilizaji kati yetu+ ikiwa hatutafanya kulingana na neno lako.”+ 11 Basi Yeftha akaenda pamoja na wanaume wazee wa Gileadi, na watu wakamweka juu yao awe kichwa na kiongozi.+ Na Yeftha akasema maneno yake yote mbele za Yehova+ katika Mispa.+
12 Ndipo Yeftha akatuma wajumbe kwa mfalme wa wana wa Amoni,+ akisema: “Nina nini na wewe,+ kwa kuwa umekuja juu yangu ili kupigana katika nchi yangu?” 13 Basi mfalme wa wana wa Amoni akawaambia wale wajumbe wa Yeftha: “Ni kwa sababu Israeli walichukua nchi yangu walipopanda kutoka Misri,+ kuanzia Arnoni+ mpaka Yaboki na mpaka Yordani.+ Basi sasa irudishe kwa amani.” 14 Lakini Yeftha akatuma wajumbe tena kwa mfalme wa wana wa Amoni 15 na kumwambia:
“Yeftha amesema hivi, ‘Israeli hawakuchukua nchi ya Moabu+ wala nchi ya wana wa Amoni.+ 16 Kwa maana Israeli walipopanda kutoka Misri, walitembea kupitia nyika mpaka Bahari Nyekundu,+ wakaja Kadeshi.+ 17 Ndipo Israeli wakatuma wajumbe kwa mfalme wa Edomu,+ wakisema: “Tafadhali, niache nipite katika nchi yako,” naye mfalme wa Edomu hakusikiliza. Pia wakatuma wajumbe kwa mfalme wa Moabu,+ naye hakukubali. Basi Israeli wakaendelea kukaa katika Kadeshi.+ 18 Walipotembea kupitia nyika, waliizunguka nchi ya Edomu+ na nchi ya Moabu, nao wakaenda upande wa mashariki wa nchi ya Moabu,+ wakakaa katika eneo la Arnoni; nao hawakuja katika mpaka wa Moabu,+ kwa sababu Arnoni ulikuwa ni mpaka wa Moabu.+
19 “‘Baada ya hayo Israeli wakatuma wajumbe kwa Sihoni mfalme wa Waamori, mfalme wa Heshboni,+ na Israeli wakamwambia: “Tafadhali, tuache tupite katika nchi yako kwenda mahali pangu mwenyewe.”+ 20 Naye Sihoni hakuwaamini Israeli kwamba wavukie katika eneo lake, na Sihoni akakusanya watu wake wote pamoja, akapiga kambi katika Yahazi,+ wakapigana na Israeli.+ 21 Kwa hiyo Yehova Mungu wa Israeli akamtia Sihoni na watu wake wote mkononi mwa Israeli, nao wakawapiga na Israeli wakaimiliki nchi yote ya Waamori waliokuwa wakikaa katika nchi hiyo.+ 22 Kwa hiyo wakarithi eneo lote la Waamori kutoka Arnoni mpaka Yaboki na kutoka ile nyika mpaka Yordani.+
23 “‘Na sasa Yehova Mungu wa Israeli ndiye aliyewafukuza Waamori kutoka mbele ya watu wake Israeli,+ nawe kwa upande wako, unataka kuwafukuza. 24 Je, hutamfukuza yule ambaye Kemoshi+ mungu wako anakufanya umfukuze? Na kila mmoja ambaye Yehova Mungu wetu amemfukuza mbele yetu ndiye tutakayemfukuza.+ 25 Na sasa je, wewe ni bora kuliko Balaki mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu?+ Je, alipata kushindana na Israeli, au je, alipata kupigana nao? 26 Wakati Israeli walipokuwa wakikaa katika Heshboni na miji yake ya kandokando+ na katika Aroeri+ na miji yake ya kandokando na katika majiji yote yaliyo kando ya kingo za Arnoni kwa miaka mia tatu, kwa nini, basi, hamkuinyakua wakati huo?+ 27 Kwa upande wangu, mimi sikukutendea dhambi, lakini wewe unanitendea vibaya kwa kupigana nami. Yehova aliye Mwamuzi+ na ahukumu leo kati ya wana wa Israeli na wana wa Amoni.’”
28 Na mfalme wa wana wa Amoni hakuyasikiliza maneno ya Yeftha ambayo alikuwa amemtumia.+
29 Sasa roho ya Yehova ikaja juu ya Yeftha,+ naye akapita katika Gileadi na Manase, akapita katika Mispe la Gileadi,+ na kutoka Mispe la Gileadi akapita kwenda kwa wana wa Amoni.
30 Ndipo Yeftha akaweka nadhiri+ kwa Yehova na kusema: “Hakika ukiwatia wana wa Amoni mkononi mwangu, 31 itatukia pia kwamba yule atakayetoka nje, atakayetoka nje ya milango ya nyumba yangu kuja kunipokea nitakaporudi kwa amani+ kutoka kwa wana wa Amoni, lazima atakuwa wa Yehova,+ nami nitamtoa huyo kuwa toleo la kuteketezwa.”+
32 Basi Yeftha akapita kwenda kwa wana wa Amoni ili kupigana nao, na Yehova akawatia mkononi mwake. 33 Akawapiga kwa mauaji makubwa sana kutoka Aroeri mpaka Minithi,+ majiji 20, na mpaka Abel-keramimu. Basi wana wa Amoni wakatiishwa mbele ya wana wa Israeli.
34 Mwishowe Yeftha akaja Mispa+ nyumbani kwake, na, tazama! binti yake akatoka nje kumpokea, akipiga tari na kucheza dansi!+ Naye alikuwa ndiye mtoto pekee. Hakuwa na mwana wala binti isipokuwa yeye. 35 Na ikawa kwamba alipomwona, akaanza kuyararua mavazi+ yake na kusema: “Ole, binti yangu! Kwa kweli umenifanya niiname chini, nawe mwenyewe umekuwa ndiye yule ambaye nilikuwa nikitenga. Mimi nimemfungulia Yehova kinywa changu, nami siwezi kurudi nyuma.”+
36 Lakini akamwambia: “Baba yangu, ikiwa umemfungulia Yehova kinywa chako, nitendee kulingana na neno lililotoka katika kinywa chako,+ kwa kuwa Yehova amekulipizia kisasi juu ya adui zako, wana wa Amoni.” 37 Naye akaendelea kumwambia baba yake: “Na nifanyiwe jambo hili: Niache kwa miezi miwili, niende, nami nitashuka milimani, na acha niulilie ubikira wangu,+ mimi pamoja na wasichana wenzangu.”
38 Ndipo akasema: “Nenda!” Basi akamwacha aende kwa miezi miwili; naye akaenda, yeye pamoja na wasichana wenzake, akiulilia ubikira wake juu ya milima. 39 Na ikawa kwamba mwishoni mwa miezi miwili, akarudi kwa baba yake, kisha baba yake akatimiza ile nadhiri yake ambayo alikuwa ameweka kumwelekea.+ Naye hakupata kamwe kulala na mwanamume. Nayo ikawa sharti katika Israeli: 40 Mwaka baada ya mwaka binti za Israeli wakawa wakienda kumpongeza binti ya Yeftha Mgileadi, siku nne kwa mwaka.+
12 Ndipo watu wa Efraimu wakakusanywa pamoja na kuvuka kuelekea kaskazini, nao wakamwambia Yeftha: “Kwa nini ulivuka kupigana na wana wa Amoni, nawe hukutuita twende pamoja nawe?+ Nyumba yako tutaiteketeza juu yako kwa moto.”+ 2 Lakini Yeftha akawaambia: “Mimi na watu wangu tulikuwa na ugomvi mkubwa pamoja na wana wa Amoni.+ Nami nikawaomba ninyi msaada, wala hamkuniokoa kutoka mkononi mwao. 3 Nilipoona kwamba hamniokoi, nikaazimia kuitia nafsi yangu mkononi+ mwangu mwenyewe, nikavuka kupigana na wana wa Amoni.+ Hivyo Yehova akawatia mkononi mwangu. Basi kwa nini mmekuja juu yangu kupigana nami leo?”
4 Basi bila kukawia Yeftha akakusanya watu wote wa Gileadi,+ akapigana na Efraimu; na watu wa Gileadi wakapiga Efraimu, kwa maana walikuwa wamesema: “Ninyi Gileadi ni watu walioponyoka kutoka Efraimu, kutoka ndani ya Efraimu, kutoka ndani ya Manase.” 5 Nao Gileadi wakateka vivuko vya Yordani+ mbele ya Efraimu; ndipo ikatukia kwamba wakati watu wa Efraimu waliokuwa wakikimbia waliposema: “Niache nivuke,” ndipo watu wa Gileadi wakawa wakimwambia kila mmoja wao: “Je, wewe ni Mwefraimu?” Akisema: “Hapana!” 6 ndipo walipomwambia: “Tafadhali sema Shibolethi.”+ Naye alisema: “Sibolethi,” kwa kuwa hakuweza kutamka neno hilo kwa usahihi. Nao walimshika na kumuua kwenye vivuko vya Yordani. Basi wakati huo wakaanguka watu 42,000 kutoka katika Efraimu.+
7 Na Yeftha akaendelea kuhukumu Israeli kwa miaka sita, kisha Yeftha Mgileadi akafa, akazikwa katika jiji lake kule Gileadi.
8 Naye Ibzani kutoka Bethlehemu+ akaanza kuhukumu Israeli baada yake.+ 9 Naye akawa na wana 30 na binti 30. Akatuma watu nje kuleta binti 30 kwa ajili ya wanawe kutoka nje. Naye akaendelea kuhukumu Israeli kwa miaka saba. 10 Kisha Ibzani akafa, akazikwa Bethlehemu.
11 Na baada yake Eloni Mzabuloni+ akaanza kuhukumu Israeli. Naye akaendelea kuhukumu Israeli kwa miaka kumi. 12 Kisha Eloni Mzabuloni akafa, akazikwa Aiyaloni katika nchi ya Zabuloni.
13 Na baada yake Abdoni mwana wa Hileli Mpirathoni+ akaanza kuhukumu Israeli. 14 Naye akaja kuwa na wana 40 na wajukuu 30 waliopanda punda wakomavu+ 70. Naye akaendelea kuhukumu Israeli kwa miaka minane. 15 Kisha Abdoni mwana wa Hileli Mpirathoni akafa, akazikwa Pirathoni katika nchi ya Efraimu katika mlima wa Mwamaleki.+
13 Wana wa Israeli wakaanza tena kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ na hivyo Yehova akawatia mkononi mwa Wafilisti+ kwa miaka 40.
2 Wakati huo palikuwa na mtu mmoja wa Sora+ wa familia ya Wadani,+ na jina lake lilikuwa Manoa.+ Na mke wake alikuwa tasa naye hakuwa amezaa mtoto yeyote.+ 3 Ndipo malaika wa Yehova akamtokea huyo mwanamke,+ akamwambia: “Tazama, sasa, wewe ni tasa nawe hujazaa mtoto yeyote. Nawe hakika utachukua mimba na kuzaa mwana.+ 4 Basi sasa jiangalie, tafadhali, usinywe divai wala kileo,+ wala usile kitu chochote kisicho safi.+ 5 Kwa maana, tazama! utachukua mimba, nawe utazaa mwana, na wembe wowote usipite juu ya kichwa chake,+ kwa maana mtoto huyo atakuwa Mnadhiri+ wa Mungu tangu atakapotoka tumboni;+ naye ndiye atakayeongoza katika kuokoa Israeli kutoka mkononi mwa Wafilisti.”+
6 Ndipo mwanamke huyo akaenda, akamwambia mume wake: “Kuna mtu fulani wa Mungu wa kweli ambaye alinijia, na sura yake ilikuwa kama sura ya malaika wa Mungu wa kweli,+ yenye kuogopesha sana.+ Nami sikumuuliza mahali alikotoka, wala hakuniambia jina lake.+ 7 Lakini aliniambia, ‘Tazama! Utachukua mimba, nawe hakika utazaa mwana.+ Basi sasa usinywe divai wala kileo, wala usile kitu chochote kisicho safi, kwa maana mtoto huyo atakuwa Mnadhiri wa Mungu tangu atakapotoka tumboni mpaka siku ya kufa kwake.’”+
8 Na Manoa akaanza kumsihi Yehova, akisema: “Nakuomba radhi, Yehova.+ Tafadhali, yule mtu wa Mungu wa kweli ambaye ulimtuma na arudi kwetu tena, atufundishe+ yale tunayopaswa kumtendea huyo mtoto atakayezaliwa.”+ 9 Basi Mungu wa kweli akaisikiliza sauti ya Manoa,+ na yule malaika wa Mungu wa kweli akamjia tena yule mwanamke alipokuwa ameketi shambani, lakini Manoa mume wake hakuwa pamoja naye. 10 Bila kukawia huyo mwanamke akafanya haraka na kukimbia, akamwambia mume+ wake na kusema: “Tazama! Yule mtu aliyenijia siku ile amenitokea.”+
11 Kwa hiyo Manoa akasimama, akafuatana na mke wake, akamjia yule mtu na kumwambia: “Je, wewe ndiye yule mtu aliyesema na huyu mwanamke?”+ naye akajibu: “Ni mimi.” 12 Ndipo Manoa akasema: “Basi maneno yako na yatimie. Mtoto huyo ataishi maisha ya aina gani, naye atafanya kazi gani?”+ 13 Basi malaika wa Yehova akamwambia Manoa: “Kila jambo ambalo nilimtajia huyu mwanamke ajiepushe nalo.+ 14 Asile kitu chochote kinachotokana na mzabibu wa divai, wala asinywe divai yoyote wala kileo,+ wala asile kitu chochote kisicho safi.+ Naye ashike kila jambo ambalo nimemwamuru.”+
15 Sasa Manoa akamwambia malaika wa Yehova: “Tafadhali, acha tukuzuilie, tukuandalie mwana-mbuzi.”+ 16 Lakini malaika wa Yehova akamwambia Manoa: “Ukinizuilia, sitakula mkate wako; bali ukitaka kutoa toleo la kuteketezwa kwa Yehova,+ unaweza kulitoa.” Kwa maana Manoa hakujua kwamba huyo alikuwa ni malaika wa Yehova. 17 Kisha Manoa akamwambia malaika wa Yehova: “Jina lako ni nani,+ ili neno lako litakapotimia, tukupe heshima?” 18 Hata hivyo, malaika wa Yehova akamwambia: “Kwa nini unauliza juu ya jina langu, wakati jina hilo ni la ajabu?”
19 Basi Manoa akachukua mwana-mbuzi na toleo la nafaka, akamtolea Yehova juu ya mwamba.+ Naye huyo alikuwa akifanya jambo fulani kwa njia ya ajabu huku Manoa na mke wake wakitazama. 20 Basi ikawa kwamba, mwali wa moto ulipokuwa ukipaa kutoka katika madhabahu kuelekea mbinguni, malaika wa Yehova akapaa katika ule mwali wa madhabahu huku Manoa na mke wake wakitazama.+ Wakaanguka kifudifudi mara moja.+ 21 Na malaika wa Yehova hakumtokea tena Manoa na mke wake. Ndipo Manoa akajua kwamba huyo alikuwa ni malaika wa Yehova.+ 22 Basi Manoa akamwambia mke wake: “Hakika tutakufa,+ kwa sababu yule ambaye tumemwona ni Mungu.”+ 23 Lakini mke wake akamwambia: “Ikiwa Yehova alitaka tu kutuua, basi hangekubali toleo la kuteketezwa na toleo la nafaka kutoka mkononi mwetu,+ naye hangetuonyesha mambo haya yote, naye kufikia sasa hangetuacha tusikie jambo lolote kama hili.”+
24 Baadaye huyo mwanamke akazaa mwana, akamwita jina Samsoni;+ na mvulana huyo akazidi kukua, na Yehova akaendelea kumbariki.+ 25 Baada ya muda roho ya Yehova+ ikaanza kumchochea katika Mahane-dani+ kati ya Sora+ na Eshtaoli.+
14 Ndipo Samsoni akashuka mpaka Timna,+ akamwona mwanamke mmoja huko Timna kati ya binti za Wafilisti. 2 Basi akapanda, akamwambia baba yake na mama yake, akisema: “Nimemwona mwanamke mmoja huko Timna kati ya binti za Wafilisti, basi sasa mniletee mwanamke huyo awe mke wangu.”+ 3 Lakini baba yake na mama yake wakamwambia: “Je, hakuna mwanamke yeyote kati ya binti za ndugu zako na kati ya watu wangu wote,+ hivi kwamba uende kumchukua mwanamke kutoka kwa Wafilisti wasiotahiriwa?”+ Lakini bado Samsoni akamwambia baba yake: “Nileteeni huyo, kwa maana ndiye anayestahili kabisa machoni pangu.” 4 Lakini baba yake na mama yake hawakujua kwamba jambo hilo lilitoka kwa Yehova,+ kwamba alikuwa akitafuta nafasi ya kuwapiga Wafilisti, kwa kuwa wakati huo hasa Wafilisti walikuwa wakitawala juu ya Israeli.+
5 Basi Samsoni akashuka pamoja na baba yake na mama yake, wakaenda Timna.+ Alipofika katika mashamba ya mizabibu ya Timna, tazama! mwana-simba mwenye manyoya shingoni akamngurumia alipokutana naye. 6 Ndipo roho ya Yehova ikaanza kutenda kazi juu yake,+ naye akampasua vipande viwili, kama vile mtu anavyompasua mwana-mbuzi vipande viwili, wala hapakuwa na kitu chochote mkononi mwake. Naye hakumwambia baba yake wala mama yake jambo alilokuwa amefanya. 7 Naye akaendelea kushuka, akaanza kusema na yule mwanamke; na huyo mwanamke alikuwa bado ni mwenye kustahili machoni pa Samsoni.+
8 Basi baada ya muda akarudi kumchukua mwanamke yule nyumbani kwake.+ Naye akageuka kando kuuangalia ule mzoga wa simba, na tazama, kulikuwa na bumba la nyuki ndani ya huo mzoga wa simba, na asali.+ 9 Basi akaiparura na kuitia mkononi mwake, akaendelea kutembea, huku akila alipokuwa akitembea.+ Alipojiunga tena na baba yake na mama yake, ndipo mara moja akawapa sehemu ya asali hiyo, nao wakaanza kula. Naye hakuwaambia kwamba aliitoa asali hiyo katika ule mzoga wa simba.
10 Na baba yake akaendelea kushuka mpaka kwa yule mwanamke, naye Samsoni akafanya karamu huko;+ kwa maana hivyo ndivyo vijana walivyokuwa na desturi ya kufanya. 11 Na ikawa kwamba, walipomwona, bila kukawia wakachukua rafiki 30 za bwana-arusi, ili wakae naye. 12 Ndipo Samsoni akawaambia: “Tafadhali, acheni niwategee kitendawili.+ Mkiniambia kwa hakika kitendawili hicho kwa muda wa siku saba+ za karamu hii, nanyi mkitegue, ndipo nitakapowapa mavazi 30 ya ndani na nguo 30.+ 13 Lakini mkishindwa kuniambia kitendawili hicho, ninyi mtanipa mavazi 30 ya ndani na nguo 30.” Kwa hiyo wakamwambia: “Tega kitendawili chako, tukisikie.” 14 Hivyo akawaambia:
“Katika mwenye kula+ kilitoka kitu fulani cha kula,
Na katika mwenye nguvu kilitoka kitu fulani kitamu.”+
Nao hawakuweza kukitegua kitendawili hicho kwa muda wa siku tatu. 15 Na ikawa kwamba, katika siku ya nne wakaanza kumwambia mke wa Samsoni: “Mdanganye mume wako ili atutegulie kitendawili hicho.+ Kama sivyo tutakuteketeza kwa moto+ wewe na nyumba ya baba yako. Je, mlitualika hapa ili mchukue mali zetu?”+ 16 Basi mke wa Samsoni akaanza kumlilia+ na kusema: “Wewe unanichukia tu, unanichukia, wala hunipendi.+ Kuna kitendawili ambacho uliwategea wana wa watu wangu,+ lakini mimi hukuniambia.” Ndipo akamwambia: “Angalia, hata sikumwambia baba yangu wala mama yangu,+ nami je, nikuambie wewe?” 17 Lakini akaendelea kumlilia zile siku saba ambazo waliendelea na karamu, basi mwishowe ikawa kwenye siku ya saba akamwambia, kwa sababu mwanamke huyo alikuwa amemkaza.+ Kwa hiyo mwanamke huyo akawaambia wana wa watu wake kitendawili hicho.+ 18 Basi watu wa jiji wakamwambia siku ya saba kabla hajaenda katika chumba cha ndani:+
“Ni nini kilicho kitamu kuliko asali,
Na ni nini kilicho na nguvu kuliko simba?”+
Ndipo naye akawaambia:
“Kama hamngelima na ng’ombe wangu mchanga,+
Hamngekitegua kitendawili changu.”+
19 Halafu roho ya Yehova ikaanza kutenda kazi juu yake,+ kisha akashuka Ashkeloni,+ akawapiga watu 30 kati yao, akachukua mavazi aliyowavua, akawapa mavazi hayo wale wasemaji wa kile kitendawili.+ Na hasira yake ikaendelea kuwaka, akapanda kwenda zake kwa nyumba ya baba yake.
20 Na mke wa Samsoni+ akaja kuwa mke wa mmoja wa rafiki+ zake aliyekuwa ameshirikiana naye.
15 Na ikawa kwamba baada ya muda, katika siku za mavuno ya ngano, Samsoni akaenda kumtembelea mke wake akiwa na mwana-mbuzi.+ Basi akasema: “Nitaingia kwa mke wangu katika chumba cha ndani.”+ Na baba ya mwanamke huyo hakumruhusu kuingia. 2 Lakini baba yake akasema: “Kwa kweli nilisema moyoni mwangu, ‘Bila shaka unamchukia.’+ Kwa hiyo nikampa rafiki yako mwanamke huyo.+ Je, dada yake mdogo si bora kuliko yeye? Tafadhali, yeye na awe wako badala ya yule mwingine.” 3 Hata hivyo, Samsoni akawaambia: “Wakati huu sitakuwa na hatia yoyote juu ya Wafilisti nikiwadhuru.”+
4 Na Samsoni akaondoka, akaenda zake, akawakamata mbweha+ mia tatu, akachukua mienge na kuwageuza mkia kwa mkia na kuweka mwenge mmoja kati ya mikia miwili, katikati kabisa. 5 Ndipo akaiwasha moto ile mienge na kuwapeleka mbweha hao katika mashamba ya Wafilisti ya nafaka inayosimama. Basi akawasha moto kila kitu kuanzia mganda mpaka nafaka inayosimama na mashamba ya mizabibu na mashamba ya mizeituni.+
6 Na Wafilisti wakaanza kusema: “Ni nani aliyefanya jambo hili?” Ndipo wakasema: “Ni Samsoni mwana-mkwe wa yule Mtimna, kwa sababu alimchukua mke wake, akampa rafiki yake.”+ Kwa hiyo Wafilisti wakaenda na kumteketeza kwa moto mwanamke huyo na baba yake.+ 7 Kisha Samsoni akawaambia: “Mkifanya hivi, sina jambo lingine isipokuwa kujilipiza kisasi juu yenu,+ kisha nitaachia hapo.” 8 Naye akawapiga, akirundika miguu juu ya mapaja kwa mauaji makubwa, kisha akashuka, akaanza kukaa katika mpasuko wa mwamba Etamu.+
9 Baadaye Wafilisti+ wakapanda na kupiga kambi katika Yuda,+ wakaanza kutembea huku na huku katika Lehi.+ 10 Ndipo watu wa Yuda wakasema: “Kwa nini mmekuja juu yetu?” nao wakasema: “Tumekuja kumfunga Samsoni, tumtendee kama vile alivyotutendea.” 11 Basi watu elfu tatu wa Yuda wakashuka kwenye mpasuko wa mwamba Etamu,+ wakamwambia Samsoni: “Je, hujui kwamba Wafilisti wanatutawala?+ Basi jambo hili ambalo umetutendea linamaanisha nini?” Ndipo akawaambia: “Nimewatendea wao kama walivyonitendea mimi.”+ 12 Lakini wakamwambia: “Tumeshuka kuja kukufunga, tukutie mkononi mwa Wafilisti.” Kwa hiyo Samsoni akawaambia: “Niapieni kwamba ninyi wenyewe hamtanishambulia.” 13 Nao wakamwambia: “Hapana, tutakufunga tu, na kukutia mkononi mwao; lakini hakika hatutakuua.”
Basi wakamfunga kwa kamba mbili mpya,+ wakamtoa nje ya ule mwamba. 14 Naye akaja mpaka Lehi, nao Wafilisti wakapaaza sauti kwa shangwe walipokutana naye.+ Na roho ya Yehova+ ikaanza kutenda kazi juu yake, na zile kamba zilizokuwa kwenye mikono yake zikawa kama nyuzi za kitani ambazo zimeunguzwa kwa moto,+ nazo pingu zake zikayeyuka kutoka kwenye mikono yake. 15 Akaona mfupa mbichi wa taya ya punda-dume, akanyoosha mkono wake akauchukua, akapiga nao watu elfu moja.+ 16 Ndipo Samsoni akasema:
“Kwa mfupa wa taya ya punda-dume—fungu moja, mafungu mawili!
Kwa mfupa wa taya ya punda-dume nimepiga watu elfu moja.”+
17 Na ikawa kwamba, alipomaliza kusema, bila kukawia akautupa ule mfupa kutoka mkononi mwake, akaita mahali hapo Ramath-lehi.+ 18 Kisha akawa na kiu sana, na kuanza kumwita Yehova, akisema: “Wewe ndiye uliyetia wokovu huu mkubwa mkononi mwa mtumishi wako,+ na je, sasa nife kutokana na kiu, na je, nianguke mkononi mwa wasiotahiriwa?”+ 19 Kwa hiyo Mungu akapasua shimo lenye umbo la kinu lililokuwa katika Lehi, na maji+ yakaanza kutoka ndani yake, naye akanywa, kisha roho+ yake ikarudi na nguvu zikamrudia.+ Ndiyo sababu aliliita kwa jina la En-hakore, nalo lipo katika Lehi mpaka leo hii.
20 Naye akaendelea kuhukumu Israeli katika siku za Wafilisti kwa miaka 20.+
16 Wakati mmoja Samsoni alienda Gaza,+ akaona mwanamke kahaba huko, akaingia kwake.+ 2 Na Wagaza wakapewa habari, kusema: “Samsoni ameingia hapa.” Basi wakamzunguka+ na kumvizia usiku kucha katika lango la jiji.+ Nao wakakaa kimya usiku wote, wakisema: “Mara kutakapopambazuka asubuhi, tutamuua.”+
3 Hata hivyo, Samsoni akaendelea kulala mpaka katikati ya usiku, kisha akaamka katikati ya usiku, akakamata milango ya lango+ la jiji na miimo yake miwili, akaing’oa pamoja na pingo, akaiweka juu ya mabega yake, akaichukua+ mpaka kwenye kilele cha mlima ulio mbele ya Hebroni.+
4 Na ikawa kwamba baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika bonde la mto la Soreki, na jina lake lilikuwa Delila.+ 5 Ndipo wakuu wa muungano wa Wafilisti+ wakamfikia mwanamke huyo na kumwambia: “Mdanganye+ ili uone nguvu zake nyingi zinatokana na nini, na kile tunachoweza kutumia ili kumshinda, na kile tunachoweza kutumia kumfunga ili kumtawala; nasi tutakupa kila mmoja wetu vipande elfu moja na mia moja vya fedha.”+
6 Baadaye Delila akamwambia Samsoni: “Tafadhali niambie, Hizi nguvu zako nyingi zinatokana na nini, nawe unaweza kufungwa kwa kitu gani ili mtu akutawale?”+ 7 Ndipo Samsoni akamwambia: “Wakinifunga kwa kamba mbichi saba za kano,+ ambazo hazijakaushwa, ndipo nitakuwa dhaifu na kuwa kama mwanadamu wa kawaida.” 8 Basi wakuu wa muungano wa Wafilisti+ wakamletea mwanamke huyo kamba mbichi saba ambazo hazijakaushwa. Baadaye akamfunga kwa kamba hizo. 9 Na watu wenye kuvizia walikuwa wameketi katika chumba cha ndani cha mwanamke huyo,+ naye akaanza kumwambia: “Wafilisti+ wako juu yako, Samsoni!” Ndipo akazikata kamba hizo vipande viwili, kama vile nyuzi za kitani zilizosokotwa zinavyokatika vipande viwili zinaponusa harufu ya moto.+ Na nguvu zake hazikujulikana.+
10 Basi Delila+ akamwambia Samsoni: “Tazama! Umenichezea, ukaniambia uwongo.+ Sasa niambie tafadhali, unaweza kufungwa na kitu gani.” 11 Kwa hiyo akamwambia: “Wakinifunga kwa kamba mpya ambazo hazijafanyiwa kazi yoyote, nitakuwa dhaifu na kuwa kama mwanadamu wa kawaida.” 12 Basi Delila akachukua kamba mpya akamfunga nazo, akamwambia: “Wafilisti wako juu yako, Samsoni!” Wakati huo wote wale watu wenye kuvizia walikuwa wameketi katika chumba cha ndani.+ Ndipo akazikata vipande viwili kutoka mikononi mwake kama uzi.+
13 Kisha Delila akamwambia Samsoni: “Mpaka sasa umenichezea, ukaniambia uwongo.+ Niambie unaweza kufungwa na kitu gani.”+ Ndipo akamwambia: “Ukifuma hii misuko saba ya nywele za kichwa changu kwa uzi wa mtande.”+ 14 Basi akazikaza kwa msumari, kisha akamwambia: “Wafilisti wako juu yako, Samsoni!”+ Ndipo akaamka kutoka katika usingizi wake, akaung’oa ule msumari wa wafumaji na ule uzi wa mtande.
15 Mwanamke akamwambia: “Unawezaje kuthubutu kusema, ‘Nakupenda,’+ ingawa moyo wako haupo pamoja nami? Umenichezea mara tatu hizi nawe hujaniambia nguvu zako zinatokana na nini.”+ 16 Na ikawa kwamba kwa sababu mwanamke huyo alimkaza+ kwa maneno yake wakati wote na kuendelea kumsihi, nafsi yake ikakosa subira kufikia hatua ya kutaka kufa.+ 17 Mwishowe akamfunulia moyo wake+ wote na kumwambia: “Wembe+ haujapita kamwe juu ya kichwa changu, kwa kuwa mimi ni Mnadhiri wa Mungu tangu tumboni mwa mama yangu.+ Nikinyolewa, hakika nguvu zangu zitanitoka, nami hakika nitakuwa dhaifu na kuwa kama wanadamu wengine wote.”+
18 Delila alipoona kwamba amemfunulia moyo wake wote, akapeleka neno haraka na kuwaita wakuu wa muungano wa Wafilisti,+ akisema: “Njooni safari hii, kwa maana amenifunulia moyo wake wote.”+ Na wakuu wa muungano wa Wafilisti wakamfikia huyo mwanamke ili walete zile pesa mkononi mwao.+ 19 Na ndipo huyo mwanamke akamlaza magotini pake. Akamwita mtu akamnyoa ile misuko saba ya nywele za kichwa chake, kisha mwanamke huyo akaanza kumtawala, na nguvu zake zikaendelea kumtoka. 20 Basi akasema: “Wafilisti wako juu yako, Samsoni!” Naye akaamka kutoka katika usingizi na kusema: “Nitatoka nje kama safari zile nyingine+ na kujitikisa niwe huru.” Naye hakujua kwamba Yehova alikuwa amemwacha.+ 21 Basi Wafilisti wakamkamata, wakayang’oa macho+ yake na kumshusha mpaka Gaza,+ wakamfunga kwa pingu mbili za shaba;+ naye akawa mtu mwenye kusaga+ katika nyumba ya gereza.+ 22 Wakati huo nywele za kichwa chake zikaanza kukua sana mara baada ya kunyolewa.+
23 Lakini wale wakuu wa muungano wa Wafilisti wakakusanyika pamoja ili kutoa dhabihu kubwa kwa Dagoni+ mungu wao na ili washangilie, nao wakawa wakisema: “Mungu wetu amemtia mkononi mwetu Samsoni adui yetu!”+ 24 Na watu walipomwona, mara moja wakaanza kumsifu mungu wao,+ “kwa sababu,” wakasema, “mungu wetu amemtia katika mkono wetu adui yetu+ na mwenye kuharibu nchi yetu+ na mtu aliyezidisha hesabu ya watu wetu waliouawa.”+
25 Na ikawa kwamba kwa kuwa moyo wao ulikuwa na furaha,+ wakaanza kusema: “Mwite Samsoni apate kututumbuiza.”+ Basi wakamwita Samsoni kutoka katika ile nyumba ya gereza apate kucheza mbele yao;+ nao wakamsimamisha katikati ya nguzo. 26 Ndipo Samsoni akamwambia yule mvulana aliyekuwa amemshika mkono: “Niruhusu niguse nguzo ambazo nyumba imesimamishwa imara juu yake, nami niziegemee.” 27 (Basi nyumba hiyo ilikuwa imejaa wanaume na wanawake na wakuu wote wa muungano wa Wafilisti walikuwa humo;+ na juu ya dari walikuwapo karibu watu elfu tatu, wanaume na wanawake, waliokuwa wakitazama huku Samsoni akitumbuiza.)+
28 Sasa Samsoni+ akamwita Yehova+ na kusema: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, tafadhali nikumbuke,+ tafadhali unitie nguvu,+ mara hii moja tu, Ee Mungu wa kweli, ili nijilipize kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya jicho langu moja kati ya macho yangu mawili.”+
29 Ndipo Samsoni akajiinamisha kwa zile nguzo mbili za katikati ambazo juu yake nyumba ilikuwa imesimamishwa imara, naye akazishika, moja kwa mkono wake wa kuume na ile nyingine kwa mkono wake wa kushoto. 30 Kisha Samsoni akasema: “Nafsi yangu na ife+ pamoja na Wafilisti.” Ndipo akajiinamisha kwa nguvu, na nyumba ile ikawaangukia wale wakuu wa muungano na watu wote waliokuwamo ndani,+ hivi kwamba wafu alioua wakati wa kifo chake wakawa wengi kuliko wale alioua wakati wa maisha yake.+
31 Baadaye ndugu zake na nyumba yote ya baba yake wakashuka, wakamwinua, wakamleta na kumzika kati ya Sora+ na Eshtaoli+ katika kaburi la Manoa+ baba yake. Naye alikuwa amehukumu Israeli kwa miaka 20.+
17 Basi palikuwa na mwanamume kutoka katika eneo lenye milima la Efraimu+ ambaye jina lake lilikuwa Mika. 2 Baada ya muda akamwambia mama yake: “Vile vipande elfu moja na mia moja vya fedha vilivyochukuliwa kutoka kwako na ambavyo ulitoa laana+ juu yake na pia ukasema masikioni mwangu—tazama! mimi nina fedha hizo. Mimi ndiye niliyezichukua.”+ Ndipo mama yake akasema: “Mwanangu na awe mbarikiwa wa Yehova.”+ 3 Basi akamrudishia mama yake+ vile vipande elfu moja na mia moja vya fedha; naye mama yake akaendelea kusema: “Bila shaka nitazitakasa fedha hizi kwa Yehova kutoka mkononi mwangu kwa ajili ya mwanangu, ili kutengeneza sanamu ya kuchongwa+ na sanamu ya kuyeyushwa;+ na sasa nitairudisha kwako.”
4 Basi akamrudishia mama yake fedha hizo, kisha mama yake akachukua vipande mia mbili vya fedha akampa fundi wa fedha.+ Naye akatengeneza sanamu ya kuchongwa+ na sanamu ya kuyeyushwa;+ nayo ikawa katika nyumba ya Mika. 5 Na mtu huyo Mika, alikuwa na nyumba ya miungu,+ naye akafanya efodi+ na terafimu,+ akaujaza nguvu mkono+ wa mmoja wa wanawe, ili awe kuhani+ wake. 6 Siku hizo hapakuwa na mfalme katika Israeli.+ Kila mtu alikuwa akifanya yaliyo sawa machoni pake mwenyewe kulingana na alivyozoea kufanya.+
7 Basi palikuwa na kijana wa Bethlehemu+ katika Yuda wa familia ya Yuda, naye alikuwa Mlawi.+ Alikuwa anakaa hapo kwa muda. 8 Na mtu huyo akaondoka jiji la Bethlehemu katika Yuda ili akae kwa muda mahali popote ambapo angepata makao. Baadaye alipokuwa akienda zake akaja katika eneo lenye milima la Efraimu mpaka kwenye nyumba ya Mika.+ 9 Ndipo Mika akamwambia: “Unatoka wapi?” Naye akamjibu: “Mimi ni Mlawi kutoka Bethlehemu katika Yuda, nami niko njiani ili nikakae kwa muda mahali popote nitakapopata makao.” 10 Basi Mika akamwambia: “Kaa pamoja na mimi, uwe kama baba+ na kuhani+ kwangu, nami nitakupa vipande kumi vya fedha kwa mwaka na mavazi ya kawaida na chakula chako.” Ndipo Mlawi huyo akaingia ndani. 11 Basi Mlawi huyo akajiamulia mwenyewe kukaa pamoja na mtu yule, na huyo kijana akawa kama mmoja wa wanawe. 12 Na zaidi, Mika akaujaza nguvu mkono+ wa huyo Mlawi, ili huyo kijana awe kuhani+ kwake na apate kuendelea kuishi katika nyumba ya Mika. 13 Basi Mika akasema: “Sasa najua kwamba Yehova atanitendea mema, kwa maana Mlawi amekuwa kuhani kwangu.”+
18 Siku hizo hapakuwa na mfalme katika Israeli.+ Na katika siku hizo kabila la Wadani+ walikuwa wakijitafutia urithi ili wakae humo; kwa sababu kufikia wakati huo, urithi haukuwa umewaangukia katikati ya makabila ya Israeli.+
2 Mwishowe wana wa Dani wakatuma watu watano wa familia yao, wanaume kutoka kati yao, wanaume waliokuwa watu mashujaa, kutoka katika Sora+ na Eshtaoli,+ wapate kuipeleleza+ nchi na kuichunguza. Basi wakawaambia: “Nendeni, chunguzeni nchi.” Baadaye wakaja katika eneo lenye milima la Efraimu+ mpaka kwenye nyumba ya Mika,+ wakalala hapo usiku kucha. 3 Walipokuwa karibu na nyumba ya Mika, wakatambua sauti ya yule kijana, Mlawi, kisha wakageuka kando kuingia humo. Nao wakamwambia: “Ni nani aliyekuleta hapa, nawe unafanya nini hapa, nawe una shughuli gani hapa?” 4 Naye akawaambia: “Mika alinitendea hivi na hivi ili anikodishe,+ na ili niwe kuhani+ kwake.” 5 Ndipo wakamwambia: “Tafadhali, uliza+ kutoka kwa Mungu+ ili tupate kujua kama njia yetu tunayoiendea itafanikiwa.” 6 Basi kuhani huyo akawaambia: “Nendeni kwa amani. Njia yenu mnayoiendea iko mbele za Yehova.”
7 Basi hao watu watano wakaendelea, wakaja Laishi,+ wakaona jinsi ambavyo watu waliokuwa humo walikaa kwa kujitegemea kulingana na desturi ya Wasidoni, watulivu na wasio na shaka,+ wala hapakuwa na mshindi mwenye kukandamiza aliyekuwa akileta usumbufu wowote katika nchi, nao walikuwa mbali sana na Wasidoni,+ wala hawakuwa na shughuli yoyote na wanadamu.
8 Mwishowe wakaja kwa ndugu zao huko Sora+ na Eshtaoli,+ nao ndugu zao wakawaambia: “Haya, mna habari gani?” 9 Nao wakasema: “Simameni, nasi tupande juu yao; kwa maana tumeiona nchi, na tazama! ni nzuri sana.+ Nanyi mnasitasita. Msiwe goigoi kuhusu kwenda kuingia kuimiliki nchi ile.+ 10 Mtakapoingia, mtawafikia watu wasio na shaka,+ na nchi ile ni pana sana; kwa maana Mungu ameitia mkononi mwenu,+ mahali ambapo hakuna ukosefu wa kitu cha aina yoyote kilicho duniani.”+
11 Ndipo watu mia sita waliojifunga silaha za vita, kutoka katika familia ya Wadani,+ wakaondoka hapo, yaani, kutoka Sora na Eshtaoli.+ 12 Nao wakaondoka, wakapanda, wakapiga kambi huko Kiriath-yearimu+ katika Yuda. Ndiyo sababu wamepaita mahali hapo Mahane-dani+ mpaka leo hii. Tazama! Pako upande wa magharibi wa Kiriath-yearimu. 13 Baadaye wakapita kutoka hapo mpaka eneo lenye milima la Efraimu, wakaja mpaka nyumba ya Mika.+
14 Ndipo wale watu watano waliokuwa wameenda kuipeleleza+ nchi ya Laishi+ wakajibu na kuwaambia ndugu zao: “Je, mlijua kwamba katika nyumba hizi mna efodi na terafimu+ na sanamu ya kuchongwa+ na sanamu ya kuyeyushwa?+ Na sasa mfikirie akilini yale mtakayofanya.”+ 15 Basi wakageuka kando hapo, wakaja katika nyumba ya yule kijana, Mlawi,+ nyumbani kwa Mika, wakaanza kuuliza habari+ za hali yake. 16 Na wakati huo wale wanaume mia sita waliojifunga silaha za vita,+ waliokuwa ni wana wa Dani,+ walikuwa wamesimama kwenye mwingilio wa lango. 17 Kisha wale watu watano ambao walikuwa wametoka kwenda kuipeleleza nchi+ wakapanda, ili waingie humo ndani, waichukue ile sanamu ya kuchongwa+ na ile efodi+ na ile terafimu+ na ile sanamu ya kuyeyushwa.+ (Na yule kuhani+ alikuwa amesimama kwenye mwingilio wa lango pamoja na wale watu mia sita waliojifunga silaha za vita.) 18 Nao wakaingia katika nyumba ya Mika, wakachukua ile sanamu ya kuchongwa, ile efodi na ile terafimu na ile sanamu ya kuyeyushwa.+ Kisha yule kuhani+ akawaambia: “Mnafanya nini?” 19 Lakini wakamwambia: “Nyamaza. Weka mkono wako juu ya kinywa chako, na uende pamoja nasi, uwe baba+ na kuhani+ kwetu. Ni jambo gani lililo bora, wewe uendelee kuwa kuhani kwa nyumba ya mtu mmoja+ au kuwa kuhani kwa kabila na familia katika Israeli?”+ 20 Ndipo moyo wa kuhani huyo ukafurahi,+ basi akachukua ile efodi na ile terafimu na ile sanamu ya kuchongwa,+ akaja katikati ya wale watu.
21 Nao wakageuka wakaenda zao, wakaweka watoto wadogo na mifugo na vitu vyenye thamani mbele yao.+ 22 Walikuwa wameenda mwendo fulani kutoka nyumba ya Mika wakati wanaume waliokuwa katika nyumba zilizo karibu na nyumba ya Mika+ walipokusanywa pamoja na kujaribu kuwafikia wana wa Dani. 23 Walipozidi kuwalilia wana wa Dani, ndipo wakageuza nyuso zao na kumwambia Mika: “Una nini wewe,+ hata mkakusanyika?” 24 Basi akasema: “Mmeichukua miungu+ ambayo nilitengeneza,+ kuhani+ pia, nanyi mnaenda zenu, nami nina nini tena?+ Basi mnawezaje kuniambia, ‘Una nini wewe?’” 25 Ndipo wana wa Dani wakamwambia: “Usiache sauti yako isikike karibu nasi, ili kwamba watu wenye uchungu wa nafsi+ wasije wakawashambulia ninyi, nawe upoteze nafsi yako mwenyewe na nafsi za watu wa nyumbani mwako.” 26 Nao wana wa Dani wakaendelea kwenda zao; na Mika akaona kwamba wana nguvu kuliko yeye,+ basi akageuka, akarudi nyumbani kwake.
27 Lakini wao walichukua vitu ambavyo Mika alikuwa ametengeneza na yule kuhani+ aliyekuwa wake, wakaelekea Laishi,+ juu ya watu watulivu na wasio na shaka.+ Nao wakaanza kuwapiga kwa makali ya upanga,+ wakaliteketeza jiji kwa moto.+ 28 Wala hapakuwa na mkombozi, kwa maana lilikuwa mbali sana na Sidoni,+ nao hawakuwa na shughuli yoyote kabisa na wanadamu; na ilikuwa katika nchi tambarare ya chini iliyokuwa ya Beth-rehobu.+ Kisha wakalijenga jiji na kuanza kukaa ndani yake.+ 29 Zaidi ya hayo, wakaita jiji hilo jina Dani kulingana na jina la baba yao, Dani,+ aliyezaliwa kwa Israeli.+ Hata hivyo, jina la jiji hilo hapo zamani lilikuwa Laishi.+ 30 Kisha wana wa Dani wakajisimamishia ile sanamu ya kuchongwa;+ naye Yonathani+ mwana wa Gershomu,+ mwana wa Musa, yeye na wanawe wakawa makuhani kwa kabila la Wadani mpaka siku ile nchi ilipopelekwa uhamishoni.+ 31 Nao wakaendelea kujisimamishia ile sanamu ya kuchongwa ya Mika, ambayo alikuwa ameitengeneza, siku zote ambazo ile nyumba+ ya Mungu wa kweli iliendelea kuwa katika Shilo.+
19 Basi ikawa katika siku hizo kwamba hapakuwa na mfalme katika Israeli.+ Na ikawa kwamba Mlawi fulani alikuwa anakaa kwa muda katika sehemu za mbali zaidi za eneo lenye milima la Efraimu.+ Baadaye akachukua suria+ kutoka Bethlehemu+ katika Yuda awe mke wake. 2 Ndipo suria wake akaanza kufanya uasherati+ dhidi yake. Mwishowe suria huyo akamwacha, akaenda nyumbani kwa baba yake huko Bethlehemu katika Yuda, akaendelea kukaa huko miezi minne kamili. 3 Ndipo mume wake akasimama, akamfuata ili kuzungumza naye kwa sauti ya kufariji ili amrudishe; naye alikuwa pamoja na mtumishi+ wake na punda-dume wawili. Basi mwanamke huyo akamleta katika nyumba ya baba yake. Wakati baba ya huyo mwanamke kijana alipomwona, mara moja akafurahi kuonana naye. 4 Basi baba-mkwe wake, baba ya yule mwanamke kijana, akamzuia, akaendelea kukaa pamoja naye kwa siku tatu; nao wakawa wakila na kunywa, naye akawa akilala hapo usiku kucha.+
5 Na ikawa kwamba katika siku ya nne, walipoamka asubuhi na mapema kama kawaida, akasimama ili kwenda, lakini baba ya yule mwanamke kijana akamwambia mwana-mkwe wake: “Lisha moyo wako kipande cha mkate,+ kisha baadaye mwende zenu.” 6 Basi wakaketi, na wote wawili wakaanza kula na kunywa pamoja; kisha baba ya yule mwanamke kijana akamwambia yule mwanamume: “Kubali, tafadhali, kulala usiku kucha,+ na acha moyo wako uchangamke.”+ 7 Wakati huyo mwanamume aliposimama ili aende, baba-mkwe wake akaendelea kumsihi, hivi kwamba akalala hapo tena usiku kucha.+
8 Alipoamka asubuhi na mapema katika siku ya tano ili aende, baba ya yule mwanamke kijana akasema: “Tafadhali, kula kitu fulani kwa ajili ya moyo wako.”+ Nao wakakawia mpaka mchana kutwa. Na wote wawili wakaendelea kula. 9 Ndipo yule mwanamume+ akasimama ili aende, yeye pamoja na suria+ wake na mtumishi+ wake; lakini baba-mkwe wake, baba ya yule mwanamke kijana, akamwambia: “Tazama, sasa! Mchana umesonga kuelekea kuwa jioni. Tafadhali, laleni usiku kucha.+ Tazama mchana unakaribia mwisho wake. Lala hapa usiku kucha, na acha moyo wako uchangamke.+ Nanyi kesho mwamke mapema kwa ajili ya safari yenu, nawe uende hemani kwako.” 10 Hata hivyo, mwanamume huyo hakukubali kulala usiku kucha, bali alisimama, akaondoka na kwenda mpaka mbele ya Yebusi,+ yaani, Yerusalemu;+ naye alikuwa na wale punda-dume wawili waliotandikwa, na suria wake na mtumishi wake.
11 Walipokuwa karibu na Yebusi, kwa kuwa mchana ulikuwa umeendelea sana,+ yule mtumishi akamwambia bwana wake: “Haya, tafadhali, na tugeuke kando tuingie katika jiji hili la Wayebusi,+ tulale humo usiku kucha.” 12 Lakini bwana wake akamwambia: “Tusigeuke kando kuingia katika jiji la wageni+ ambao si sehemu ya wana wa Israeli; basi tuvuke mpaka Gibea.”+ 13 Naye akamwambia tena mtumishi wake: “Haya, na tukaribie mojawapo ya mahali hapa, tulale usiku kucha ama katika Gibea au katika Rama.”+ 14 Basi wakavuka, wakazidi kwenda zao, ndipo jua likaanza kutua juu yao walipokuwa karibu na Gibea, jiji la Benyamini.
15 Basi wakageuka kando hapo ili kuingia ndani walale usiku kucha katika Gibea. Kisha wakaingia na kuketi katika kiwanja cha watu wote cha jiji, wala hakuna yeyote aliyewakaribisha ndani ya nyumba ili walale usiku kucha.+ 16 Mwishowe, tazama! mwanamume fulani mzee akaingia, akitoka kufanya kazi yake shambani wakati wa jioni,+ na mtu huyo alikuwa wa kutoka katika eneo lenye milima la Efraimu,+ naye alikuwa anakaa kwa muda katika Gibea; lakini watu wa mahali hapo walikuwa Wabenyamini.+ 17 Alipoinua macho yake, akamwona yule mtu, yule msafiri, katika kiwanja cha watu wote cha jiji. Basi huyo mwanamume mzee akauliza: “Unaenda wapi, nawe unatoka wapi?”+ 18 Naye akamwambia: “Tunavuka kutokea Bethlehemu ya Yuda kwenda katika sehemu za mbali zaidi za eneo lenye milima la Efraimu.+ Huko ndiko ninakotoka, lakini nilienda Bethlehemu ya Yuda;+ nami ninaiendea nyumba yangu mwenyewe, wala hakuna yeyote anayenikaribisha ndani ya nyumba yake.+ 19 Na kuna majani na pia chakula cha mifugo+ kwa ajili ya punda zetu, na kuna mkate+ na divai pia kwa ajili yangu na kwa ajili ya kijakazi+ wako na kwa ajili ya mtumishi+ aliye pamoja na mtumishi wako. Hakuna ukosefu wa hata kitu kimoja.” 20 Hata hivyo, yule mzee akasema: “Uwe na amani!+ Upungufu wowote upande wako na uwe juu yangu.+ Lakini usilale usiku kucha katika kiwanja cha watu wote.” 21 Ndipo akamwingiza ndani ya nyumba yake,+ akawatupia wale punda chakula cha mchanganyiko.+ Kisha wakaosha miguu yao,+ wakaanza kula na kunywa.
22 Walipokuwa wakichangamsha mioyo yao,+ tazama! wanaume wa jiji lile, watu wasiofaa kitu,+ wakaizunguka nyumba,+ wakisukumana mlangoni; nao wakazidi kumwambia yule mzee, mwenye nyumba: “Mtoe nje yule mwanamume aliyeingia nyumbani mwako, ili tulale naye.”+ 23 Ndipo mwenye nyumba akatoka nje, akawaendea na kuwaambia:+ “Hapana, ndugu zangu,+ tafadhali msifanye jambo lolote baya, kwa kuwa mtu huyu ameingia nyumbani mwangu. Msitende upumbavu huu wenye kufedhehesha.+ 24 Hapa pana binti yangu aliye bikira na suria wa mtu huyu. Tafadhali, acheni niwalete nje, nanyi mpate kuwalala kinguvu+ na kuwatendea yaliyo mema machoni penu. Lakini msimtendee mwanamume huyu jambo hili la upumbavu na lenye kufedhehesha.”
25 Lakini wanaume hao hawakutaka kumsikiliza. Basi mtu huyo akamchukua suria+ wake na kumleta kwao nje; nao wakaanza kulala na mwanamke huyo,+ wakaendelea kumtendea vibaya+ usiku wote mpaka asubuhi, kisha wakamwacha aende wakati wa mapambazuko. 26 Ndipo mwanamke huyo akaja asubuhi ilipokuwa ikikaribia, akaanguka mlangoni pa nyumba ya yule mtu ambapo bwana wake alikuwa,+—mpaka wakati wa mapambazuko. 27 Baadaye bwana wake akaamka asubuhi, akafungua milango ya nyumba, akatoka nje kwenda zake, na tazama! yule mwanamke, suria wake,+ ameanguka kwenye mlango wa nyumba, mikono yake ikiwa juu ya kizingiti! 28 Basi akamwambia: “Simama, twende.” Lakini hakuna aliyejibu.+ Kwa hiyo mwanamume huyo akamchukua juu ya punda, akaondoka, akaenda kwake.+
29 Ndipo akaingia ndani ya nyumba yake, akachukua kisu cha kuchinjia, akamshika yule suria wake, akamkatakata vipande kwa kufuatisha mifupa yake, vipande kumi na viwili+ naye akampeleka katika kila eneo la Israeli.+ 30 Na ikatukia kwamba kila mtu aliyeona jambo hilo akasema: “Jambo kama hili halijawahi kutokea kamwe wala kuonekana tangu siku wana wa Israeli walipopanda kutoka nchi ya Misri mpaka leo. Wekeni jambo hili mioyoni mwenu, fanyeni shauri+ na mseme.”
20 Basi wana wote wa Israeli wakatoka,+ na kusanyiko likakutanika kama mtu mmoja,+ kutoka Dani+ mpaka Beer-sheba+ pamoja na nchi ya Gileadi,+ likamkutanikia Yehova katika Mispa.+ 2 Kwa hiyo wakuu wa watu wote na makabila yote ya Israeli wakasimama katika kutaniko la watu wa Mungu wa kweli,+ wanaume mia nne elfu wanaoenda kwa miguu, wenye kutumia upanga.+
3 Na wana wa Benyamini wakasikia kwamba wana wa Israeli wamepanda kwenda Mispa.+
Ndipo wana wa Israeli wakasema: “Semeni. Jambo hili baya limetokea namna gani?”+ 4 Kwa hiyo yule mtu, Mlawi,+ mume wa mwanamke aliyeuawa, akajibu na kusema: “Nilienda Gibea,+ la Benyamini, mimi na suria+ wangu, ili tulale usiku kucha. 5 Na wenye mashamba wote wa Gibea wakasimama kunipinga, wakaizunguka nyumba juu yangu wakati wa usiku. Walikusudia kuniua mimi, lakini wakamlala kinguvu+ suria wangu, naye mwishowe akafa.+ 6 Basi nikamshika suria wangu, nikamkatakata vipande na kumpeleka katika kila shamba la urithi wa Israeli,+ kwa sababu walikuwa wametenda mwenendo mpotovu+ na upumbavu wenye kufedhehesha katika Israeli.+ 7 Tazameni! Enyi nyote wana wa Israeli, semeni neno na shauri lenu+ hapa.”
8 Basi watu wote wakasimama kama mtu mmoja,+ wakisema: “Hatutaenda hata mmoja wetu katika hema lake, wala hatutageuka hata mmoja wetu kwenda nyumbani kwake.+ 9 Na sasa hili ndilo jambo tutakalotendea Gibea. Na tupande kwa kura+ kwenda kupigana na jiji hilo. 10 Nasi tuchukue watu kumi kati ya mia moja wa makabila yote ya Israeli, na mia moja kati ya elfu moja, na elfu moja kati ya elfu kumi, ili kuwachukulia watu vyakula, ili wachukue hatua kwa kwenda kupigana na Gibea la Benyamini, kwa sababu ya huu upumbavu wote wenye kufedhehesha+ waliotenda katika Israeli.” 11 Kwa hiyo wanaume wote wa Israeli wakakusanyika juu ya jiji hilo kama mtu mmoja, wasaidiane.
12 Ndipo makabila yote ya Israeli wakatuma watu waende kwa watu wote wa kabila la Benyamini,+ wakisema: “Ni jambo gani hili baya ambalo limefanywa kati yenu?+ 13 Na sasa watoeni wale wanaume,+ wale watu wasiofaa kitu,+ ambao wamo katika Gibea,+ ili tuwaue,+ nasi tuondolee mbali lililo baya katika Israeli.”+ Na wana wa Benyamini hawakutaka kuisikiliza sauti ya ndugu zao, wana wa Israeli.+
14 Ndipo wana wa Benyamini wakakusanyika pamoja kutoka katika majiji kwenda Gibea ili watoke kupigana na wana wa Israeli. 15 Basi wana wa Benyamini wakakusanywa siku hiyo kutoka katika majiji, watu 26,000 wenye kutumia upanga,+ mbali na wakaaji wa Gibea, ambao watu 700 waliochaguliwa walikusanywa. 16 Kati ya watu hao wote kulikuwa na watu 700 waliochaguliwa, wenye kutumia mkono wa kushoto.+ Kila mmoja wa hao alikuwa mtupa-mawe+ kwa kombeo na angeweza kupiga shabaha unywele, bila kukosea.
17 Na watu wa Israeli walikusanywa mbali na Benyamini, wanaume mia nne elfu wenye kutumia upanga.+ Kila mmoja wao alikuwa mwanamume wa vita. 18 Kisha wakasimama, wakapanda kwenda Betheli, wakaulize kutoka kwa Mungu.+ Ndipo wana wa Israeli wakasema: “Ni nani kati yetu atakayeongoza pigano juu ya wana wa Benyamini?”+ Yehova akasema: “Yuda ataongoza.”+
19 Kisha wana wa Israeli wakasimama asubuhi na kupiga kambi juu ya Gibea.
20 Basi watu wa Israeli wakatoka kwenda kupigana na Benyamini; nao wana wa Israeli wakajipanga kivita juu yao katika Gibea. 21 Kwa hiyo wana wa Benyamini wakatoka katika Gibea,+ wakawaangusha chini na kuwaangamiza watu 22,000 katika Israeli siku hiyo.+ 22 Hata hivyo, watu, wanaume wa Israeli, wakaonyesha uhodari, kisha wakajipanga kivita tena mahali pale walipokuwa wamejipanga kivita siku ya kwanza. 23 Basi wana wa Israeli wakapanda na kulia+ mbele za Yehova mpaka jioni nao wakauliza kutoka kwa Yehova, wakisema: “Je, niende nikaribie tena kupigana na wana wa Benyamini ndugu yangu?”+ Yehova akasema: “Panda upigane naye.”
24 Basi wana wa Israeli wakawakaribia wana wa Benyamini siku ya pili.+ 25 Benyamini nao wakatoka katika Gibea ili kukutana nao siku ya pili, kisha wakawaangusha chini na kuwaangamiza+ watu kumi na nane elfu tena kati ya wana wa Israeli, wote hao wakiwa wenye kutumia upanga.+ 26 Basi wana wote wa Israeli,+ watu wote, wakapanda na kuja Betheli, wakalia+ na kukaa hapo mbele za Yehova nao wakafunga+ siku hiyo mpaka jioni, wakatoa matoleo ya kuteketezwa+ na matoleo ya ushirika+ mbele za Yehova. 27 Kisha wana wa Israeli wakauliza kutoka kwa Yehova,+ kwa kuwa hapo ndipo lilipokuwa lile sanduku la agano+ la Mungu wa kweli siku hizo. 28 Basi Finehasi+ mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni, alikuwa amesimama mbele ya sanduku hilo siku hizo,+ akisema: “Je, niende tena kupigana na wana wa Benyamini ndugu yangu, au je, nisiende?”+ Na Yehova akasema: “Panda, kwa kuwa kesho nitamtia mkononi mwako.”+ 29 Ndipo Israeli wakaweka watu wa kuvizia+ Gibea pande zote.
30 Na wana wa Israeli wakapanda kwenda juu ya wana wa Benyamini siku ya tatu, wakajipanga kivita kupigana na Gibea kama vile ilivyokuwa nyakati zile nyingine.+ 31 Wana wa Benyamini walipotoka kwenda kukutana na wale watu, wakavutwa mbali na jiji.+ Ndipo, kama vile ilivyokuwa zile nyakati nyingine, wakaanza kuwapiga baadhi ya watu, karibu watu 30 katika Israeli,+ waliokuwa na majeraha ya kufisha katika njia kuu, moja ya njia hizo inapanda kwenda Betheli+ na ile nyingine inaenda Gibea,+ shambani. 32 Basi wana wa Benyamini wakaanza kusema: “Wanashindwa mbele yetu kama ilivyokuwa pale mwanzoni.”+ Lakini wana wa Israeli wakasema: “Na tukimbie,+ nasi hakika tutawavuta mbali kutoka katika jiji, waingie katika njia kuu.” 33 Na watu wote wa Israeli wakasimama kutoka mahali pao, kisha wakajipanga kivita katika Baal-tamari, huku wale wa Israeli waliokuwa wakivizia+ wakifanya mashambulizi kutoka mahali pao katika ujirani wa Gibea.+ 34 Basi wanaume elfu kumi waliochaguliwa kutoka katika Israeli yote wakaja mbele ya Gibea, na mapigano yalikuwa makali; na Wabenyamini hawakujua kwamba msiba+ ulikuwa unawakaribia.
35 Naye Yehova akashinda Benyamini+ mbele ya Israeli, hivi kwamba wana wa Israeli siku hiyo wakaangamiza katika Benyamini watu 25,100, wote hao wenye kutumia upanga.+
36 Hata hivyo, wana wa Benyamini walifikiri kwamba watu wa Israeli wangeshindwa+ walipoendelea kurudi nyuma mbele ya Benyamini kwa sababu walitegemea kile kikundi cha kuvizia ambacho walikuwa wameweka juu ya Gibea. 37 Na wale waliokuwa wakivizia, walitenda haraka, wakatimua mbio kuelekea Gibea.+ Ndipo wenye kuvizia+ wakasambaa na kulipiga jiji lote kwa makali ya upanga.+
38 Basi watu wa Israeli walikuwa wamefanya mpango na wale wenye kuvizia kwamba wafanye moshi upande juu kama ishara kutoka katika jiji hilo.+
39 Wana wa Israeli walipogeuka katika lile pigano, Benyamini wakaanza kupiga karibu watu 30 waliokuwa na majeraha ya kufisha kati ya watu wa Israeli,+ kwa maana walisema: “Bila shaka wanashindwa mbele yetu kama ilivyokuwa katika pigano la kwanza.”+ 40 Na ile ishara+ ikaanza kupanda kutoka katika jiji ikiwa nguzo ya moshi.+ Basi Benyamini alipogeuka kuangalia nyuma, tazama! jiji lote lilipaa juu kuelekea mbinguni.+ 41 Watu wa Israeli wakageuka,+ na watu wa Benyamini wakafadhaika,+ kwa kuwa waliona kwamba msiba umewafikia.+ 42 Basi wakageuka mbele ya watu wa Israeli kuelekea nyikani, na pigano likawafuata kwa ukaribu, huku wale watu waliokuwa wakitoka katika majiji wakiwaangamiza katikati yao. 43 Wakamzunguka Benyamini.+ Wakamfuatilia wasiwe na mahali pa kupumzika.+ Wakamkanyagia chini moja kwa moja mbele ya Gibea+ kuelekea upande wa mapambazuko ya jua. 44 Mwishowe watu kumi na nane elfu wa Benyamini wakaanguka, wote hao wakiwa wanaume mashujaa.+
45 Basi wakageuka, wakakimbia kuelekea nyikani mpaka kwenye mwamba wa Rimoni.+ Nao wakaokota watu elfu tano kati yao katika njia kuu,+ na kuendelea kuwafuatilia kwa ukaribu mpaka Gidomu, basi wakawapiga watu elfu mbili kati yao. 46 Na wote wa Benyamini walioanguka siku hiyo wakajumlika mwishowe kuwa watu 25,000 wenye kutumia upanga,+ wote hao wakiwa wanaume mashujaa. 47 Lakini wanaume mia sita wakageuka, wakakimbia kuelekea nyikani mpaka kwenye mwamba wa Rimoni, nao wakaendelea kukaa juu ya mwamba wa Rimoni+ kwa miezi minne.
48 Nao watu wa Israeli wakarudi tena kupigana na wana wa Benyamini, wakaendelea kuwapiga kwa makali ya upanga wale wa jiji, kuanzia mwanadamu hata mnyama wa kufugwa hata wote waliopatikana.+ Pia wakayateketeza kwa moto majiji yote waliyoyaona.+
21 Basi watu wa Israeli walikuwa wameapa katika Mispa,+ wakisema: “Hakuna mtu yeyote kati yetu atakayempa Benyamini binti yake awe mke wake.”+ 2 Kwa hiyo hao watu wakaja Betheli+ wakakaa hapo mbele za Mungu wa kweli+ mpaka jioni, wakaendelea kupaaza sauti zao na kulia sana.+ 3 Nao wakawa wakisema: “Ee Yehova Mungu wa Israeli, kwa nini jambo hili limetokea katika Israeli, kwamba kabila moja lipotee leo katika Israeli?”+ 4 Na ikawa kesho yake kwamba watu wakaamka mapema, wakajenga madhabahu hapo na kutoa matoleo ya kuteketezwa+ na matoleo ya ushirika.+
5 Ndipo wana wa Israeli wakasema: “Ni nani kati ya makabila yote ya Israeli ambaye hakumjia Yehova katika kutaniko, kwa maana kuna kiapo+ kikubwa ambacho kimefanywa kuhusu yule ambaye hakumjia Yehova katika Mispa, kusema: ‘Lazima atauawa.’”+ 6 Na wana wa Israeli wakaanza kujuta juu ya Benyamini ndugu yao. Basi wakasema: “Leo kabila moja limekatiliwa mbali kutoka katika Israeli. 7 Tutafanya nini kwa wale waliobaki kuhusiana na wake, kwa kuwa sisi wenyewe tumeapa+ kwa Yehova kwamba hatutawapa yeyote wa binti zetu ili wawe wake zao?”+
8 Nao wakaendelea kusema: “Ni kabila gani kati ya makabila ya Israeli ambalo halikuja mbele za Yehova katika Mispa?”+ Na tazama! hakuna yeyote aliyeingia kambini kutoka Yabesh-gileadi+ ili kuja kwenye kutaniko. 9 Watu walipohesabiwa, tazama! hapakuwa hata mtu mmoja kutoka kwa wakaaji wa Yabesh-gileadi. 10 Basi kusanyiko likatuma huko wanaume kumi na mbili elfu walio mashujaa zaidi na kuwaamuru, wakisema: “Nendeni, mkawapige wakaaji wa Yabesh-gileadi kwa makali ya upanga, hata wanawake na watoto wadogo.+ 11 Nanyi mfanye jambo hili: Mtamwangamiza kila mwanamume na kila mwanamke ambaye amepata kulala na mwanamume.”+ 12 Hata hivyo, wakapata kutoka kwa wakaaji wa Yabesh-gileadi+ wasichana mia nne, mabikira,+ ambao hawakuwa wamepata kulala na mwanamume. Basi wakawaleta kambini katika Shilo,+ ambalo liko katika nchi ya Kanaani.
13 Na kusanyiko lote likatuma watu na kusema na wana wa Benyamini waliokuwa juu ya mwamba wa Rimoni+ na kuwatakia amani. 14 Basi Benyamini akarudi wakati huo. Ndipo wakawapa wale wanawake ambao walikuwa wamewahifadhi hai kutoka kwa wanawake wa Yabesh-gileadi;+ lakini hawakupata wa kuwatosha.+ 15 Na watu wakajuta juu ya Benyamini+ kwa sababu Yehova alikuwa amefanya pengo kati ya makabila ya Israeli. 16 Kwa hiyo wanaume wazee wa kusanyiko wakasema: “Tutawatendea nini wale wanaume ambao wamebaki kuhusiana na wake, kwa maana wanawake wameangamizwa kutoka katika Benyamini?” 17 Ndipo wakasema: “Kunapaswa kuwa na miliki kwa hao wa Benyamini walioponyoka,+ ili kabila moja lisifutwe katika Israeli. 18 Lakini sisi, hatuna ruhusa ya kuwapa wake kutoka kwa binti zetu, kwa sababu wana wa Israeli wameapa, wakisema, ‘Alaaniwe yeyote atakayempa Benyamini mke.’”+
19 Mwishowe wakasema: “Tazama! Kuna sherehe ya Yehova kutoka mwaka mpaka mwaka katika Shilo,+ ambalo liko upande wa kaskazini wa Betheli, kuelekea upande wa mashariki wa njia kuu inayopanda kutoka Betheli kwenda Shekemu+ na kuelekea upande wa kusini wa Lebona.” 20 Basi wakawaamuru wana wa Benyamini, wakisema: “Nendeni, mkavizie katika mashamba ya mizabibu. 21 Kisha mtazame, na hapo, binti za Shilo watakapotoka nje ili kucheza katika dansi+ za mzunguko, ninyi pia mtoke katika mashamba ya mizabibu, kisha mjichukulie kwa nguvu kila mmoja mke wake kutoka kwa binti za Shilo, nanyi mwende katika nchi ya Benyamini. 22 Na itatukia kwamba baba zao au ndugu zao wakija kuendesha kesi juu yetu, sisi pia tutawaambia hivi, ‘Tupeni sisi kibali kwa ajili yao, kwa sababu hatukumchukulia kila mmoja mke wake kwa vita,+ kwa maana wala wakati huu si ninyi mliowapa wao kwamba muwe na hatia.’”+
23 Basi wana wa Benyamini wakafanya vivyo hivyo, nao wakajichukulia+ wake kutoka kati ya wanawake wenye kucheza dansi+ za kuzunguka, ambao walinyakua; kisha wakaenda zao na kurudi kwenye urithi wao, wakajenga majiji+ na kuanza kukaa ndani yake.
24 Na wana wa Israeli wakaanza kutawanyika kutoka hapo wakati huo, kila mmoja akaenda kwa kabila lake mwenyewe na kwa familia yake mwenyewe; nao wakaenda zao kutoka hapo, kila mmoja kwenye urithi wake mwenyewe.+
25 Katika siku hizo hapakuwa na mfalme katika Israeli.+ Kila mmoja alikuwa na mazoea ya kufanya yaliyokuwa mema machoni pake mwenyewe.+