Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • nwt Isaya 1:1-66:24
  • Isaya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Isaya
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Isaya

ISAYA

1 Maono ambayo Isaya*+ mwana wa Amozi aliona kuhusu Yuda na Yerusalemu katika siku za Uzia,+ Yothamu,+ Ahazi,+ na Hezekia,+ wafalme wa Yuda:+

 2 Sikieni, enyi mbingu, na usikilize, ewe dunia,+

Kwa maana Yehova amesema:

“Nimelea wana wakakua,+

Lakini wameniasi.+

 3 Ng’ombe anamjua vizuri aliyemnunua,

Na punda anaijua vizuri hori ya mmiliki wake;

Lakini Israeli hanijui,*+

Watu wangu mwenyewe hawatendi kwa uelewaji.”

 4 Ole kwa taifa lenye dhambi,+

Watu waliolemewa na dhambi,

Uzao wa watu waovu, watoto waliopotoka!

Wamemwacha Yehova;+

Wamemvunjia heshima Mtakatifu wa Israeli;

Wamemgeuzia migongo yao.

 5 Ni wapi mtakapopigwa tena kwa kuwa mnazidi kuasi?+

Kichwa chote ni kigonjwa,

Na moyo wote ni mgonjwa.+

 6 Kuanzia wayo wa mguu mpaka kichwani, hakuna sehemu yenye afya.

Kuna majeraha na michubuko na vidonda vilivyo wazi

—Havijatibiwa* wala kufungwa wala kulainishwa kwa mafuta.+

 7 Nchi yenu ni ukiwa.

Majiji yenu yameteketezwa kwa moto.

Wageni wanaila nchi yenu mbele ya macho yenu.+

Ni kama nchi iliyo ukiwa iliyoharibiwa kabisa na wageni.+

 8 Binti ya Sayuni ameachwa kama kibanda katika shamba la mizabibu,

Kama nyumba ya msonge katika shamba la matango,

Kama jiji lililozingirwa.+

 9 Kama Yehova wa majeshi hangetuachia waokokaji wachache,

Tungekuwa kama Sodoma,

Na tungefanana na Gomora.+

10 Sikieni neno la Yehova, enyi madikteta* wa Sodoma.+

Sikilizeni sheria* ya Mungu wetu, enyi watu wa Gomora.+

11 “Dhabihu zenu nyingi zina faida gani kwangu?”+ asema Yehova.

“Nimetosheka na dhabihu zenu za kuteketezwa za kondoo dume+ na mafuta ya wanyama waliolishwa vizuri,+

Nami sipendezwi na damu+ ya ng’ombe dume wachanga+ na wanakondoo na mbuzi.+

12 Mnapokuja kusimama mbele zangu,+

Ni nani ambaye amewataka mfanye hivyo,

Mzikanyage-kanyage nyua zangu?+

13 Acheni kuleta matoleo zaidi ya nafaka yasiyo na thamani.

Uvumba wenu unanichukiza.+

Miezi mipya,+ sabato,+ kuita makusanyiko+

—Siwezi kuvumilia matumizi ya nguvu za uchawi+ pamoja na kusanyiko lenu takatifu.

14 Nimechukia* miezi yenu mipya na sherehe zenu.

Zimekuwa mzigo kwangu;

Nimechoka kuzibeba.

15 Na mnaponyoosha mikono yenu,

Mimi huficha macho yangu nisiwaone.+

Ingawa mnatoa sala nyingi,+

Mimi sisikilizi;+

Mikono yenu imejaa damu.+

16 Jiosheni, jisafisheni;+

Ondoeni matendo yenu maovu mbele za macho yangu;

Acheni kutenda mabaya.+

17 Jifunzeni kutenda mema, tafuteni haki,+

Mrekebisheni mkandamizaji,

Teteeni haki za yatima,

Nanyi mteteeni mjane.”+

18 “Sasa, njooni, na tunyooshe mambo kati yetu,” asema Yehova.+

“Ingawa dhambi zenu ni kama rangi nyekundu,

Zitafanywa kuwa nyeupe kama theluji;+

Ingawa ni nyekundu kama kitambaa chekundu,

Zitakuwa kama sufu.

19 Mkionyesha utayari na kusikiliza,

Mtakula vitu vyema vya nchi.+

20 Lakini mkikataa na kuasi,

Mtaliwa na upanga,+

Kwa maana kinywa cha Yehova kimesema hayo.”

21 Jinsi mji mwaminifu+ umekuwa kahaba!+

Ulikuwa umejaa haki;+

Uadilifu ulikuwa ukikaa ndani yake,+

Lakini sasa wauaji wanakaa ndani yake.+

22 Fedha yako imekuwa takataka,+

Na pombe yako* imechanganywa na maji.

23 Wakuu wako ni wakaidi na wanashirikiana na wezi.+

Kila mmoja wao anapenda rushwa na kutafuta zawadi kwa bidii.+

Hawawatendei kwa haki mayatima,

Na kesi ya mjane haiwafikii kamwe.+

24 Kwa hiyo Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi,

Mwenye Nguvu wa Israeli, anasema:

“Ah! Nitawaondoa wapinzani wangu,

Nami nitalipiza kisasi dhidi ya maadui wangu.+

25 Nitaugeuza mkono wangu dhidi yako,

Nitayeyusha takataka yako kama kwa sabuni,

Nami nitauondoa uchafu wako wote.+

26 Nitawarudisha waamuzi wenu kama mwanzoni

Na washauri wenu kama awali.+

Kisha wewe utaitwa Jiji la Uadilifu, Mji Mwaminifu.+

27 Sayuni atakombolewa kwa haki,+

Na watu wake wanaorudi, kwa uadilifu.

28 Waasi na watenda dhambi watavunjwa pamoja,+

Na wale wanaomwacha Yehova watafikia mwisho wao.+

29 Kwa maana wataona aibu kwa sababu ya miti mikubwa ambayo mlitamani,+

Nanyi mtafedheheka kwa sababu ya bustani* ambazo mlichagua.+

30 Kwa maana mtakuwa kama mti mkubwa ambao majani yake yananyauka,+

Na kama bustani isiyo na maji.

31 Mwanamume mwenye nguvu atakuwa kitani,*

Na kazi yake itakuwa cheche ya moto;

Atateketea motoni pamoja na kazi yake,

Na hapatakuwa na yeyote wa kuwazima.”

2 Hili ndilo jambo ambalo Isaya mwana wa Amozi aliona katika maono kuhusu Yuda na Yerusalemu:+

 2 Katika siku za mwisho,*

Mlima wa nyumba ya Yehova

Utaimarishwa kabisa juu ya vilele vya milima,+

Nao utainuliwa juu ya vilima,

Na mataifa yote yatamiminika kwenye mlima huo.+

 3 Na watu wa mataifa mengi wataenda na kusema:

“Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova,

Kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+

Naye atatufundisha njia zake,

Nasi tutatembea katika vijia vyake.”+

Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,

Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.+

 4 Atatekeleza hukumu miongoni mwa mataifa

Na kunyoosha* mambo kuhusiana na watu wengi.

Watafua panga zao ziwe majembe ya plau

Na mikuki yao iwe miundu.+

Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa lingine,

Wala hawatajifunza vita tena kamwe.+

 5 Enyi nyumba ya Yakobo, njooni,

Na tutembee katika nuru ya Yehova.+

 6 Kwa maana umewaacha watu wako, nyumba ya Yakobo,+

Kwa sababu wamejaa vitu vya kutoka Mashariki;

Wanafanya uchawi+ kama Wafilisti,

Nao wana watoto wengi wa wageni.

 7 Nchi yao imejaa fedha na dhahabu,

Na hazina zao hazina kikomo.

Nchi yao imejaa farasi,

Na magari yao hayana idadi.+

 8 Nchi yao imejaa miungu ya ubatili.+

Wao huinamia kazi ya mikono yao wenyewe,

Kile ambacho vidole vyao vimetengeneza.

 9 Basi mtu huinama chini, hujishusha chini,

Nawe huwezi kuwasamehe.

10 Ingia ndani ya mwamba, ujifiche mavumbini

Kwa sababu ya uwepo wa Yehova unaoogopesha

Na fahari yake kuu.+

11 Macho ya mwanadamu yenye majivuno yatashushwa,

Na kiburi cha wanadamu kitainama chini.*

Yehova peke yake ndiye atakayekwezwa siku hiyo.

12 Kwa maana hiyo ni siku ya Yehova wa majeshi.+

Itakuja dhidi ya kila mtu mwenye majivuno na anayejiinua,

Itakuja dhidi ya kila mtu, aliyekwezwa au aliye chini,+

13 Dhidi ya mierezi yote ya Lebanoni ambayo ni mirefu na iliyo juu

Na dhidi ya mialoni yote ya Bashani,

14 Dhidi ya milima yote mirefu

Na dhidi ya vilima vyote virefu,

15 Dhidi ya kila mnara mrefu na kila ukuta wenye ngome,

16 Dhidi ya meli zote za Tarshishi+

Na dhidi ya mashua zote zinazotamanika.

17 Majivuno ya mwanadamu yatashushwa,

Na kiburi cha wanadamu kitainama chini.*

Yehova peke yake ndiye atakayekwezwa siku hiyo.

18 Miungu ya ubatili itatoweka kabisa.+

19 Na watu wataingia ndani ya mapango ya miamba

Na ndani ya mashimo ardhini,+

Kwa sababu ya uwepo wa Yehova unaoogopesha

Na fahari yake kuu,+

Anapoinuka ili kuifanya dunia itetemeke kwa hofu.

20 Siku hiyo wanadamu watachukua miungu yao ya ubatili ya fedha na dhahabu

Ambayo walijitengenezea ili waiinamie

Nao watawatupia panya* na popo,+

21 Ili kuingia katika mashimo yaliyo kwenye miamba

Na ndani ya mipasuko ya majabali,

Kwa sababu ya uwepo wa Yehova unaoogopesha

Na fahari yake kuu,

Anapoinuka ili kuifanya dunia itetemeke kwa hofu.

22 Kwa faida yenu wenyewe, acheni kumtumaini mwanadamu,

Ambaye ni pumzi tu iliyo katika mianzi ya pua yake.*

Kwa nini afikiriwe?

3 Kwa maana tazama! Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi,

Anaondoa Yerusalemu na Yuda kila aina ya tegemeo na msaada,

Tegemeo lote la kupata mkate na maji,+

 2 Mwanamume hodari na shujaa,

Mwamuzi na nabii,+ mbashiri* na mzee,

 3 Mkuu wa 50,+ mwanamume mwenye kuheshimiwa, na mshauri,

Mchawi hodari na mlozi stadi.+

 4 Nitawafanya wavulana kuwa wakuu wao,

Na watu wanaoyumbayumba* watawatawala.

 5 Watu watakandamizana,

Kila mmoja atamkandamiza mwenzake.+

Mvulana atamshambulia mwanamume mzee,

Na mtu asiyeheshimiwa sana atamdharau yule anayeheshimiwa.+

 6 Kila mmoja atamshika ndugu yake katika nyumba ya baba yake, na kusema:

“Wewe una joho—uwe kamanda wetu.

Lisimamie rundo hili la magofu.”

 7 Lakini siku hiyo atakataa akisema:

“Mimi sitakuwa mfunga-majeraha* wenu;

Sina chakula wala nguo katika nyumba yangu.

Msiniweke kuwa kamanda juu ya watu.”

 8 Kwa maana watu wa Yerusalemu wamejikwaa,

Na watu wa Yuda wameanguka,

Kwa sababu wanampinga Yehova kwa maneno na matendo;

Wanatenda kwa ukaidi mbele za uwepo wake mtukufu.*+

 9 Hali ya nyuso zao inatoa ushahidi dhidi yao,

Nazo zinatangaza dhambi yao kama Sodoma;+

Hawajaribu kuificha.

Ole wao,* kwa maana wanajiletea msiba!

10 Waambie waadilifu kwamba mambo yatawaendea vema;

Watathawabishwa kwa yale wanayotenda.*+

11 Ole wake mtu mwovu!

Atapatwa na msiba,

Atatendewa yale ambayo mikono yake imetenda!

12 Na kuhusu watu wangu, wasimamizi wao wa kazi wanawatesa,

Na wanawake huwatawala.

Watu wangu, viongozi wenu wanawafanya mtangetange,

Nao wanavuruga mwelekeo wa njia zenu.+

13 Yehova anachukua nafasi yake ili kutoa mashtaka;

Anasimama ili kuwahukumu watu.

14 Yehova atawahukumu wazee na wakuu wa watu wake.

“Mmeliteketeza kabisa shamba la mizabibu,

Na vitu mlivyowaibia maskini vimo ndani ya nyumba zenu.+

15 Mnawezaje kuwaponda watu wangu

Na kusaga nyuso za maskini mavumbini?”+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi.

16 Yehova anasema: “Kwa sababu mabinti wa Sayuni ni wenye majivuno,

Nao wanatembea wakiwa wameinua vichwa vyao juu,*

Wakipepesa-pepesa macho kwa utongozi, wakitembea kwa hatua fupifupi,

Wakiwa na vikuku vinavyotoa milio kwenye vifundo vya miguu,

17 Yehova pia atawapiga mabinti wa Sayuni kwa upele kichwani,

Na Yehova atafunua wazi paji la uso wao.+

18 Siku hiyo Yehova ataondoa umaridadi wa bangili zao,

Tepe za kichwani na mapambo yenye umbo la mwezi mwandamo,+

19 Herini,* vikuku, na shela,

20 Vitambaa vya kichwani, mafurungu, na mavazi ya kifuani,*

Chupa za marashi* na hirizi,*

21 Pete za vidole na pete za puani,

22 Kanzu za sherehe, kanzu fupi za nje, majoho, na mikoba,

23 Vioo vya mkononi+ na mavazi ya kitani,*

Vilemba na shela.

24 “Badala ya mafuta ya zeri,+ kutakuwa na harufu ya uozo;

Badala ya mshipi, kamba;

Badala ya mtindo maridadi wa nywele, upara;+

Badala ya vazi lenye thamani, nguo ya magunia;+

Na alama iliyotiwa mwilini badala ya urembo.

25 Wanaume wako watauawa kwa upanga,

Na wanaume wako hodari watauawa vitani.+

26 Milango yake italia na kuomboleza,+

Naye ataketi ardhini katika hali ya ukiwa.”+

4 Siku hiyo, wanawake saba watamkamata mwanamume mmoja,+ wakisema:

“Tutakula mkate wetu wenyewe

Na kuvaa nguo zetu wenyewe;

Lakini turuhusu tu tuitwe kwa jina lako

Ili kuondoa aibu yetu.”*+

2 Siku hiyo kile ambacho Yehova atachipusha kitakuwa kizuri sana na chenye utukufu, na mazao ya nchi yatakuwa kitu cha kujivunia na urembo kwa ajili ya waokokaji wa Israeli.+ 3 Yeyote atakayebaki Sayuni na kuachwa Yerusalemu ataitwa mtakatifu, wale wote walio Yerusalemu walioandikwa kwa ajili ya uzima.+

4 Yehova atakapoosha uchafu wa* mabinti wa Sayuni+ na kusafisha umwagaji wa damu wa Yerusalemu kutoka ndani yake kwa roho ya hukumu na kwa roho ya kuteketeza,*+ 5 Yehova pia ataumba juu ya eneo lote la Mlima Sayuni na juu ya mahali pa makusanyiko yake wingu na moshi wakati wa mchana na moto mwangavu unaowaka wakati wa usiku;+ kwa maana juu ya utukufu wote kutakuwa na mahali pa kujificha. 6 Na kutakuwa na kibanda chenye kivuli cha kujikinga na joto wakati wa mchana,+ nacho kitakuwa kimbilio na ulinzi wakati wa dhoruba na mvua.+

5 Tafadhali, acha nimwimbie mpenzi wangu

Wimbo kuhusu mpenzi wangu na shamba lake la mizabibu.+

Mpenzi wangu alikuwa na shamba la mizabibu kwenye kilima kinachozaa sana.

 2 Akalilima na kuondoa mawe ndani yake.

Akapanda mzabibu bora mwekundu,

Akajenga mnara katikati yake,

Naye akachimba shinikizo la divai ndani yake.+

Kisha akaendelea kutumaini kwamba litazaa zabibu,

Lakini lilizaa zabibu za mwituni peke yake.+

 3 “Na sasa, enyi wakaaji wa Yerusalemu na watu wa Yuda,

Tafadhali hukumuni kati yangu na shamba langu la mizabibu.+

 4 Ningelifanyia nini kingine shamba langu la mizabibu

Ambacho bado sijafanya?+

Kwa nini, nilipotumaini kwamba litazaa zabibu,

Lilizaa zabibu za mwituni peke yake?

 5 Sasa, tafadhali, acheni niwaambie

Kile nitakacholifanyia shamba langu la mizabibu:

Nitaondoa uzio wake,

Nalo litateketezwa kabisa.+

Nitaubomoa ukuta wake wa mawe,

Nalo litakanyagwa-kanyagwa.

 6 Nami nitalifanya liwe ukiwa;+

Halitapunguzwa matawi wala kulimwa.

Litamea vichaka vya miiba na magugu,+

Nami nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua yoyote juu yake.+

 7 Kwa maana shamba la mizabibu la Yehova wa majeshi ni nyumba ya Israeli;+

Watu wa Yuda ndilo shamba alilolipenda sana.

Aliendelea kutumaini haki itendwe,+

Lakini tazama! kulikuwa na ukosefu wa haki;

Alitumaini uadilifu ufanywe,

Lakini tazama! kulikuwa na kilio cha huzuni.”+

 8 Ole wao wanaounganisha nyumba moja na nyingine+

Na wanaounganisha shamba moja na lingine+

Mpaka nafasi inapokosekana kabisa

Nanyi mnaishi peke yenu nchini!

 9 Yehova wa majeshi ameapa masikioni mwangu

Kwamba nyumba nyingi, ingawa ni kubwa na maridadi,

Zitakuwa kitu cha kutisha,

Bila mkaaji.+

10 Kwa maana ekari kumi za* shamba la mizabibu zitazaa kipimo kimoja tu cha bathi,*

Na kipimo kimoja cha homeri* ya mbegu kitazaa efa* moja tu.+

11 Ole wao wanaoamka asubuhi na mapema ili wanywe kileo,+

Wanaokawia hadi giza linapoingia jioni mpaka divai inapowawasha!

12 Wana kinubi na kinanda,

Tari, filimbi, na divai katika karamu zao;

Lakini hawafikirii utendaji wa Yehova,

Wala hawaioni kazi ya mikono yake.

13 Kwa hiyo watu wangu wataenda uhamishoni

Kwa sababu ya kukosa ujuzi;+

Wanaume wao wenye utukufu watakuwa na njaa,+

Na watu wao wote watakauka kwa kiu.

14 Kwa hiyo Kaburi* limejipanua*

Nalo limefungua kinywa chake bila kikomo;+

Na fahari yake,* umati wake wenye kelele, na watu wake wanaosherehekea

Hakika watashuka na kuingia ndani yake.

15 Na mwanadamu atainama,

Mwanadamu atashushwa,

Na macho ya wenye majivuno yatashushwa.

16 Yehova wa majeshi atakwezwa kupitia hukumu yake;*

Mungu wa kweli, Aliye Mtakatifu,+ atajitakasa mwenyewe kupitia uadilifu.+

17 Na wanakondoo watalisha kama katika malisho yao;

Wakaaji wageni watakula katika maeneo yenye ukiwa ya wanyama waliolishwa vizuri.

18 Ole wao wanaokokota hatia yao kwa kamba za udanganyifu

Na dhambi yao kwa kamba za gari la kukokotwa;

19 Wale wanaosema: “Na aharakishe kazi yake;

Na ije upesi ili tuione.

Kusudi la* Mtakatifu wa Israeli na litimizwe

Ili tulijue!”+

20 Ole wao wanaosema kwamba wema ni uovu na uovu ni wema,+

Wale wanaoweka giza badala ya nuru na nuru badala ya giza,

Wale wanaoweka uchungu badala ya utamu na utamu badala ya uchungu!

21 Ole wao walio na hekima katika macho yao wenyewe

Na walio na busara machoni pao wenyewe!+

22 Ole wao walio hodari katika kunywa divai

Na wanaume walio stadi katika kuchanganya vileo,+

23 Wale wanaomwondolea mwovu hatia kwa rushwa+

Na wanaomnyima haki mwadilifu!+

24 Kwa hiyo, kama mwali wa moto unavyoteketeza majani makavu

Na majani makavu yanavyonyauka katika moto,

Mizizi yao wenyewe itaoza,

Na maua yao yatatawanyika kama ungaunga,

Kwa sababu walikataa sheria* ya Yehova wa majeshi,

Na kulidharau neno la Mtakatifu wa Israeli.+

25 Ndiyo sababu hasira ya Yehova inawaka dhidi ya watu wake,

Naye ataunyoosha mkono wake dhidi yao na kuwapiga.+

Milima itatetemeka,

Na maiti zao zitakuwa kama takataka barabarani.+

Kwa sababu ya hayo yote, hasira yake haijapoa,

Lakini mkono wake bado umenyooshwa ili kupiga.

26 Ameliinulia ishara* taifa lililo mbali;+

Amewapigia mluzi waje kutoka miisho ya dunia;+

Na tazama! wanakuja upesi sana.+

27 Hakuna yeyote kati yao aliyechoka wala kujikwaa.

Hakuna yeyote anayesinzia au kulala.

Mshipi ulio kwenye kiuno chao haujalegezwa,

Wala kamba za viatu vyao hazijakatika.

28 Mishale yao yote ni mikali,

Na pinde zao zote zimepindika.*

Kwato za farasi wao ni kama jiwe gumu lenye makali,

Na magurudumu yao kama upepo wa dhoruba.+

29 Mngurumo wao ni kama wa simba;

Wananguruma kama wanasimba.*+

Watanguruma na kukamata mawindo

Na kuyabeba bila mtu wa kuyaokoa.

30 Siku hiyo watanguruma juu yake

Kama mngurumo wa bahari.+

Mtu yeyote anayeitazama nchi ataona giza lenye kutaabisha;

Hata nuru imetiwa giza kwa sababu ya mawingu.+

6 Katika mwaka ambao Mfalme Uzia alikufa,+ nilimwona Yehova akiwa ameketi kwenye kiti cha ufalme kilicho juu na kilichoinuliwa,+ na pindo za kanzu yake zilijaa hekaluni. 2 Maserafi walikuwa wamesimama juu yake; kila mmoja wao alikuwa na mabawa sita. Kila mmoja aliufunika uso wake kwa mabawa mawili na alifunika miguu yake kwa mawili, na kila mmoja wao aliruka huku na huku kwa mawili.

 3 Na kila mmoja alimwambia mwenzake:

“Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Yehova wa majeshi.+

Dunia yote imejaa utukufu wake.”

4 Na viegemeo vya milango vikatetemeka kwa sababu ya ile sauti kubwa,* na nyumba ikajaa moshi.+

 5 Kisha nikasema: “Ole wangu!

Kwa maana ni kama nimekufa,*

Kwa maana mimi ni mtu asiye na midomo safi,

Nami ninaishi kati ya watu wasio na midomo safi;+

Kwa maana macho yangu yamemwona Mfalme, Yehova wa majeshi mwenyewe!”

6 Ndipo mmoja wa maserafi akaruka kunijia, na mkononi mwake alikuwa na kaa linalowaka+ alilokuwa amechukua kwa koleo kutoka kwenye madhabahu.+ 7 Akakigusa kinywa changu na kusema:

“Tazama! Hili limeigusa midomo yako.

Hatia yako imeondolewa,

Na dhambi yako imefunikwa.”

8 Kisha nikasikia sauti ya Yehova ikiuliza: “Nimtume nani, na ni nani atakayeenda kwa ajili yetu?”+ Nami nikasema: “Mimi hapa! Nitume mimi!”+

 9 Ndipo akasema, “Nenda, uwaambie hivi watu hawa:

‘Mtasikia tena na tena,

Lakini hamtaelewa;

Mtaona tena na tena,

Lakini hamtapata ujuzi wowote.’+

10 Ufanye moyo wa watu hawa uwe mgumu,+

Yafanye masikio yao yawe mazito,+

Na uyafunge kabisa macho yao,

Ili wasione kwa macho yao

Na wasisikie kwa masikio yao,

Ili moyo wao usielewe

Nao wasigeuke na kuponywa.”

11 Ndipo nikauliza: “Ni mpaka lini, Ee Yehova?” Kisha akasema:

“Mpaka majiji yabomoke yawe magofu bila mkaaji

Na nyumba zisiwe na watu

Na nchi iharibiwe na kubaki ukiwa;+

12 Mpaka Yehova awaondoe watu na kuwapeleka mbali+

Na hali ya ukiwa ya nchi ienee sana.

13 “Lakini bado kutakuwa na sehemu ya kumi ndani yake, nayo itateketezwa tena, kama mti mkubwa na kama mwaloni, ambayo inapokatwa huacha kisiki; mbegu takatifu itakuwa* kisiki chake.”

7 Sasa katika siku za Ahazi+ mwana wa Yothamu mwana wa Uzia, mfalme wa Yuda, Mfalme Resini wa Siria na Peka+ mwana wa Remalia, mfalme wa Israeli, walipanda ili kuja kupigana vita dhidi ya Yerusalemu, lakini alishindwa* kuliteka.+ 2 Habari ikapelekwa kwa nyumba ya Daudi: “Siria imeungana na Efraimu.”

Na moyo wa Ahazi na moyo wa watu wake ukaanza kutetemeka, kama miti ya msituni inavyotikiswa na upepo.

3 Kisha Yehova akamwambia Isaya: “Tafadhali ondoka, wewe na mwana wako Shear-yashubu,*+ uende kukutana na Ahazi, kwenye mwisho wa mfereji* wa kidimbwi cha juu+ karibu na barabara kuu ya uwanja wa mfuaji wa nguo. 4 Umwambie, ‘Jitahidi kuwa mtulivu. Usiogope, na usivunjike moyo kwa sababu ya haya magogo mawili yanayotoa moshi, kwa sababu ya hasira kali ya Resini na Siria na mwana wa Remalia.+ 5 Kwa maana Siria pamoja na Efraimu na mwana wa Remalia wamepanga njama ya kukudhuru, wakisema: 6 “Na tupande dhidi ya Yuda na kuirarua* na kuishinda* iwe yetu, nasi tumweke mwana wa Tabeeli kuwa mfalme wake.”+

 7 “‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:

“Haitafanikiwa,

Wala haitatimia.

 8 Kwa maana kichwa cha Siria ni Damasko,

Na kichwa cha Damasko ni Resini.

Katika muda wa miaka 65 tu

Efraimu litavunjwa kabisa na halitakuwa taifa tena.+

 9 Kichwa cha Efraimu ni Samaria,+

Na kichwa cha Samaria ni mwana wa Remalia.+

Msipokuwa na imani thabiti,

Hamtakuwa imara.”’”

10 Yehova akaendelea kumwambia Ahazi: 11 “Mwombe Yehova Mungu wako+ ishara; inaweza kuwa yenye kina kama Kaburi* au iwe juu kama anga.” 12 Lakini Ahazi akasema: “Sitaomba, wala sitamjaribu Yehova.”

13 Kisha Isaya akasema: “Tafadhali, sikilizeni, enyi nyumba ya Daudi. Je, haitoshi kwamba mnaijaribu subira ya wanadamu? Je, ni lazima pia muijaribu subira ya Mungu?+ 14 Kwa hiyo Yehova mwenyewe atawapa ishara: Tazama! Mwanamke kijana* atapata mimba naye atazaa mwana,+ na kumwita jina Imanueli.*+ 15 Atakula siagi na asali kufikia wakati atakapojua jinsi ya kukataa lililo baya na kuchagua lililo jema. 16 Kwa maana kabla ya mvulana huyo kujua jinsi ya kukataa lililo baya na kuchagua lililo jema, nchi ya wale wafalme wawili mnaowahofu itaachwa kabisa.+ 17 Yehova ataleta dhidi yako na dhidi ya watu wako na dhidi ya nyumba ya baba yako wakati ambao haujawahi kuonekana tangu Efraimu lilipojitenga na Yuda,+ kwa maana Yeye atamleta mfalme wa Ashuru.+

18 “Siku hiyo Yehova atawapigia mluzi nzi kutoka katika vijito vya mbali vya Mto Nile wa Misri na nyuki kutoka katika nchi ya Ashuru, 19 nao wote watakuja na kutua kwenye mabonde yenye mteremko mkali,* kwenye mipasuko ya miamba, kwenye vichaka vyote vya miiba, na sehemu zote za kunyweshea.

20 “Siku hiyo, kwa kutumia wembe uliokodiwa kutoka eneo la ule Mto,* kwa kumtumia mfalme wa Ashuru,+ Yehova atanyoa kichwa na nywele za miguu, nao utafagilia mbali ndevu pia.

21 “Siku hiyo mtu atamhifadhi hai ng’ombe mchanga aliye kundini na kondoo wawili. 22 Na kwa sababu ya wingi wa maziwa, atakula siagi, kwa maana kila mtu anayebaki katika nchi atakula siagi na asali.

23 “Siku hiyo mahali popote palipokuwa na mizabibu 1,000 yenye thamani ya vipande 1,000 vya fedha, patakuwa na vichaka vya miiba na magugu peke yake. 24 Watu wataenda huko wakiwa na mishale na upinde, kwa sababu nchi yote itakuwa vichaka vya miiba na magugu. 25 Na milima yote iliyokuwa ikilimwa kwa jembe, hutaikaribia kwa kuogopa vichaka vya miiba na magugu; itakuwa mahali pa kulisha ng’ombe na mahali pa kukanyagwa na kondoo.”

8 Yehova akaniambia: “Chukua bamba kubwa+ na uandike juu yake kwa kalamu ya kawaida,* ‘Maher-shalal-hash-bazi.’* 2 Nami nihakikishe kwamba limethibitishwa kwa maandishi* na mashahidi waaminifu, kuhani Uria+ na Zekaria mwana wa Yeberekia.”

3 Ndipo nikalala na* yule nabii wa kike,* naye akapata mimba na baada ya muda akazaa mwana.+ Kisha Yehova akaniambia: “Mwite jina Maher-shalal-hash-bazi, 4 kwa maana kabla mvulana huyo hajajua jinsi ya kuita, ‘Baba yangu!’ na ‘Mama yangu!’ mali za Damasko na nyara za Samaria zitachukuliwa mbele ya mfalme wa Ashuru.”+

5 Yehova akaniambia tena:

 6 “Kwa sababu watu hawa wamekataa maji ya Shiloa* yanayotiririka polepole+

Nao wanamshangilia Resini na mwana wa Remalia,+

 7 Kwa hiyo tazama! Yehova ataleta dhidi yao

Maji yenye nguvu na yaliyo mengi ya ule Mto,*

Mfalme wa Ashuru+ na utukufu wake wote.

Atakuja juu ya sakafu zake zote za vijito

Na kufurika kwenye kingo zake zote

 8 Na kupita katika nchi yote ya Yuda.

Atafurika na kuvuka, na kufika shingoni;+

Mabawa yake yaliyonyooshwa yatajaza upana wa nchi yako,

Ewe Imanueli!”*+

 9 Sababisheni madhara, enyi watu, lakini mtavunjwa vipandevipande.

Sikilizeni, nyote mnaotoka sehemu za mbali za dunia!

Jitayarisheni kwa ajili ya vita,* lakini mtavunjwa vipandevipande!+

Jitayarisheni kwa ajili ya vita, lakini mtavunjwa vipandevipande!

10 Fanyeni mpango, lakini utavunjwa!

Semeni mnachotaka, lakini hakitafanikiwa,

Kwa maana Mungu yuko pamoja nasi!*+

11 Kwa mkono wake wenye nguvu ulio juu yangu, Yehova aliniambia hivi ili kunionya nisifuate njia ya watu hawa:

12 “Usikiite njama kitu ambacho watu hawa wanakiita njama!

Usiogope kitu wanachoogopa;

Usitetemeshwe nacho.

13 Yehova wa majeshi—Yeye ndiye mnayepaswa kumwona kuwa mtakatifu,+

Yeye ndiye mnayepaswa kumwogopa,

Na Yeye ndiye anayepaswa kuwatetemesha ninyi.”+

14 Atakuwa kama mahali patakatifu,

Lakini kama jiwe la kujigonga juu yake

Na kama mwamba wa kujikwaa juu yake+

Kwa nyumba zote mbili za Israeli,

Kama mtego na kama kitu kinachonasa

Kwa wakaaji wa Yerusalemu.

15 Wengi wao watajikwaa na kuanguka na kuvunjwa;

Watanaswa na kukamatwa.

16 Funga ule uthibitisho ulioandikwa,*

Tia muhuri sheria* kati ya wanafunzi wangu!

17 Nitaendelea kumtarajia* Yehova,+ ambaye anauficha uso wake kutoka kwa nyumba ya Yakobo,+ nami nitamtumainia.

18 Tazama! Mimi na watoto ambao Yehova amenipa+ ni kama ishara+ na kama miujiza katika Israeli kutoka kwa Yehova wa majeshi, anayekaa kwenye Mlima Sayuni.

19 Nao wakiwaambia: “Tafuteni habari kutoka kwa wale wanaowasiliana na roho au wabashiri wanaonong’oneza na kutoa sauti za chini,” je, watu hawapaswi kutafuta habari kutoka kwa Mungu wao? Je, wanapaswa kutafuta habari kutoka kwa wafu kwa ajili ya walio hai?+ 20 Badala yake, wanapaswa kutafuta habari katika sheria na uthibitisho ulioandikwa!*

Wasiposema kulingana na neno hili, hawana nuru.*+ 21 Na kila mtu atapita katika nchi akiteseka na akiwa na njaa;+ na kwa sababu ana njaa na ghadhabu, atamtukana mfalme wake na Mungu wake huku akitazama juu. 22 Kisha ataiangalia dunia na kuona taabu na giza peke yake, gizagiza na nyakati ngumu, na utusitusi bila mwangaza.

9 Hata hivyo, utusitusi huo hautakuwa kama nchi ilipokuwa na taabu, kama nyakati za zamani nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali zilipodharauliwa.+ Lakini baadaye Yeye ataifanya iheshimiwe—njia iliyo kando ya bahari, katika eneo la Yordani, Galilaya ya mataifa.

 2 Watu waliokuwa wakitembea gizani

Wameona nuru kuu.

Na wale wanaokaa katika nchi ya kivuli kizito,

Nuru imewaangazia.+

 3 Umelifanya taifa hilo liwe na watu wengi;

Umefanya shangwe yake iwe kubwa

Wanashangilia mbele zako

Kama watu wanavyoshangilia wakati wa mavuno,

Kama wale wanaogawana nyara kwa shangwe.

 4 Kwa maana umeivunjavunja nira ya mzigo wao,

Fimbo iliyo kwenye mabega yao, gongo la msimamizi wa kazi,

Kama katika siku ya Midiani.+

 5 Kila kiatu cha askari kinachotikisa dunia kinapopiga mwendo

Na kila vazi lililoloweshwa katika damu

Litakuwa kuni kwa ajili ya moto.

 6 Kwa maana mtoto amezaliwa kwetu,+

Tumepewa mwana

Na utawala* utakaa juu ya bega lake.+

Jina lake litakuwa Mshauri wa Ajabu,+ Mungu Mwenye Nguvu,+ Baba wa Milele, Mkuu wa Amani.

 7 Kwa wingi wa utawala wake*

Na amani, hakutakuwa na mwisho,+

Kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ na juu ya ufalme wake

Ili kuuimarisha kabisa+ na kuutegemeza

Kupitia haki+ na uadilifu,+

Kuanzia sasa mpaka milele.

Bidii ya Yehova wa majeshi itafanya hayo.

 8 Yehova alituma neno dhidi ya Yakobo,

Nalo limekuja dhidi ya Israeli.+

 9 Na watu wote watalijua

—Efraimu na wakaaji wa Samaria—

Ambao wanasema kwa kiburi chao na mioyo yao yenye dharau:

10 “Matofali yameanguka,

Lakini tutajenga kwa mawe yaliyochongwa.+

Mikuyu imekatwa,

Lakini tutaweka mierezi badala yake.”

11 Yehova atawainua wapinzani wa Resini dhidi yake

Naye atawachochea maadui wake wachukue hatua,

12 Siria kutoka mashariki na Wafilisti kutoka magharibi,*+

Watamnyafua Israeli kwa vinywa vilivyo wazi.+

Kwa sababu ya hayo yote, hasira yake haijapoa,

Lakini mkono wake bado umenyooshwa ili kupiga.+

13 Kwa maana watu hawajarudi kwa Yule anayewapiga;

Hawajamtafuta Yehova wa majeshi.+

14 Yehova atakata kabisa kutoka Israeli

Kichwa na mkia, chipukizi na utete,* katika siku moja.+

15 Mzee na anayeheshimiwa sana ndiye kichwa,

Na nabii anayetoa mafundisho ya uwongo ndiye mkia.+

16 Wale wanaowaongoza watu hawa wanawafanya watangetange;

Na wale wanaoongozwa wamevurugika.

17 Ndiyo sababu Yehova hatawashangilia vijana wao,

Naye hatawaonyesha rehema mayatima wao na wajane wao;

Kwa sababu wote ni waasi imani na watenda maovu+

Na kila kinywa kinasema kwa upumbavu.

Kwa sababu ya hayo yote, hasira yake haijapoa,

Lakini mkono wake bado umenyooshwa ili kupiga.+

18 Kwa maana uovu unawaka kama moto,

Ukiteketeza vichaka vya miiba na magugu.

Utawasha moto vichaka vya msitu,

Navyo vitapanda juu katika mawingu ya moshi.

19 Katika ghadhabu ya Yehova wa majeshi

Nchi imewashwa moto,

Na watu watakuwa kuni kwa ajili ya huo moto.

Hakuna yeyote atakayemhurumia hata ndugu yake.

20 Mtu atakata upande wa kulia

Lakini bado atakuwa na njaa,

Na mtu atakula upande wa kushoto

Lakini hatashiba.

Kila mtu atainyafua nyama ya mkono wake mwenyewe,

21 Manase atamnyafua Efraimu,

Na Efraimu atamnyafua Manase.

Wote pamoja watapigana na Yuda.+

Kwa sababu ya hayo yote, hasira yake haijapoa,

Lakini mkono wake bado umenyooshwa ili kupiga.+

10 Ole wao wanaotunga sheria zinazodhuru,*+

Ambao sikuzote huandika amri zinazokandamiza,

 2 Ili kuwanyima maskini haki zao za kisheria,

Ili kuwanyang’anya haki watu wa hali ya chini kati ya watu wangu,+

Kuwafanya wajane kuwa nyara yao

Na kuwapora mayatima!+

 3 Mtafanya nini katika siku ya kuadhibiwa,*+

Uharibifu utakapokuja kutoka mbali?+

Mtamkimbilia nani ili kupata msaada+

Nanyi mtauacha wapi utajiri* wenu?

 4 Hakuna kinachobaki isipokuwa kujikunyata kati ya wafungwa

Au kuanguka kati ya waliouawa.

Kwa sababu ya hayo yote, hasira yake haijapoa,

Lakini mkono wake bado umenyooshwa ili kupiga.+

 5 “Aha! Mwashuru,+

Fimbo ya kuonyesha hasira yangu,+

Na gongo lililo mkononi mwao kwa ajili ya shutuma yangu!

 6 Nitamtuma yeye dhidi ya taifa lililoasi imani,+

Dhidi ya watu walionikasirisha,

Nitamwamuru achukue nyara nyingi na kupora mali nyingi

Na kuzikanyaga kama matope barabarani.+

 7 Lakini hatataka kufanya hivyo

Na moyo wake hautapanga hila kwa njia hiyo;

Kwa maana moyo wake umeazimia kuangamiza

Kuangamiza kabisa mataifa mengi, si machache.

 8 Kwa maana anasema,

‘Je, wakuu wangu wote si wafalme?+

 9 Je, Kalno+ si kama tu Karkemishi?+

Je, Hamathi+ si kama Arpadi?+

Je, Samaria+ si kama Damasko?+

10 Mkono wangu umeziteka falme za miungu ya ubatili,

Ambazo sanamu zao za kuchongwa zilikuwa nyingi kuliko zile za Yerusalemu na Samaria!+

11 Je, sitaitendea pia Yerusalemu na sanamu zake

Kama vile nilivyoitendea Samaria na miungu yake ya ubatili?’+

12 “Yehova atakapomaliza kazi yake yote kwenye Mlima Sayuni na Yerusalemu, atamwadhibu* mfalme wa Ashuru kwa sababu ya moyo wake wenye dharau na macho yake yanayotazama kwa kiburi na majivuno.+ 13 Kwa maana anasema,

‘Nitafanya hivyo kwa nguvu za mkono wangu

Na kwa hekima yangu, kwa maana nina hekima.

Nitaiondoa mipaka ya mataifa+

Na kupora hazina zao,+

Nami nitawatiisha wakaaji kama mwenye nguvu.+

14 Kama mtu anayeingiza mkono katika kiota,

Mkono wangu utateka mali za mataifa;

Na kama mtu anayekusanya mayai yaliyoachwa,

Nitaikusanya dunia nzima!

Hakuna atakayepiga mabawa yake au kufungua kinywa chake wala kunong’oneza.’”

15 Je, shoka litajikweza juu ya yule anayelitumia kukata?

Je, msumeno utajikweza juu ya yule anayeutumia kukata?

Je, gongo+ linaweza kumtikisa yule anayeliinua?

Au je, fimbo inaweza kumwinua yule ambaye hajatengenezwa kwa mbao?

16 Kwa hiyo Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi,

Atawafanya watu wake walionenepa wakonde,+

Na chini ya utukufu wake atawasha moto mkubwa unaoteketeza.+

17 Nuru+ ya Israeli itakuwa moto,+

Na Mtakatifu wake mwali wa moto;

Utawaka na kuteketeza magugu yake na vichaka vyake vya miiba kwa siku moja.

18 Ataondoa kabisa* utukufu wa msitu wake na shamba lake la matunda;

Itakuwa kama mtu mgonjwa anavyodhoofika.+

19 Miti itakayobaki katika msitu wake

Itakuwa michache sana hivi kwamba mvulana ataweza kuihesabu.

20 Siku hiyo watu wa Israeli waliobaki

Na waliookoka wa nyumba ya Yakobo

Hawatamtegemea tena yule aliyewapiga;+

Bali watamtegemea Yehova,

Mtakatifu wa Israeli, kwa uaminifu.

21 Ni watu wachache tu waliobaki watakaorudi,

Watu wa Yakobo waliobaki, watarudi kwa Mungu Mwenye Nguvu.+

22 Kwa maana ingawa watu wako, ewe Israeli,

Ni kama chembe za mchanga wa bahari,

Ni watu wachache tu waliobaki watakaorudi.+

Maangamizi yameamuliwa,+

Na haki* itawafunika.+

23 Naam, maangamizi yaliyoamuliwa na Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi,

Yatatekelezwa katika nchi yote.+

24 Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, anasema: “Msiogope, watu wangu mnaokaa Sayuni, kwa sababu ya Mwashuru, aliyekuwa akiwapiga kwa fimbo+ na kuinua gongo lake dhidi yenu kama Misri ilivyofanya.+ 25 Kwa maana kwa muda mfupi sana shutuma itafika mwisho; hasira yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.+ 26 Yehova wa majeshi atatikisa mjeledi dhidi yake,+ kama aliposhinda Midiani kando ya mwamba wa Orebu.+ Na gongo lake litakuwa juu ya bahari, naye ataliinua kama alivyoitendea Misri.+

27 “Siku hiyo mzigo wake utaondoka juu ya bega lako,+

Na nira yake itaondoka kwenye shingo yako,+

Na nira itavunjwa+ kwa sababu ya mafuta.”

28 Amekuja Aiathi;+

Amepitia Migroni;

Ameweka mizigo yake huko Mikmashi.+

29 Wamevuka kivuko;

Wamekaa Geba usiku kucha;+

Rama inatetemeka, Gibea+ ya Sauli imekimbia.+

30 Paza sauti yako na upige mayowe, Ee binti ya Galimu!

Sikiliza, Ee Laisha!

Ewe maskini Anathothi!+

31 Madmena amekimbia.

Wakaaji wa Gebimu wametafuta mahali pa kujificha.

32 Leo hiihii atasimama Nobu.+

Anautikisia ngumi mlima wa binti ya Sayuni,

Kilima cha Yerusalemu.

33 Tazama! Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi,

Anakata matawi kwa kishindo kikubwa sana;+

Miti mirefu zaidi inakatwa,

Na walio juu wanashushwa.

34 Anapiga vichaka vya msitu kwa kifaa cha chuma,*

Na Lebanoni utaangushwa na mwenye nguvu.

11 Na tawi+ litakua kutoka kwenye kisiki cha Yese,+

Na chipukizi+ kutoka kwenye mizizi yake litazaa matunda.

 2 Na roho ya Yehova itatua juu yake,+

Roho ya hekima+ na ya uelewaji,

Roho ya shauri na ya nguvu,+

Roho ya ujuzi na ya kumwogopa Yehova.

 3 Naye atafurahia kumwogopa Yehova.+

Hatahukumu kwa mambo anayoona kwa macho yake,

Wala kukaripia kulingana tu na mambo anayosikia kwa masikio yake.+

 4 Atawahukumu kwa haki* watu wa hali ya chini,

Na kwa unyoofu atakaripia kwa ajili ya wapole wa dunia.

Ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake+

Na kuwaua waovu kwa pumzi* ya midomo yake.+

 5 Uadilifu utakuwa mshipi kiunoni mwake,

Na uaminifu mshipi wa kiuno chake.+

 6 Mbwamwitu atakaa pamoja na mwanakondoo kwa muda fulani,+

Na chui atalala pamoja na mwanambuzi,

Na ndama na simba* na mnyama aliyenoneshwa wote watakuwa pamoja;*+

Na mvulana mdogo atawaongoza.

 7 Ng’ombe na dubu watakula pamoja,

Na watoto wao watalala pamoja.

Simba atakula majani kama ng’ombe dume.+

 8 Na mtoto anayenyonya atacheza juu ya shimo la swila,

Na mtoto aliyeachishwa kunyonya atatia mkono wake juu ya shimo la nyoka mwenye sumu.

 9 Hawatasababisha madhara yoyote+

Wala uharibifu wowote katika mlima wangu wote mtakatifu,+

Kwa maana kwa hakika dunia itajaa ujuzi kumhusu Yehova

Kama maji yanavyoifunika bahari.+

10 Siku hiyo mzizi wa Yese+ utasimama kama ishara* kwa ajili ya mataifa.+

Mataifa yatatafuta mwongozo kutoka kwake,*+

Na mahali pake pa kupumzikia patakuwa na utukufu.

11 Siku hiyo Yehova ataunyoosha tena mkono wake, mara ya pili, ili kuwakomboa watu wake waliobaki kutoka Ashuru,+ kutoka Misri,+ kutoka Pathrosi,+ kutoka Kushi,+ kutoka Elamu,+ kutoka Shinari,*+ kutoka Hamathi, na kutoka katika visiwa vya bahari. 12 Atainua ishara* kwa ajili ya mataifa na kuwakusanya watu wa Israeli+ waliotawanywa, na watu wa Yuda waliotawanywa atawakusanya pamoja kutoka katika pembe nne za dunia.+

13 Wivu wa Efraimu utakuwa umetoweka,+

Na wale wanaomwonyesha Yuda uadui wataangamizwa.

Efraimu hatamwonea Yuda wivu,

Wala Yuda hatamwonyesha Efraimu uadui.+

14 Nao watashuka chini kwa ghafla kwenye miteremko ya* Wafilisti upande wa magharibi;

Wakiwa pamoja watawapora watu wa Mashariki.

Wataunyoosha mkono wao dhidi ya* Edomu+ na Moabu,+

Na Waamoni watakuwa raia wao.+

15 Yehova ataigawanya* ghuba ya* bahari ya Misri+

Na kuutikisa mkono wake juu ya ule Mto.*+

Kwa pumzi* yake inayounguza ataipiga katika vijito vyake saba,*

Naye atawafanya watu watembee na kuvuka wakiwa wamevaa viatu vyao.

16 Na kutakuwa na barabara kuu+ kutoka Ashuru kwa ajili ya watu wake waliobaki,+

Kama ilivyokuwa kwa ajili ya Israeli siku aliyotoka nchini Misri.

12 Siku hiyo hakika utasema:

“Ninakushukuru, Ee Yehova,

Kwa maana ingawa ulinikasirikia,

Hasira yako ilipoa hatua kwa hatua, nawe ukanifariji.+

 2 Tazama! Mungu ni wokovu wangu.+

Nitamtumaini nami sitaogopa;+

Kwa maana Yah* Yehova ni nguvu zangu na uwezo wangu,

Naye amekuwa wokovu wangu.”+

 3 Mtateka maji kwa kushangilia

Kutoka kwenye chemchemi za wokovu.+

 4 Na siku hiyo mtasema:

“Mshukuruni Yehova, liitieni jina lake,

Yajulisheni mataifa matendo yake!+

Tangazeni kwamba jina lake limekwezwa.+

 5 Mwimbieni sifa* Yehova+ kwa maana ametenda mambo makuu.+

Jambo hilo na litangazwe duniani kote.

 6 “Paza sauti na upige kelele kwa shangwe, ewe mkaaji* wa Sayuni,

Kwa maana Mtakatifu wa Israeli ni mkuu katikati yako.”

13 Tangazo dhidi ya Babiloni,+ ambalo Isaya+ mwana wa Amozi aliona katika maono:

 2 “Simamisheni ishara*+ juu ya mlima wa miamba isiyo na kitu.

Wapazieni sauti, wapungieni mkono,

Ili waingie katika milango ya watu wenye vyeo.

 3 Nimewapa amri wale ambao nimewaweka rasmi.*+

Nimewaita mashujaa wangu ili kuonyesha hasira yangu,

Watu wangu wanaoshangilia kwa majivuno.

 4 Sikilizeni! Umati milimani;

Ni kama sauti ya watu wengi sana!

Sikilizeni! Ghasia za falme,

Za mataifa yaliyokusanyika pamoja!+

Yehova wa majeshi anakusanya jeshi kwa ajili ya vita.+

 5 Wanakuja kutoka nchi ya mbali,+

Kutoka mwisho wa mbingu,

Yehova na silaha za ghadhabu yake,

Ili kuiangamiza dunia yote.+

 6 Ombolezeni kwa sauti, kwa maana siku ya Yehova iko karibu!

Itakuja kama maangamizi kutoka kwa Mweza-Yote.+

 7 Ndiyo maana mikono yote italegea,

Na moyo wa kila mwanadamu utayeyuka kwa woga.+

 8 Watu wameshikwa na wasiwasi.+

Wanafurukuta na kushikwa na uchungu,

Kama mwanamke anayezaa.

Wanatazamana kwa hofu,

Wakiwa na nyuso zinazowaka kwa maumivu.

 9 Tazama! Siku ya Yehova inakuja,

Ikiwa na ukali na ghadhabu na hasira inayowaka,

Ili kuifanya nchi iwe kitu cha kutisha,+

Na kuwaangamiza watenda dhambi wa nchi kutoka ndani yake.

10 Kwa maana nyota za mbinguni na makundi yake ya nyota*+

Hazitatoa nuru yake;

Jua litakuwa na giza linapochomoza,

Nao mwezi hautatoa mwanga wake.

11 Nitaiadhibu* dunia inayokaliwa kwa sababu ya ubaya wake,+

Na waovu kwa sababu ya uovu wao.

Nitakikomesha kiburi cha wenye kimbelembele,

Nami nitayashusha majivuno ya waonevu.+

12 Nitamfanya mwanadamu anayeweza kufa kuwa haba kuliko dhahabu safi,+

Na wanadamu kuwa haba kuliko dhahabu ya Ofiri.+

13 Ndiyo maana nitazifanya mbingu zitetemeke

Na dunia itatikiswa itoke mahali pake+

Kwa sababu ya ghadhabu ya Yehova wa majeshi katika siku ya hasira yake inayowaka.

14 Kama swala anayewindwa na kama kondoo wasio na mtu wa kuwakusanya

Kila mtu atarudi kwa watu wake mwenyewe;

Kila mtu atakimbilia nchi yake mwenyewe.+

15 Yeyote atakayepatikana atachomwa kwa silaha,

Na yeyote atakayekamatwa atauawa kwa upanga.+

16 Watoto wao watavunjwa vipandevipande mbele ya macho yao,+

Nyumba zao zitaporwa,

Na wake zao watabakwa.

17 Tazama, ninawainua Wamedi dhidi yao,+

Ambao hawaioni fedha kuwa kitu

Na ambao hawapendezwi na dhahabu.

18 Pinde zao zitawavunjavunja vijana;+

Hawatausikitikia uzao wa tumbo

Wala kuwahurumia watoto.

19 Na Babiloni, ufalme wenye utukufu zaidi,*+

Uzuri na fahari ya Wakaldayo,+

Litakuwa kama Sodoma na Gomora yalipoangamizwa na Mungu.+

20 Halitakaliwa kamwe,

Wala halitakuwa makao ya watu kwa vizazi vyote.+

Hakuna Mwarabu atakayepiga hema lake huko,

Na hakuna wachungaji watakaopumzisha mifugo yao huko.

21 Viumbe wa jangwani watalala huko;

Nyumba zao zitajaa bundi-tai.

Mbuni watakaa huko,+

Mbuzi wa mwituni* watarukaruka huko.

22 Wanyama wanaopiga mayowe watalia kwa sauti katika minara yake,

Na mbwamwitu katika majumba yake ya kifahari.

Wakati wake umekaribia, na siku zake hazitarefushwa.”+

14 Kwa maana Yehova atamwonyesha rehema Yakobo,+ naye atawachagua tena Waisraeli.+ Atawafanya waishi* katika nchi yao,+ na wakaaji wageni watajiunga nao na kushikamana na nyumba ya Yakobo.+ 2 Na watu watawachukua na kuwaleta mahali pao wenyewe, na nyumba ya Israeli itawamiliki katika nchi ya Yehova wakiwa watumishi wa kiume na wa kike;+ nao watawateka wale waliokuwa wamewateka, nao watawatiisha wale waliokuwa wakiwalazimisha kufanya kazi.*

3 Siku ambayo Yehova atakupumzisha kutokana na uchungu wako na kutokana na msukosuko wako na kutokana na utumwa mgumu uliowekwa chini yake,+ 4 utaisema methali* hii dhidi ya mfalme wa Babiloni:

“Jinsi yule anayewalazimisha wengine kufanya kazi* alivyofikia mwisho wake!

Jinsi ukandamizaji ulivyokwisha!+

 5 Yehova ameivunja fimbo ya waovu,

Gongo la watawala,+

 6 Yule anayewapiga watu kwa hasira kwa mapigo yasiyokoma,+

Yule anayeyatiisha mataifa kwa hasira kwa mateso yasiyoisha.+

 7 Dunia nzima imepumzika sasa, haina usumbufu.

Watu wanapaza sauti kwa shangwe.+

 8 Hata miberoshi inakushangilia,

Pamoja na mierezi ya Lebanoni.

Inasema, ‘Tangu ulipoanguka,

Hakuna mkataji wa miti anayekuja kutukata.’

 9 Hata Kaburi* chini limevurugika

Ili likupokee utakapoingia.

Kwa sababu yako, linawaamsha wale waliokufa ambao hawana uwezo,

Viongozi wote wa dunia wanaokandamiza.*

Linawafanya wafalme wote wa mataifa wasimame kutoka kwenye viti vyao vya ufalme.

10 Wote wanaanza kusema na kukuambia,

‘Je, wewe pia umedhoofika kama sisi?

Je, umekuwa kama sisi?

11 Kiburi chako kimeshushwa chini mpaka Kaburini,*

Sauti ya vinanda vyako.+

Funza wametandikwa chini yako kama kitanda,

Na blanketi lako ni minyoo.’

12 Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni,

Ewe unayeng’aa, mwana wa mapambazuko!

Jinsi ulivyokatwa ukaangushwa duniani,

Wewe uliyeyashinda mataifa!+

13 Ulisema moyoni mwako, ‘Nitapanda juu mbinguni.+

Nitakiinua kiti changu cha ufalme juu ya nyota za Mungu,+

Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano,

Katika sehemu za mbali zaidi za kaskazini.+

14 Nitaenda juu ya mawingu;

Nitajifananisha na Aliye Juu Zaidi.’

15 Badala yake, utashushwa chini mpaka Kaburini,*

Katika sehemu zenye kina zaidi za shimo.

16 Wale wanaokuona watakukodolea macho;

Watakuchunguza kwa makini, wakisema,

‘Je, huyu ndiye yule mtu aliyekuwa akiitikisa dunia,

Aliyekuwa akizitetemesha falme,+

17 Aliyeifanya dunia inayokaliwa iwe kama nyika

Na kuyapindua majiji yake,+

Aliyekataa kuwaruhusu wafungwa wake waende nyumbani?’+

18 Wafalme wengine wote wa mataifa,

Naam, wote, wamelala chini katika utukufu,

Kila mmoja katika kaburi lake* mwenyewe.

19 Lakini wewe, umetupwa bila kaburi,

Kama chipukizi* lililochukiwa,

Ukiwa umevishwa watu waliouawa kwa kuchomwa upanga,

Wanaoshuka chini kwenye mawe ya shimoni,

Kama mzoga uliokanyagiwa chini kwa miguu.

20 Hutaungana nao kaburini,

Kwa maana uliiharibu nchi yako mwenyewe,

Uliwaua watu wako mwenyewe.

Uzao wa watenda maovu hautatajwa tena kamwe.

21 Tayarisheni ubao wa kuwachinjia wanawe

Kwa sababu ya hatia ya mababu zao,

Ili wasiinuke na kuimiliki dunia

Na kuyajaza majiji yao katika nchi.”

22 “Nitainuka dhidi yao,”+ asema Yehova wa majeshi.

“Nami nitafuta kabisa kutoka Babiloni jina na watu waliobaki na watoto na wazao,”+ asema Yehova.

23 “Nami nitamfanya kuwa makao ya nungunungu na eneo lenye umajimaji, nami nitamfagia kwa ufagio wa maangamizi,”+ asema Yehova wa majeshi.

24 Yehova wa majeshi ameapa hivi:

“Kama nilivyokusudia, ndivyo itakavyotukia,

Na kama nilivyoamua, ndivyo itakavyotimia.

25 Nitamponda Mwashuru katika nchi yangu

Nami nitamkanyaga-kanyaga kwenye milima yangu.+

Nira yake itaondolewa juu yao,

Na mzigo wake utaondolewa juu ya bega lao.”+

26 Hili ndilo jambo lililoamuliwa* dhidi ya dunia yote,

Na huu ndio mkono ulionyooshwa* dhidi ya mataifa yote.

27 Kwa maana Yehova wa majeshi ameamua,

Na ni nani anayeweza kulizuia?+

Mkono wake umenyooshwa,

Ni nani anayeweza kuurudisha nyuma?+

28 Katika mwaka ambao Mfalme Ahazi alikufa,+ tangazo hili lilitolewa:

29 “Usishangilie, ewe Ufilisti, yeyote kati yenu,

Kwa sababu tu gongo la yule anayewapiga limevunjwa.

Kwa maana kwenye mzizi wa nyoka+ atatoka nyoka mwenye sumu,+

Na uzao wake utakuwa nyoka wa moto arukaye.*

30 Huku wazaliwa wa kwanza wa watu wa hali ya chini wakila

Na maskini wakilala kwa usalama,

Nitauua mzizi wako kwa njaa kali,

Na kile kitakachobaki kwako kitauawa.+

31 Omboleza kwa sauti, ewe lango! Paza kilio, ewe jiji!

Ninyi nyote mtavunjika moyo, ewe Ufilisti!

Kwa maana moshi unakuja kutoka kaskazini,

Na hakuna wavivu katika vikosi vyake.”

32 Watawajibuje wajumbe wa taifa lile?

Kwamba Yehova ameuweka msingi wa Sayuni,+

Na kwamba watu wa hali ya chini kati ya watu wake watakimbilia ndani yake.

15 Tangazo dhidi ya Moabu:+

Kwa sababu limeharibiwa kwa usiku mmoja,

Jiji la Ari+ la Moabu limenyamazishwa.

Kwa sababu limeharibiwa kwa usiku mmoja,

Jiji la Kiri+ la Moabu limenyamazishwa.

 2 Amepanda mpaka kwenye Nyumba* na mpaka Diboni,+

Kwenye mahali pa juu ili kulia.

Moabu inaombolezea Nebo+ na Medeba.+

Kila kichwa kimenyolewa upara,+ ndevu zote zimenyolewa.+

 3 Wamevaa nguo za magunia katika barabara zake.

Kwenye paa zao na katika viwanja vyao vya jiji, wote wanaomboleza kwa sauti;

Wanashuka chini wakilia.+

 4 Heshboni na Eleale+ wanalia kwa sauti;

Sauti yao inasikika mpaka Yahazi.+

Ndiyo sababu watu wenye silaha wa Moabu wanaendelea kupaza sauti.

Anatetemeka.*

 5 Moyo wangu unamlilia Moabu.

Wakimbizi wake wamekimbia mpaka Soari+ na Eglath-shelishiya.+

Kwenye njia inayopanda kwenda Luhithi wanalia wakipanda;

Kwenye njia ya kwenda Horonaimu wanalia kwa sauti kwa sababu ya msiba.+

 6 Kwa maana maji ya Nimrimu yamekuwa ukiwa;

Majani mabichi yamekauka,

Majani yamekwisha na hakuna chochote kibichi kilichobaki.

 7 Ndiyo sababu wanabeba kilichobaki katika maghala yao na utajiri wao;

Wanavuka bonde* la mierebi.

 8 Kwa maana kilio kinasikika katika eneo lote la Moabu.+

Maombolezo yanafika Eglaimu;

Maombolezo yanafika Beer-elimu.

 9 Kwa maana maji ya Dimoni yamejaa damu,

Nami nina mengi zaidi kwa ajili ya Dimoni:

Simba kwa ajili ya watu wa Moabu wanaoponyoka

Na kwa ajili ya wale wanaobaki nchini.+

16 Pelekeni kondoo dume kwa mtawala wa nchi,

Kutoka Sela kupitia nyikani

Mpaka kwenye mlima wa binti ya Sayuni.

 2 Kama ndege aliyefukuzwa kwenye kiota chake,+

Ndivyo mabinti wa Moabu watakavyokuwa kwenye vivuko vya Arnoni.+

 3 “Toeni shauri, tekelezeni uamuzi.

Fanya kivuli chako cha adhuhuri kiwe kama usiku.

Wafiche waliotawanyika na usiwasaliti wale wanaokimbia.

 4 Watu wangu waliotawanyika na wakae ndani yako, Ee Moabu.

Uwe maficho kwao kwa sababu ya mwangamizaji.+

Mkandamizaji ataufikia mwisho wake,

Uharibifu utafikia mwisho,

Na wale wanaowakanyaga wengine wataangamia kutoka duniani.

 5 Kisha kiti cha ufalme kitaimarishwa kabisa katika upendo mshikamanifu.

Yule anayekikalia katika hema la Daudi atakuwa mwaminifu;+

Atahukumu kwa haki na kutekeleza uadilifu upesi.”+

 6 Tumesikia kuhusu kiburi cha Moabu—ana kiburi sana+—

Majivuno yake na kiburi chake na ghadhabu yake;+

Lakini maneno yake matupu yatakuwa ya bure.

 7 Basi Moabu atamwombolezea Moabu;

Wote wataomboleza.+

Wale waliopigwa wataomboleza kwa sababu ya keki za zabibu kavu za Kir-haresethi.+

 8 Kwa maana matuta ya Heshboni+ yamenyauka.

Mzabibu wa Sibma,+

Watawala wa mataifa wameyakanyaga matawi yake mekundu sana;*

Walikuwa wamefika mpaka Yazeri;+

Walikuwa wameenea mpaka nyikani.

Machipukizi yake yalikuwa yameenea mpaka baharini.

 9 Hiyo ndiyo sababu nitaulilia mzabibu wa Sibma kama ninavyolilia Yazeri.

Machozi yangu yatakulowesha ewe Heshboni na Eleale,+

Kwa sababu vigelegele vya matunda yako ya kiangazi na vya mavuno yako vimekoma.*

10 Furaha na shangwe zimeondolewa katika shamba la matunda,

Na hakuna nyimbo za shangwe au vigelegele katika mashamba ya mizabibu.+

Anayekanyaga hakanyagi tena divai katika mashinikizo,

Kwa maana nimekomesha vigelegele.+

11 Ndiyo sababu nina msukosuko ndani yangu kwa ajili ya Moabu,+

Kama kinubi kinapopigwa,

Na sehemu yangu ya ndani kabisa kwa ajili ya Kir-haresethi.+

12 Hata Moabu akijichosha mahali pa juu na kwenda kusali katika patakatifu pake, hatatimiza lolote.+

13 Hilo ndilo neno ambalo Yehova alisema awali kuhusu Moabu. 14 Na sasa Yehova anasema: “Katika muda wa miaka mitatu, kama miaka ya kibarua,* utukufu wa Moabu utafedheheshwa kwa vurugu nyingi za kila aina, na wale watakaobaki watakuwa wachache sana na wanyonge.”+

17 Tangazo dhidi ya Damasko:+

“Tazama! Damasko halitakuwa jiji tena,

Nalo litakuwa rundo la magofu.+

 2 Majiji ya Aroeri+ yataachwa;

Yatakuwa mahali ambapo mifugo italala

Na hakuna yeyote atakayeiogopesha.

 3 Majiji yenye ngome yatatoweka Efraimu,+

Na ufalme kutoka Damasko;+

Na wale wanaobaki wa Siria

Watakuwa kama utukufu wa Waisraeli,”* asema Yehova wa majeshi.

 4 “Siku hiyo utukufu wa Yakobo utafifia,

Na mwili wake wenye afya utakonda.*

 5 Itakuwa kama mvunaji anapovuna nafaka iliyo shambani

Na mkono wake unapovuna masuke ya nafaka,

Kama mtu anayeokota masalio ya nafaka katika Bonde la* Refaimu.+

 6 Ni masalio tu yatakayobaki,

Kama mzeituni unapopigwa:

Ni zeituni mbili au tatu tu zilizoiva zinazobaki kwenye tawi refu zaidi,

Ni nne au tano tu kwenye matawi yanayozaa matunda,”+ asema Yehova Mungu wa Israeli.

7 Siku hiyo mwanadamu atamtazama Muumba wake, na macho yake yatamtazama Mtakatifu wa Israeli. 8 Hatazitazama madhabahu,+ kazi ya mikono yake;+ naye hatatazama kile ambacho vidole vyake vimetengeneza, iwe ni miti mitakatifu* au vinara vya uvumba.

 9 Siku hiyo majiji yake yenye ngome yatakuwa kama mahali palipoachwa mwituni,+

Kama tawi lililoachwa mbele ya Waisraeli;

Litakuwa ukiwa.

10 Kwa maana umemsahau Mungu+ wa wokovu wako;

Hukumkumbuka Mwamba+ wa ngome yako.

Ndiyo sababu unapanda mashamba makubwa maridadi*

Na kupanda humo chipukizi la mgeni.*

11 Mchana unalizungushia shamba lako ua kwa uangalifu,

Asubuhi unachipusha mbegu zako,

Lakini mavuno yatatoweka katika siku ya ugonjwa na maumivu yasiyoweza kuponywa.+

12 Sikilizeni! Kuna vurugu za watu wengi,

Walio na msukosuko kama wa bahari!

Kuna kelele za mataifa,

Ambao sauti yao ni kama mngurumo wa maji yenye nguvu!

13 Mataifa yatatoa sauti kama mngurumo wa maji mengi.

Atayakemea, nayo yatakimbia mbali sana,

Yakifukuzwa kama makapi ya milima mbele ya upepo

Kama mchongoma unaopeperushwa na* upepo wa dhoruba.

14 Jioni kuna tisho la ghafla.

Kabla ya asubuhi hayapo tena.

Hilo ndilo fungu la wale wanaotupora

Na kura ya wale wanaotunyang’anya mali zetu.

18 Ole wa nchi ya wadudu wenye mabawa yanayovuma

Katika eneo la mito ya Ethiopia!+

 2 Inatuma wajumbe kupitia baharini,

Wanaovuka maji katika vyombo vya mafunjo, ikisema:

“Nendeni, enyi wajumbe wenye mbio,

Kwa taifa lenye watu warefu na walio na ngozi laini,*

Kwa watu wanaoogopwa kila mahali,+

Kwa taifa lenye nguvu, linaloshinda,*

Ambalo nchi yake imefagiliwa na mito.”

 3 Enyi wakaaji wote wa nchi nanyi wakaaji wa dunia,

Mtakachoona kitakuwa kama ishara* iliyoinuliwa juu ya milima,

Nanyi mtasikia sauti kama ya pembe inapopigwa.

 4 Kwa maana Yehova aliniambia hivi:

“Nitaendelea kutulia na kutazama* mahali pangu palipofanywa imara,

Kama joto linalometameta pamoja na mwangaza wa jua,

Kama wingu la umande katika joto la mavuno.

 5 Kwa maana kabla ya mavuno,

Ua linapokamilika na kuwa zabibu inayoiva,

Machipukizi yake yatakatwa kwa miundu

Vikonyo vitakatwa na kuondolewa.

 6 Wote wataachwa waliwe na ndege wanaowinda wa milimani

Na wanyama wa duniani.

Ndege wanaowinda watawala wakati wa kiangazi,

Na wanyama wote wa dunia watawala wakati wa mavuno.

 7 Wakati huo zawadi italetwa kwa Yehova wa majeshi,

Kutoka kwa taifa lenye watu warefu na walio na ngozi laini,*

Kutoka kwa watu wanaoogopwa kila mahali,

Kutoka kwa taifa lenye nguvu, linaloshinda,*

Ambalo nchi yake imefagiliwa na mito,

Mpaka mahali pa jina la Yehova wa majeshi, Mlima Sayuni.”+

19 Tangazo dhidi ya Misri:+

Tazama! Yehova amepanda juu ya wingu linaloenda kwa kasi, naye anakuja Misri.

Miungu ya ubatili ya Misri itatetemeka mbele zake,+

Na moyo wa Misri utayeyuka ndani yake.

 2 “Nitawachochea Wamisri dhidi ya Wamisri,

Nao watapigana,

Kila mmoja atapigana na ndugu yake na jirani yake,

Jiji litapigana na jiji, ufalme utapigana na ufalme.

 3 Na roho ya Misri itakuwa na msukosuko ndani yake,

Nami nitavuruga mipango yake.+

Watatafuta msaada kutoka kwa miungu ya ubatili,

Kwa wachawi na kwa wanaowasiliana na roho na kwa wabashiri.+

 4 Nitaitia Misri mikononi mwa bwana aliye katili,

Na mfalme mkali atawatawala,”+ asema Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi.

 5 Na maji ya bahari yatakaushwa,

Na mto utakauka na kuwa mkavu.+

 6 Na mito itanuka;

Mifereji ya Nile ya Misri itapungua na kukauka.

Matete na mafunjo yataoza.+

 7 Mimea iliyo kandokando ya Mto Nile, kwenye kinywa cha Mto Nile,

Na ardhi yote iliyopandwa mbegu kandokando ya Nile+ itakauka.+

Itapeperushwa mbali, nayo haitakuwepo tena.

 8 Na wavuvi wataomboleza,

Wale wanaotupa ndoano ndani ya Mto Nile wataomboleza,

Na wale wanaotandaza nyavu zao juu ya maji watapungua.

 9 Mafundi wa kitani kilichochambuliwa+

Na wafumaji wa vitambaa vyeupe wataaibishwa.

10 Wafumaji wake watapondwa;

Vibarua wote watahuzunika.*

11 Wakuu wa Soani+ ni wapumbavu.

Washauri wenye hekima zaidi wa Farao wanatoa ushauri usio wa busara.+

Mnawezaje kumwambia Farao:

“Mimi ni mzao wa watu wenye hekima,

Mzao wa wafalme wa kale”?

12 Basi, wako wapi watu wenu wenye hekima?+

Acheni wawaambie kama wanajua kile ambacho Yehova wa majeshi ameamua kuhusu Misri.

13 Wakuu wa Soani wametenda kwa upumbavu;

Wakuu wa Nofu*+ wamedanganywa;

Wakuu wa makabila yake wameipotosha Misri.

14 Yehova amemmwagia roho ya mvurugo;+

Nao wameipotosha Misri katika kila jambo inalofanya,

Kama mlevi anavyogaagaa kwenye matapishi yake.

15 Na Misri haitakuwa na kazi yoyote ya kufanya,

Iwe ni kwa ajili ya kichwa au mkia, chipukizi au utete.*

16 Siku hiyo Misri itakuwa kama wanawake, itatetemeka na kuogopa kwa sababu ya mkono wenye kutisha ambao Yehova wa majeshi anainua dhidi yake.+ 17 Na nchi ya Yuda itaifanya Misri iogope. Watahofu kila mara Yuda inapotajwa kwa sababu ya uamuzi ambao Yehova wa majeshi amefanya dhidi yao.+

18 Siku hiyo kutakuwa na majiji matano katika nchi ya Misri yanayozungumza lugha ya Kanaani+ na kuapa kuwa washikamanifu kwa Yehova wa majeshi. Jiji moja litaitwa Jiji la Kubomoa.

19 Siku hiyo kutakuwa na madhabahu kwa ajili ya Yehova katikati ya nchi ya Misri na nguzo kwa ajili ya Yehova kwenye mpaka wake. 20 Itakuwa ishara na ushahidi kwa Yehova wa majeshi nchini Misri; kwa maana watamlilia Yehova kwa sauti kwa sababu ya wakandamizaji, naye atawapelekea mwokozi, aliye mkuu, ambaye atawaokoa. 21 Na Yehova atajulikana kwa Wamisri, na Wamisri watamjua Yehova siku hiyo, nao watatoa dhabihu na zawadi na kuweka nadhiri kwa Yehova na kuitimiza. 22 Yehova ataipiga Misri,+ ataipiga na kuiponya; nao watamrudia Yehova, naye atasikiliza maombi yao ya kusihi na kuwaponya.

23 Siku hiyo kutakuwa na barabara kuu+ kutoka Misri kwenda Ashuru. Kisha Ashuru itakuja Misri, na Misri itaenda Ashuru; na Misri itamtumikia Mungu pamoja na Ashuru. 24 Siku hiyo Israeli itakuwa ya tatu pamoja na Misri na pamoja na Ashuru,+ baraka katikati ya dunia, 25 kwa maana Yehova wa majeshi atakuwa amewabariki, akisema: “Wabarikiwe watu wangu, Misri, na kazi ya mikono yangu, Ashuru, na urithi wangu, Israeli.”+

20 Mwaka ambao Mfalme Sargoni wa Ashuru alimtuma Tartani* aende Ashdodi,+ alipigana na Ashdodi na kuliteka.+ 2 Wakati huo Yehova alisema hivi kupitia Isaya+ mwana wa Amozi: “Nenda ukavue nguo ya magunia kutoka kiunoni mwako, na uvue viatu vilivyo miguuni mwako.” Naye akafanya hivyo, akatembea akiwa uchi* na bila viatu.

3 Kisha Yehova akasema: “Kama mtumishi wangu Isaya alivyotembea akiwa uchi na bila viatu kwa miaka mitatu ili kuwa ishara+ na dalili dhidi ya Misri+ na dhidi ya Ethiopia,+ 4 hivyo ndivyo mfalme wa Ashuru atakavyowaongoza mateka wa Misri+ na wahamishwa wa Ethiopia, wavulana na wanaume wazee, wakiwa uchi na bila viatu na matako yakiwa wazi, uchi wa* Misri. 5 Nao wataogopa na kuona aibu kwa ajili ya Ethiopia tumaini lao na kwa ajili ya Misri fahari yao.* 6 Wakaaji wa eneo hili la pwani watasema siku hiyo, ‘Tazama kilicholipata tumaini letu, tulilolikimbilia ili kupata msaada na kuokolewa kutoka kwa mfalme wa Ashuru! Tutaokokaje sasa?’”

21 Tangazo dhidi ya nyika ya bahari:*+

Msiba unakuja kama pepo za dhoruba zinazovuma kusini,

Kutoka nyikani, kutoka katika nchi inayotisha.+

 2 Nimeambiwa maono ya kutisha:

Mwenye hila anatenda kwa hila,

Na mwangamizaji, anaangamiza.

Nenda juu, ewe Elamu! Zingira, ewe Umedi!+

Nitakomesha kilio chote cha uchungu alichosababisha.+

 3 Ndiyo sababu nina maumivu makali.*+

Ninafurukuta kwa uchungu,

Uchungu kama wa mwanamke anayezaa.

Nimetaabika sana hivi kwamba siwezi kusikia;

Nimesumbuka sana hivi kwamba siwezi kuona.

 4 Moyo wangu unadundadunda; ninatetemeka kwa hofu.

Gizagiza la jioni nililotamani sana linanifanya nitetemeke.

 5 Andaeni meza na mpange viti!

Mle na mnywe!+

Simameni, enyi wakuu, itieni* ngao mafuta.

 6 Kwa maana Yehova aliniambia hivi:

“Nenda, mweke mlinzi na umwambie aseme yale anayoyaona.”

 7 Naye akaona gari la vita pamoja na kundi la farasi,

Gari la vita la punda,

Gari la vita la ngamia.

Alitazama kwa makini, akiwa amekaza fikira sana.

 8 Kisha akaita kwa sauti kama simba:

“Ee Yehova, ninasimama daima juu ya mnara wa mlinzi wakati wa mchana,

Nami ninasimama katika kituo changu cha ulinzi kila usiku.+

 9 Tazama kinachokuja:

Wanaume wakiwa katika gari la vita na kundi la farasi wa vita!”+

Kisha akasema:

“Ameanguka! Babiloni ameanguka!+

Sanamu zake zote za kuchongwa za miungu yake amezivunjavunja na kuziangusha chini!”+

10 Enyi watu wangu waliopurwa,

Mazao ya* uwanja wangu wa kupuria,+

Nimewaambia yale niliyosikia kutoka kwa Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli.

11 Tangazo dhidi ya Duma:*

Kuna mtu anayeniita kutoka Seiri:+

“Mlinzi, kuna habari gani za usiku?

Mlinzi, kuna habari gani za usiku?”

12 Mlinzi akasema:

“Asubuhi inakuja, na usiku pia.

Ikiwa mnataka kuuliza, ulizeni.

Njooni tena!”

13 Tangazo dhidi ya jangwa tambarare:

Mtakaa usiku kucha msituni katika nchi tambarare ya jangwani,

Enyi misafara ya Dedani.+

14 Leteni maji ili mkampokee mwenye kiu,

Enyi wakaaji wa nchi ya Tema,+

Mleteeni mkate yule anayekimbia.

15 Kwa maana wamekimbia kwa sababu ya panga, kwa sababu ya upanga uliochomolewa,

Kwa sababu ya upinde uliopindwa, na kwa sababu ya ukatili wa vita.

16 Kwa maana Yehova aliniambia hivi: “Katika muda wa mwaka mmoja, kulingana na miaka ya kibarua,* utukufu wote wa Kedari+ utafikia mwisho. 17 Wapiga upinde waliobaki kati ya mashujaa wa Kedari watakuwa wachache, kwa maana Yehova Mungu wa Israeli amesema hivyo.”

22 Tangazo kuhusu Bonde la Maono:*+

Una tatizo gani hivi kwamba watu wako wote wamepanda juu ya paa?

 2 Ulijaa machafuko,

Jiji lenye msukosuko, mji wenye furaha.

Watu wako waliouawa hawakuuawa kwa upanga,

Wala hawakufa vitani.+

 3 Madikteta wako wote wamekimbia pamoja.+

Walichukuliwa kuwa wafungwa bila kutumia upinde.

Wote waliopatikana walichukuliwa kuwa wafungwa,+

Ingawa walikuwa wamekimbilia mbali sana.

 4 Ndiyo sababu nilisema: “Msinitazame,

Nami nitalia kwa uchungu.+

Msisisitize kunifariji

Kwa sababu ya kuangamizwa kwa binti ya* watu wangu.+

 5 Kwa maana ni siku ya mvurugo na ya kushindwa na ya wasiwasi,+

Kutoka kwa Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi,

Katika Bonde la Maono.

Ukuta unabomolewa+

Na kuna kilio kwenye mlima.

 6 Elamu+ inachukua podo

Pamoja na magari ya vita yenye watu na farasi,*

Na Kiri+ inafunua* ngao.

 7 Mabonde yako yaliyo mazuri zaidi

Yatajaa magari ya vita,

Na farasi* watajipanga langoni,

 8 Na pazia la Yuda litaondolewa.*

“Siku hiyo utatazama kuelekea ghala la silaha la Nyumba ya Msitu,+ 9 nanyi mtayaona yale mashimo mengi yaliyo katika ukuta wa Jiji la Daudi.+ Nanyi mtayakusanya maji ya kidimbwi cha chini.+ 10 Mtazihesabu nyumba za Yerusalemu, nanyi mtazibomoa nyumba hizo ili kuimarisha ukuta. 11 Nanyi mtatengeneza beseni kati ya hizo kuta mbili kwa ajili ya maji ya kidimbwi cha zamani, lakini hamtamtegemea Muumba* wake Mkuu, nanyi hamtamwona Yule aliyeibuni zamani.

12 Siku hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi,

Atawaambia watu walie na kuomboleza,+

Wanyoe vichwa na kuvaa nguo za magunia.

13 Lakini badala yake, kuna sherehe na kushangilia,

Kuchinja ng’ombe na kuchinja kondoo,

Kula nyama na kunywa divai.+

‘Acheni tule na tunywe, kwa maana kesho tutakufa.’”+

14 Kisha Yehova wa majeshi akajifunua masikioni mwangu: “‘Uovu huu hautafunikwa kwa ajili yenu mpaka ninyi watu mtakapokufa,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi.”

15 Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, anasema hivi: “Ingia kwa huyu msimamizi-nyumba, kwa Shebna,+ anayesimamia nyumba,* na umwambie,⁠ 16 ‘Una masilahi gani hapa, na je, una mtu wako hapa hivi kwamba umejichimbia kaburi hapa?’ Anachimba kaburi lake mahali palipoinuka; anajichongea mahali pa kupumzika* katika jabali. 17 ‘Tazama! Yehova atakutupa chini kwa nguvu, ewe mwanamume, na kukukamata kwa nguvu. 18 Hakika atakufunga kwa nguvu na kukurusha kama mpira katika nchi pana. Utafia huko, na huko magari yako yenye utukufu yatakuwa fedheha kwa nyumba ya bwana wako. 19 Nami nitakung’oa madarakani na kukufukuza kutoka katika cheo chako.

20 “‘Siku hiyo nitamwita mtumishi wangu Eliakimu+ mwana wa Hilkia, 21 nami nitamvisha kanzu yako na kumfunga kwa nguvu ukumbuu wako,+ nami nitatia mamlaka yako* mkononi mwake. Naye atakuwa baba kwa wakaaji wa Yerusalemu na nyumba ya Yuda. 22 Nami nitauweka ufunguo wa nyumba ya Daudi+ juu ya bega lake. Atafungua na hakuna yeyote atakayefunga; naye atafunga na hakuna yeyote atakayefungua. 23 Nitampigilia kama kigingi mahali panapodumu, naye atakuwa kama kiti cha ufalme cha utukufu kwa nyumba ya baba yake. 24 Nao watauning’iniza juu yake utukufu* wote wa nyumba ya baba yake, wazao na watoto,* vyombo vyote vidogo, vyombo vyenye umbo la bakuli, na pia mitungi yote mikubwa.

25 “‘Siku hiyo,’ asema Yehova wa majeshi, ‘kigingi kilichopigiliwa mahali panapodumu kitang’olewa,+ nacho kitakatwa na kuanguka, na mzigo ulio juu yake utaanguka na kuharibika, kwa maana Yehova mwenyewe amesema hayo.’”

23 Tangazo kuhusu Tiro:+

Ombolezeni kwa sauti, enyi meli za Tarshishi!+

Kwa maana bandari imeharibiwa; haiwezi kuingiwa.

Wamefunuliwa habari kutoka katika nchi ya Kitimu.+

 2 Nyamazeni, enyi wakaaji wa pwani.

Wafanyabiashara kutoka Sidoni+ wanaovuka bahari wamekujaza.

 3 Nafaka* ya Shihori* ilienda juu ya maji mengi,+

Mavuno ya Nile, mapato yake,

Yalileta faida ya mataifa.+

 4 Ona aibu, Ee Sidoni, ngome ya bahari,

Kwa sababu bahari imesema:

“Sijapata uchungu wa kuzaa, nami sijazaa,

Wala sijalea vijana wa kiume wala wa kike.”*+

 5 Kama wakati waliposikia habari kuhusu Misri,+

Watu watateseka kwa sababu ya habari kuhusu Tiro.+

 6 Vukeni mpaka Tarshishi!

Ombolezeni kwa sauti, enyi wakaaji wa pwani!

 7 Je, hili ndilo jiji lenu lililokuwa na furaha tangu kale, tangu nyakati zake za zamani?

Miguu yake ilikuwa ikimpeleka nchi za mbali ili akae huko.

 8 Ni nani ambaye ameamua jambo hili dhidi ya Tiro,

Anayewavika watu mataji,

Ambaye wafanyabiashara wake walikuwa wakuu,

Ambaye wafanyabiashara wake waliheshimiwa duniani kote?+

 9 Yehova wa majeshi mwenyewe ameamua hivi,

Kutia unajisi kiburi chake kwenye uzuri wake wote,

Kuwafedhehesha wote walioheshimiwa duniani kote.+

10 Vuka nchi yako kama Mto Nile, ewe binti ya Tarshishi.

Hakuna tena kiwanda cha meli.*+

11 Ameunyoosha mkono wake juu ya bahari;

Amezitikisa falme.

Yehova ameamuru ngome za Foinike ziangamizwe.+

12 Naye anasema: “Hutafurahi tena,+

Ewe uliyekandamizwa, binti bikira wa Sidoni.

Simama, vuka mpaka Kitimu.+

Hata huko hutapata utulivu.”

13 Tazama! Nchi ya Wakaldayo.+

Hawa ndio watu—haikuwa Ashuru+—

Walimfanya kuwa mahali pa wale wanaokaa jangwani.

Wamesimamisha minara yao ya kuzingira;

Wameivua minara yake yenye ngome;+

Na kumfanya awe magofu yanayoporomoka.

14 Ombolezeni kwa sauti, enyi meli za Tarshishi,

Kwa maana ngome yenu imeharibiwa.+

15 Siku hiyo Tiro litasahauliwa kwa miaka 70,+ sawa na muda wa* maisha ya mfalme mmoja. Mwishoni mwa miaka 70, Tiro litakuwa kama wimbo huu wa kahaba unavyosema:

16 “Chukua kinubi, lizunguke jiji, ewe kahaba uliyesahauliwa.

Piga kinubi chako kwa ustadi;

Imba nyimbo nyingi,

Ili wakukumbuke.”

17 Mwishoni mwa miaka 70, Yehova atalikazia fikira Tiro, nalo litarudia malipo yake na kufanya ukahaba na falme zote za ulimwengu zilizo duniani. 18 Lakini faida yake na malipo yake yatakuwa kitu kitakatifu kwa Yehova. Hayatahifadhiwa wala kuwekwa akiba, kwa sababu malipo yake yatakuwa kwa ajili ya wale wanaokaa mbele za Yehova, ili wale na kushiba na kuvaa mavazi ya kifahari.+

24 Tazama! Yehova anaifanya nchi* kuwa tupu na ukiwa.+

Anaigeuza juu chini*+ na kuwatawanya wakaaji wake.+

 2 Kila mtu atapatwa na hali ileile:

Watu na pia kuhani,

Mtumishi na bwana wake,

Kijakazi na bimkubwa wake,

Mnunuzi na muuzaji,

Mkopeshaji na mkopaji,

Anayedai na anayedaiwa.+

 3 Nchi itafanywa kuwa tupu kabisa,

Itaporwa kabisa,+

Kwa maana Yehova amesema neno hilo.

 4 Nchi inaomboleza;*+ inadhoofika.

Nchi inayozaa inanyauka; inafifia.

Watu mashuhuri wa nchi wananyauka.

 5 Nchi imechafuliwa na wakaaji wake,+

Kwa maana wamezivunja sheria,+

Wamebadili amri,+

Na kuvunja agano linalodumu.*+

 6 Ndiyo sababu laana inaimeza nchi,+

Na wakaaji wake wamehesabiwa kuwa na hatia.

Ndiyo sababu wakaaji wa nchi wamepungua,

Na watu wachache sana wamebaki.+

 7 Divai mpya inaomboleza,* mzabibu unanyauka,+

Na wote walio wachangamfu moyoni wanalia kwa uchungu.+

 8 Furaha ya matari imekoma;

Kelele za wanaosherehekea zimekoma;

Sauti ya furaha ya kinubi imekoma.+

 9 Wanakunywa divai bila wimbo,

Na kileo ni kichungu kwa wale wanaokinywa.

10 Mji uliohamwa umebomolewa kabisa;+

Kila nyumba imefungwa ili mtu yeyote asiweze kuingia.

11 Wanalilia divai barabarani.

Kushangilia kote kumetoweka;

Shangwe ya nchi imetokomea.+

12 Jiji limeachwa likiwa magofu;

Lango limevunjwavunjwa na kuwa rundo la kifusi.+

13 Kwa maana hivi ndivyo itakavyokuwa katika nchi, miongoni mwa mataifa:

Kama mzeituni unapopigwa,+

Kama masalio yanavyokusanywa baada ya mavuno ya zabibu kuisha.+

14 Watapaza sauti zao,

Watapiga vigelegele kwa shangwe.

Kutoka baharini* watatangaza ukuu wa Yehova.+

15 Ndiyo sababu watamtukuza Yehova katika eneo la nuru;*+

Katika visiwa vya bahari watalitukuza jina la Yehova Mungu wa Israeli.+

16 Kutoka miisho ya dunia tunasikia nyimbo:

“Utukufu* kwa Aliye Mwadilifu!”+

Lakini ninasema: “Ninadhoofika, ninadhoofika!

Ole wangu! Wenye hila wametenda kwa hila;

Kwa hila wenye hila wametenda kwa hila.”+

17 Hofu na mashimo na mitego inakusubiri, mkaaji wa nchi.+

18 Yeyote anayeikimbia sauti inayotia hofu ataanguka shimoni,

Na yeyote anayetoka shimoni atanaswa na mtego.+

Kwa maana malango ya mafuriko yaliyo juu yatafunguliwa,

Na misingi ya nchi itatetemeka.

19 Nchi imepasuka;

Nchi imetikiswa;

Nchi inafurukuta kwa fujo.+

20 Nchi inapepesuka kama mlevi,

Nayo inayumbayumba kama kibanda katika upepo.

Makosa yake yameilemea sana,+

Nayo itaanguka, hivi kwamba haitasimama tena.

21 Siku hiyo Yehova atalielekezea fikira zake jeshi lililo juu

Na wafalme wa dunia walio duniani.

22 Nao watakusanywa pamoja

Kama wafungwa waliokusanywa shimoni,

Nao watafungiwa katika gereza lililo chini ya ardhi;

Baada ya siku nyingi watakaziwa uangalifu.

23 Mwezi mpevu utafedheheshwa,

Na jua linalong’aa litaaibishwa,+

Kwa maana Yehova wa majeshi amekuwa Mfalme+ katika Mlima Sayuni+ na Yerusalemu

Akiwa na utukufu mbele ya wazee wa watu wake.*+

25 Ee Yehova, wewe ni Mungu wangu.

Ninakukweza, ninalisifu jina lako,

Kwa maana umetenda mambo yanayostaajabisha,+

Mambo yaliyokusudiwa* tangu nyakati za kale,+

Kwa uaminifu,+ kwa kutegemeka.

 2 Kwa maana umelifanya jiji kuwa rundo la mawe,

Mji wenye ngome kuwa magofu yanayoporomoka.

Mnara wa wageni si jiji tena;

Halitajengwa tena kamwe.

 3 Ndiyo sababu watu wenye nguvu watakutukuza;

Jiji la mataifa yenye uonevu litakuogopa.+

 4 Kwa maana umekuwa ngome kwa mtu wa hali ya chini,

Ngome kwa maskini katika taabu yake,+

Kimbilio kutokana na dhoruba ya mvua,

Na kivuli wakati wa joto.+

Wakati mlipuko wa waonevu ni kama dhoruba ya mvua inayopiga ukuta,

 5 Kama joto katika nchi iliyokauka,

Unazikomesha ghasia za wageni.

Kama joto linavyokomeshwa na kivuli cha wingu,

Ndivyo wimbo wa waonevu unavyonyamazishwa.

 6 Katika mlima huu+ Yehova wa majeshi atawaandalia watu wa mataifa yote

Karamu ya vyakula vinono,+

Karamu ya divai bora,*

Ya vyakula vinono vilivyojazwa urojorojo,

Ya divai bora, iliyochujwa.

 7 Katika mlima huu ataondoa* kifuniko kinachowafunika watu wote

Na kifuniko kilichosokotwa* juu ya mataifa yote.

 8 Atameza* kifo milele,+

Na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atafuta kabisa machozi katika nyuso zote.+

Shutuma ya watu wake ataiondoa katika dunia yote,

Kwa maana Yehova mwenyewe amesema hayo.

 9 Siku hiyo watasema:

“Tazama! Huyu ndiye Mungu wetu!+

Tumemtumaini yeye,+

Naye atatuokoa.+

Huyu ndiye Yehova!

Tumemtumaini yeye.

Na tufurahi na kushangilia katika wokovu wake.”+

10 Kwa maana mkono wa Yehova utatulia juu ya mlima huu,+

Na Moabu itakanyagwa-kanyagwa mahali pake+

Kama nyasi zinavyokanyagwa-kanyagwa na kuwa rundo la mbolea.

11 Atapigapiga mikono yake ndani yake

Kama mwogeleaji anavyopigapiga mikono yake ili kuogelea,

Naye atakishusha kiburi chake+

Kwa mwendo stadi wa mikono yake.

12 Na jiji lenye ngome, pamoja na kuta zako ndefu za usalama,

Ataziangusha chini;

Atazibomoa na kuziangusha ardhini, mpaka mavumbini kabisa.

26 Siku hiyo wimbo huu utaimbwa+ katika nchi ya Yuda:+

“Tuna jiji imara.+

Anaufanya wokovu uwe kuta zake na maboma yake.+

 2 Fungueni malango+ ili taifa la uadilifu liingie,

Taifa linalodumisha mwenendo wa uaminifu.

 3 Utawalinda wale wanaokutegemea kikamili;*

Utawapa amani inayodumu,+

Kwa sababu wanakutumaini wewe.+

 4 Mtumainini Yehova milele,+

Kwa maana Yah* Yehova ni Mwamba wa milele.+

 5 Kwa maana amewashusha chini wale wanaokaa juu, jiji lililoinuliwa.

Analiangusha chini,

Analiangusha chini duniani;

Analitupa chini mavumbini.

 6 Mguu utalikanyaga-kanyaga,

Miguu ya wanaoteseka, nyayo za watu wa hali ya chini.”

 7 Njia ya mwadilifu imenyooka.*

Kwa sababu wewe ni mnyoofu,

Utailainisha njia ya mwadilifu.

 8 Tunapofuata njia ya hukumu zako, Ee Yehova,

Tumaini letu liko kwako.

Tunatamani* sana jina lako na ukumbusho wako.*

 9 Usiku ninakutamani sana kwa nafsi yangu yote,

Naam, roho yangu inaendelea kukutafuta;+

Kwa maana hukumu zinapotoka kwako kwa ajili ya dunia,

Wakaaji wa nchi hujifunza kuhusu uadilifu.+

10 Hata mwovu akionyeshwa kibali,

Hatajifunza uadilifu.+

Hata katika nchi ya unyoofu, atatenda uovu,+

Naye hatauona ukuu wa Yehova.+

11 Ee Yehova, mkono wako umeinuliwa, lakini hawauoni.+

Wataona bidii yako kwa ajili ya watu wako na kuaibishwa.

Naam, moto uliokusudiwa maadui wako utawateketeza.

12 Ee Yehova, utatupatia amani,+

Kwa sababu kila kitu ambacho tumefanya

Ni wewe uliyetutimizia.

13 Ee Yehova Mungu wetu, mabwana wengine mbali na wewe wametutawala,+

Lakini tunalitaja jina lako peke yake.+

14 Wamekufa; hawataishi.

Hawana uwezo katika kifo, hawataamka.+

Kwa maana umewaelekezea fikira

Ili uwaangamize na kufutilia mbali kabisa majina yao.

15 Umeongeza ukubwa wa taifa, Ee Yehova,

Umeongeza ukubwa wa taifa;

Umejitukuza mwenyewe.+

Umepanua sana mipaka yote ya nchi.+

16 Ee Yehova, wakati wa taabu walikutafuta;

Walikumwagia sala yao kwa kunong’ona ulipowatia nidhamu.+

17 Kama vile mwanamke mwenye mimba aliye karibu kuzaa

Anavyopata maumivu na kulia kwa uchungu,

Ndivyo hali yetu ilivyo kwa sababu yako, Ee Yehova.

18 Tulipata mimba, tulikuwa na maumivu ya kuzaa,

Lakini ni kama tumezaa upepo.

Hatujaleta wokovu nchini,

Na hakuna mtu aliyezaliwa ili aishi nchini.

19 “Wafu wako wataishi.

Maiti zangu zitaamka.*+

Amkeni na mpige vigelegele kwa shangwe,

Enyi mnaokaa mavumbini!+

Kwa maana umande wako ni kama umande wa asubuhi,*

Na dunia itawaacha wale waliokufa ambao hawana uwezo wawe hai tena.*

20 Nendeni, watu wangu, ingieni katika vyumba vyenu vya ndani,

Na mfunge milango nyuma yenu.+

Jificheni kwa muda mfupi

Mpaka ghadhabu* itakapopita.+

21 Kwa maana tazama! Yehova anakuja kutoka mahali pake

Ili kuwaita wakaaji wa nchi wawajibike kwa sababu ya uovu wao,

Na nchi itafunua umwagaji wake wa damu

Nayo haitawafunika tena watu wake waliouawa.”

27 Siku hiyo Yehova, akiwa na upanga wake mkali na mkubwa na wenye nguvu,+

Atamwelekezea fikira Lewiathani,* yule nyoka anayenyiririka,

Lewiathani, yule nyoka anayepindapinda,

Naye atamuua mnyama mkubwa sana aliye baharini.

 2 Siku hiyo mwimbieni hivi huyo mwanamke:*

“Shamba la mizabibu la divai inayotoa povu!+

 3 Mimi, Yehova, ninamlinda.+

Kila wakati ninammwagilia maji.+

Ninamlinda usiku na mchana,

Ili mtu yeyote asimdhuru.+

 4 Mimi sina ghadhabu.+

Ni nani atakayenikabili kwa vichaka vya miiba na magugu katika vita?

Nitavikanyaga-kanyaga na kuvichoma moto vyote pamoja.

 5 La sivyo, na ashikilie ngome yangu kwa nguvu,

Na afanye amani pamoja nami;

Acheni afanye amani pamoja nami.”

 6 Siku zinazokuja Yakobo atatia mizizi,

Israeli atachanua maua na kuchipuka,+

Nao watajaza mazao katika nchi.+

 7 Je, ni lazima apigwe kwa pigo la yule anayempiga?

Au, je, ni lazima auawe kama watu wake walivyouawa?

 8 Utashindana naye kwa mlio wa kushtua utakapokuwa ukimfukuza.

Atamfukuza kwa mlipuko wake mkali katika siku ya upepo wa mashariki.+

 9 Basi kwa njia hii uovu wa Yakobo utafunikwa,+

Na haya ndiyo yatakayokuwa mazao kamili dhambi yake itakapoondolewa:

Atayafanya mawe yote ya madhabahu

Yawe kama mawe ya chokaa yaliyopondwa na kuwa ungaunga,

Na hakuna miti mitakatifu* au vinara vya uvumba vitakavyobaki.+

10 Kwa maana jiji lenye ngome litaachwa tupu;

Malisho yataachwa na kubaki kama nyika.+

Ndama atalisha humo na kulala humo

Naye atakula matawi yake.+

11 Vitawi vyake vitakapokauka,

Wanawake watakuja kuvivunja,

Na kuvitumia kuwasha moto.

Kwa maana watu hawa hawana uelewaji.+

Ndiyo sababu Muumba wao hatawaonyesha rehema,

Na Yule aliyewaumba hatawaonyesha kibali.+

12 Siku hiyo Yehova atayapiga kabisa matunda kuanzia kijito kinachotiririka cha ule Mto* mpaka kwenye Korongo* la Misri,+ nanyi mtakusanywa mmoja baada ya mwingine, enyi watu wa Israeli.+ 13 Siku hiyo pembe kubwa itapigwa,+ na wale wanaoangamia katika nchi ya Ashuru+ na wale waliotawanywa katika nchi ya Misri+ watakuja na kumwinamia Yehova kwenye mlima mtakatifu huko Yerusalemu.+

28 Ole kwa taji* la kujionyesha* la walevi wa Efraimu+

Na ua linalonyauka la uzuri wake wenye utukufu,

Lililo kwenye kichwa cha bonde lenye rutuba la wale waliolemewa na divai!

 2 Tazama! Yehova ana mtu mwenye nguvu na hodari.

Kama dhoruba ya mvua ya mawe yenye mngurumo, dhoruba ya upepo inayoharibu,

Kama dhoruba yenye mngurumo ya mafuriko yenye nguvu,

Atalitupa chini kwa nguvu duniani.

 3 Mataji ya kujionyesha* ya walevi wa Efraimu

Yatakanyagiwa chini kwa miguu.+

 4 Na ua linalonyauka la uzuri wake wenye utukufu

Lililo juu ya kichwa cha bonde lenye rutuba,

Litakuwa kama tini ya mapema kabla ya wakati wa kiangazi.

Mtu anapoiona, huimeza mara tu inapokuwa mkononi mwake.

5 Siku hiyo Yehova wa majeshi atakuwa taji la utukufu na shada maridadi kwa watu wake waliobaki.+ 6 Naye atakuwa roho ya haki kwa yule anayeketi katika hukumu na chanzo cha nguvu kwa wale wanaozuia mashambulizi langoni.+

 7 Na hawa pia wanapotea njia kwa sababu ya divai;

Wanapepesuka kwa sababu ya vileo vyao.

Kuhani na nabii wanapotea njia kwa sababu ya kileo;

Divai inawavuruga,

Nao wanapepesuka kwa sababu ya kileo chao;

Maono yao yanawafanya wapotee njia,

Nao wanajikwaa wanapohukumu.+

 8 Kwa maana meza zao zimejaa matapishi machafu

—Yamejaa kila mahali.

 9 Mtu atamfundisha nani ujuzi,

Na mtu atamfafanulia nani ujumbe?

Je, ni wale walioachishwa kunyonya hivi karibuni,

Wale walioondolewa kwenye matiti hivi karibuni?

10 Kwa maana ni “amri baada ya amri, amri baada ya amri,

Mstari kwa mstari, mstari kwa mstari,*+

Hapa kidogo, pale kidogo.”

11 Kwa maana atazungumza na watu hawa kupitia watu wenye kigugumizi* na kwa lugha ya kigeni.+ 12 Alikuwa amewaambia: “Hapa ndipo mahali pa kupumzika. Yule aliyechoka na apumzike; hapa ndipo mahali pa kuburudika,” lakini walikataa kusikiliza.+ 13 Basi neno la Yehova litakuwa kwao:

“Amri baada ya amri, amri baada ya amri,

Mstari kwa mstari, mstari kwa mstari,*+

Hapa kidogo, pale kidogo,”

Ili wanapotembea,

Wajikwae na kuanguka nyuma

Na wavunjike na kunaswa na kukamatwa.+

14 Basi sikieni neno la Yehova, ninyi mnaojigamba,

Enyi watawala wa watu hawa wa Yerusalemu,

15 Kwa maana ninyi watu mnasema:

“Tumefanya agano na Kifo,+

Na tumefanya mapatano* na Kaburi.*

Mafuriko makubwa ya ghafla yatakapopita,

Hayatatufikia,

Kwa maana tumeufanya uwongo kuwa kimbilio letu

Nasi tumejificha katika udanganyifu.”+

16 Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:

“Tazama, ninaweka jiwe lililojaribiwa liwe msingi katika Sayuni,+

Jiwe la pembeni lenye thamani+ la msingi imara.+

Hakuna yeyote anayeonyesha imani atakayeshikwa na wasiwasi.+

17 Nami nitaifanya haki kuwa kamba ya kupimia+

Na uadilifu utakuwa kifaa cha kusawazishia;*+

Na mvua ya mawe itafagilia mbali kimbilio la uwongo,

Na maji yatafurika mahali pa kujificha.

18 Agano mlilofanya na Kifo litavunjwa,

Na mapatano yenu na Kaburi* hayatasimama.+

Mafuriko makubwa ya ghafla yatakapopita,

Yatawaponda ninyi.

19 Kila mara yanapopita,

Yatawafagilia mbali;+

Kwa maana yatapita asubuhi baada ya asubuhi,

Mchana na usiku.

Ni hofu tu itakayowafanya waelewe walichosikia.”*

20 Kwa maana kitanda ni kifupi sana mtu asiweze kujinyoosha juu yake,

Na shuka iliyofumwa ni nyembamba sana isiweze kumfunika mtu.

21 Kwa maana Yehova atasimama kama katika Mlima Perasimu,

Atainuka kama katika bonde lililo* karibu na Gibeoni,+

Ili afanye tendo lake —tendo lake la ajabu—

Na ili afanye kazi yake—kazi yake isiyo ya kawaida.+

22 Sasa msidhihaki,+

Ili vifungo vyenu visikazwe zaidi,

Kwa maana nimesikia kutoka kwa Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi,

Kwamba maangamizi yamekusudiwa kuipata nchi yote.*+

23 Tegeni sikio, muisikilize sauti yangu;

Kazeni fikira na msikilize ninachosema.

24 Je, mkulima huendelea kulima mchana kutwa kabla hajapanda mbegu?

Je, huendelea kuyagongagonga mabonge ya udongo na kusawazisha shamba lake?+

25 Baada ya kusawazisha ardhi,

Je, hatawanyi jira na kupanda bizari,

Na je, hapandi ngano, mtama, na shayiri mahali pake

Na kusemethi+ kwenye mipaka?

26 Kwa maana Yeye humfundisha* njia inayofaa;

Mungu wake humfundisha.+

27 Kwa maana jira haisagwi kwa kifaa cha kupuria,+

Na gurudumu la gari la kukokotwa halizungushwi juu ya bizari.

Badala yake, jira hupigwa kwa fimbo,

Na bizari kwa gongo.

28 Je, mtu huiponda nafaka ili apate mkate?

Hapana, haendelei kuipura mfululizo;+

Na anapozungusha gurudumu la gari lake la kukokotwa juu yake akiwa na farasi wake,

Yeye haipondi.+

29 Na haya pia yanatoka kwa Yehova wa majeshi,

Ambaye shauri* lake linastaajabisha

Na ambaye ametimiza mambo makuu.*+

29 “Ole kwa Arieli,* Arieli, jiji ambalo Daudi alipiga kambi ndani yake!+

Endelea mwaka baada ya mwaka;

Mzunguko wa sherehe+ na uendelee.

 2 Lakini nitaliletea taabu Arieli,+

Na kutakuwa na kilio na maombolezo,+

Nalo litakuwa kwangu kama jiko la madhabahu ya Mungu.+

 3 Nitapiga kambi pande zote dhidi yako,

Nami nitakuzingira kwa ngome

Na kujenga maboma dhidi yako.+

 4 Utashushwa chini;

Utazungumza kutoka ardhini,

Na mambo utakayosema yatakuwa mnong’ono kwa sababu ya mavumbi.

Sauti yako itatoka ardhini+

Kama sauti ya mtu anayewasiliana na roho,

Na maneno yako yatatoka mavumbini kama sauti ya ndege.

 5 Umati wa maadui wako* utakuwa kama ungaunga laini,+

Umati wa waonevu kama tu makapi yanayopeperuka.+

Na jambo hilo litatokea haraka, ghafla.+

 6 Yehova wa majeshi atawakazia fikira

Kwa mngurumo na tetemeko la ardhi na kelele kubwa,

Kwa upepo wa dhoruba na tufani na miali ya moto unaoteketeza.”+

 7 Kisha umati wa mataifa yote yanayopigana vita na Arieli+

—Wale wote wanaopigana vita naye,

Minara inayomzingira,

Na wale wanaomsababishia taabu—

Watakuwa kama ndoto, maono ya usiku.

 8 Naam, itakuwa kama mtu aliye na njaa anayeota kwamba anakula,

Lakini anaamka akiwa na njaa,*

Na kama mtu mwenye kiu anayeota kwamba anakunywa,

Lakini anaamka akiwa amechoka na akiwa na kiu.*

Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa umati wa mataifa yote

Yanayopigana vita dhidi ya Mlima Sayuni.+

 9 Pigweni na butwaa na mshangae;+

Jipofusheni na mpofushwe.+

Wamelewa, lakini si kwa divai;

Wanapepesuka, lakini si kwa sababu ya kileo.

10 Kwa maana Yehova amewamwagia roho ya usingizi mzito;+

Ameyafunga macho yenu, enyi manabii,+

Naye amefunika vichwa vyenu, enyi waonaji.+

11 Maono yote yamekuwa kwenu kama maneno ya kitabu ambacho kimefungwa kwa muhuri.+ Wakimpa mtu anayejua kusoma na kumwambia: “Tafadhali, kisome kwa sauti,” atasema: “Siwezi, kwa maana kimefungwa kwa muhuri.” 12 Na wakimpa kitabu hicho mtu asiyejua kusoma na kumwambia: “Tafadhali, kisome kitabu hiki,” atasema: “Sijui kusoma hata kidogo.”

13 Yehova anasema: “Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyao

Nao huniheshimu kwa midomo yao,+

Lakini mioyo yao iko mbali sana nami;

Na hofu yao kunielekea inategemea amri za wanadamu ambazo wamefundishwa.+

14 Kwa hiyo, mimi Ndiye nitakayewatendea tena watu hawa mambo ya ajabu,+

Maajabu juu ya maajabu;

Na hekima ya watu wao wenye hekima itatoweka,

Na uelewaji wa watu wao wenye busara utafichwa.”+

15 Ole wao wanaojitahidi sana kumficha Yehova mipango yao.*+

Wanatenda matendo yao mahali penye giza,

Huku wakisema: “Ni nani anayetuona?

Ni nani anayejua kutuhusu?”+

16 Jinsi mnavyopotosha mambo!*

Je, mfinyanzi anapaswa kuonwa kuwa sawa na udongo?+

Je, kitu kilichotengenezwa kinapaswa kusema kuhusu yule aliyekitengeneza:

“Hakunitengeneza?”+

Na je, kitu kilichotengenezwa kinasema kuhusu yule aliyekitengeneza:

“Hana uelewaji”?+

17 Katika muda mfupi, Lebanoni itageuzwa kuwa shamba la matunda,+

Na shamba hilo la matunda litaonwa kuwa msitu.+

18 Siku hiyo viziwi watasikia maneno ya kile kitabu,

Na kutoka katika utusitusi na giza macho ya vipofu yataona.+

19 Wapole watashangilia sana katika Yehova,

Na maskini miongoni mwa watu watashangilia katika Mtakatifu wa Israeli.+

20 Kwa maana mwonevu hatakuwapo tena,

Anayejigamba ataangamia,

Na wote wanaokaa macho ili kusababisha madhara wataangamizwa,+

21 Wale ambao kwa neno la udanganyifu wanawafanya wengine wawe na hatia,

Wanaotega mitego ili kumnasa mtetezi* katika lango la jiji,+

Na wale ambao kwa mashtaka yasiyo na msingi humnyima haki mwadilifu.+

22 Basi Yehova, aliyemkomboa Abrahamu,+ anaiambia hivi nyumba ya Yakobo:

“Yakobo hataona aibu tena,

Na uso wake hautabadilika rangi tena.*+

23 Kwa maana anapowaona watoto wake,

Ambao ni kazi ya mikono yake, katikati yake,+

Watalitakasa jina langu;

Naam, watamtakasa Mtakatifu wa Yakobo,

Nao watamwogopa Mungu wa Israeli.+

24 Wale waliopotoka rohoni watapata uelewaji,

Na wale wanaolalamika watakubali mafundisho.”

30 “Ole wao wana wakaidi,”+ asema Yehova,

“Wanaotekeleza mipango ambayo si yangu,+

Wanaofanya miungano,* lakini si kwa roho yangu,

Ili kuongeza dhambi juu ya dhambi.

 2 Wanashuka kwenda Misri+ bila kuniomba ushauri,*+

Ili kupata usalama chini ya ulinzi wa Farao*

Na kupata kimbilio katika kivuli cha Misri!

 3 Lakini ulinzi wa Farao utawaletea aibu,

Na kukimbilia katika kivuli cha Misri kutawaletea fedheha.+

 4 Kwa maana wakuu wake wako Soani,+

Na wajumbe wake wamefika Hanesi.

 5 Wote wataaibishwa

Na watu ambao hawawezi kuwanufaisha,

Ambao hawawapi msaada wowote wala manufaa yoyote,

Isipokuwa aibu na fedheha.”+

6 Tangazo dhidi ya wanyama wa kusini:

Katika nchi ya taabu na hali ngumu,

Ya simba, simba anayenguruma,

Ya nyoka kipiri na nyoka wa moto arukaye,*

Wanabeba mali zao juu ya migongo ya punda

Na mizigo yao juu ya nundu za ngamia.

Lakini vitu hivyo havitawanufaisha watu.

 7 Kwa maana msaada wa Misri haufai kitu.+

Kwa hiyo nimemwita huyu: “Rahabu,+ anayeketi tuli.”

 8 “Sasa nenda, iandike juu ya bamba mbele yao,

Na uiandike katika kitabu,+

Ili itumike siku ya baadaye

Kama ushahidi wa kudumu.+

 9 Kwa maana wao ni watu waasi,+ wana wadanganyifu,+

Wana wasiotaka kusikia sheria* ya Yehova.+

10 Wanawaambia waonaji, ‘Msione,’

Na wale wanaopata maono, ‘Msituambie maono ya kweli.+

Tuambieni mambo yanayotupendeza;* oneni maono ya udanganyifu.+

11 Tokeni kwenye njia; ondokeni kwenye kijia.

Acheni kumweka Mtakatifu wa Israeli mbele yetu.’”+

12 Kwa hiyo Mtakatifu wa Israeli anasema hivi:

“Kwa kuwa mnalikataa neno hili+

Nanyi mnatumaini ulaghai na udanganyifu

Na mnayategemea mambo hayo,+

13 Kwa hiyo uovu huu utakuwa kwenu kama ukuta uliobomoka,

Kama ukuta mrefu uliofura unaokaribia kuanguka.

Utaanguka ghafla, mara moja.

14 Utavunjwa kama mtungi mkubwa wa mfinyanzi,

Utapondwapondwa kabisa hivi kwamba hakuna kigae chochote kitakachobaki

Ili kitumiwe kukusanya moto jikoni

Au kuchota maji kutoka kwenye kidimbwi.”*

15 Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, Mtakatifu wa Israeli, anasema hivi:

“Mkirudi kwangu na kupumzika, mtaokolewa;

Mtakuwa na nguvu mkiendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini.”+

Lakini hamkutaka.+

16 Badala yake, mlisema: “Hapana, tutakimbia kwa farasi!”

Basi mtakimbia.

“Nasi tutapanda farasi wenye mbio!”+

Kwa hiyo wale wanaowafuatia watakuwa na mbio.+

17 Watu elfu moja watatetemeka wakitishwa na mtu mmoja;+

Mtakapotishwa na watu watano mtakimbia

Mpaka mbaki kama mlingoti juu ya mlima,

Kama nguzo ya ishara juu ya kilima.+

18 Lakini Yehova anangoja kwa subira* ili kuwaonyesha kibali,+

Naye atainuka ili kuwaonyesha rehema.+

Kwa maana Yehova ni Mungu wa haki.+

Wenye furaha ni wote wanaoendelea kumtarajia.*+

19 Watu watakapokaa Sayuni, Yerusalemu,+ hamtalia kamwe.+ Kwa hakika atawaonyesha kibali mara tu atakaposikia kilio chenu cha kuomba msaada; atawajibu mara tu atakaposikia kilio chenu.+ 20 Ingawa Yehova atawapa taabu kama mkate na ukandamizaji kama maji,+ Mfundishaji wako Mkuu hatajificha tena, nawe utamwona Mfundishaji wako Mkuu+ kwa macho yako mwenyewe. 21 Na masikio yako mwenyewe yatasikia neno nyuma yako likisema, “Hii ndiyo njia.+ Tembeeni ndani yake,” ikiwa mtaenda upande wa kulia au mtaenda upande wa kushoto.+

22 Nanyi mtaitia unajisi fedha inayofunika sanamu zenu za kuchongwa na dhahabu inayofunika sanamu zenu za chuma.*+ Mtazitupa mbali kama kitambaa cha hedhi na kuziambia, “Potelea mbali!”*+ 23 Naye ataleta mvua kwa ajili ya mbegu mtakazopanda ardhini,+ na chakula* kitakachotoka ardhini kitakuwa kingi na chenye lishe.*+ Siku hiyo mifugo yenu italisha katika malisho makubwa.+ 24 Na ng’ombe na punda wanaolima mashamba watakula chakula cha mifugo kilichokolezwa kwa mboga chungu, kilichopepetwa kwa sepetu na kwa uma. 25 Na juu ya kila mlima mrefu na juu ya kila kilima kirefu kutakuwa na vijito na mitaro ya maji,+ katika siku ya mauaji makubwa wakati ambapo minara itaanguka. 26 Na mwangaza wa mwezi mpevu utakuwa kama mwangaza wa jua; na mwangaza wa jua utaongezeka mara saba,+ kama mwangaza wa siku saba, katika siku ambayo Yehova atalifunga jeraha* la watu wake+ na kuponya kidonda kikubwa kilichosababishwa na pigo alilowaletea.+

27 Tazama! Jina la Yehova linakuja kutoka mbali sana,

Likiwaka kwa hasira yake na kwa mawingu mazito.

Midomo yake imejaa ghadhabu,

Na ulimi wake ni kama moto unaoteketeza.+

28 Roho* yake ni kama mto unaofurika unaofika mpaka shingoni,

Ili kuyatikisa mataifa katika chujio la maangamizi;*

Na mataifa yatakuwa na lijamu katika mataya yao+ ambayo inawapotosha.

29 Lakini wimbo wenu utakuwa kama wimbo unaoimbwa usiku

Mnapojitayarisha* kwa ajili ya sherehe,+

Na moyo wenu utashangilia kama mtu

Anayetembea na* filimbi

Akielekea kwenye mlima wa Yehova, kwa Mwamba wa Israeli.+

30 Yehova atafanya sauti yake kuu+ isikiwe

Naye ataonyesha mkono wake+ unaposhuka kwa hasira kali,+

Ukiwa na mwali wa moto unaoteketeza,+

Tufani ya mvua na dhoruba yenye ngurumo+ na mvua ya mawe.+

31 Kwa maana kwa sababu ya sauti ya Yehova, Ashuru itashikwa na hofu;+

Ataipiga kwa fimbo.+

32 Na kila pigo la fimbo yake ya adhabu

Ambalo Yehova ataleta juu ya Ashuru

Litaambatana na matari na vinubi+

Anapoutikisa mkono wake dhidi yao vitani.+

33 Kwa maana tayari Tofethi*+ yake imetayarishwa;

Pia imetayarishwa kwa ajili ya mfalme.+

Amefanya rundo la kuni liwe na kina kirefu na liwe pana,

Kwa wingi wa moto na kuni.

Pumzi ya Yehova, kama mto wa kiberiti,

Itaiwasha moto.

31 Ole wao wanaoshuka kwenda Misri kutafuta msaada,+

Wanaotegemea farasi,+

Wanaotumaini magari ya vita kwa sababu ni mengi,

Na farasi wa vita* kwa sababu wana nguvu.

Lakini hawamtegemei Mtakatifu wa Israeli,

Na hawamtafuti Yehova.

 2 Lakini yeye pia ana hekima na ataleta msiba,

Naye hatayabatilisha maneno yake.

Atainuka dhidi ya nyumba ya watenda maovu

Na dhidi ya wale wanaowasaidia wakosaji.+

 3 Hata hivyo, Wamisri ni wanadamu tu, wao si Mungu;

Farasi wao ni nyama wala si roho.+

Yehova atakapounyoosha mkono wake,

Yeyote atakayetoa msaada atajikwaa

Na yeyote atakayesaidiwa ataanguka;

Wote wataangamia wakati mmoja.

 4 Kwa maana Yehova ameniambia hivi:

“Kama simba anavyonguruma, mwanasimba mwenye nguvu,* juu ya mawindo yake,

Kundi lote la wachungaji linapokusanywa kupigana naye,

Naye haogopi sauti yao

Au kutishwa na kelele zao,

Ndivyo Yehova wa majeshi atakavyoshuka ili kupigana vita

Juu ya Mlima Sayuni na juu ya kilima chake.

 5 Kama ndege wanaoshuka kwa ghafla, ndivyo Yehova wa majeshi atakavyolilinda Yerusalemu.+

Atalilinda na kuliokoa.

Atalihifadhi na kuliokoa.”

6 “Rudini kwa Yule ambaye mmemwasi bila aibu, enyi watu wa Israeli.+ 7 Kwa maana siku hiyo kila mmoja ataikataa miungu yake ya ubatili ya fedha na miungu yake ya dhahabu ambayo haina thamani, ambayo mikono yenu wenyewe ilitenda dhambi kwa kuitengeneza.

 8 Na Mwashuru atauawa kwa upanga, lakini si wa mwanadamu;+

Na upanga, usio wa mwanadamu, utamwangamiza.

Atakimbia kwa sababu ya upanga,

Na wanaume wake vijana watalazimishwa kufanya kazi za kulazimishwa.

 9 Jabali lake litapitilia mbali kwa sababu ya woga mwingi,

Na wakuu wake wataogopa kwa sababu ya nguzo ya ishara,” asema Yehova,

Ambaye nuru yake iko* Sayuni na ambaye tanuru lake liko Yerusalemu.

32 Tazama! Mfalme+ atatawala kwa uadilifu,+

Na wakuu watatawala kwa haki.

 2 Na kila mmoja atakuwa kama mahali pa kujificha* kutokana na upepo,

Na mahali pa kujisitiri* kutokana na dhoruba ya mvua,

Kama vijito vya maji katika nchi isiyo na maji,+

Kama kivuli cha jabali kubwa katika nchi iliyokauka.

 3 Kisha macho ya wale wanaoona hayatafungwa tena,

Na masikio ya wale wanaosikia yatasikiliza.

 4 Moyo wa wale wanaofanya mambo bila kufikiri utatafakari ujuzi,

Na ulimi wa wenye kigugumizi utazungumza kwa ufasaha na waziwazi.+

 5 Mtu mpumbavu hataitwa tena mkarimu,

Na mtu asiye na msimamo hataitwa mheshimiwa;

 6 Kwa maana mtu mpumbavu atazungumza upumbavu,

Na moyo wake utatunga mambo yanayodhuru,+

Ili kuendeleza uasi imani* na kusema mambo mapotovu dhidi ya Yehova,

Kusababisha mwenye njaa akae njaa

Na kumnyima mwenye kiu maji ya kunywa.

 7 Mipango ya mtu asiye na msimamo ni mibaya;+

Anaendeleza mwenendo wa aibu

Ili kumwangamiza kwa uwongo mtu anayeteseka,+

Hata maskini anaposema jambo lililo sawa.

 8 Lakini mtu mkarimu ana nia ya ukarimu,

Naye huendelea kutenda matendo ya ukarimu.*

 9 “Enyi wanawake mnaopuuza mambo, simameni msikilize sauti yangu!

Enyi mabinti msiojali,+ sikilizeni ninachosema!

10 Katika muda unaozidi mwaka mmoja hivi, ninyi msiojali mtatetemeka,

Kwa sababu hakuna matunda yatakayokuwa yamekusanywa mavuno ya zabibu yatakapokwisha.+

11 Tetemekeni, ninyi wanawake mnaopuuza mambo!

Tetemekeni, ninyi msiojali!

Vueni nguo mbaki uchi,

Na mvae nguo za magunia viunoni.+

12 Pigeni vifua vyenu kwa kuomboleza

Kwa sababu ya mashamba yanayotamanika na mzabibu unaozaa matunda mengi.

13 Kwa maana ardhi ya watu wangu itafunikwa kwa miiba na michongoma;

Itazifunika nyumba zote zenye furaha,

Naam, jiji la shangwe.+

14 Kwa maana mnara wenye ngome umeachwa;

Jiji lenye kelele limeachwa.+

Ofeli+ na mnara wa mlinzi vimebaki ukiwa daima,

Mahali panapopendwa na punda wa mwituni,

Malisho ya mifugo,+

15 Mpaka roho itakapomiminwa juu yetu kutoka juu,+

Na nyika iwe shamba la matunda,

Na shamba la matunda lionwe kuwa msitu.+

16 Kisha haki itakaa nyikani,

Na uadilifu utakaa katika shamba la matunda.+

17 Matokeo ya uadilifu wa kweli yatakuwa amani,+

Na mazao ya uadilifu wa kweli yatakuwa utulivu wa kudumu na usalama wa kudumu.+

18 Watu wangu watakaa katika makao ya kudumu yenye amani,

Katika makao salama na mahali pa kupumzika penye utulivu.+

19 Lakini mvua ya mawe itauangusha chini msitu,

Na jiji litabomolewa kabisa.

20 Wenye furaha ni ninyi mnaopanda mbegu kando ya maji yote,

Mnaowatoa nje* ng’ombe dume na punda.”+

33 Ole wako wewe, mwangamizaji ambaye hujaangamizwa;+

Ewe msaliti ambaye hujasalitiwa!

Utakapomaliza kuangamiza, utaangamizwa.+

Utakapomaliza kusaliti, utasalitiwa.

 2 Ee Yehova, tuonyeshe kibali.+

Tunakutumaini wewe.

Uwe mkono wetu*+ kila asubuhi,

Naam, wokovu wetu wakati wa taabu.+

 3 Watu wanakimbia kwa sababu ya sauti ya ghasia.

Unapoinuka, mataifa yanatawanyika.+

 4 Kama nzige wanaokula sana wanavyokusanyika, ndivyo nyara zako zitakavyokusanywa;

Watu watazikimbilia kama makundi ya nzige.

 5 Yehova atakwezwa,

Kwa maana anakaa katika vilele vilivyo juu.

Ataijaza Sayuni haki na uadilifu.

 6 Yeye ndiye tegemeo imara la nyakati zako;

Wingi wa wokovu,+ hekima, ujuzi, na kumwogopa Yehova+

—Hiyo ndiyo hazina yake.

 7 Tazama! Mashujaa wao wanalia kwa sauti barabarani;

Wajumbe wa amani wanalia kwa uchungu.

 8 Barabara kuu zimebaki tupu;

Hakuna mtu anayesafiri kwenye vijia.

Amelivunja* agano;

Ameyakataa majiji;

Hamheshimu mwanadamu anayeweza kufa.+

 9 Nchi inaomboleza* na kunyauka kabisa.

Lebanoni imeaibika;+ imeoza.

Sharoni imekuwa kama jangwa,

Na Bashani na Karmeli zinapukutisha majani yake.+

10 “Sasa nitainuka,” asema Yehova,

“Sasa nitajikweza mwenyewe;+

Sasa nitajitukuza mwenyewe.

11 Mnachukua mimba ya majani yaliyokauka na kuzaa majani makavu.

Roho yenu wenyewe itawateketeza kama moto.+

12 Na watu watakuwa kama chokaa iliyoteketea.

Watawashwa moto kama miiba iliyokatwa.+

13 Ninyi mlio mbali sana, sikieni jambo nitakalofanya!

Nanyi mlio karibu, tambueni uwezo wangu!

14 Watenda dhambi walio Sayuni wanaogopa;+

Waasi imani wanatetemeka:

‘Ni nani kati yetu anayeweza kuishi mahali palipo na moto unaoteketeza?+

Ni nani kati yetu anayeweza kuishi na miale isiyoweza kuzimwa?’

15 Yule anayetembea katika uadilifu wa daima,+

Anayesema mambo manyoofu,+

Anayekataa faida isiyo ya haki, ya ulaghai,

Ambaye mikono yake inakataa rushwa badala ya kuichukua kwa nguvu,+

Anayeziba sikio lake ili lisisikilize mazungumzo ya umwagaji wa damu,

Na anayefunga macho yake ili yasione maovu

16 —Atakaa katika vilele;

Kimbilio lake salama* litakuwa katika ngome zilizo kwenye miamba,

Atapewa mkate wake,

Naye maji yake hayataisha kamwe.”+

17 Macho yako yatamwona mfalme katika fahari yake;

Yataona nchi iliyo mbali sana.

18 Moyoni mwako utakumbuka* jambo linaloogopesha:

“Yuko wapi mwandishi?

Yuko wapi yule aliyepima ushuru?+

Yuko wapi yule aliyeihesabu minara?”

19 Hutawaona tena watu wenye dharau,

Watu ambao lugha yao ni ngumu sana kueleweka,*

Ambao huwezi kuelewa ulimi wao wenye kigugumizi.+

20 Tazama Sayuni, jiji la sherehe zetu!+

Macho yako yataona Yerusalemu kama makao matulivu,

Hema ambalo halitaondolewa.+

Vigingi vyake vya mahema havitang’olewa kamwe,

Na hakuna kamba yake yoyote itakayokatwa.

21 Lakini huko, yule Aliye Mkuu, Yehova,

Atakuwa kwetu eneo la mito, la mifereji mipana,

Ambako hakuna kundi la merikebu litakaloenda huko

Na hakuna meli za kifahari zitakazopita huko.

22 Kwa maana Yehova ni Mwamuzi wetu,+

Yehova ni Mpaji-sheria wetu,+

Yehova ni Mfalme wetu;+

Yeye Ndiye atakayetuokoa.+

23 Kamba zako zitalegea na kuning’inia;

Haziwezi kushika mlingoti usimame imara wala kutandaza tanga.

Wakati huo nyara nyingi zitagawanywa;

Hata mtu mlemavu atachukua nyara nyingi.+

24 Na hakuna mkaaji* atakayesema: “Mimi ni mgonjwa.”+

Watu wanaokaa katika nchi watasamehewa dhambi yao.+

34 Njooni karibu ili msikie, enyi mataifa,

Na msikilize, enyi watu.

Dunia na vyote vinavyoijaza na visikilize,

Nchi na mazao yake yote.

 2 Kwa maana hasira ya Yehova inawaka dhidi ya mataifa yote,+

Na ghadhabu yake dhidi ya jeshi lao lote.+

Atawaangamiza;

Atawachinja.+

 3 Watu wao waliouawa watatupwa nje,

Na uvundo wa maiti zao utapaa;+

Milima itayeyuka kwa sababu ya* damu yao.+

 4 Jeshi lote la mbinguni litaoza kabisa,

Na mbingu zitakunjwa kama kitabu cha kukunjwa.

Jeshi lake lote litanyauka kabisa,

Kama jani lililonyauka linavyoanguka kutoka kwenye mzabibu

Na tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.

 5 “Kwa maana upanga wangu utaloweshwa mbinguni.+

Utashuka juu ya Edomu katika hukumu,+

Juu ya watu ambao niliamua kuwaangamiza.

 6 Yehova ana upanga; utafunikwa kwa damu.

Utafunikwa kwa mafuta,+

Kwa damu ya wanakondoo dume na mbuzi,

Kwa mafuta ya figo za kondoo dume.

Kwa maana Yehova ana dhabihu kule Bosra,

Machinjo makubwa katika nchi ya Edomu.+

 7 Fahali mwitu watashuka pamoja nao,

Ng’ombe dume wachanga watashuka pamoja na wenye nguvu.

Nchi yao itajaa damu,

Na mavumbi yao yatalowa mafuta.”

 8 Kwa maana Yehova ana siku ya kisasi,+

Mwaka wa malipo ya kesi dhidi ya Sayuni.+

 9 Vijito vyake* vitabadilishwa kuwa lami,

Na mavumbi yake kuwa kiberiti,

Na nchi yake itakuwa kama lami inayowaka.

10 Haitazimwa usiku wala mchana;

Moshi wake utaendelea kupaa milele.

Itabaki ukiwa kizazi baada ya kizazi;

Hakuna yeyote atakayepita katikati yake milele na milele.+

11 Mwari na nungunungu wataimiliki,

Na bundi wenye masikio marefu na kunguru watakaa ndani yake.

Atanyoosha juu yake kamba ya kupimia ya utupu

Na timazi* ya ukiwa.

12 Hakuna yeyote kati ya watu wake mashuhuri atakayepewa ufalme,

Na wakuu wake wote watakuwa si kitu.

13 Miiba itaota katika minara yake yenye ngome,

Upupu na magugu yenye miiba katika ngome yake.

Nchi hiyo itakuwa makao ya mbwamwitu,+

Boma la mbuni.

14 Viumbe wa jangwani watakutana na wanyama wanaopiga mayowe,

Na mbuzi wa mwituni* atamwita mwenzake.

Naam, huko babewatoto atakaa na kupata mahali pa kupumzika.

15 Nyoka-pili atatengeneza kiota chake huko na kutaga mayai,

Naye atayaangua na kuyakusanya katika kivuli chake.

Naam, vipanga watakusanyika huko, kila mmoja na mwenzake.

16 Tafuteni katika kitabu cha Yehova na mkisome kwa sauti:

Hakuna hata mmoja wao atakayekosekana;

Hakuna hata mmoja wao atakayekosa mwenzake,

Kwa maana kinywa cha Yehova ndicho kimeamuru,

Na roho yake ndiyo imewakusanya pamoja.

17 Yeye Ndiye amewapigia kura,

Na mkono wake mwenyewe umewapimia mahali walipogawiwa.*

Wataimiliki daima;

Watakaa ndani yake kwa vizazi vyote.

35 Nyika na nchi iliyokauka zitafurahi,+

Na jangwa tambarare litashangilia na kuchanua maua kama zafarani.+

 2 Hakika itachanua maua;+

Itashangilia na kupiga vigelegele vya shangwe.

Itapewa utukufu wa Lebanoni,+

Fahari ya Karmeli+ na ya Sharoni.+

Watauona utukufu wa Yehova, fahari ya Mungu wetu.

 3 Itieni nguvu mikono iliyo dhaifu,

Na myaimarishe magoti yanayotetemeka.+

 4 Waambieni wale wanaohangaika moyoni:

“Iweni na nguvu. Msiogope.

Tazameni! Mungu wenu atakuja na kisasi,

Mungu atakuja na malipo.+

Atakuja na kuwaokoa ninyi.”+

 5 Wakati huo macho ya vipofu yatafunguliwa,+

Na masikio ya viziwi yatazibuliwa.+

 6 Wakati huo kilema ataruka kama paa,+

Na ulimi wa bubu utapiga vigelegele vya shangwe.+

Kwa maana maji yatabubujika nyikani,

Na vijito katika jangwa tambarare.

 7 Na ardhi iliyokaushwa na joto itakuwa kama dimbwi lenye matete,

Na ardhi yenye kiu itakuwa kama mabubujiko ya maji.+

Katika makao ambamo mbwamwitu walipumzika,+

Kutakuwa na majani mabichi na matete na mafunjo.

 8 Na huko kutakuwa na barabara kuu,+

Naam, njia inayoitwa Njia ya Utakatifu.

Mtu asiye safi hatasafiri kwenye njia hiyo.+

Imetengwa kwa ajili ya yule anayetembea katika njia hiyo;

Hakuna mtu yeyote mpumbavu atakayepotea na kuingia katika njia hiyo.

 9 Hakuna simba atakayekuwa huko,

Na hakuna wanyama hatari wa mwituni watakaokuja kwenye njia hiyo.

Hawatapatikana huko;+

Wale waliokombolewa tu ndio watakaotembea katika njia hiyo.+

10 Wale waliokombolewa na Yehova watarudi+ na kuja Sayuni kwa kilio cha shangwe.+

Shangwe isiyo na kikomo itakuwa taji la vichwa vyao.+

Watapata shangwe na furaha,

Na huzuni na kilio cha uchungu vitatoweka.+

36 Katika mwaka wa 14 wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru+ alipanda kuja kuyashambulia majiji yote yenye ngome ya Yuda na kuyateka.+ 2 Kisha mfalme wa Ashuru akamtuma Rabshake*+ pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi+ kwenda kwa Mfalme Hezekia kule Yerusalemu. Wakajipanga karibu na mfereji wa kidimbwi cha juu,+ kwenye barabara kuu ya uwanja wa mfuaji wa nguo.+ 3 Ndipo Eliakimu+ mwana wa Hilkia, aliyekuwa msimamizi wa nyumba,* Shebna+ aliyekuwa mwandishi, na Yoa mwana wa Asafu aliyefanya kazi ya kuweka kumbukumbu wakaenda nje kukutana naye.

4 Basi Rabshake akawaambia: “Tafadhali, mwambieni hivi Hezekia: ‘Mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru, anauliza, “Ujasiri wako unategemea msingi gani?+ 5 Unasema, ‘Nina mbinu na nguvu za kupigana vita,’ lakini hayo ni maneno matupu. Unamtumaini nani, hivi kwamba unathubutu kuniasi?+ 6 Tazama! Unautumaini msaada wa utete huu uliopondeka, Misri, ambao mtu yeyote akiuegemea utamchoma kiganja na kukitoboa. Hivyo ndivyo Farao mfalme wa Misri alivyo kwa wote wanaomtumaini.+ 7 Nawe ukiniambia, ‘Tunamtumaini Yehova Mungu wetu,’ je, si yeye ndiye ambaye mahali pake pa juu na madhabahu zake zimeondolewa na Hezekia,+ huku akiwaambia watu wa Yuda na Yerusalemu, ‘Mnapaswa kuinama mbele ya madhabahu hii’?”’+ 8 Basi sasa, tafadhali, fanya mkataba huu pamoja na bwana wangu mfalme wa Ashuru:+ nitakupa farasi 2,000 ikiwa unaweza kupata wapanda farasi wa kutosha idadi hiyo. 9 Basi, unawezaje kumzuia hata gavana mmoja aliye mdogo zaidi kati ya watumishi wa bwana wangu, huku ukiitumaini nchi ya Misri ili upate magari ya vita na wapanda farasi? 10 Sasa je, nimepanda kuja kuishambulia nchi hii ili kuiharibu bila kupewa idhini na Yehova? Yehova mwenyewe aliniambia, ‘Panda uende kuishambulia nchi hii na kuiharibu.’”

11 Ndipo Eliakimu na Shebna+ na Yoa wakamwambia Rabshake:+ “Tafadhali, zungumza nasi watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu*+ kwa maana tunaweza kuielewa; usizungumze nasi kwa lugha ya Wayahudi huku watu walio ukutani wakisikia.”+ 12 Lakini Rabshake akasema: “Je, bwana wangu amenituma niwaambie ninyi na bwana wenu tu maneno haya? Je, sipaswi kuwaambia pia wanaume wanaoketi ukutani, wale watakaokula kinyesi chao wenyewe na kunywa mkojo wao wenyewe pamoja nanyi?”

13 Kisha Rabshake akasimama na kusema hivi kwa sauti kubwa kwa lugha ya Wayahudi:+ “Sikieni neno la mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru.+ 14 Mfalme anasema hivi, ‘Msikubali Hezekia awadanganye, kwa maana hawezi kuwaokoa.+ 15 Na msikubali Hezekia awafanye mumtumaini Yehova+ mkisema: “Kwa hakika Yehova atatuokoa, na jiji hili halitatiwa mikononi mwa mfalme wa Ashuru.” 16 Msimsikilize Hezekia, kwa maana mfalme wa Ashuru anasema hivi: “Fanyeni amani pamoja nami na mjisalimishe,* na kila mmoja wenu atakula matunda ya mzabibu wake mwenyewe na matunda ya mtini wake mwenyewe na kunywa maji kutoka katika tangi lake mwenyewe, 17 mpaka nitakapokuja na kuwapeleka katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe,+ nchi yenye nafaka na divai mpya, nchi yenye mikate na mashamba ya mizabibu. 18 Msikubali Hezekia awapotoshe akisema, ‘Yehova atatuokoa.’ Je, kuna mungu yeyote kati ya miungu ya mataifa ambaye amewahi kuiokoa nchi yake kutoka mikononi mwa mfalme wa Ashuru?+ 19 Iko wapi miungu ya Hamathi na Arpadi?+ Iko wapi miungu ya Sefarvaimu?+ Na je, imeokoa Samaria kutoka mikononi mwangu?+ 20 Ni mungu yupi kati ya miungu yote ya nchi hizi ambaye ameokoa nchi yake kutoka mikononi mwangu, hivi kwamba Yehova aokoe Yerusalemu kutoka mikononi mwangu?”’”+

21 Lakini walikaa kimya, hawakumjibu neno lolote, kwa maana mfalme aliwaagiza hivi: “Msimjibu.”+ 22 Lakini Eliakimu mwana wa Hilkia, aliyekuwa msimamizi wa nyumba,* Shebna+ aliyekuwa mwandishi, na Yoa mwana wa Asafu aliyekuwa akifanya kazi ya kuweka kumbukumbu wakaja kwa Hezekia mavazi yao yakiwa yameraruliwa, wakamwambia maneno ya Rabshake.

37 Mara tu Mfalme Hezekia aliposikia hilo, akayararua mavazi yake na kuvaa nguo za magunia na kuingia katika nyumba ya Yehova.+ 2 Kisha akamtuma Eliakimu, aliyekuwa msimamizi wa nyumba,* Shebna aliyekuwa mwandishi, na wazee miongoni mwa makuhani, wakiwa wamevaa nguo za magunia, waende kwa nabii Isaya,+ mwana wa Amozi. 3 Wakamwambia: “Hezekia anasema hivi: ‘Leo ni siku ya taabu, ya kemeo,* na ya aibu; kwa maana watoto wako tayari kuzaliwa* lakini hakuna nguvu za kuwazaa.+ 4 Huenda Yehova Mungu wako atayasikia maneno ya Rabshake, aliyetumwa na bwana wake mfalme wa Ashuru ili amdhihaki Mungu aliye hai,+ naye atamfanya awajibike kwa sababu ya maneno ambayo Yehova Mungu wako amesikia. Basi toa sala+ kwa niaba ya watu waliobaki ambao wameokoka.’”+

5 Kwa hiyo watumishi wa Mfalme Hezekia wakaenda kwa Isaya,+ 6 naye Isaya akawaambia: “Mwambieni hivi bwana wenu, ‘Yehova anasema hivi: “Usiogope+ kwa sababu ya maneno uliyosikia, maneno ambayo watumishi wa mfalme wa Ashuru+ waliyasema na kunikufuru. 7 Sasa ninatia wazo fulani akilini mwake,* naye atasikia habari na kurudi katika nchi yake mwenyewe;+ nami nitamuua kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.”’”+

8 Baada ya Rabshake kusikia kwamba mfalme wa Ashuru ameondoka Lakishi, alirudi na kumkuta akipigana vita na Libna.+ 9 Ndipo mfalme akasikia maneno haya yakisemwa kumhusu Tirhaka mfalme wa Ethiopia: “Amekuja ili kupigana nawe.” Aliposikia hivyo, akawatuma tena wajumbe kwa Hezekia,+ akisema: 10 “Mwambieni hivi Mfalme Hezekia wa Yuda, ‘Usikubali Mungu wako unayemtumaini akudanganye akisema: “Yerusalemu halitatiwa mikononi mwa mfalme wa Ashuru.”+ 11 Tazama! Umesikia mambo ambayo wafalme wa Ashuru walizitendea nchi zote kwa kuziangamiza.+ Je, ni wewe peke yako utakayeokolewa? 12 Je, miungu ya mataifa yaliyoangamizwa na mababu zangu iliyaokoa mataifa hayo?+ Gozani, Harani,+ Resefu, na watu wa Edeni waliokuwa Tel-asari wako wapi? 13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, na mfalme wa majiji ya Sefarvaimu,+ na wa Hena, na wa Iva?’”

14 Hezekia akachukua barua hizo kutoka mikononi mwa wajumbe na kuzisoma. Kisha Hezekia akapanda kwenda katika nyumba ya Yehova, akazitandaza* mbele za Yehova.+ 15 Hezekia akaanza kusali kwa Yehova+ akisema: 16 “Ee Yehova wa majeshi,+ Mungu wa Israeli, unayeketi kwenye kiti cha ufalme juu ya* makerubi, wewe peke yako ndiye Mungu wa kweli wa falme zote za dunia. Uliumba mbingu na dunia. 17 Tega sikio lako, Ee Yehova, usikie!+ Fungua macho yako, Ee Yehova, uone!+ Sikia maneno yote ambayo Senakeribu amesema ili kukudhihaki wewe Mungu uliye hai.+ 18 Ee Yehova, ni kweli kwamba wafalme wa Ashuru wameharibu nchi zote,+ na pia nchi yao. 19 Nao wameitupa miungu yao motoni,+ kwa sababu haikuwa miungu bali kazi ya mikono ya wanadamu,+ miti na mawe. Ndiyo sababu waliweza kuiangamiza. 20 Lakini sasa, Ee Yehova Mungu wetu, tuokoe kutoka mikononi mwake, ili falme zote duniani zijue kwamba wewe peke yako ndiye Mungu, Ee Yehova.”+

21 Kisha Isaya mwana wa Amozi akatuma ujumbe huu kwa Hezekia: “Yehova Mungu wa Israeli anasema, ‘Kwa sababu ulisali kwangu kuhusu Mfalme Senakeribu wa Ashuru,+ 22 Hili ndilo neno ambalo Yehova amesema dhidi yake:

“Binti bikira wa Sayuni anakudharau, anakudhihaki.

Binti ya Yerusalemu anakutikisia kichwa.

23 Umemdhihaki+ na kumkufuru nani?

Umepaza sauti yako dhidi ya nani+

Na kuinua macho yako yenye kiburi?

Ni dhidi ya Mtakatifu wa Israeli!+

24 Kupitia watumishi wako umemdhihaki Yehova+ ukisema,

‘Kwa wingi wa magari yangu ya vita

Nitapanda vilele vya milima,+

Sehemu za mbali sana za Lebanoni.

Nitakata mierezi yake mirefu sana, miberoshi yake iliyo bora.

Nitaingia mahali pake palipo juu zaidi, misitu yake yenye miti mingi sana.

25 Nitachimba visima na kunywa maji;

Nitavikausha vijito vya* Misri kwa nyayo za miguu yangu.’

26 Je, hujasikia? Tangu zamani za kale liliamuliwa.*

Tangu siku zilizopita nimelitayarisha.*+

Sasa nitalitimiza.+

Utayabadili majiji yenye ngome yawe marundo ya magofu yenye ukiwa.+

27 Wakaaji wake hawatakuwa na uwezo;

Wataogopeshwa na kuaibishwa.

Watakuwa kama mimea ya shambani na nyasi mbichi,

Kama nyasi zilizo kwenye paa zinazokaushwa na upepo wa mashariki.

28 Lakini ninajua vizuri unapoketi, unapotoka nje, unapoingia,+

Na unapokuwa na ghadhabu dhidi yangu,+

29 Kwa sababu ghadhabu yako dhidi yangu+ na mngurumo wako umefika masikioni mwangu.+

Basi nitatia kulabu yangu puani mwako na lijamu yangu+ katikati ya midomo yako,

Nami nitakurudisha kupitia njia uliyotumia kuja.”

30 “‘Na hii ndiyo itakayokuwa ishara kwako:* Mwaka huu utakula mimea inayoota yenyewe;* na katika mwaka wa pili utakula nafaka inayochipuka kutoka katika mimea hiyo; lakini katika mwaka wa tatu utapanda mbegu na kuvuna, nawe utapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.+ 31 Watu wa nyumba ya Yuda watakaoponyoka, wale wanaobaki,+ watatia mizizi chini na kuzaa matunda kwenda juu. 32 Kwa maana waliobaki watatoka Yerusalemu na waokokaji watatoka katika Mlima Sayuni.+ Bidii ya Yehova wa majeshi itatenda hayo.+

33 “‘Kwa hiyo Yehova anasema hivi kuhusu mfalme wa Ashuru:+

“Hataingia katika jiji hili+

Wala hatapiga mshale humo

Wala kulikabili kwa ngao

Wala kujenga boma la kulizingira.”’+

34 ‘Atarudi kupitia njia aliyotumia kuja;

Hataingia katika jiji hili,’ asema Yehova.

35 ‘Nitalilinda jiji hili+ na kuliokoa kwa ajili yangu+ mwenyewe

Na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.’”+

36 Na malaika wa Yehova akaenda na kuwaua wanaume 185,000 katika kambi ya Waashuru. Watu walipoamka asubuhi na mapema, waliona maiti zote hizo.+ 37 Basi Mfalme Senakeribu wa Ashuru akaondoka, akarudi Ninawi+ na kukaa huko.+ 38 Na alipokuwa akiinama katika nyumba ya* Nisroki mungu wake, watoto wake mwenyewe wa kiume Adrameleki na Shareza, walimuua kwa upanga+ na kutorokea nchi ya Ararati.+ Na Esar-hadoni+ mwanawe akawa mfalme baada yake.

38 Katika siku hizo Hezekia akawa mgonjwa karibu afe.+ Nabii Isaya+ mwana wa Amozi akaja na kumwambia, “Yehova anasema hivi: ‘Wape maagizo watu wa nyumba yako, kwa maana utakufa; hutapona.’”+ 2 Ndipo Hezekia akaugeuza uso wake kuelekea ukutani, akaanza kusali hivi kwa Yehova: 3 “Nakusihi, Ee Yehova, tafadhali, kumbuka+ jinsi ambavyo nimetembea mbele zako kwa uaminifu na kwa moyo kamili,+ nami nimetenda mambo mema machoni pako.” Kisha Hezekia akaanza kulia sana na kububujikwa na machozi.

4 Kisha neno la Yehova likamjia Isaya, likisema: 5 “Rudi ukamwambie Hezekia,+ ‘Yehova, Mungu wa Daudi babu yako anasema hivi: “Nimesikia sala yako.+ Nimeona machozi yako.+ Sasa ninakuongezea miaka 15 ya kuishi,*+ 6 nami nitakuokoa wewe na jiji hili kutoka mikononi mwa mfalme wa Ashuru, nami nitalilinda jiji hili.+ 7 Hii ndiyo ishara kutoka kwa Yehova itakayokuonyesha kwamba Yehova atatimiza neno alilosema:+ 8 Nitafanya kivuli cha jua kinachoshuka kwenye ngazi* ya Ahazi kirudi nyuma hatua kumi.”’”+ Basi jua likarudi nyuma hatua kumi kwenye ngazi ambayo tayari lilikuwa limeshuka.

9 Haya ni maandishi ya* Mfalme Hezekia wa Yuda, aliposhikwa na ugonjwa na kupona ugonjwa wake.

10 Nilisema: “Katikati ya maisha yangu

Lazima niingie katika malango ya Kaburi.*

Nitanyimwa miaka yangu iliyobaki.”

11 Nilisema: “Sitamwona Yah,* Yah katika nchi ya walio hai.+

Sitawaona tena wanadamu

Nitakapokuwa pamoja na wakaaji wa mahali ambapo kila kitu hukoma.

12 Makao yangu yameng’olewa na kuondolewa kwangu+

Kama hema la mchungaji.

Nimeukunja uhai wangu kama mfumaji wa nguo;

Ananikata kabisa kama nyuzi za mtande.

Kuanzia mapambazuko mpaka usiku unaendelea kunimaliza.+

13 Nimejituliza mpaka asubuhi.

Kama simba, anaendelea kuivunja mifupa yangu yote;

Kuanzia mapambazuko mpaka usiku unaendelea kunimaliza.+

14 Ninaendelea kulia kama mbayuwayu au teleka;*+

Ninaendelea kulia kama njiwa.+

Macho yangu yanatazama kileleni kwa uchovu:+

‘Ee Yehova, ninataabika sana;

Uwe msaada wangu!’*+

15 Niseme nini?

Amezungumza nami na kutenda.

Nitatembea kwa unyenyekevu* miaka yangu yote

Kwa sababu ya mateso yangu makali.*

16 ‘Ee Yehova, kila mwanadamu anaishi kwa mambo haya,*

Na katika mambo hayo kuna uhai wa roho yangu.

Utaniponya na kunihifadhi hai.+

17 Tazama! Badala ya amani, nilikuwa na uchungu mwingi;

Lakini kwa sababu ulinipenda sana,*

Uliniokoa kutokana na shimo la maangamizi.+

Umezitupa dhambi zangu zote nyuma ya mgongo wako.*+

18 Kwa maana Kaburi* haliwezi kukutukuza,+

Kifo hakiwezi kukusifu.+

Wale wanaoshuka shimoni hawawezi kuutumaini uaminifu wako.+

19 Walio hai, walio hai wanaweza kukusifu,

Kama ninavyoweza leo hii.

Baba anaweza kuwapa wanawe ujuzi kuhusu uaminifu wako.+

20 Ee Yehova, niokoe,

Nasi tutapiga nyimbo zangu kwa vinanda+

Siku zote za maisha yetu katika nyumba ya Yehova.’”+

21 Ndipo Isaya akasema: “Leteni keki ya tini kavu zilizoshinikizwa mlipake jipu hilo, ili apone.”+ 22 Hezekia alikuwa ameuliza: “Ni ishara gani itakayonionyesha kwamba nitapanda kwenda katika nyumba ya Yehova?”+

39 Wakati huo mfalme wa Babiloni, Merodak-baladani mwana wa Baladani alimtumia Hezekia barua na zawadi,+ kwa maana alisikia kwamba alikuwa mgonjwa na sasa amepona.+ 2 Hezekia akawakaribisha kwa furaha* na kuwaonyesha nyumba yake yenye hazina+—fedha, dhahabu, mafuta ya zeri na mafuta mengine yenye thamani, ghala lake lote la silaha, na kila kitu kilichokuwa katika hazina zake. Hakuna kitu chochote ambacho Hezekia hakuwaonyesha katika nyumba yake mwenyewe* na katika milki yake yote.

3 Kisha nabii Isaya akaenda kwa Mfalme Hezekia na kumuuliza: “Watu hawa walisema nini, nao walitoka wapi?” Hezekia akajibu: “Walitoka katika nchi ya mbali, kutoka Babiloni.”+ 4 Kisha akauliza: “Waliona nini katika nyumba yako?”* Hezekia akajibu: “Waliona kila kitu katika nyumba yangu.* Hakuna chochote ambacho sikuwaonyesha katika hazina zangu.”

5 Sasa Isaya akamwambia Hezekia: “Sikia neno la Yehova wa majeshi, 6 ‘Tazama! Siku zinakuja, na vitu vyote vilivyo katika nyumba yako* na vitu vyote ambavyo mababu zako wamehifadhi mpaka leo hii vitapelekwa Babiloni. Hakuna chochote kitakachobaki,’+ asema Yehova.+ 7 ‘Na baadhi ya wana wako mwenyewe utakaowazaa watachukuliwa na kuwa maofisa wa makao ya mfalme katika jumba la mfalme wa Babiloni.’”+

8 Ndipo Hezekia akamwambia Isaya: “Neno la Yehova ambalo umesema ni jema.” Kisha akasema: “Kwa sababu kutakuwa na amani na utulivu* wakati wa maisha yangu.”*+

40 “Wafarijini, wafarijini watu wangu,” asema Mungu wenu.+

 2 “Zungumzeni na moyo wa* Yerusalemu,

Na kulitangazia kwamba utumishi wake wa kulazimishwa umetimizwa,

Kwamba hatia yake imelipwa.+

Limepokea kutoka mkononi mwa Yehova malipo kamili* kwa ajili ya dhambi zake zote.”+

 3 Kuna mtu anayepaza sauti nyikani:

“Fungueni* njia ya Yehova!+

Tengenezeni barabara kuu iliyonyooka+ inayopitia jangwani kwa ajili ya Mungu wetu.+

 4 Kila bonde na liinuliwe,

Na kila mlima na kilima kishushwe.

Na ardhi yenye mashimo-mashimo itasawazishwa,

Na ardhi yenye mawemawe itakuwa bonde tambarare.+

 5 Utukufu wa Yehova utafunuliwa,+

Na wote wenye mwili* watauona pamoja,+

Kwa maana kinywa cha Yehova kimesema hayo.”

 6 Sikilizeni! Kuna mtu anayesema: “Tangaza!”

Mwingine anauliza: “Nitangaze nini?”

“Wote wenye mwili* ni majani mabichi.

Upendo wao wote mshikamanifu ni kama ua la shambani.+

 7 Majani mabichi hukauka,

Ua hunyauka,+

Kwa sababu pumzi* ya Yehova hupuliza juu yake.+

Kwa hakika watu ni majani mabichi tu.

 8 Majani mabichi hukauka,

Ua hunyauka,

Lakini neno la Mungu wetu linadumu milele.”+

 9 Panda juu ya mlima mrefu,

Ewe mwanamke unayeletea Sayuni habari njema.+

Paza sauti yako kwa nguvu,

Ewe mwanamke unayeliletea Yerusalemu habari njema.

Ipaze, usiogope.

Yatangazie majiji ya Yuda: “Tazameni Mungu wenu.”+

10 Tazameni! Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atakuja kwa nguvu,

Na mkono wake utatawala kwa ajili yake.+

Tazameni! Anakuja na thawabu yake,

Na malipo anayotoa yako mbele zake.+

11 Atalitunza* kundi lake kama mchungaji.+

Atawakusanya pamoja wanakondoo kwa mkono wake,

Naye atawabeba kwenye kifua chake.

Atawaongoza kwa upole wale wanaonyonyesha watoto wao.+

12 Ni nani amepima maji katika konzi ya mkono wake+

Na kupima vipimo vya* mbingu kwa shubiri* ya mkono wake?

Ni nani ameyakusanya mavumbi ya dunia katika kipimio+

Au kupima milima katika mizani

Na vilima katika mizani?

13 Ni nani ambaye ameipima* roho ya Yehova,

Na ni nani anayeweza kumfundisha akiwa mshauri wake?+

14 Alishauriana na nani ili apate uelewaji,

Au ni nani anayemfundisha njia ya haki,

Au kumfundisha ujuzi,

Au kumwonyesha njia ya uelewaji wa kweli?+

15 Tazameni! Mataifa ni kama tone kutoka katika ndoo,

Naye huyaona kuwa kama mavumbi membamba juu ya mizani.+

Tazameni! Anaviinua visiwa kama mavumbi laini.

16 Hata Lebanoni haitoshi kufanya moto uendelee kuwaka,*

Na wanyama wake wa mwituni hawatoshi kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa.

17 Mbele zake mataifa yote ni kama kitu kisichokuwepo;+

Anayaona kuwa si kitu, kama ubatili.+

18 Mnaweza kumlinganisha Mungu na nani?+

Mnaweza kumfananisha na nini?+

19 Fundi hutengeneza sanamu,*

Mfua chuma huifunika kwa dhahabu,+

Naye huitengenezea mikufu ya fedha.

20 Huchagua mti fulani uwe mchango wake,+

Mti ambao hautaoza.

Humtafuta fundi stadi

Ili atengeneze sanamu ya kuchongwa ambayo haitaanguka.+

21 Je, hamjui?

Je, hamjasikia?

Je, hamkuambiwa tangu mwanzoni?

Je, hamjaelewa tangu misingi ya dunia ilipowekwa?+

22 Kuna Yule anayekaa juu ya duara ya* dunia,+

Na wakaaji wake ni kama panzi.

Anazitandaza mbingu kama wavu laini,

Naye huzitandaza kama hema la kuishi.+

23 Huwafanya maofisa wakuu kuwa si kitu

Na kuwafanya waamuzi* wa dunia wawe ubatili.

24 Bado hawajapandwa,

Bado hawajatiwa ardhini,

Bado shina lao halijatia mizizi ardhini,

Nao hupuliziwa na kukauka,

Na upepo huwapeperusha mbali kama majani makavu.+

25 “Mnaweza kunifananisha na nani ili niwe sawa naye?” auliza Yule Mtakatifu.

26 “Inueni macho yenu mbinguni mwone.

Ni nani aliyeviumba vitu hivi?+

Ni Yule anayelileta nje jeshi lao kwa hesabu;

Huziita zote kwa majina.+

Kwa sababu ya nguvu zake nyingi zenye msukumo na nguvu zake zenye kuogopesha,+

Hakuna hata moja inayokosekana.

27 Ewe Yakobo, kwa nini unasema, na ewe Israeli, kwa nini unatangaza,

‘Njia yangu imefichwa kutoka kwa Yehova,

Nami sipati haki kutoka kwa Mungu’?+

28 Je, hujui? Je, hujasikia?

Yehova, Muumba wa miisho ya dunia, ni Mungu kwa umilele wote.+

Yeye hachoki kamwe wala haishiwi na nguvu.+

Uelewaji wake hauchunguziki.*+

29 Yeye humpa nguvu mtu aliyechoka

Na kuwapa uwezo kamili wale wasio na nguvu.*+

30 Wavulana watachoka na kuishiwa na nguvu,

Na vijana watajikwaa na kuanguka,

31 Lakini wale wanaomtumaini Yehova watapata nguvu tena.

Watapaa juu kwa mabawa kama tai.+

Watakimbia na hawataishiwa na nguvu;

Watatembea na hawatachoka.”+

41 “Nisikilizeni mkiwa kimya,* enyi visiwa;

Mataifa na yapate nguvu tena.

Na yakaribie; kisha yaongee.+

Na tukutane pamoja kwenye hukumu.

 2 Ni nani amemwinua mtu kutoka mashariki,*+

Akimwita katika uadilifu aje miguuni Pake,*

Ili amkabidhi mataifa

Na kumfanya awatiishe wafalme?+

Ambaye anawafanya wawe mavumbi mbele ya upanga wake,

Kama majani makavu yanayopeperushwa na upepo mbele ya upinde wake?

 3 Anawafuatia, anapita bila kuzuiwa

Kwenye njia ambazo miguu yake haijawahi kupita.

 4 Ni nani ametenda na kufanya jambo hili,

Kuviita vizazi tangu mwanzoni?

Mimi, Yehova, Ndiye wa Kwanza;+

Na kwa wale wa mwisho mimi ni yuleyule.”+

 5 Visiwa vimeona hivyo na kuogopa.

Miisho ya dunia ilianza kutetemeka.

Wanakaribia na kuja mbele.

 6 Kila mmoja anamsaidia mwenzake

Na kumwambia ndugu yake: “Uwe imara.”

 7 Kwa hiyo fundi anamwimarisha mfua chuma;+

Yule anayelainisha kwa nyundo ya chuma

Anamwimarisha yule agongaye kwenye fuawe.

Anasema hivi kuhusu lehemu: “Ni nzuri.”

Kisha inapigiliwa misumari ili isianguke.

 8 “Lakini wewe ni mtumishi wangu, Ee Israeli,+

Wewe niliyekuchagua, Ee Yakobo,+

Uzao wa* rafiki yangu Abrahamu,+

 9 Wewe, niliyekuchukua kutoka kwenye miisho ya dunia,+

Na wewe, niliyekuita kutoka sehemu zake za mbali zaidi.

Nilikuambia, ‘Wewe ni mtumishi wangu;+

Nimekuchagua wewe; sijakukataa.+

10 Usiogope, kwa maana mimi niko pamoja nawe.+

Usihangaike, kwa maana mimi ni Mungu wako.+

Nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia,+

Nitakushika kwelikweli kwa mkono wangu wa kuume wa uadilifu.’

11 Tazama! Wale wote wanaowaka hasira dhidi yako wataaibishwa na kufedheheshwa.+

Wale wanaopigana nawe watafanywa kuwa si kitu na wataangamia.+

12 Utawatafuta watu wanaopambana nawe, lakini hutawapata;

Watu wanaopigana nawe watakuwa kama kitu kisichokuwepo, watakuwa si kitu kabisa.+

13 Kwa maana mimi, Yehova Mungu wako, ninaushika kwa nguvu mkono wako wa kulia,

Mimi ninayekuambia, ‘Usiogope. Nitakusaidia.’+

14 Usiogope, wewe mnyoo* Yakobo,+

Ninyi watu wa Israeli, nitawasaidia,” asema Yehova, Mkombozi wenu,+ Mtakatifu wa Israeli.

15 “Tazama! Nimekufanya uwe kifaa cha kupuria,+

Kifaa kipya cha kupuria chenye meno yenye makali pande mbili.

Utaikanyaga-kanyaga milima na kuipondaponda

Na kuvifanya vilima viwe kama makapi.

16 Utawapepeta,

Na upepo utawapeperusha mbali;

Dhoruba ya upepo itawatawanya.

Utashangilia katika Yehova,+

Nawe utajigamba katika Mtakatifu wa Israeli.”+

17 “Wenye uhitaji na maskini wanatafuta maji, lakini hayapo.

Ulimi wao umekauka kwa sababu ya kiu.+

Mimi, Yehova, nitawajibu.+

Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.+

18 Nitafanya mito itiririke kwenye vilima visivyo na kitu+

Na chemchemi katika mabonde tambarare.+

Nitaigeuza nyika kuwa dimbwi la maji lenye matete

Na nchi isiyo na maji kuwa chemchemi za maji.+

19 Nitapanda mwerezi jangwani,

Mshita na mhadasi na msonobari,+

Nitapanda mberoshi katika jangwa tambarare,

Pamoja na mtidhari na mvinje,+

20 Ili watu wote waone na kujua

Wakaze fikira na kuelewa

Kwamba mkono wa Yehova umetenda hayo,

Na Mtakatifu wa Israeli ameliumba jambo hilo.”+

21 “Leteni kesi yenu,” asema Yehova.

“Toeni hoja zenu,” asema Mfalme wa Yakobo.

22 “Leteni ushahidi na mtuambie mambo yatakayotendeka.

Tuambieni kuhusu mambo ya zamani,*

Ili tuyatafakari* na kujua matokeo yake

Au mtutangazie mambo yanayokuja.+

23 Tuambieni mambo yatakayotokea wakati ujao,

Ili tujue kwamba ninyi ni miungu.+

Naam, fanyeni jambo, zuri au baya,

Ili tushangae tutakapoliona.+

24 Tazameni! Ninyi ni kitu kisichokuwepo,

Na mafanikio yenu si kitu.+

Mtu yeyote anayewachagua ninyi anachukiza.+

25 Nimemwinua mtu kutoka kaskazini, naye atakuja,+

Kutoka upande wa mapambazuko ya jua,*+ atakayeliitia jina langu.

Atawakanyaga-kanyaga watawala* kana kwamba wao ni udongo,+

Kama mfinyanzi anayeukanyaga-kanyaga udongo wenye maji.

26 Ni nani aliyesema jambo hilo tangu mwanzoni, ili tulijue,

Au kutoka nyakati za zamani, ili tuseme, ‘Yeye anasema kweli’?+

Kwa kweli, hakuna mtu aliyelitangaza!

Hakuna mtu aliyelisema!

Hakuna mtu aliyesikia lolote kutoka kwenu!”+

27 Nilikuwa wa kwanza kumwambia Sayuni: “Tazama! Wako hapa!”+

Na kwa Yerusalemu nitamtuma mtu anayepeleka habari njema.+

28 Lakini niliendelea kutazama, na hapakuwa na mtu;

Hakukuwa na mtu yeyote kati yao ambaye angetoa ushauri.

Nami niliendelea kuwaomba wanijibu.

29 Tazameni! Wote ni udanganyifu.*

Kazi zao si kitu.

Sanamu zao za chuma* ni upepo na ubatili.+

42 Tazama! Mtumishi wangu,+ ninayemtegemeza!

Mchaguliwa wangu,+ ambaye nimemkubali!*+

Nimeitia roho yangu ndani yake;+

Atayaletea mataifa haki.+

 2 Hatalia kwa sauti wala kupaza sauti yake,

Naye hatafanya sauti yake isikike barabarani.+

 3 Hataponda tete lililovunjika,

Wala hatazima utambi unaofifia.+

Ataleta haki kwa uaminifu.+

 4 Hatafifia wala kupondwa mpaka atakapoimarisha haki duniani;+

Na visiwa vinaendelea kungojea sheria* yake.

 5 Hivi ndivyo anavyosema Mungu wa kweli, Yehova,

Muumba wa mbingu na Mkuu aliyezitandaza,+

Yule aliyeitandaza dunia na mazao yake,+

Yule anayewapa pumzi watu waliomo+

Na kuwapa roho wale wanaotembea humo:+

 6 “Mimi, Yehova, nimekuita katika uadilifu;

Nimekushika mkono wako.

Nitakulinda na kukutoa uwe agano kwa ajili ya watu+

Na uwe nuru kwa mataifa,+

 7 Ili uyafungue macho yaliyopofuka,+

Ili umtoe mfungwa katika gereza lililo chini ya ardhi

Na wale wanaoketi gizani kutoka gerezani.+

 8 Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu;

Simpi yeyote utukufu wangu,*

Wala kuzipa sanamu za kuchongwa sifa yangu.+

 9 Tazameni, mambo ya kwanza yametokea;

Sasa ninatangaza mambo mapya.

Kabla hayajatokea, ninawaambia kuyahusu.”+

10 Mwimbieni Yehova wimbo mpya,+

Sifa yake kutoka kwenye miisho ya dunia,+

Ninyi mnaoshuka baharini na pia vyote vinavyoijaza,

Ninyi visiwa na wakaaji wake.+

11 Nyika na majiji yake na yapaze sauti yao,+

Makao ambamo Kedari anaishi.+

Wale wanaokaa kwenye jabali na wapige vigelegele kwa shangwe;

Na wapaze sauti kutoka kwenye vilele vya milima.

12 Na wamtukuze Yehova

Na watangaze sifa zake katika visiwa.+

13 Yehova atatoka kama mwanamume hodari.+

Ataamsha bidii yake kama shujaa.+

Atapaza sauti, naam, atapiga kelele za vita;

Ataonyesha kwamba ana nguvu kuliko maadui wake.+

14 “Nimenyamaza kwa muda mrefu.

Niliendelea kukaa kimya na kujizuia.

Kama mwanamke anayezaa,

Nitalia kwa uchungu, nitahemahema, na kutweta wakati uleule.

15 Nitaiharibu milima na vilima

Na kukausha kabisa majani yake yote.

Nitaibadili mito iwe visiwa*

Na kuyakausha kabisa madimbwi ya maji yenye matete.+

16 Nitawaongoza vipofu kwenye njia wasiyoijua+

Na kuwafanya watembee kwenye vijia wasivyovijua.+

Nitabadili giza lililo mbele yao liwe nuru+

Na kubadili eneo lenye mawemawe kuwa nchi tambarare.+

Hivyo ndivyo nitakavyowatendea, nami sitawaacha.”

17 Watarudishwa nyuma na kuaibishwa kabisa,

Wale wanaotumaini sanamu za kuchongwa,

Wale wanaoziambia sanamu za chuma:* “Ninyi ni miungu yetu.”+

18 Sikilizeni, ninyi viziwi;

Tazameni na mwone, ninyi vipofu.+

19 Ni nani aliye kipofu isipokuwa mtumishi wangu,

Aliye kiziwi sana kama mjumbe ninayemtuma?

Ni nani aliye kipofu sana kama yule ambaye amethawabishwa,

Aliye kipofu sana kama mtumishi wa Yehova?+

20 Unaona mambo mengi, lakini huendelei kukaa macho.

Unafungua masikio yako, lakini husikilizi.+

21 Kwa sababu ya uadilifu wake,

Yehova amependezwa kuitukuza sheria* na kuifanya iwe na utukufu.

22 Lakini watu hawa ni watu walioporwa na kutekwa nyara;+

Wote wamenaswa katika mashimo na kufichwa magerezani.+

Wameporwa na hakuna yeyote wa kuwaokoa,+

Nao wametekwa nyara na hakuna yeyote wa kusema: “Warudisheni!”

23 Ni nani kati yenu atakayesikia jambo hili?

Ni nani atakayetega sikio na kusikiliza kwa ajili ya wakati ujao?

24 Ni nani aliyemtia Yakobo mikononi mwa watekaji nyara

Na Israeli mikononi mwa waporaji?

Je, si Yehova, Yule ambaye tumemtendea dhambi?

Walikataa kutembea katika njia Zake,

Nao hawakutii sheria* Yake.+

25 Basi Yeye akaendelea kummwagia ghadhabu,

Hasira yake na ghadhabu ya vita.+

Iliteketeza kila kitu kumzunguka, lakini hakulikazia jambo hilo fikira.+

Iliwaka dhidi yake, lakini hakulitia jambo hilo moyoni.+

43 Sasa hivi ndivyo anavyosema Yehova,

Muumba wako, Ee Yakobo, Yule aliyekuumba, Ee Israeli:+

“Usiogope, kwa maana nimekukomboa.+

Nimekuita kwa jina lako.

Wewe ni mali yangu.

 2 Unapopita katika maji, nitakuwa pamoja nawe,+

Na unapopita katika mito, haitafurika na kukufunika.+

Unapotembea katika moto, hutateketea,

Wala mwali wa moto hautakuunguza.

 3 Kwa maana mimi ni Yehova Mungu wako,

Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako.

Nimeitoa Misri kuwa fidia kwa ajili yako,

Ethiopia na Seba badala yako.

 4 Kwa sababu ulikuwa mwenye thamani machoni pangu,+

Uliheshimiwa, nami nimekupenda.+

Basi nitawatoa watu badala yako

Na mataifa badala ya uhai wako.*

 5 Usiogope, kwa maana nipo pamoja nawe.+

Nitauleta uzao wako* kutoka mashariki

Na kukukusanya kutoka magharibi.+

 6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’+

Na kusini, ‘Usiwazuie.

Walete wanangu kutoka mbali, na mabinti wangu kutoka kwenye miisho ya dunia,+

 7 Kila mtu anayeitwa kwa jina langu+

Na niliyemuumba kwa ajili ya utukufu wangu,

Ambaye nimemuumba na kumtokeza.’+

 8 Waleteni watu walio vipofu, ingawa wana macho,

Na walio viziwi, ingawa wana masikio.+

 9 Mataifa yote na yakusanyike mahali pamoja,

Na watu wakusanyike pamoja.+

Ni nani kati yao anayeweza kutangaza haya?

Au, je, wanaweza kutufanya tusikie mambo ya kwanza?*+

Na watoe mashahidi wao ili kuthibitisha kwamba wanasema ukweli,

Au acha wasikie na kusema, ‘Ni ukweli!’”+

10 “Ninyi ni mashahidi wangu,”+ asema Yehova,

“Naam, mtumishi wangu ambaye nimemchagua,+

Ili mjue na kuwa na imani kwangu*

Na mwelewe kwamba mimi ni yuleyule.+

Kabla yangu hakuna Mungu aliyefanyizwa,

Na baada yangu hakutakuwa na mwingine.+

11 Mimi—mimi ni Yehova,+ na zaidi yangu hakuna mwokozi.”+

12 “Mimi ndiye niliyetangaza na kuokoa na kujulisha

Kulipokuwa hakuna mungu wa kigeni miongoni mwenu.+

Basi ninyi ni mashahidi wangu,” asema Yehova, “nami ni Mungu.+

13 Pia, mimi ni yuleyule sikuzote;+

Na hakuna yeyote anayeweza kunyakua chochote kutoka mkononi mwangu.+

Ninapotenda, ni nani anayeweza kunizuia?”+

14 Yehova, Mkombozi wenu,+ Mtakatifu wa Israeli,+ anasema hivi:

“Nitatuma ujumbe huko Babiloni kwa ajili yenu na kuyashusha makomeo yote ya malango,+

Na Wakaldayo, katika meli zao, watalia kwa sababu ya mateso.+

15 Mimi ni Yehova, Mtakatifu wenu,+ Muumba wa Israeli,+ Mfalme wenu.”+

16 Yehova anasema hivi:

Yule anayetengeneza njia baharini

Na mahali pa kupita hata katika maji yenye msukosuko,+

17 Yule anayelivuta gari la vita na farasi,+

Jeshi pamoja na mashujaa hodari:

“Watalala chini na hawataamka.+

Watazimwa, watazimwa mara moja kama utambi unaowaka.”

18 “Msikumbuke mambo ya kwanza,

Wala msifikirie sana mambo ya zamani.

19 Tazameni! Ninatenda jambo jipya;+

Hata sasa linachipuka.

Je, hamlitambui?

Nitatengeneza njia nyikani+

Na mito jangwani.+

20 Mnyama wa mwituni ataniheshimu,

Mbwamwitu na mbuni,

Kwa maana ninatokeza maji nyikani,

Mito jangwani,+

Ili watu wangu wanywe, naam, mchaguliwa wangu,+

21 Watu niliojiumbia

Ili watangaze sifa zangu.+

22 Lakini hujaniita mimi, Ee Yakobo,+

Kwa sababu ulichoshwa nami, Ee Israeli.+

23 Hujaniletea kondoo kwa ajili ya dhabihu zako nzima za kuteketezwa

Wala kunitukuza kwa dhabihu zako.

Sijakulazimisha uniletee zawadi,

Wala sijakuchosha kwa kudai ubani.+

24 Hukuninunulia utete wenye manukato kwa pesa zako,

Wala hukuniridhisha kwa mafuta ya dhabihu zako.+

Badala yake, umenilemea kwa dhambi zako

Na kunichosha kwa maovu yako.+

25 Mimi, mimi ndiye ninayeyafuta kabisa makosa*+ yako kwa ajili yangu,+

Nami sitazikumbuka dhambi zako.+

26 Nikumbushe; na tukutane ili tufanye kesi;

Toa hoja zako ili kuthibitisha kwamba unasema ukweli.

27 Babu yako wa kwanza alitenda dhambi,

Na wasemaji* wako mwenyewe wameniasi.+

28 Kwa hiyo nitawatia unajisi wakuu wa mahali patakatifu,

Nami nitamtoa Yakobo aangamizwe

Na kumfanya Israeli atukanwe.+

44 “Sasa sikiliza, Ee Yakobo mtumishi wangu,

Nawe, Ee Israeli, ambaye nimekuchagua.+

 2 Hivi ndivyo anavyosema Yehova,

Muumba wako, Yule aliyekutokeza,+

Ambaye amekusaidia tangu ulipokuwa tumboni:*

‘Usiogope, mtumishi wangu Yakobo,+

Na wewe, Yeshuruni,*+ ambaye nimekuchagua.

 3 Kwa maana nitammiminia maji mwenye kiu*+

Na kumimina vijito vinavyotiririka kwenye ardhi iliyokauka.

Nitaimimina roho yangu juu ya uzao wako*+

Na baraka yangu juu ya wazao wako.

 4 Nao watachipuka kama majani mabichi,+

Kama mierebi kando ya vijito vya maji.

 5 Mtu mmoja atasema: “Mimi ni mali ya Yehova.”+

Mwingine atajiita kwa jina la Yakobo,

Na mwingine ataandika kwenye mkono wake: “Mali ya Yehova.”

Naye atalichukua jina la Israeli.’

 6 Yehova, Mfalme wa Israeli+ na Mkombozi wake,+

Yehova wa majeshi, anasema hivi:

‘Mimi ndiye wa kwanza na mimi ndiye wa mwisho.+

Hakuna Mungu ila mimi.+

 7 Ni nani aliye kama mimi?+

Na aseme kwa sauti, atangaze, na kunithibitishia!+

Tangu nilipowatokeza watu wa zamani za kale,

Na waseme mambo yatakayokuja

Na yale yatakayotokea.

 8 Msiogope,

Wala msilemazwe na woga.+

Je, sikumwambia kila mmoja wenu mapema na kutangaza jambo hilo?

Ninyi ni mashahidi wangu.+

Je, kuna Mungu zaidi yangu?

Hapana, hakuna Mwamba mwingine;+ simjui mwingine.’”

 9 Wale wote wanaotengeneza sanamu za kuchongwa hawana thamani yoyote,

Na vitu wanavyovipenda sana havitakuwa na faida yoyote.+

Vikiwa kama mashahidi wao, havioni* chochote wala havijui chochote,+

Basi waliovitengeneza vitu hivyo wataaibishwa.+

10 Ni nani anayeweza kutengeneza mungu au sanamu ya chuma*

Ambayo haina faida yoyote?+

11 Tazameni! Wenzake wote wataaibishwa!+

Mafundi ni wanadamu tu.

Wote na wakusanyike na kusimama.

Watashikwa na hofu na kuaibishwa pamoja.

12 Mhunzi hutengeneza sanamu ya chuma kwenye makaa kwa kifaa chake.*

Anaiunda kwa nyundo,

Anaitengeneza kwa mkono wake wenye nguvu.+

Kisha anahisi njaa na kuishiwa na nguvu;

Hanywi maji na anachoka.

13 Mchongaji wa mbao huinyoosha kamba ya kupimia, huchora umbo akitumia chokaa nyekundu.

Huchonga sanamu kwa patasi na kuchora kwa bikari.

Anaichonga kwa umbo la mwanadamu,+

Kwa uzuri wa mwanadamu,

Ili ikae katika nyumba.*+

14 Kuna mtu ambaye kazi yake ni kukata mierezi.

Huchagua mti wa aina fulani, mwaloni,

Naye huuacha uwe imara kati ya miti ya msituni.+

Hupanda mlaurusi, na mvua huufanya ukue.

15 Kisha unakuwa kuni zinazotumiwa na mwanadamu kuwasha moto.

Huchukua baadhi yake ili aote moto;

Huwasha moto na kuoka mkate.

Lakini pia hutengeneza mungu na kumwabudu.

Huutengeneza kuwa sanamu ya kuchongwa, na kuiinamia.+

16 Nusu yake huiteketeza motoni;

Kwa nusu hiyo huchoma nyama anayokula, naye hushiba.

Pia huota moto na kusema:

“Aha! Ninahisi joto ninapotazama moto.”

17 Lakini sehemu inayobaki anaifanya kuwa mungu, kuwa sanamu yake ya kuchongwa.

Anaiinamia na kuiabudu.

Anasali kwake na kusema:

“Niokoe, kwa maana wewe ni mungu wangu.”+

18 Hawajui chochote, hawaelewi chochote,+

Kwa sababu macho yao yamefungwa kabisa na hayawezi kuona,

Na moyo wao hauna ufahamu.

19 Hakuna mtu anayetafakari moyoni mwake

Wala aliye na ujuzi na uelewaji, anayesema:

“Nusu yake niliiteketeza motoni,

Nami nimeoka mkate juu ya makaa yake na kuchoma nyama ya kula.

Basi, je, ninapaswa kutumia sehemu inayobaki kutengeneza kitu kinachochukiza?+

Je, ninapaswa kuabudu kipande cha mbao?”*

20 Anakula majivu.

Moyo wake mwenyewe uliodanganyika umempotosha.

Hawezi kujiokoa,* wala hasemi:

“Je, hamna uwongo katika mkono wangu wa kulia?”

21 “Kumbuka mambo haya, Ee Yakobo, na wewe, Ee Israeli,

Kwa maana wewe ni mtumishi wangu.

Nilikutokeza, nawe ni mtumishi wangu.+

Ee Israeli, sitakusahau.+

22 Nitayafuta kabisa makosa yako kama kwa wingu+

Na dhambi zako kama kwa wingu zito.

Rudi kwangu, kwa maana nitakukomboa.+

23 Pigeni vigelegele kwa shangwe, enyi mbingu,

Kwa maana Yehova ametenda!

Pazeni sauti kwa ushindi, enyi sehemu zenye kina za dunia!

Pazeni sauti kwa shangwe, enyi milima,+

Ewe msitu, na miti yako yote!

Kwa maana Yehova amemkomboa Yakobo,

Na juu ya Israeli anaonyesha fahari yake.”+

24 Yehova, Mkombozi wako,+

Aliyekuumba tangu ulipokuwa tumboni, anasema hivi:

“Mimi ni Yehova, niliyeumba kila kitu.

Nilizitandaza mbingu mimi mwenyewe,+

Na kuitandaza dunia.+

Ni nani aliyekuwa pamoja nami?

25 Ninazivuruga ishara za wale wanaoongea maneno matupu,*

Na mimi ndiye ninayewafanya wabashiri watende kama wapumbavu;+

Ninayewavuruga watu wenye hekima

Na kubadili ujuzi wao kuwa upumbavu;+

26 Ni mimi ninayefanya neno la mtumishi wangu litimie

Na kutimiza kikamili utabiri wa wajumbe wangu;+

Ninayesema kuhusu Yerusalemu, ‘Litakaliwa,’+

Na kuhusu majiji ya Yuda, ‘Yatajengwa upya,+

Nami nitajenga upya magofu yake’;+

27 Ninayeviambia vilindi vya maji, ‘Kauka,

Nami nitaikausha mito yako yote’;+

28 Ninayesema kumhusu Koreshi,+ ‘Yeye ni mchungaji wangu,

Naye atatimiza kikamili mapenzi yangu yote’;+

Ninayesema kuhusu Yerusalemu, ‘Litajengwa upya,’

Na kuhusu hekalu, ‘Msingi wako utawekwa.’”+

45 Hivi ndivyo Yehova anavyomwambia mtiwa-mafuta wake, Koreshi,+

Ambaye nimeushika mkono wake wa kulia+

Ili kuyatiisha mataifa mbele yake,+

Kuwanyang’anya silaha* wafalme,

Kufungua mbele yake milango yenye pande mbili,

Hivi kwamba malango hayatafungwa:

 2 “Mimi nitaenda mbele yako,+

Nami nitavisawazisha vilima.

Nitaivunja milango ya shaba vipandevipande,

Nami nitayakata makomeo ya chuma.+

 3 Nitakupa hazina zilizo gizani

Na hazina zilizofichwa mafichoni,+

Ili ujue kwamba mimi ni Yehova,

Mungu wa Israeli, anayekuita kwa jina lako.+

 4 Kwa ajili ya mtumishi wangu Yakobo na Israeli niliyemchagua,

Ninakuita kwa jina.

Ninakupa jina la heshima, ingawa hukunijua.

 5 Mimi ni Yehova, na hakuna mwingine yeyote.

Hakuna Mungu ila mimi.+

Nitakuimarisha,* ingawa hukunijua,

 6 Ili watu wajue

Kutoka mashariki hadi magharibi*

Kwamba hakuna mwingine ila mimi.+

Mimi ni Yehova, na hakuna mwingine yeyote.+

 7 Ninatengeneza nuru+ na kuumba giza,+

Ninatokeza amani+ na kuumba msiba;+

Mimi, Yehova, ninafanya mambo hayo yote.

 8 Enyi mbingu, leteni mvua kutoka juu;+

Mawingu na yamwage uadilifu.

Dunia na ifunguke na kuzaa wokovu kwa wingi,

Na ichipushe uadilifu wakati uleule.+

Mimi, Yehova, nimeiumba.”

 9 Ole wake yule anayeshindana* na Muumba wake,*

Kwa maana yeye ni kigae cha udongo tu

Kati ya vigae vingine vya udongo vilivyo ardhini!

Je, udongo unapaswa kumuuliza Mfinyanzi:* “Unatengeneza nini?”+

Au kitu ulichokitengeneza kinapaswa kuuliza: “Yeye hana mikono”?*

10 Ole wake anayemwambia baba: “Unazaa nini?”

Na kumwambia mwanamke: “Unajifungua nini?”*

11 Yehova, Mtakatifu wa Israeli na Muumba wake,+ anasema hivi:

“Je, mnathubutu kuniuliza kuhusu mambo yanayokuja

Na kuniamuru kuhusu wanangu+ na kuhusu kazi za mikono yangu?

12 Niliiumba dunia+ na kumuumba mwanadamu juu yake.+

Nilizitandaza mbingu kwa mikono yangu mwenyewe,+

Nami ninaliamuru jeshi lake lote.”+

13 “Nimemwinua mtu katika uadilifu,+

Nami nitazinyoosha njia zake zote.

Yeye ndiye atakayelijenga jiji langu+

Na kuwaweka huru bila bei au rushwa+ watu wangu waliotekwa,”+ asema Yehova wa majeshi.

14 Yehova anasema hivi:

“Faida ya* Misri na bidhaa za* Ethiopia na Wasabea, watu warefu,

Watakuja kwako na kuwa wako.

Watatembea nyuma yako wakiwa na minyororo.

Watakuja na kukuinamia.+

Watasali kwako wakisema, ‘Kwa hakika Mungu yuko pamoja nawe,+

Na hakuna mwingine yeyote; hakuna Mungu mwingine.’”

15 Kwa kweli wewe ni Mungu anayejificha,

Ee Mungu wa Israeli, Mwokozi.+

16 Wote wataaibishwa na kufedheheshwa;

Watengenezaji wote wa sanamu wataenda zao kwa aibu.+

17 Lakini Israeli ataokolewa na Yehova kwa wokovu wa milele.+

Hamtaaibishwa wala kufedheheshwa kwa umilele wote.+

18 Kwa maana Yehova,

Muumba wa mbingu,+ Mungu wa kweli,

Yule aliyeiumba dunia, Yule aliyeitengeneza na kuifanya imara kabisa,+

Ambaye hakuiumba tu bila sababu,* lakini aliiumba ili ikaliwe, anasema hivi:+

“Mimi ni Yehova, wala hakuna mwingine.

19 Sikusema nikiwa mafichoni,+ katika nchi yenye giza;

Sikuuambia uzao wa* Yakobo,

‘Nitafuteni tu bila sababu.’*

Mimi ni Yehova, ninayesema mambo ya uadilifu na kutangaza mambo manyoofu.+

20 Kusanyikeni pamoja mje.

Karibieni pamoja, ninyi mlioponyoka kutoka kwa mataifa.+

Wale wanaobeba sanamu zilizochongwa hawajui chochote

Na wanasali kwa mungu ambaye hawezi kuwaokoa.+

21 Toeni taarifa yenu, leteni kesi yenu.

Na washauriane pamoja kwa umoja.

Ni nani aliyetabiri jambo hili zamani za kale

Na kulitangaza tangu nyakati zilizopita?

Je, si mimi, Yehova?

Hakuna Mungu mwingine ila mimi;

Mungu mwadilifu na Mwokozi,+ hakuna mwingine isipokuwa mimi.+

22 Geukeni mje kwangu mwokolewe,+ miisho yote ya dunia,

Kwa maana mimi ni Mungu, na hakuna mwingine.+

23 Nimeapa kwa nafsi yangu;

Neno limetoka kinywani mwangu katika uadilifu,

Nalo halitarudi:+

Kila goti litapigwa mbele zangu,

Kila ulimi utaapa kuwa mshikamanifu+

24 Na useme, ‘Kwa hakika katika Yehova kuna uadilifu wa kweli na nguvu.

Wale wote wenye ghadhabu dhidi yake watakuja mbele zake kwa aibu.

25 Katika Yehova uzao* wote wa Israeli utathibitika kuwa sawa,+

Nao watajigamba katika yeye.’”

46 Beli anainama chini,+ Nebo anainama.

Sanamu zao zimewekwa juu ya wanyama, juu ya wanyama wanaobeba mizigo,+

Kama mizigo inayowalemea wanyama waliochoka.

 2 Wanainama na kujiinamisha pamoja;

Hawawezi kuiokoa mizigo,*

Nao wenyewe wanaenda utekwani.

 3 “Nisikilize mimi, Ee nyumba ya Yakobo, nanyi nyote mnaobaki wa nyumba ya Israeli,+

Ninyi niliowategemeza tangu mlipozaliwa na kuwabeba tangu tumboni.+

 4 Hata utakapozeeka nitakuwa yuleyule;+

Hata kichwa chako kikiwa na mvi nitaendelea kukubeba.

Kama nilivyofanya, nitakubeba na kukuchukua na kukuokoa.+

 5 Mtanifananisha na nani au kunifanya niwe sawa na nani au kunilinganisha na nani,+

Ili tufanane naye?+

 6 Kuna wale wanaomwaga dhahabu kwa wingi kutoka kwenye mikoba yao;

Wanapima fedha katika mizani.

Wanamwajiri mfua chuma, naye huitengeneza kuwa mungu.+

Kisha wanasujudu, naam, wanaiabudu.*+

 7 Wanaiinua na kujitwika mabegani;+

Wanaibeba na kuiweka mahali pake, nayo husimama papo hapo.

Haiondoki mahali pake.+

Wanaipazia sauti, lakini haiwajibu;

Haiwezi kumwokoa yeyote kutoka katika taabu yake.+

 8 Kumbukeni hilo, na mjipe ujasiri.

Litieni moyoni, ninyi wakosaji.

 9 Kumbukeni mambo ya kwanza* ya zamani za kale,

Kwamba mimi ni Mungu, na hakuna mwingine.

Mimi ni Mungu, na hakuna aliye kama mimi.+

10 Tangu mwanzo ninatabiri matokeo,

Na tangu zamani za kale mambo ambayo bado hayajafanywa.+

Ninasema, ‘Uamuzi* wangu utasimama,+

Nami nitafanya jambo lolote ninalopenda.’+

11 Ninamwita kutoka mashariki* ndege anayewinda,+

Kutoka nchi ya mbali mtu atakayetekeleza uamuzi* wangu.+

Nimesema, nami nitalitimiza.

Nimekusudia, nami pia nitalitekeleza.+

12 Nisikilizeni, ninyi mlio na moyo mkaidi,*

Ninyi mlio mbali sana na uadilifu.

13 Nimeuleta karibu uadilifu wangu;

Hauko mbali sana,

Na wokovu wangu hautakawia.+

Nitaleta wokovu katika Sayuni, na fahari yangu kwa Israeli.”+

47 Shuka uje uketi mavumbini,

Ewe binti ya Babiloni uliye bikira.+

Keti ardhini ambapo hakuna kiti cha ufalme,+

Ewe binti ya Wakaldayo,

Kwa maana watu hawatakuita tena wewe mwororo na aliyedekezwa.

 2 Chukua jiwe la kusagia na usage unga.

Vua shela yako.

Vua rinda lako, funua miguu yako.

Vuka mito.

 3 Uchi wako utafunuliwa.

Aibu yako itaonekana.

Nitalipiza kisasi,+ na hakuna mtu atakayenizuia.*

 4 “Yule anayetukomboa

—Yehova wa majeshi ndilo jina lake—

Ndiye Mtakatifu wa Israeli.”+

 5 Keti hapo kimya na uingie gizani,

Ewe binti ya Wakaldayo;+

Hawatakuita tena Bimkubwa* wa Falme.+

 6 Nilikuwa na ghadhabu kuwaelekea watu wangu.+

Niliutia unajisi urithi wangu,+

Nami nikawatia mkononi mwako.+

Lakini hukuwaonyesha rehema.+

Hata juu ya wazee uliweka nira nzito.+

 7 Ulisema: “Sikuzote nitakuwa Bimkubwa,* milele.”+

Hukutia mambo haya moyoni mwako;

Hukufikiria mwisho wa jambo hilo.

 8 Sasa sikia jambo hili, ewe mpenda raha,+

Unayeketi kwa usalama, unayesema moyoni mwako:

“Mimi ndiye, na hakuna mwingine.+

Sitakuwa mjane.

Sitajua kamwe inavyokuwa kupoteza watoto.”+

 9 Lakini mambo haya mawili yatakupata ghafla, kwa siku moja:+

Kupoteza watoto na ujane.

Yatakupata kwa kipimo kamili+

Kwa sababu ya* ulozi wako mwingi na uchawi wako wenye nguvu.+

10 Uliutumaini uovu wako.

Ulisema: “Hakuna anayeniona.”

Hekima na ujuzi wako ndivyo vilivyokupotosha,

Nawe unasema moyoni mwako: “Mimi ndiye, na hakuna mwingine.”

11 Lakini utapatwa na msiba,

Na hakuna hirizi yako yoyote itakayouzuia.*

Utapatwa na shida; nawe hutaweza kuizuia.

Utakumbwa na uharibifu wa ghafla ambao hujawahi kamwe kuona.+

12 Basi, endelea kufanya uchawi na ulozi wako mwingi,+

Ambao umeutaabikia tangu ujana wako.

Labda utafaidika;

Labda utawatisha watu.

13 Umechoka kwa wingi wa washauri wako.

Na wasimame sasa na kukuokoa,

Wale wanaoabudu mbingu,* wanaotazama nyota,+

Wale wanaotoa ujuzi wakati wa miezi mipya

Kuhusu mambo yatakayokupata.

14 Tazameni! Wao ni kama majani makavu.

Moto utawateketeza kabisa.

Hawawezi kujiokoa* kutoka kwenye nguvu za mwali wa moto.

Hawa si makaa ya kujipasha moto,

Na huu si moto wa kuota.

15 Ndivyo wachawi wako watakavyokuwa kwako,

Wale ambao ulitaabika nao tangu ujana wako.

Watatangatanga, kila mmoja kuelekea upande wake.*

Hakutakuwa na yeyote wa kukuokoa.+

48 Sikieni hili, enyi watu wa nyumba ya Yakobo,

Ninyi mnaojiita kwa jina la Israeli+

Na ambao mmetoka katika maji ya Yuda,*

Ninyi mnaoapa kwa jina la Yehova+

Na mnaomwitia Mungu wa Israeli,

Ingawa si katika kweli na uadilifu.+

 2 Kwa maana wanajiita kwa jina la jiji takatifu+

Na kutafuta msaada wa Mungu wa Israeli,+

Ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi.

 3 “Mambo ya kwanza* niliwaambia zamani za kale.

Yalitoka kinywani mwangu,

Nami niliyatangaza.+

Kwa ghafla nilichukua hatua, nayo yakatokea.+

 4 Kwa sababu nilijua jinsi ulivyo mkaidi

—Kwamba shingo yako ni kano ya chuma na paji la uso wako ni shaba+—

 5 Nilikuambia zamani za kale.

Kabla halijatukia, nilikufanya ulisikie,

Hivi kwamba hungeweza kusema, ‘Sanamu yangu ilifanya hivi;

Sanamu yangu ya kuchongwa na sanamu yangu ya chuma* ziliamuru jambo hili.’

 6 Umesikia na kuona mambo haya yote.

Je, hutayatangaza?+

Kuanzia sasa na kuendelea ninakutangazia mambo mapya,+

Siri zilizofichwa ambazo hujazijua.

 7 Ni sasa yanapoumbwa, si zamani za kale,

Mambo ambayo kabla ya leo hukuwahi kuyasikia,

Hivi kwamba huwezi kusema, ‘Tazama! Tayari ninayajua.’

 8 Hapana, hujasikia,+ hujajua,

Na zamani masikio yako hayakuwa yamefunguliwa.

Kwa maana ninajua kwamba wewe ni mwenye hila sana,+

Nawe umeitwa mkosaji tangu ulipozaliwa.+

 9 Lakini kwa sababu ya jina langu nitaizuia hasira yangu;+

Kwa ajili ya sifa yangu mwenyewe nitajizuia,

Nami sitakuangamiza.+

10 Tazama! Nimekusafisha, lakini si kama fedha.+

Nimekujaribu* katika tanuru la kuyeyushia la mateso.+

11 Nitatenda kwa ajili yangu mwenyewe, kwa ajili yangu mwenyewe nitatenda,+

Ninawezaje kukubali nitiwe unajisi?+

Simpi yeyote utukufu wangu.*

12 Nisikilize mimi, Ee Yakobo, na Israeli, ambaye nimemwita.

Mimi ni yuleyule.+ Mimi ndiye wa kwanza; mimi pia ndiye wa mwisho.+

13 Mkono wangu mwenyewe uliuweka msingi wa dunia,+

Na mkono wangu wa kuume ulizitandaza mbingu.+

Ninapoziita, zinasimama pamoja.

14 Kusanyikeni pamoja, ninyi nyote, msikilize.

Ni nani kati yao ameyatangaza mambo haya?

Yehova amempenda.+

Atatekeleza mapenzi yake dhidi ya Babiloni,+

Na mkono wake utawashambulia Wakaldayo.+

15 Mimi mwenyewe nimesema, nami nimemwita.+

Nimemleta, na njia yake itafanikiwa.+

16 Nikaribieni, msikie jambo hili.

Tangu mwanzoni kabisa sijasema kwa siri.+

Tangu lilipotokea nilikuwapo.”

Na sasa Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amenituma, na* roho yake.

17 Yehova, Mkombozi wako, Mtakatifu wa Israeli,+ anasema hivi:

“Mimi, Yehova, ni Mungu wako,

Ninayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe,*+

Ninayekuongoza katika njia unayopaswa kutembea.+

18 Laiti ungesikiliza amri zangu!+

Ndipo amani yako ingekuwa kama mto+

Na uadilifu wako kama mawimbi ya bahari.+

19 Uzao wako ungekuwa mwingi* kama mchanga

Na wazao wako kama chembe zake.+

Jina lao halingefutiliwa mbali kamwe wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”

20 Tokeni Babiloni!+

Kimbieni kutoka kwa Wakaldayo!

Litangazeni kwa vigelegele vya shangwe! Litangazeni!+

Lijulisheni mpaka kwenye miisho ya dunia.+

Semeni: “Yehova amemkomboa mtumishi wake Yakobo.+

21 Hawakupata kiu alipowaongoza katika maeneo yaliyoharibiwa.+

Alifanya maji yatiririke kutoka kwenye mwamba kwa ajili yao;

Aliupasua mwamba maji yakabubujika.”+

22 “Hakuna amani kwa waovu,”+ asema Yehova.

49 Nisikilizeni, enyi visiwa,

Kazeni fikira, enyi mataifa yaliyo mbali.+

Yehova aliniita kabla sijazaliwa.*+

Tangu nilipokuwa katika tumbo la mama yangu amelitaja jina langu.

 2 Alikifanya kinywa changu kuwa kama upanga mkali;

Amenificha katika kivuli cha mkono wake.+

Alinifanya kuwa mshale uliosuguliwa;*

Alinisitiri katika podo lake.

 3 Aliniambia: “Wewe ni mtumishi wangu, Ee Israeli,+

Ambaye kupitia kwake nitaonyesha fahari yangu.”+

 4 Lakini nilisema: “Nimejitaabisha bure.

Nilitumia nguvu zangu kwa ajili ya jambo lisilo halisi, kwa ubatili.

Lakini kwa hakika hukumu yangu iko na Yehova,*

Na malipo yangu yako* na Mungu wangu.”+

 5 Na sasa Yehova, Yule aliyeniumba tangu tumboni niwe mtumishi wake,

Amesema kwamba nimrudishe Yakobo kwake,

Ili watu wa Israeli wakusanyike kwake.+

Nitatukuzwa machoni pa Yehova,

Na Mungu wangu tayari atakuwa nguvu zangu.

 6 Naye akasema: “Haitoshi tu wewe kuwa mtumishi wangu

Ili kuyainua makabila ya Yakobo

Na kuwarudisha wale waliohifadhiwa wa Israeli.

Nimekutoa pia ili uwe nuru ya mataifa,+

Ili wokovu wangu ufike kwenye miisho ya dunia.”+

7 Yehova, Mkombozi wa Israeli, Mtakatifu wake,+ anamwambia hivi yule anayedharauliwa,+ yule anayechukiwa na taifa, mtumishi wa watawala:

“Wafalme wataona na kusimama,

Na wakuu watainama chini

Kwa sababu ya Yehova, ambaye ni mwaminifu,+

Mtakatifu wa Israeli, ambaye amekuchagua.”+

 8 Yehova anasema hivi:

“Wakati wa kibali* nilikujibu,+

Na katika siku ya wokovu nilikusaidia;+

Niliendelea kukulinda ili nikutoe uwe agano kwa ajili ya watu,+

Ili kuitengeneza upya nchi,

Ili kuwafanya wamiliki urithi wao ulio ukiwa,+

 9 Ili kuwaambia wafungwa, ‘Tokeni nje!’+

Na wale walio gizani,+ ‘Tokeni nje mwonekane!’

Watalisha kando ya barabara,

Malisho yao yatakuwa kando ya njia zilizokanyagwa.*

10 Hawatakuwa na njaa, wala hawatakuwa na kiu,+

Wala joto kali wala jua halitawachoma.+

Kwa maana Yule anayewaonyesha rehema atawaongoza,+

Naye atawaongoza kando ya chemchemi za maji.+

11 Nitaifanya milima yangu yote kuwa barabara,

Na barabara zangu kuu zitainuliwa.+

12 Tazameni! Hawa wanakuja kutoka mbali sana,+

Na tazameni! hawa wanatoka kaskazini na kutoka magharibi,

Na hawa kutoka nchi ya Sinimu.”+

13 Pigeni vigelegele vya shangwe, enyi mbingu, na ushangilie, Ee dunia.+

Milima na ichangamke kwa kilio cha shangwe.+

Kwa maana Yehova amewafariji watu wake,+

Naye huwaonyesha rehema watu wake mwenyewe wanaoteseka.+

14 Lakini Sayuni aliendelea kusema:

“Yehova ameniacha,+ na Yehova amenisahau.”+

15 Je, mwanamke anaweza kumsahau mtoto wake anayenyonya

Au asimhurumie mwana wa tumbo lake?

Hata wanawake hawa wakisahau, mimi siwezi kamwe kukusahau.+

16 Tazama! Nimekuchonga kwenye viganja vyangu.

Kuta zako ziko mbele zangu daima.

17 Wana wako wanarudi haraka.

Wale waliokubomoa na kukuharibu wataondoka kwako.

18 Inua macho yako utazame pande zote.

Wote wanakusanyika pamoja.+

Wanakuja kwako.

“Kwa hakika kama ninavyoishi,” asema Yehova,

“Utajivika hao wote kana kwamba ni mapambo,

Nawe utajifunga watu hao kama bibi harusi anavyofanya.

19 Ingawa maeneo yako yaliharibiwa na kuwa ukiwa na nchi yako ikawa magofu,+

Sasa itakuwa ndogo sana kwa wale wanaokaa humo,+

Na wale waliokumeza+ watakuwa mbali sana.+

20 Wana waliozaliwa ulipokuwa umefiwa watasema hivi ukisikia,

‘Mahali hapa ni padogo sana kwangu.

Nipeni nafasi zaidi hapa nikae.’+

21 Nawe utasema moyoni mwako,

‘Ni baba gani aliyenizalia watoto hawa,

Kwa kuwa mimi ni mwanamke niliyefiwa na watoto, nami ni tasa,

Nami nilipelekwa uhamishoni na kufungwa?

Ni nani aliyewalea hawa?+

Tazameni! Nilibaki peke yangu,+

Sasa hawa wametoka wapi?’”+

22 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:

“Tazameni! Nitayainulia mataifa mkono wangu,

Nami nitawainulia watu ishara yangu.*+

Watawaleta wana wako wakiwa wamewabeba mikononi mwao*

Na kuwabeba mabinti wako kwenye mabega yao.+

23 Wafalme watakuwa watunzaji wako,+

Na mabinti wao wa kifalme watakuwa walezi wako.

Watakuinamia kifudifudi+

Na kuyaramba mavumbi ya miguu yako,+

Nawe utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova;

Wale wanaonitumaini hawataaibika.”+

24 Je, wale waliotekwa wanaweza kuchukuliwa kutoka kwa mtu mwenye nguvu,

Au, je, mateka wa mtu mkatili wanaweza kuokolewa?

25 Lakini Yehova anasema hivi:

“Hata mateka wa mtu mwenye nguvu watachukuliwa,+

Na wale waliotekwa na mtu mkatili wataokolewa.+

Nitawapinga wale wanaokupinga,+

Nami nitawaokoa wana wako mwenyewe.

26 Nitawafanya wale wanaokutesa wale nyama yao wenyewe,

Nao watalewa kwa damu yao wenyewe kana kwamba ni kwa divai tamu.

Na watu wote* watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,+

Mwokozi wako+ na Mkombozi wako,+

Mwenye Nguvu wa Yakobo.”+

50 Yehova anasema hivi:

“Kiko wapi cheti cha talaka+ cha mama yenu, ambaye nilimfukuza?

Au niliwauza kwa yupi kati ya wakopeshaji wangu?

Tazameni! Mliuzwa kwa sababu ya uovu wenu,+

Na mama yenu alifukuzwa kwa sababu ya makosa yenu wenyewe.+

 2 Basi, kwa nini nilipokuja, hapakuwa na mtu yeyote mahali hapa?

Kwa nini hakuna aliyejibu nilipoita?+

Je, mkono wangu ni mfupi usiweze kukomboa,

Au je, sina nguvu za kuokoa?+

Tazameni! Mimi huikausha bahari kwa kemeo langu;+

Ninaifanya mito kuwa jangwa.+

Samaki waliomo huoza kwa kukosa maji,

Nao hufa kwa sababu ya kiu.

 3 Mimi hulivisha mbingu giza,+

Nami huzifunika kwa nguo za magunia.”

 4 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amenipa ulimi wa waliofundishwa,*+

Ili nijue jinsi ya kumjibu* aliyechoka kwa neno linalofaa.*+

Yeye huniamsha asubuhi baada ya asubuhi;

Huliamsha sikio langu ili lisikilize kama wale waliofundishwa.+

 5 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amelifungua sikio langu,

Nami sikuwa mwasi.+

Sikugeuka upande ulio kinyume.+

 6 Niliwapa mgongo wangu wale waliokuwa wakinipiga

Na mashavu yangu wale waliozing’oa ndevu zangu.

Sikuuficha uso wangu kutoka kwa mambo yenye kufedhehesha na kutoka kwa mate.+

 7 Lakini Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atanisaidia.+

Ndiyo sababu sitafedheheka.

Ndiyo sababu nimeufanya uso wangu uwe kama jiwe gumu,+

Nami ninajua kwamba sitaaibika.

 8 Yule anayenitangaza kuwa mwadilifu yu karibu.

Ni nani anayeweza kunishtaki?*+

Na tusimame pamoja.*

Ni nani aliye na kesi dhidi yangu?

Na anikaribie.

 9 Tazameni! Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atanisaidia.

Ni nani atakayenitangaza kuwa na hatia?

Tazameni! Wote watachakaa kama vazi.

Nondo* atawala.

10 Ni nani kati yenu anayemwogopa Yehova

Na kusikiliza sauti ya mtumishi wake?+

Ambaye ametembea katika giza zito, bila mwangaza wowote?

Na alitumaini jina la Yehova na kujitegemeza juu ya* Mungu wake.

11 “Tazameni! Ninyi nyote mnaowasha moto,

Mnaorusha cheche,

Tembeeni katika nuru ya moto wenu,

Kati ya cheche ambazo mmewasha.

Hili ndilo mtakalopata kutoka mkononi mwangu:

Mtalala kwa maumivu makali.

51 “Nisikilizeni mimi, ninyi mnaofuatia uadilifu,

Ninyi mnaomtafuta Yehova.

Uangalieni mwamba ambao mlichongwa kutoka kwake

Na machimbo ambamo mlichimbwa kutoka ndani yake.

 2 Mwangalieni Abrahamu baba yenu

Na Sara+ aliyewazaa.*

Kwa maana Abrahamu alikuwa mmoja tu nilipomwita,+

Nami nilimbariki na kumfanya kuwa wengi.+

 3 Kwa maana Yehova atalifariji Sayuni.+

Ataleta faraja kwa magofu yake yote,+

Naye ataifanya nyika yake kuwa kama Edeni+

Na jangwa lake tambarare kama bustani ya Yehova.+

Kutakuwa na furaha na shangwe ndani yake,

Kutoa shukrani na nyimbo tamu.+

 4 Nisikilizeni, enyi watu wangu,

Na mnitegee sikio, taifa langu.+

Kwa maana sheria itatoka kwangu,+

Nami nitaifanya haki yangu kuwa nuru kwa watu.+

 5 Uadilifu wangu unakaribia.+

Wokovu wangu utatoka,+

Na mikono yangu itayahukumu mataifa.+

Visiwa vitanitumaini mimi,+

Navyo vitaungojea mkono wangu.*

 6 Inueni macho yenu mbinguni,

Na mtazame chini duniani.

Kwa maana mbingu zitatawanyika vipandevipande kama moshi;

Nayo dunia itachakaa kama vazi,

Na wakaaji wake watakufa kama mbu.*

Lakini wokovu wangu utadumu milele,+

Na uadilifu wangu hautashindwa kamwe.*+

 7 Nisikilizeni mimi, ninyi mnaoujua uadilifu,

Watu walio na sheria* yangu moyoni mwao.+

Msiogope dhihaka za wanadamu wanaoweza kufa,

Na msiogopeshwe na matusi yao.

 8 Kwa maana nondo atawala kabisa kama vazi;

Nondo* alaye nguo atawala kabisa kama sufu.+

Lakini uadilifu wangu utadumu milele,

Na wokovu wangu kwa vizazi vyote.”+

 9 Amka! Amka! Jivike nguvu,

Ee mkono wa Yehova!+

Amka kama katika siku za zamani za kale, kama katika vizazi vilivyopita.

Je, si wewe uliyemvunja Rahabu*+ vipandevipande,

Uliyemchoma kwa silaha yule mnyama mkubwa sana wa baharini?+

10 Je, si wewe uliyeikausha bahari, maji ya kilindi kikubwa?+

Uliyevifanya vilindi vya bahari kuwa njia ili watu waliokombolewa wavuke?+

11 Watu wa Yehova waliokombolewa watarudi.+

Watakuja Sayuni kwa vigelegele vya shangwe,+

Na shangwe isiyokoma itakuwa taji lao.*+

Watakuwa na furaha na shangwe.

Huzuni na kilio cha uchungu vitakimbia.+

12 “Mimi mwenyewe Ndiye ninayewafariji.+

Kwa nini umwogope mwanadamu anayeweza kufa ambaye atakufa+

Na mwana wa binadamu atakayenyauka kama majani mabichi?

13 Kwa nini unamsahau Yehova Muumba wako,+

Yule aliyezitandaza mbingu+ na kuweka msingi wa dunia?

Mchana kutwa uliendelea kuhofu ghadhabu ya mkandamizaji,*

Kana kwamba angeweza kukuangamiza.

Iko wapi sasa ghadhabu ya mkandamizaji?

14 Yule aliyejikunja katika minyororo atawekwa huru hivi karibuni;+

Hatakufa na kuingia shimoni,

Wala hatakosa mkate.

15 Lakini mimi ni Yehova Mungu wako,

Ninayeitibua bahari na kuyavuruga mawimbi yake+

—Yehova wa majeshi ndilo jina lake.+

16 Nitayaweka maneno yangu katika kinywa chako,

Nami nitakufunika kwa kivuli cha mkono wangu,+

Ili kuzipanda mbingu na kuuweka msingi wa dunia+

Na kuwaambia watu wa Sayuni, ‘Ninyi ni watu wangu.’+

17 Amka! Amka! Simama, Ee Yerusalemu,+

Wewe ambaye umekunywa kutoka mkononi mwa Yehova kikombe chake cha ghadhabu.

Umekunywa bilauri;

Umemaliza kabisa kikombe kinachofanya watu wapepesuke.+

18 Kati ya wana wote aliowazaa hakuna hata mmoja aliye hapo ili kumwongoza,

Na kati ya wana wote aliowalea hakuna hata mmoja ambaye anamshika mkono.

19 Mambo hayo mawili yamekupata.

Ni nani atakayekusikitikia?

Maangamizi na uharibifu, njaa na upanga!+

Ni nani atakayekufariji?+

20 Wana wako wamezimia.+

Wanalala chini katika kila pembe ya barabara

Kama kondoo mwitu katika wavu.

Wamejaa ghadhabu ya Yehova, kemeo la Mungu wako.”

21 Kwa hiyo tafadhali sikiliza jambo hili,

Ewe mwanamke uliyeteseka na kulewa, lakini si kwa divai.

22 Bwana wako Yehova, Mungu wako anayewatetea watu wake anasema hivi:

“Tazama! Nitakichukua kutoka mkononi mwako kile kikombe kinachofanya watu wapepesuke,+

Ile bilauri, kikombe changu cha ghadhabu;

Hutakinywa tena.+

23 Nitakitia mkononi mwa wale wanaokutesa,+

Wale waliokuambia, ‘Inama chini ili tutembee juu yako!’

Basi ukaufanya mgongo wako kama ardhi,

Kama barabara yao ya kutembea juu yake.”

52 Amka! Amka! Jivike nguvu,+ ewe Sayuni!+

Vaa mavazi yako maridadi,+ ewe Yerusalemu, jiji takatifu!

Kwa maana mtu ambaye hajatahiriwa na mtu asiye safi hawataingia ndani yako tena.+

 2 Yakung’ute mavumbi, inuka na uketi, ewe Yerusalemu.

Fungua pingu zilizo shingoni mwako, ewe binti ya Sayuni uliye mateka.+

 3 Kwa maana Yehova anasema hivi:

“Ninyi mliuzwa bila malipo,+

Na mtakombolewa bila pesa.”+

 4 Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:

“Mwanzoni watu wangu walishuka kwenda Misri ili waishi huko wakiwa wageni;+

Kisha Ashuru ikawakandamiza bila sababu.”

 5 “Basi nifanye nini hapa?” auliza Yehova.

“Kwa maana watu wangu walichukuliwa bila malipo.

Wale wanaowatawala wanaendelea kupiga mayowe ya ushindi,”+ asema Yehova,

“Na daima, mchana kutwa, jina langu linavunjiwa heshima.+

 6 Kwa sababu hiyo watu wangu watalijua jina langu;+

Kwa sababu hiyo watajua siku hiyo kwamba mimi Ndiye ninayesema.

Tazama, ni mimi!”

 7 Jinsi inavyopendeza juu ya milima, miguu ya yule anayeleta habari njema,+

Anayetangaza amani,+

Anayeleta habari njema za jambo bora,

Anayetangaza wokovu,

Anayeambia Sayuni: “Mungu wako amekuwa Mfalme!”+

 8 Sikiliza! Walinzi wako wanapaza sauti.

Wanapiga vigelegele kwa shangwe pamoja,

Kwa maana wataona waziwazi* Yehova atakapokusanya Sayuni tena.

 9 Changamkeni, pigeni pamoja vigelegele kwa shangwe, enyi magofu ya Yerusalemu,+

Kwa maana Yehova amewafariji watu wake;+ amekomboa Yerusalemu.+

10 Yehova ameufunua wazi mkono wake mtakatifu mbele ya macho ya mataifa yote;+

Miisho yote ya dunia itayaona matendo ya wokovu ya* Mungu wetu.+

11 Ondokeni, ondokeni, tokeni humo,+ msiguse kitu chochote kichafu!+

Tokeni kati yake,+ iweni safi,

Ninyi mnaobeba vyombo vya Yehova.+

12 Kwa maana hamtaondoka kwa wasiwasi,

Wala hamtahitaji kukimbia,

Kwa maana Yehova atawatangulia,+

Na Mungu wa Israeli atakuwa mlinzi nyuma yenu.+

13 Tazameni! Mtumishi wangu+ atatenda kwa ufahamu.

Atainuliwa juu,

Atainuliwa na kukwezwa sana.+

14 Kama alivyotazamwa na wengi kwa mshangao

—Kwa maana sura yake ilikuwa imeharibiwa kuliko ya mwanadamu mwingine yeyote

Na umbo lake lenye fahari kuliko la binadamu—

15 Ndivyo atakavyoyashtua mataifa mengi.+

Wafalme watafunga vinywa vyao* mbele yake,+

Kwa sababu wataona mambo ambayo hawakuwa wameambiwa

Na kufikiria mambo ambayo hawakuwa wamesikia.+

53 Ni nani ambaye ameamini jambo alilosikia kutoka kwetu?*+

Na mkono wa Yehova,+ umefunuliwa kwa nani?+

 2 Atapanda kama tawi+ mbele yake,* kama mzizi kutoka katika nchi iliyokauka.

Hana umbo la kifahari, wala utukufu wowote;+

Na tunapomwona, sura yake haituvutii.*

 3 Alidharauliwa na kuepukwa na wanadamu,+

Mtu aliyekusudiwa kupata* maumivu na aliyezoea magonjwa.

Ilikuwa kana kwamba uso wake ulifichwa kutoka kwetu.*

Alidharauliwa, nasi tulimwona kuwa asiye na maana.+

 4 Kwa kweli yeye mwenyewe aliyabeba magonjwa yetu,+

Na kujitwika maumivu yetu.+

Lakini tulimwona kama mtu aliyepata mapigo, aliyepigwa na Mungu na kuteswa.

 5 Lakini alichomwa*+ kwa sababu ya makosa yetu;+

Alipondwa kwa sababu ya dhambi zetu.+

Aliibeba adhabu ili tupate amani,+

Na kwa sababu ya majeraha yake tuliponywa.+

 6 Sisi sote tumetangatanga kama kondoo,+

Kila mmoja ameifuata njia yake mwenyewe,

Na Yehova amefanya dhambi yetu sote ikutane naye.+

 7 Alikandamizwa+ na alikubali kuteswa,+

Lakini hakuthubutu kufungua kinywa chake.

Aliletwa kama kondoo machinjioni,+

Kama kondoo jike aliye kimya mbele ya wanaomkata manyoya,

Na hakuthubutu kufungua kinywa chake.+

 8 Kwa sababu ya kizuizi* na hukumu alichukuliwa;

Na ni nani atakayejishughulisha na habari za kizazi chake?*

Kwa maana aliondolewa katika nchi ya walio hai;+

Alipata pigo* kwa sababu ya makosa ya watu wangu.+

 9 Naye alipewa kaburi* pamoja na waovu,+

Na pamoja na matajiri* katika kifo chake,+

Ingawa hakuwa amefanya kosa*

Na hakukuwa na udanganyifu kinywani mwake.+

10 Lakini yalikuwa mapenzi ya Yehova* kumponda, naye aliruhusu awe mgonjwa.

Ukitoa uhai wake* uwe dhabihu ya hatia,+

Atauona uzao wake,* ataongeza siku zake,+

Na kupitia kwake mapenzi* ya Yehova yatafanikiwa.+

11 Kwa sababu ya mateso* yake, ataona na kuridhika.

Kupitia ujuzi wake, yule mwadilifu, mtumishi wangu,+

Atawaletea watu wengi msimamo wa uadilifu,+

Na dhambi zao atazibeba.+

12 Kwa sababu hiyo nitampa fungu kati ya wengi,

Naye atagawa nyara pamoja na wenye nguvu,

Kwa sababu aliumwaga uhai wake* mpaka kifo+

Naye alihesabiwa miongoni mwa wakosaji;+

Aliibeba dhambi ya watu wengi,+

Naye aliwatetea wakosaji.+

54 “Piga vigelegele kwa shangwe, wewe mwanamke tasa ambaye hujazaa!+

Changamka na upaze sauti kwa shangwe,+ wewe ambaye hukuwahi kupata uchungu wa kuzaa,+

Kwa maana wana* wa aliye ukiwa ni wengi

Kuliko wana wa mwanamke aliye na mume,”*+ asema Yehova.

 2 “Pafanye mahali pa hema lako pawe na nafasi kubwa zaidi.+

Vitandaze vitambaa vya hema lako tukufu la ibada.

Usizuie, refusha kamba za hema lako,

Na uviimarishe vigingi vya hema lako.+

 3 Kwa maana utaenea kulia na kushoto.

Uzao wako utayamiliki mataifa,

Nao watakaa katika majiji yaliyoachwa ukiwa.+

 4 Usiogope,+ kwa maana hutaaibishwa;+

Usifedheheke, kwa maana hutakatishwa tamaa.

Kwa maana utaisahau aibu ya ujana wako,

Nawe hutaikumbuka tena fedheha ya ujane wako.”

 5 “Kwa maana Muumba*+ wako Mkuu ni kama mume* wako,+

Yehova wa majeshi ndilo jina lake,

Na Mtakatifu wa Israeli ni Mkombozi wako.+

Ataitwa Mungu wa dunia yote.+

 6 Kwa maana Yehova alikuita kana kwamba wewe ni mke aliyeachwa na aliye na huzuni,*+

Kama mke aliyeolewa wakati wa ujana kisha akakataliwa,” asema Mungu wako.

 7 “Kwa maana nilikuacha kwa muda mfupi,

Lakini nitakukusanya tena kwa rehema nyingi.+

 8 Kwa furiko la hasira niliuficha uso wangu kutoka kwako kwa muda mfupi,+

Lakini nitakuonyesha rehema kwa upendo mshikamanifu wa milele,”+ asema Mkombozi+ wako, Yehova.

 9 “Jambo hili kwangu ni kama siku za Noa.+

Kama nilivyoapa kwamba maji ya Noa hayataifunika tena dunia,+

Ndivyo ninavyoapa kwamba sitawaka hasira tena kukuelekea wewe wala kukukemea.+

10 Kwa maana huenda milima ikaondolewa

Na huenda vilima vikatikiswa,

Lakini upendo wangu mshikamanifu hautaondolewa kwako,+

Wala agano langu la amani halitatikiswa,”+ asema Yehova, Yule anayekuonyesha rehema.+

11 “Ee mwanamke uliyeteseka,+ uliyerushwa na dhoruba, ambaye hajafarijiwa,+

Ninayaweka mawe yako kwa saruji ngumu

Na msingi wako kwa yakuti.+

12 Nitatengeneza minara yako kwa zabarijadi,

Na malango yako kwa mawe yanayong’aa,*

Na mipaka yako yote kwa mawe yenye thamani.

13 Na wana* wako wote watafundishwa na Yehova,+

Na amani ya wana* wako itakuwa nyingi.+

14 Utaimarishwa kabisa katika uadilifu.+

Utakuwa mbali sana na ukandamizaji,+

Hutaogopa chochote na hutakuwa na sababu yoyote ya kuhofu,

Kwa maana haitakukaribia.+

15 Mtu yeyote akikushambulia,

Haitakuwa kwa maagizo yangu.

Yeyote anayekushambulia ataanguka kwa sababu yako.”+

16 “Tazama! Mimi mwenyewe nilimuumba fundi,

Anayefukuta moto wa makaa,

Naye hutengeneza silaha kwa kazi yake.

Mimi mwenyewe pia nilimuumba yule mtu mharibifu ili alete uharibifu.+

17 Hakuna silaha yoyote itakayotokezwa dhidi yako itakayofanikiwa,+

Nawe utauhukumu ulimi wowote utakaoinuka dhidi yako katika hukumu.

Huu ndio urithi wa watumishi wa Yehova,

Na uadilifu wao unatoka kwangu,” asema Yehova.+

55 Njooni, ninyi nyote mlio na kiu,+ njooni kwenye maji!+

Ninyi msio na pesa, njooni, nunueni na mle!

Naam, njooni, mnunue divai na maziwa+ bila pesa na bila gharama.+

 2 Kwa nini mnaendelea kulipa pesa kwa ajili ya kitu ambacho si mkate,

Na kwa nini mtumie mapato yenu* kwa ajili ya kitu ambacho hakishibishi?

Nisikilizeni kwa makini, mle kilicho chema,+

Nanyi mtafurahia sana vitu vyenye lishe kwelikweli.*+

 3 Tegeni sikio na mje kwangu.+

Sikilizeni, nanyi mtaendelea* kuwa hai,

Nami nitafanya agano la milele pamoja nanyi bila kusita+

Kulingana na matendo ya upendo mshikamanifu kwa Daudi, ambayo ni ya uaminifu.*+

 4 Tazameni! Nilimfanya awe shahidi+ kwa mataifa,

Kiongozi+ na kamanda+ kwa mataifa.

 5 Tazama! Utaliita taifa ambalo hulijui,

Na watu wa taifa ambao hawajakujua watakukimbilia

Kwa ajili ya Yehova Mungu wako,+ Mtakatifu wa Israeli,

Kwa sababu atakutukuza.+

 6 Mtafuteni Yehova wakati bado anapatikana.+

Mwiteni maadamu yuko karibu.+

 7 Mtu mwovu na aiache njia yake+

Na mtu mbaya mawazo yake;

Na arudi kwa Yehova, ambaye atamwonyesha rehema,+

Kwa Mungu wetu, kwa maana atasamehe kwa njia kubwa.*+

 8 “Kwa maana mawazo yangu si mawazo yenu,+

Na njia zenu si njia zangu,” asema Yehova.

 9 “Kwa maana kama mbingu zilivyo juu kuliko dunia,

Ndivyo njia zangu zilivyo juu kuliko njia zenu

Na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.+

10 Kwa maana kama mvua na theluji inavyomwagika kutoka mbinguni

Nayo hairudi huko mpaka iiloweshe dunia na kuifanya izae na kuchipuka,

Na kumpa mbegu mpandaji na mkate yule anayekula,

11 Hivyo ndivyo neno langu linalotoka katika kinywa changu litakavyokuwa.*+

Halitarudi kwangu bila matokeo,+

Bali hakika litatimiza jambo lolote linalonipendeza,*+

Na hakika litafanikiwa katika yale ambayo nimelituma.

12 Kwa maana ninyi mtatoka nje kwa shangwe,+

Nanyi mtarudishwa kwa amani.+

Milima na vilima vitachangamka mbele yenu kwa vigelegele vya shangwe,+

Na miti yote ya msituni itapiga makofi.+

13 Badala ya vichaka vya miiba, mberoshi utakua,+

Na badala ya upupu unaowasha, mhadasi utakua.

Na jambo hilo litamletea Yehova sifa,*+

Ishara ya milele ambayo haitatoweka kamwe.”

56 Yehova anasema hivi:

“Tekelezeni haki,+ na mtende uadilifu,

Kwa maana wokovu wangu utakuja hivi karibuni

Na uadilifu wangu utafunuliwa.+

 2 Mwenye furaha ni mtu anayefanya jambo hili

Na mwana wa mtu anayeendelea kulishika kabisa,

Anayeishika Sabato na asiyeitia unajisi+

Na ambaye anauzuia mkono wake usitende uovu wowote.

 3 Mgeni anayejiunga na Yehova+ asiseme,

‘Bila shaka Yehova atanitenga na watu wake.’

Naye towashi asiseme, ‘Tazama! Mimi ni mti uliokauka.’”

4 Kwa maana mimi Yehova ninawaambia hivi matowashi wanaozishika sabato zangu na kuchagua mambo yanayonipendeza na kulishika kabisa agano langu:

 5 “Nitawapa mnara wa ukumbusho na jina katika nyumba yangu na katika kuta zangu,

Jambo bora kuliko wana na mabinti.

Nitawapa jina linalodumu milele,

Ambalo halitaangamia.

 6 Na wageni wanaojiunga nami Yehova ili kunihudumia,

Kulipenda jina langu mimi Yehova+

Na kuwa watumishi wangu,

Wote wanaoishika Sabato na wasioitia unajisi

Na wanaolishika kabisa agano langu,

 7 Nitawaleta pia kwenye mlima wangu mtakatifu+

Na kuwafanya washangilie ndani ya nyumba yangu ya sala.

Dhabihu zao nzima za kuteketezwa na matoleo yao yatakubaliwa kwenye madhabahu yangu.

Kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote.”+

8 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, anayewakusanya waliotawanyika wa Israeli,+ anasema hivi:

“Nitawakusanya wengine wajiunge naye mbali na wale ambao tayari wamekusanywa.”+

 9 Ninyi nyote wanyama wa mwituni, njooni mle,

Ninyi nyote wanyama wa mwituni mlio msituni.+

10 Walinzi wake ni vipofu,+ hakuna hata mmoja ambaye ameona.+

Wote ni mbwa walio bubu, wasioweza kubweka.+

Wanahemahema na kulala chini; wanapenda kulala.

11 Wao ni mbwa walafi;*

Hawashibi kamwe.

Wao ni wachungaji wasio na uelewaji.+

Wote wamefuata njia yao wenyewe;

Kila mmoja wao anatafuta faida isiyo ya haki na kusema:

12 “Njooni, acheni nichukue divai,

Na acheni tunywe kileo kingi.+

Na kesho itakuwa kama leo, itakuwa bora hata zaidi!”

57 Mwadilifu ameangamia,

Lakini hakuna yeyote anayetia jambo hilo moyoni.

Watu washikamanifu wanaondolewa,*+

Na hakuna mtu anayetambua kwamba mwadilifu ameondolewa

Kwa sababu ya* msiba.

 2 Yeye huingia katika amani.

Wanapumzika vitandani mwao,* wote wanaotembea kwa unyoofu.

 3 “Lakini ninyi karibieni,

Enyi wana wa mwanamke mlozi,

Ninyi watoto wa mzinzi na kahaba:

 4 Mnamkejeli nani?

Ni nani mnayemfungulia kinywa wazi na kumtolea ulimi?

Je, ninyi si watoto wa ukosaji,

Watoto wa udanganyifu,+

 5 Wale wanaowaka tamaa kati ya miti mikubwa,+

Chini ya kila mti wenye majani mengi,+

Wanaowachinja watoto kwenye mabonde,*+

Chini ya mipasuko ya majabali?

 6 Mawe laini ya bondeni* ndilo fungu lako.

Naam, hayo ndiyo fungu lako.+

Hata unayamiminia matoleo ya kinywaji na kutoa zawadi juu yake.+

Je, niridhike* na mambo hayo?

 7 Ulikitayarisha kitanda chako juu ya mlima mrefu ulioinuka,+

Nawe ukapanda huko ili kutoa dhabihu.+

 8 Uliweka ukumbusho wako nyuma ya mlango na nyuma ya mwimo wa mlango.

Uliniacha nawe ukajifunua;

Ulipanda huko na kukipanua kitanda chako.

Nawe ukafanya agano pamoja nao.

Ulipenda kulala nao kitandani mwao,+

Nawe ulikitazama kiungo cha kiume.*

 9 Ulishuka kwa Meleki* ukiwa na mafuta

Na ukiwa na manukato mengi.

Uliwatuma wajumbe wako mbali,

Hivi kwamba ukashuka Kaburini.*

10 Umejitaabisha ukifuata njia zako nyingi,

Lakini hukusema, ‘Hakuna matumaini!’

Ulipata nguvu mpya.

Ndiyo sababu hukati tamaa.*

11 Ulimhofu na kumwogopa nani

Hivi kwamba ukaanza kusema uwongo?+

Hukunikumbuka mimi.+

Hukutia jambo lolote moyoni mwako.+

Je, sijakaa kimya na kujiondoa?*+

Kwa hiyo hukuniogopa mimi.

12 Nitatangaza ‘uadilifu’ wako+ na kazi zako,+

Nazo hazitakunufaisha.+

13 Unapolilia msaada,

Sanamu ulizojikusanyia hazitakuokoa.+

Upepo utazipeperusha zote mbali sana,

Zitapeperushwa na pumzi tu,

Lakini yule anayenikimbilia atairithi nchi

Naye ataumiliki mlima wangu mtakatifu.+

14 Itasemwa, ‘Tengenezeni, tengenezeni barabara! Tayarisheni njia!+

Ondoeni kizuizi chochote katika njia ya watu wangu.’”

15 Kwa maana Yule Aliye Juu na Aliyetukuka Sana,

Anayeishi* milele+ na ambaye jina lake ni takatifu+ anasema hivi:

“Ninaishi mahali palipo juu na patakatifu,+

Lakini ninaishi pia na wale waliopondwa na wenye roho ya unyenyekevu,

Ili kuihuisha roho ya watu wa hali ya chini

Na kuuhuisha moyo wa wale wanaopondwa.+

16 Kwa maana sitawapinga milele

Wala kuwa na hasira daima;+

Kwa sababu roho ya mwanadamu itadhoofika kwa sababu yangu,+

Hata viumbe wanaopumua ambao niliwaumba.

17 Nilikasirika kwa sababu alitenda dhambi kwa kufuatilia faida isiyo ya haki,+

Basi nikampiga, nikauficha uso wangu, nami nikashikwa na hasira.

Lakini aliendelea kuwa mwasi+ akifuata njia ya moyo wake.

18 Nimeziona njia zake,

Lakini nitamponya+ na kumwongoza+

Na kumrudishia* faraja yeye+ na watu wake wanaoomboleza.”+

19 “Ninaumba matunda ya midomo.

Yule aliye mbali sana atapewa amani ya kudumu na pia yule aliye karibu,”+ asema Yehova,

“Nami nitamponya.”

20 “Lakini waovu ni kama bahari iliyochafuka ambayo haiwezi kutulia,

Na maji yake yanaendelea kurusharusha juu magugu ya baharini na matope.

21 Hakuna amani kwa waovu,”+ asema Mungu wangu.

58 “Ita kwa sauti yote kutoka kooni; usijizuie!

Paza sauti yako kama pembe.

Watangazie watu wangu uasi wao,+

Na nyumba ya Yakobo dhambi zao.

 2 Wananitafuta siku baada ya siku,

Nao wanafurahia kuzijua njia zangu,

Kana kwamba walikuwa taifa lililotenda uadilifu

Na ambalo halikuacha haki ya Mungu wao.+

Wananiomba hukumu za uadilifu,

Wakifurahia kumkaribia Mungu:+

 3 ‘Kwa nini huoni, tunapofunga?+

Na kwa nini hutambui tunapojitesa?’*+

Kwa sababu siku mnayofunga mnafuatia mapendezi yenu wenyewe,*

Nanyi mnawakandamiza wafanyakazi wenu.+

 4 Kufunga kwenu huishia kwenye ugomvi na vita,

Nanyi mnashambulia kwa ngumi ya uovu.

Hamwezi kufunga kama mnavyofanya leo na sauti yenu isikiwe mbinguni.

 5 Je, kufunga ambako ninachagua kunapaswa kuwa hivi,

Siku ya mtu kujitesa,*

Kuinamisha chini kichwa chake kama utete,

Na kufanya nguo za magunia na majivu yawe kitanda chake?

Je, huko ndiko unakoita kufunga na siku inayompendeza Yehova?

 6 Hapana, huku ndiko kufunga ambako ninachagua:

Kuondoa pingu za uovu,

Kufungua vifungo vya nira,+

Kuwaachilia huru waliokandamizwa,+

Na kuivunja kila nira mara mbili;

 7 Ni kumgawia aliye na njaa mkate wako,+

Kuwaleta maskini na wasio na makao nyumbani mwako,

Kumvisha aliye uchi unapokutana naye,+

Na kutowageuzia mgongo watu wako wa ukoo.

 8 Ndipo nuru yako itakapochomoza kama mapambazuko,+

Na uponyaji wako utatokea upesi.

Uadilifu wako utakutangulia,

Na utukufu wa Yehova utakuwa ulinzi nyuma yako.+

 9 Kisha utaita, na Yehova atakujibu;

Utalilia msaada, naye atasema, ‘Mimi hapa!’

Ukiiondoa nira kati yako

Ukiacha kunyoosha kidole chako na kuacha kuongea mambo yanayodhuru,+

10 Ukimpa mwenye njaa kile ambacho wewe mwenyewe unatamani*+

Na kuwashibisha wale wanaoteseka,*

Ndipo nuru yako itakapong’aa hata gizani,

Na giza lako litakuwa kama adhuhuri.+

11 Yehova atakuongoza daima

Na kukushibisha* hata katika nchi iliyokauka;+

Ataitia nguvu mifupa yako,

Nawe utakuwa kama bustani iliyonyweshwa maji vizuri,+

Kama chemchemi ambayo maji yake hayakauki kamwe.

12 Watajenga upya magofu ya kale kwa sababu yako,+

Nawe utairudisha misingi ya vizazi vilivyopita.+

Utaitwa mrekebishaji wa kuta zilizobomoka,*+

Mrekebishaji wa barabara zinazopita kwenye makao.

13 Ikiwa kwa sababu ya Sabato unaacha kufuatilia* mapendezi yako mwenyewe* katika siku yangu takatifu+

Nawe uiite Sabato kuwa ni furaha tele, siku takatifu ya Yehova, siku ya kutukuzwa,+

Nawe uitukuze badala ya kufuatilia mapendezi yako mwenyewe na kusema maneno ya upuuzi,

14 Ndipo utakapopata furaha tele katika Yehova,

Nami nitakufanya upande sehemu za juu za dunia.+

Nitakufanya ule kutokana na* urithi wa Yakobo babu yako,+

Kwa maana kinywa cha Yehova kimesema hivyo.”

59 Tazama! Mkono wa Yehova si mfupi usiweze kuokoa,+

Wala sikio lake si zito lisiweze kusikia.+

 2 Hapana, makosa yenu wenyewe yamewatenganisha na Mungu wenu.+

Dhambi zenu zimemfanya aufiche uso wake kutoka kwenu,

Naye anakataa kuwasikiliza.+

 3 Kwa maana viganja vyenu vimechafuliwa kwa damu+

Na vidole vyenu kwa kosa.

Midomo yenu inasema uwongo,+ na ulimi wenu unanong’ona ukosefu wa uadilifu.

 4 Hakuna yeyote anayedai uadilifu utendeke,+

Na hakuna anayeenda mahakamani akiwa na ukweli.

Wanatumaini mambo ambayo si halisi*+ na kusema mambo yasiyo na maana.

Wanatunga mimba ya taabu na kuzaa madhara.+

 5 Wanaangua mayai ya nyoka mwenye sumu,

Nao wanafuma utando wa buibui.+

Yeyote anayekula mayai yao atakufa,

Na yai linalovunjwa linaangua nyoka kipiri.

 6 Utando wao wa buibui hautatumika kama vazi,

Wala hawatajifunika kwa wanachotengeneza.+

Kazi zao zinadhuru,

Na matendo ya ukatili yamo mikononi mwao.+

 7 Miguu yao hukimbilia kutenda maovu,

Nao wanafanya haraka kumwaga damu isiyo na hatia.+

Mawazo yao ni mawazo yanayodhuru;

Njia zao zina uharibifu na maumivu.+

 8 Hawajaijua njia ya amani,

Na hakuna haki katika vijia vyao.+

Wanazipotosha barabara zao;

Hakuna yeyote anayetembea humo atakayejua amani.+

 9 Ndiyo sababu haki iko mbali sana nasi,

Na uadilifu hautufikii na kututangulia.

Tunaendelea kutumainia nuru, lakini, tazama! kuna giza;

Kutumainia mwangaza, lakini tunaendelea kutembea katika utusitusi.+

10 Tunapapasa-papasa tukiutafuta ukuta kama vipofu;

Tunaendelea kupapasa-papasa kama watu wasio na macho.+

Tunajikwaa wakati wa adhuhuri kama wakati wa giza la jioni;

Miongoni mwa wenye nguvu sisi ni kama tu watu waliokufa.

11 Sote tunaendelea kunguruma kama dubu

Na kulia kwa huzuni kama njiwa.

Tunatumaini kupata haki, lakini hakuna haki yoyote;

Kupata wokovu, lakini uko mbali sana nasi.

12 Kwa maana maasi yetu ni mengi mbele zako;+

Kila moja ya dhambi zetu inashuhudia dhidi yetu.+

Kwa maana maasi yetu yako pamoja nasi;

Tunayajua vema makosa yetu.+

13 Tumemkosea na kumkana Yehova;

Tumemgeuzia mgongo Mungu wetu.

Tumesema kuhusu ukandamizaji na maasi;+

Tumetunga uwongo na kunong’ona maneno ya uwongo kutoka moyoni.+

14 Haki imerudishwa nyuma,+

Na uadilifu unasimama mbali sana;+

Kwa maana ukweli* umejikwaa katika kiwanja cha jiji,

Na jambo la unyoofu haliwezi kuingia.

15 Ukweli* umetoweka,+

Na yeyote anayeacha ubaya anaporwa.

Yehova aliona jambo hilo naye akachukizwa,*

Kwa maana hakukuwa na haki.+

16 Aliona kwamba hakuna mtu,

Naye akashangaa kwamba hakuna yeyote aliyeingilia kati,

Basi mkono wake mwenyewe ukaleta wokovu,*

Na uadilifu wake mwenyewe ukamtegemeza.

17 Kisha akavaa uadilifu kama koti la vita

Na kofia ya chuma ya wokovu* juu ya kichwa chake.+

Alivaa nguo za kisasi kama mavazi yake+

Na kujifunga bidii kama koti.*

18 Atawathawabisha kulingana na matendo yao:+

Ghadhabu kwa wapinzani wake, kisasi kwa maadui wake.+

Naye atavilipa visiwa kile kinachostahili.

19 Wataliogopa jina la Yehova kuanzia magharibi

Na kuanzia mashariki watauogopa utukufu wake,

Kwa maana ataingia kama mto unaoenda kasi,

Ambao unaendeshwa na roho ya Yehova.

20 “Mkombozi+ atakuja Sayuni,+

Kwa wale wa Yakobo wanaoacha makosa yao,”+ asema Yehova.

21 “Lakini mimi, hili ndilo agano langu pamoja nao,”+ asema Yehova. “Roho yangu iliyo juu yako na maneno yangu niliyoweka kinywani mwako—hayataondolewa kutoka kinywani mwako, kutoka kinywani mwa watoto wako,* au kutoka kinywani mwa wajukuu wako,”* asema Yehova, “kuanzia sasa mpaka milele.”

60 “Inuka, Ee mwanamke,+ angaza nuru, kwa maana nuru yako imekuja.

Utukufu wa Yehova unakuangazia.+

 2 Kwa maana tazama! giza litaifunika dunia

Na utusitusi mzito utayafunika mataifa;

Lakini Yehova atakuangazia,

Na utukufu wake utaonekana juu yako.

 3 Mataifa yataenda kwenye nuru yako+

Na wafalme+ kwenye fahari yako inayong’aa.*+

 4 Inua macho yako utazame pande zote kukuzunguka!

Wote wamekusanywa; wanakuja kwako.

Wana wako wanaendelea kuja kutoka mbali sana,+

Na mabinti wako wakiwa wametegemezwa viunoni.+

 5 Wakati huo utaona na kung’aa,+

Na moyo wako utadundadunda na kufurika,

Kwa sababu utajiri wa bahari utaelekezwa kwako;

Mali za mataifa zitakuja kwako.+

 6 Makundi ya ngamia yataifunika nchi yako,*

Ngamia dume wachanga wa Midiani na Efa.+

Wote kutoka Sheba—watakuja;

Watabeba dhahabu na ubani.

Watatangaza sifa za Yehova.+

 7 Makundi yote ya Kedari+ yatakusanywa kwako.

Kondoo dume wa Nebayothi+ watakutumikia.

Watakuja kwenye madhabahu yangu wakiwa na kibali,+

Nami nitairembesha nyumba yangu yenye utukufu.*+

 8 Ni nani hawa wanaokuja wakiruka kama mawingu,

Kama njiwa kwenye viota vyao?*

 9 Kwa maana visiwa vitanitumaini;+

Meli za Tarshishi zinaongoza,*

Kuwaleta wana wako kutoka mbali sana,+

Pamoja na fedha yao na dhahabu yao,

Kwa sifa ya jina la Yehova Mungu wako na ya Mtakatifu wa Israeli,

Kwa maana atakutukuza.*+

10 Wageni watazijenga kuta zako,

Na wafalme wao watakuhudumia,+

Kwa maana nilikupiga kwa hasira yangu,

Lakini kwa kibali changu* nitakuonyesha rehema.+

11 Malango yako yatakuwa wazi daima;+

Hayatafungwa mchana wala usiku,

Ili kukuletea mali za mataifa,

Na wafalme wao wataongoza.+

12 Kwa maana taifa lolote na ufalme wowote ambao hautakutumikia utaangamia,

Nayo mataifa yataharibiwa kabisa.+

13 Utukufu wa Lebanoni utakuja kwako,+

Mberoshi, mtidhari, na mvinje pamoja,+

Ili kuparembesha mahali pangu patakatifu;

Nitapatukuza mahali pa miguu yangu.+

14 Wana wa wale waliokukandamiza watakuja na kuinama chini mbele yako;

Wote wanaokudharau watainama chini miguuni pako,

Nao watalazimika kukuita jiji la Yehova,

Sayuni la Mtakatifu wa Israeli.+

15 Badala ya kuwa aliyeachwa na kuchukiwa, bila yeyote kupita ndani yako,+

Nitakufanya uwe chanzo cha fahari ya milele,

Chanzo cha shangwe kwa vizazi vyote.+

16 Nawe kwa kweli utakunywa maziwa ya mataifa,+

Utanyonya matiti ya wafalme;+

Nawe hakika utajua kwamba mimi, Yehova, ni Mwokozi wako,

Na Mwenye Nguvu wa Yakobo ni Mkombozi wako.+

17 Badala ya shaba nitaleta dhahabu,

Na badala ya chuma nitaleta fedha,

Badala ya mbao, shaba,

Na badala ya mawe, chuma;

Nitaweka amani kuwa waangalizi wako

Na uadilifu kuwa watu wako wanaogawa kazi.+

18 Ukatili hautasikiwa tena katika nchi yako

Wala maangamizi na uharibifu katika mipaka yako.+

Nawe utaziita kuta zako Wokovu+ na malango yako Sifa.

19 Kwa maana jua halitakuwa tena nuru ya mchana kwako,

Wala nuru ya mwezi haitakuangazia,

Kwa maana Yehova atakuwa nuru ya milele kwako,+

Na Mungu wako atakuwa urembo wako.+

20 Jua lako halitatua tena,

Wala mwezi wako hautafifia,

Kwa maana Yehova atakuwa nuru yako ya milele,+

Na siku zako za kuomboleza zitakuwa zimekwisha.+

21 Na watu wako wote watakuwa waadilifu;

Wataimiliki nchi milele.

Wao ndio chipukizi nililopanda,

Kazi ya mikono yangu,+ ili nirembeshwe.+

22 Mdogo atakuwa elfu

Na mnyonge atakuwa taifa lenye nguvu.

Mimi mwenyewe, Yehova, nitaliharakisha jambo hilo kwa wakati wake.”

61 Roho ya Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova iko juu yangu,+

Kwa sababu Yehova alinitia mafuta niwatangazie wapole habari njema.+

Alinituma kuyafunga majeraha ya waliovunjika moyo,

Kuwatangazia mateka uhuru

Na kutangaza kwamba macho ya wafungwa yatafunguliwa kabisa,+

 2 Kutangaza mwaka wa nia njema ya* Yehova

Na siku ya kisasi ya Mungu wetu,+

Kuwafariji wote wanaoomboleza,+

 3 Kuwaandalia mahitaji wale wanaoombolezea Sayuni,

Kuwapa vazi la kichwani badala ya majivu,

Mafuta ya furaha badala ya maombolezo,

Vazi la sifa badala ya roho iliyovunjika.

Nao wataitwa miti mikubwa ya uadilifu,

Bustani ya Yehova, ili kumtukuza.*+

 4 Watajenga upya magofu ya kale;

Watasimamisha sehemu zilizoachwa ukiwa za zamani,+

Nao watajenga upya majiji yaliyoharibiwa,+

Sehemu zilizoachwa ukiwa kizazi baada ya kizazi.+

 5 “Wageni watakuja na kuichunga mifugo yenu,

Nao watu wa nchi nyingine+ watakuwa wakulima wenu na watunzaji wa mizabibu yenu.+

 6 Nanyi mtaitwa makuhani wa Yehova;+

Watawaita wahudumu wa Mungu wetu.

Mtakula mali za mataifa,+

Nanyi mtajivunia utukufu* wao.

 7 Badala ya aibu mtakuwa na fungu mara mbili,

Na badala ya fedheha watapiga vigelegele kwa shangwe kwa sababu ya fungu lao.

Naam, watamiliki fungu mara mbili katika nchi yao.+

Watakuwa na shangwe milele.+

 8 Kwa maana mimi, Yehova, ninapenda haki;+

Ninachukia unyang’anyi na ukosefu wa uadilifu.+

Nitawapa malipo yao kwa uaminifu,

Nami nitafanya agano la milele pamoja nao.+

 9 Uzao wao utajulikana* miongoni mwa mataifa+

Na wazao wao miongoni mwa watu.

Wote wanaowaona watawatambua,

Kwamba wao ni uzao ambao* Yehova amebariki.”+

10 Nitashangilia sana katika Yehova.

Nafsi yangu yote itashangilia katika Mungu wangu.+

Kwa maana amenivisha mavazi ya wokovu;+

Amenifunika kwa joho* la uadilifu,

Kama bwana harusi anayevaa kilemba kama cha kuhani,+

Na kama bibi harusi anayejipamba kwa mapambo yake.

11 Kwa maana kama dunia inavyochipusha mimea

Na kama bustani inavyochipusha vitu vilivyopandwa humo,

Ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova

Atakavyofanya uadilifu+ na sifa zichipuke+ mbele ya mataifa yote.

62 Sitanyamaza kwa ajili ya Sayuni,+

Nami sitatulia kwa ajili ya Yerusalemu

Mpaka uadilifu wake ung’ae kama mwangaza mkali+

Na wokovu wake uwake kama mwenge.+

 2 “Mataifa yatauona uadilifu wako, ewe mwanamke,+

Na wafalme wote utukufu wako.+

Nawe utaitwa kwa jina jipya,+

Ambalo kinywa cha Yehova mwenyewe kitalichagua.

 3 Utakuwa taji la urembo mkononi mwa Yehova,

Kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako.

 4 Hutaitwa tena mwanamke aliyeachwa,+

Na nchi yako haitaitwa tena ukiwa.+

Lakini utaitwa Furaha Yangu Imo Ndani Yake,+

Na nchi yako itaitwa Aliyeolewa.

Kwa maana Yehova atafurahishwa nawe,

Na nchi yako itakuwa kama aliyeolewa.

 5 Kwa maana kama kijana wa kiume anavyomwoa msichana bikira,

Ndivyo wana wako watakavyokuoa.

Kama bwana harusi anavyomfurahia bibi harusi

Ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia.+

 6 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu.

Hawapaswi kukaa kimya daima, mchana kutwa na usiku kucha.

Ninyi mnaomtaja Yehova,

Msipumzike,

 7 Na msiache kamwe apumzike mpaka aliimarishe kabisa Yerusalemu,

Naam, mpaka alifanye kuwa sifa ya dunia.”+

 8 Yehova ameapa kiapo kwa mkono wake wa kuume, kwa mkono wake wenye nguvu:

“Sitawapa tena maadui wako nafaka yako iwe chakula chao,

Wala wageni hawatakunywa divai yako mpya, ambayo umetaabika kuipata.+

 9 Lakini wale wanaoikusanya wataila nao watamsifu Yehova;

Na wale wanaoikusanya watainywa katika nyua zangu takatifu.”+

10 Piteni humo, piteni katika malango.

Watayarishieni watu njia.+

Tengenezeni, tengenezeni barabara kuu.

Ondoeni mawe juu yake.+

Inueni ishara* kwa ajili ya watu.+

11 Tazama! Yehova ametangaza mpaka kwenye miisho ya dunia:

“Mwambieni binti ya Sayuni,

‘Tazama! Wokovu wako unakuja.+

Tazama! Anakuja na thawabu yake,

Na malipo anayotoa yako mbele zake.’”+

12 Wataitwa watu watakatifu, wale waliokombolewa na Yehova,+

Nawe utaitwa Aliyetafutwa, Jiji Ambalo Halikuachwa.+

63 Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu,+

Kutoka Bosra+ akiwa na mavazi yenye rangi zinazong’aa,*

Huyu aliye na mavazi ya kifahari,

Anayetembea kwa nguvu zake nyingi?

“Ni mimi, Yule anayesema kwa uadilifu,

Yule aliye na nguvu nyingi za kuokoa.”

 2 Kwa nini mavazi yako ni mekundu,

Na kwa nini mavazi yako ni kama ya mtu anayekanyaga shinikizo la divai?+

 3 “Nimelikanyaga pipa la divai nikiwa peke yangu.

Hakuna mtu yeyote kutoka katika mataifa aliyekuwa pamoja nami.

Niliendelea kuwakanyaga kwa hasira yangu,

Nami niliendelea kuwakanyaga kwa ghadhabu yangu.+

Mavazi yangu yalijaa madoa ya damu yao,

Nami nimezichafua nguo zangu zote.

 4 Kwa maana siku ya kisasi imo moyoni mwangu,+

Na mwaka wa watu wangu waliokombolewa umefika.

 5 Nilitazama, lakini hapakuwa na yeyote wa kunisaidia;

Nilishangaa kwamba hakuna yeyote aliyenitegemeza.

Basi mkono wangu ukaniletea wokovu,*+

Na ghadhabu yangu mwenyewe ikanitegemeza.

 6 Niliwakanyaga watu kwa hasira yangu,

Niliwalewesha kwa ghadhabu yangu+

Niliimwaga damu yao ardhini.”

 7 Nitayataja matendo ya Yehova ya upendo mshikamanifu,

Matendo ya Yehova yanayostahili sifa,

Kwa sababu ya mambo yote ambayo Yehova ametutendea,+

Mambo mengi mema ambayo ameitendea nyumba ya Israeli,

Kulingana na rehema zake na upendo wake mshikamanifu ulio mwingi.

 8 Kwa maana alisema: “Kwa hakika hawa ni watu wangu, wana ambao hawatakosa kuwa washikamanifu.”*+

Basi akawa Mwokozi wao.+

 9 Katika taabu zao zote, yeye alitaabika.+

Na mjumbe wake binafsi* akawaokoa.+

Kwa upendo na huruma yake aliwakomboa,+

Naye aliwainua na kuwabeba siku zote za zamani.+

10 Lakini waliasi+ na kuihuzunisha roho yake takatifu.+

Naye akageuka na kuwa adui yao,+

Naye akawapiga vita.+

11 Nao wakazikumbuka siku za zamani,

Siku za Musa mtumishi wake:

“Yuko wapi Yule aliyewapandisha kutoka katika bahari+ pamoja na wachungaji wa kundi lake?+

Yuko wapi Yule aliyetia ndani yake roho Yake takatifu,+

12 Yule aliyeufanya mkono Wake mtukufu uende pamoja na mkono wa kulia wa Musa,+

Yule aliyeyatenganisha maji mbele yao+

Ili kujifanyia jina la milele,+

13 Yule aliyewafanya watembee katika maji yenye mawimbi makubwa,*

Hivi kwamba wakatembea bila kujikwaa,

Kama farasi katika nchi iliyo wazi?*

14 Kama mifugo wanavyoteremka katika bonde tambarare,

Ndivyo roho ya Yehova ilivyowapumzisha.”+

Hivyo ndivyo ulivyowaongoza watu wako,

Ili ujijengee jina kuu.*+

15 Tazama kutoka mbinguni uone

Kutoka kwenye makao yako yaliyoinuliwa ya utakatifu na utukufu.*

Iko wapi bidii yako na nguvu zako,

Shauku ya huruma*+ na rehema yako?+

Zimeondolewa kwangu.

16 Kwa maana wewe ni Baba yetu;+

Ingawa huenda Abrahamu asitujue

Na huenda Israeli asitutambue,

Wewe, Ee Yehova, ni Baba yetu.

Mkombozi wetu wa zamani za kale ndilo jina lako.+

17 Kwa nini, Ee Yehova, unaruhusu* tutangetange kutoka kwenye njia zako?

Kwa nini unaruhusu* mioyo yetu iwe migumu ili tusikuogope?+

Rudi, kwa ajili ya watumishi wako,

Makabila ya urithi wako.+

18 Watu wako watakatifu waliimiliki kwa muda mfupi.

Maadui wetu walipakanyaga-kanyaga mahali pako patakatifu.+

19 Kwa muda mrefu sana tumekuwa kama watu ambao hukuwatawala kamwe,

Kama watu ambao hawakuitwa kamwe kwa jina lako.

64 Laiti ungezipasua mbingu ushuke chini,

Ili milima itetemeke kwa sababu yako,

 2 Kama moto unavyoteketeza vichaka,

Na moto huo unachemsha maji,

Basi jina lako litajulikana kwa maadui wako,

Na mataifa yatatetemeka mbele zako!

 3 Ulipofanya mambo yanayoogopesha ambayo hatungeweza kuyatazamia,+

Ulishuka, nayo milima ikatetemeka mbele zako.+

 4 Tangu zamani hakuna mtu aliyesikia wala kutega sikio,

Wala hakuna jicho lililomwona Mungu, isipokuwa wewe,

Yule anayetenda kwa ajili ya wale wanaoendelea kumtarajia.*+

 5 Umekutana na wale wanaoshangilia kutenda mambo yanayofaa,+

Wale wanaokukumbuka na kufuata njia zako.

Tazama! Ulikuwa na ghadhabu, huku sisi tukiendelea kutenda dhambi,+

Tulifanya hivyo kwa muda mrefu.

Je, sasa tuokolewe?

 6 Na sisi sote tumekuwa kama mtu asiye safi,

Na matendo yetu yote ya uadilifu ni kama kitambaa cha hedhi.+

Sisi sote tutanyauka kama jani,

Na makosa yetu yatatupeperusha kama upepo.

 7 Hakuna yeyote anayeliitia jina lako,

Hakuna yeyote anayejichochea kukushika,

Kwa maana umeuficha uso wako kutoka kwetu,+

Nawe unatufanya tudhoofike* kwa sababu ya* kosa letu.

 8 Lakini sasa, Ee Yehova, wewe ni Baba yetu.+

Sisi ni udongo, nawe ni Mfinyanzi wetu;*+

Sisi sote ni kazi ya mkono wako.

 9 Usiwe na ghadhabu nyingi, Ee Yehova,+

Nawe usilikumbuke kosa letu milele.

Tafadhali, tutazame, kwa maana sisi sote ni watu wako.

10 Majiji yako matakatifu yamekuwa nyika.

Sayuni imekuwa nyika,

Yerusalemu limekuwa ukiwa.+

11 Nyumba yetu ya* utakatifu na utukufu,*

Ambamo mababu zetu walikusifu,

Imeteketezwa kwa moto,+

Na vitu vyote tulivyovithamini sana vimeharibiwa.

12 Baada ya hayo yote, je, bado utajizuia, Ee Yehova?

Je, utaendelea kunyamaza na kuacha tuteseke kupita kiasi?+

65 “Nimeruhusu wale ambao hawakuuliza kunihusu wanitafute;

Nimeruhusu wale ambao hawakunitafuta wanipate.+

Nililiambia taifa ambalo halikuwa linaliitia jina langu, ‘Nipo hapa, nipo hapa!’+

 2 Mchana kutwa nimewanyooshea mikono yangu watu wakaidi,+

Wale wanaotembea katika njia isiyo nzuri,+

Wanaofuata mawazo yao wenyewe;+

 3 Watu wanaonikasirisha daima mbele za uso wangu,+

Wanaotoa dhabihu katika bustani+ na kufukiza moshi wa dhabihu kwenye matofali.

 4 Wanaketi kati ya makaburi,+

Nao wanakaa usiku kucha mafichoni,*

Wakila nyama ya nguruwe,+

Na mchuzi wa vitu vichafu* umo katika vyombo vyao.+

 5 Wanasema, ‘Kaa peke yako; usinikaribie,

Kwa maana mimi ni mtakatifu kuliko wewe.’*

Hawa ni moshi katika mianzi ya pua yangu, moto unaowaka mchana kutwa.

 6 Tazama! Imeandikwa mbele zangu;

Sitasimama tuli,

Lakini nitawalipa,+

Nitawalipa kikamili*

 7 Kwa ajili ya makosa yao na kwa ajili ya makosa ya mababu zao pia,”+ asema Yehova.

“Kwa sababu wamefukiza moshi wa dhabihu juu ya milima

Nao wamenishutumu juu ya vilima,+

Kwanza nitawapimia malipo yao kamili.”*

 8 Yehova anasema hivi:

“Kama divai mpya inapopatikana katika kishada cha zabibu

Kisha mtu anasema, ‘Usikiharibu, kwa sababu kuna kitu kizuri* ndani yake,’

Ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu;

Sitawaangamiza wote.+

 9 Nitatoa uzao* katika Yakobo

Na katika Yuda mrithi wa milima yangu;+

Watu wangu niliowachagua wataumiliki,

Na watumishi wangu watakaa huko.+

10 Sharoni+ itakuwa malisho ya kondoo

Na Bonde la* Akori+ mahali pa kupumzika pa ng’ombe,

Kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta.

11 Lakini ninyi ni kati ya wale wanaomwacha Yehova,+

Wanaousahau mlima wangu mtakatifu,+

Wanaoandaa meza kwa ajili ya mungu wa Bahati Njema,

Na wale wanaovijaza vikombe divai iliyochanganywa kwa ajili ya mungu wa Majaliwa.

12 Basi nitawaamulia muuawe kwa upanga,+

Nanyi nyote mtainama chini ili mchinjwe,+

Kwa sababu niliita, lakini hamkuitika,

Nilizungumza lakini hamkusikiliza;+

Mliendelea kutenda maovu machoni pangu,

Nanyi mkachagua mambo yaliyonichukiza.”+

13 Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:

“Tazama! Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mtakuwa na njaa.+

Tazama! Watumishi wangu watakunywa,+ lakini ninyi mtakuwa na kiu.

Tazama! Watumishi wangu watashangilia,+ lakini ninyi mtaona aibu.+

14 Tazama! Watumishi wangu watapiga vigelegele kwa shangwe kwa sababu ya hali nzuri ya moyo,

Lakini ninyi mtalia kwa sababu ya maumivu ya moyo

Nanyi mtaomboleza kwa sababu ya roho iliyovunjika.

15 Mtaacha jina ambalo watu wangu niliowachagua watalitumia kama laana,

Na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atamuua kila mmoja wenu,

Lakini atawaita watumishi wake mwenyewe kwa jina lingine;+

16 Ili kila mtu anayejitafutia baraka duniani

Abarikiwe na Mungu wa kweli,*

Na yeyote anayeapa kiapo duniani

Aape kwa Mungu wa kweli;*+

Kwa maana taabu za zamani zitasahauliwa;*

Zitafichwa kutoka machoni pangu.+

17 Kwa maana, tazama! ninaumba mbingu mpya na dunia mpya;+

Na mambo ya zamani hayataingia tena akilini,*

Wala hayataingia tena moyoni.+

18 Basi furahini na kushangilia milele kwa sababu ya vitu ninavyoumba.

Kwa maana tazama! ninaumba Yerusalemu kuwa sababu ya shangwe

Na watu wake kuwa sababu ya furaha.+

19 Nami nitashangilia kwa sababu ya Yerusalemu na kufurahi kwa sababu ya watu wangu;+

Sauti ya kulia na ya maombolezo kwa sababu ya taabu haitasikika tena ndani yake.”+

20 “Hakutakuwemo tena ndani yake mtoto mchanga anayeishi siku chache tu,

Wala mzee asiyetimiza siku zake.

Kwa maana mtu anayekufa akiwa na miaka mia moja ataonwa kuwa mvulana tu,

Na mtenda dhambi atalaaniwa, hata ingawa ana umri wa miaka mia moja.*

21 Watajenga nyumba na kuishi ndani yake,+

Nao watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.+

22 Hawatajenga na mtu mwingine akae ndani yake,

Wala hawatapanda na watu wengine wale.

Kwa maana siku za watu wangu zitakuwa kama siku za mti,+

Na watu wangu niliowachagua watafurahia kikamili kazi ya mikono yao.

23 Hawatafanya kazi* ya bure,+

Wala hawatazaa watoto ili wataabike,

Kwa sababu wao ni uzao wa* watu waliobarikiwa na Yehova,+

Na wazao wao pamoja nao.+

24 Hata kabla hawajaita, nitajibu;

Wakiwa bado wanasema, nitasikia.

25 Mbwamwitu na mwanakondoo watalisha pamoja,

Simba atakula majani kama ng’ombe dume,+

Na chakula cha nyoka kitakuwa mavumbi.

Hawatadhuru wala kusababisha uharibifu wowote katika mlima wangu wote mtakatifu,”+ asema Yehova.

66 Yehova anasema hivi:

“Mbingu ni kiti changu cha ufalme, na dunia ni kiti cha miguu yangu.+

Hivyo basi, iko wapi nyumba mnayoweza kunijengea,+

Na pako wapi mahali pangu pa kupumzikia?”+

 2 “Sasa mkono wangu mwenyewe uliumba vitu hivi vyote,

Na vitu vyote vilikuja kuwapo kwa njia hiyo,” asema Yehova.+

“Basi, nitamtazama huyu,

Yule aliye mnyenyekevu na aliyevunjika rohoni na anayelitetemekea* neno langu.+

 3 Anayemchinja ng’ombe dume ni kama yule anayemuua mwanadamu.+

Anayemchinja kondoo ni kama yule anayevunja shingo ya mbwa.+

Anayetoa zawadi—kama damu ya nguruwe!+

Anayetoa toleo la ubani la ukumbusho+ ni kama yule anayebariki kwa maneno ya uchawi.*+

Wamechagua njia zao wenyewe,

Nao wanapenda* mambo yanayochukiza.

 4 Basi nitachagua njia za kuwaadhibu,+

Nami nitawaletea mambo yaleyale wanayoogopa sana.

Kwa sababu nilipoita, hakuna aliyejibu;

Nilipozungumza, hakuna aliyesikiliza.+

Waliendelea kutenda maovu machoni pangu,

Nao wakachagua kufanya mambo yaliyonichukiza.”+

 5 Sikieni neno la Yehova, ninyi mnaolitetemekea* neno lake:

“Ndugu zenu wanaowachukia na kuwatenga kwa sababu ya jina langu, walisema, ‘Yehova na atukuzwe!’+

Lakini atatokea na kuwaletea shangwe,

Nao ndio watakaoaibishwa.”+

 6 Kuna sauti ya ghasia kutoka jijini, sauti kutoka hekaluni!

Ni sauti ya Yehova akiwalipa maadui wake kile wanachostahili.

 7 Kabla hajawa na uchungu wa kuzaa, alizaa.+

Kabla ya kushikwa na uchungu wa kuzaa, alijifungua mtoto wa kiume.

 8 Ni nani amewahi kusikia jambo kama hilo?

Ni nani ameona mambo kama hayo?

Je, nchi itazaliwa katika siku moja?

Au, je, taifa lote litazaliwa mara moja?

Hata hivyo, mara tu Sayuni aliposhikwa na uchungu wa kuzaa, aliwazaa wanawe.

 9 “Je, nimfanye mtoto akaribie kuzaliwa kisha nifanye asizaliwe?” asema Yehova.

“Au, je, nisababishe afikie hatua ya kuzaliwa kisha nifunge tumbo la uzazi?” asema Mungu wako.

10 Shangilieni pamoja na Yerusalemu na mfurahi pamoja naye,+ ninyi nyote mnaompenda.+

Furahini sana pamoja naye, ninyi nyote mnaomwombolezea,

11 Kwa maana mtanyonya na kushiba kabisa maziwa ya titi lake la faraja,

Nanyi mtakunywa sana na kufurahia utukufu wake mwingi.

12 Kwa maana Yehova anasema hivi:

“Tazama, ninampa amani kama mto+

Na utukufu wa mataifa kama mto unaofurika.+

Mtanyonya na kubebwa kiunoni,

Nanyi mtachezeshwa kwenye magoti yake.

13 Kama mama anavyomfariji mwanawe,

Ndivyo nitakavyoendelea kuwafariji;+

Nanyi mtafarijiwa kwa sababu ya Yerusalemu.+

14 Mtaona jambo hilo, na moyo wenu utashangilia,

Mifupa yenu itanawiri kama majani mabichi.

Na mkono wa Yehova utajulikana* kwa watumishi wake,

Lakini atawashutumu maadui wake.”+

15 “Kwa maana Yehova atakuja kama moto,+

Na magari yake ya vita kama upepo wa dhoruba,+

Ili kulipa kwa hasira kali,

Ili kukemea kwa miali ya moto.+

16 Kwa maana Yehova atatekeleza hukumu kwa moto,

Naam, kwa upanga wake, dhidi ya wote wenye mwili;*

Na watakaouawa na Yehova watakuwa wengi.

17 “Wale wanaojitakasa na kujisafisha ili waingie kwenye bustani*+ wakimfuata yule aliye katikati, wale wanaokula nyama ya nguruwe+ na vitu vinavyochukiza na panya,+ wote watafikia mwisho wao pamoja,” asema Yehova. 18 “Kwa kuwa ninajua kazi zao na mawazo yao, ninakuja kuwakusanya watu wa mataifa yote na lugha zote, nao watakuja na kuuona utukufu wangu.”

19 “Nitaweka ishara miongoni mwao, nami nitawapeleka baadhi ya wale wanaoponyoka waende kwa mataifa—waende Tarshishi,+ Pulu, na Ludi,+ wale wanaouvuta upinde, waende Tubali na Yavani,+ na kwenye visiwa vilivyo mbali sana—mataifa ambayo hayajasikia habari kunihusu wala kuuona utukufu wangu; nao watatangaza utukufu wangu miongoni mwa mataifa.+ 20 Watawaleta ndugu zenu wote kutoka katika mataifa yote+ wawe zawadi kwa Yehova, wakiwa juu ya farasi, ndani ya magari ya vita, ndani ya magari ya kukokotwa yaliyofunikwa, juu ya nyumbu, juu ya ngamia wenye kasi, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu, Yerusalemu,” asema Yehova, “kama watu wa Israeli wanavyoleta zawadi zao ndani ya nyumba ya Yehova zikiwa katika chombo safi.”

21 “Pia nitawachukua baadhi yao wawe makuhani na Walawi,” asema Yehova.

22 “Kwa maana kama vile mbingu mpya na dunia mpya+ ninazoumba zitakavyoendelea kusimama mbele zangu,” asema Yehova, “ndivyo uzao wenu* na jina lenu litakavyoendelea kudumu.”+

23 “Na kutoka mwezi mpya mpaka mwezi mpya na kutoka sabato mpaka sabato,

Wote wenye mwili* wataingia ili kuinama chini* mbele zangu,”+ asema Yehova.

24 “Nao watatoka nje na kuzitazama maiti za watu walioniasi;

Kwa maana funza walio juu yao hawatakufa,

Na moto wao hautazimwa,+

Nao watakuwa kitu cha kuchukiza sana kwa watu wote.”*

Maana yake “Wokovu wa Yehova.”

Au “hamjui bwana wake.”

Tnn., “Havijafinywa; Havijatumbuliwa.”

Au “watawala.”

Au “mafundisho.”

Au “Nafsi yangu imechukia.”

Au “pombe yako ya ngano.”

Inaonekana ni miti na bustani zilizohusiana na ibada ya sanamu.

Nyuzi zinazoshika moto kwa urahisi ambazo zinafanana na kamba.

Au “Katika kipindi cha mwisho cha zile siku.”

Au “mafundisho yatatoka.”

Au “kurekebisha.”

Au “kitanyenyekezwa.”

Au “kitanyenyekezwa.”

Au “wanyama wanaoguguna ambao hula sana.”

Au “Ambaye pumzi yake iko katika mianzi ya pua yake.”

Au “mwaguzi.”

Au “wasio na msimamo.”

Au “tabibu.”

Tnn., “machoni pa utukufu wake.”

Au “Ole wa nafsi zao.”

Tnn., “Watakula matunda ya matendo yao.”

Tnn., “wakiwa wamerefusha shingo (koo) zao.”

Au “Kigwe.”

Au “ukumbuu.”

Tnn., “nyumba za nafsi.”

Au “kauri zinazovuma zinazotumiwa kama mapambo.”

Au “nguo za ndani.”

Yaani, aibu ya kutoolewa na kutokuwa na watoto.

Tnn., “kinyesi cha.”

Au “kuondoa.”

Tnn., “viganja kumi vya”

Angalia Nyongeza B14.

Angalia Nyongeza B14.

Angalia Nyongeza B14.

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “limepanua nafsi yake.”

Au “wakuu wake.”

Au “haki yake.”

Au “Uamuzi wa; Shauri la.”

Au “mafundisho.”

Au “nguzo ya ishara.”

Au “ziko tayari kupiga mshale.”

Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”

Tnn., “sauti ya yule aliyekuwa akiita.”

Tnn., “nimenyamazishwa.”

Au “uzao mtakatifu utakuwa.”

Au labda, “walishindwa.”

Maana yake “Ni Mabaki tu Watakaorudi.”

Au “mtaro wa maji.”

Au labda, “kuishambulia.”

Au “bomoa kuta zake.” Tnn., “kulipasua.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “Mwanamwali.”

Maana yake “Mungu Yuko Pamoja Nasi.”

Au “makorongo.”

Yaani, Mto Efrati.

Tnn., “kalamu ya mwanadamu anayeweza kufa.”

Huenda jina hili linamaanisha “Kuharakisha Kwenda Kwenye Nyara, Kuja Upesi Kwenye Nyara.”

Au “limeshuhudiwa.”

Tnn., “nikamkaribia.”

Yaani, mke wa Isaya.

Shiloa ulikuwa mfereji wa maji.

Yaani, Mto Efrati.

Angalia Isa Isa 7:14.

Au “Jifungeni viuno.”

Katika Kiebrania maana ya neno Imanueli ni “Mungu yuko pamoja nasi.” Angalia Isa 7:14; 8:8.

Au “ushahidi.”

Au “mafundisho.”

Au “kumsubiri kwa hamu.”

Au “ushahidi.”

Tnn., “mapambazuko.”

Au “serikali; utawala wa kifalme.”

Au “serikali yake; utawala wake wa kifalme.”

Tnn., “kutoka nyuma.”

Au labda, “tawi la mtende na tete.”

Au “masharti yanayodhuru.”

Au “kuwajibishwa.”

Au “utukufu.”

Tnn., “nitamwadhibu.”

Au “Kuanzia kwenye nafsi hadi kwenye mwili ataondoa.”

Au “adhabu.”

Au “shoka.”

Au “uadilifu.”

Au “roho.”

Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”

Au labda, “Na ndama na simba watakula pamoja.”

Au “nguzo ya ishara.”

Au “Mataifa yatamtafuta.”

Yaani, Babilonia.

Au “nguzo ya ishara.”

Tnn., “bega la.”

Au “Mamlaka yao itafika juu ya.”

Au labda, “ataikausha.”

Tnn., “ulimi wa.”

Yaani, Mto Efrati.

Au “roho.”

Au labda, “ataipiga iwe mito saba.”

“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “Mpigieni muziki.”

Tnn., “mkaaji wa kike.” Usemi huu unarejelea wakaaji wote kuwa kama mwanamke.

Au “nguzo ya ishara.”

Tnn., “watu wangu waliotakaswa.”

Tnn., “na Kesili zao,” labda maneno haya yanarejelea kundi la nyota la Orioni na makundi mengine ya nyota yaliyo karibu.

Au “Nitaiwajibisha.”

Au “pambo la falme.”

Au labda, “Na roho waovu walio kama mbuzi.”

Au “Atawapumzisha.”

Au “wasimamizi wao wa kazi.”

Au “dhihaka.”

Au “msimamizi wa kazi.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Tnn., “Mbuzi dume wote wa dunia wanaokandamiza.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Tnn., “nyumba yake.”

Au “tawi.”

Tnn., “Hili ndilo shauri lililotolewa.”

Au “ulio tayari kupiga.”

Au “nyoka mwenye sumu anayerukaruka.”

Au “Hekalu.”

Au “Nafsi yake inatetemeka.”

Au “korongo.”

Au “matawi yake yaliyojaa zabibu nyekundu.”

Au labda, “Kwa sababu kelele za vita zimeshuka juu ya matunda yako ya kiangazi na mavuno yako.”

Au “iliyohesabiwa kwa uangalifu kama kibarua anavyofanya”; yaani, kwa miaka mitatu kamili.

Tnn., “wana wa Israeli.”

Tnn., “mafuta ya nyama yake yatapungua.”

Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”

Angalia Kamusi.

Au “yanayopendeza.”

Au “mungu wa kigeni.”

Au “mbaruti katika.”

Tnn., “taifa lenye watu waliochomoza juu na kusuguliwa.”

Au “taifa lenye nguvu nyingi linaloyakanyaga mataifa mengine.”

Au “nguzo ya ishara.”

Au labda, “kutazama kutoka.”

Tnn., “taifa lenye watu waliochomoza juu na kusuguliwa.”

Au “taifa lenye nguvu nyingi linaloyakanyaga mataifa mengine.”

Au “watahuzunika katika nafsi.”

Au “Memfisi.”

Au labda, “tawi la mtende au tete.”

Au “kamanda.”

Au “akiwa amevaa mavazi machache.”

Au “aibu ya.”

Au “Misri ambayo walivutiwa na urembo wake.”

Inaonekana kwamba usemi huu unarejelea eneo la Babilonia ya kale.

Tnn., “kiuno changu kimejaa maumivu.”

Au “ipakeni.”

Tnn., “Mwana wa.”

Maana yake “Kimya.”

Au “iliyohesabiwa kwa uangalifu kama kibarua anavyofanya”; yaani, kwa mwaka mmoja kamili.

Inaonekana maneno haya yanarejelea Yerusalemu.

Tashihisi ya kishairi, ambayo labda inaonyesha sikitiko au huruma.

Au “wapanda farasi.”

Au “inatayarisha.”

Au “wapanda farasi.”

Au “ulinzi wa Yuda utaondolewa.”

Au “Mtengenezaji.”

Au “jumba la mfalme.”

Tnn., “makao.”

Au “milki yako.”

Tnn., “uzito.”

Au “machipukizi.”

Tnn., “Mbegu.”

Yaani, kijito cha Mto Nile.

Tnn., “mabikira.”

Au labda, “bandari.”

Tnn., “siku za.”

Au “dunia.”

Au “Anausokota uso wa dunia.”

Au labda, “inakauka.”

Au “la kale.”

Au labda, “inakauka.”

Au “magharibi.”

Au “mashariki.”

Au “Pambo.”

Tnn., “mbele ya wazee wake.”

Au “Mashauri ya.”

Au “divai iliyowekwa kwenye machicha.”

Tnn., “atameza.”

Au “shela iliyosokotwa.”

Au “Ataondoa.”

Au labda, “wale ambao mwelekeo wao hautikisiki.”

“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “ni tambarare.”

Au “Kwa nafsi zetu tunatamani.”

Yaani, kwamba Mungu na jina lake likumbukwe, litangazwe.

Tnn., “Maiti yangu itaamka.”

Au labda, “umande wa mimea (miholi).”

Au “itawazaa wale waliokufa ambao hawana uwezo.”

Au “shutuma.”

Angalia Kamusi.

Inaonekana ni Israeli, hapa anarejelewa kuwa mwanamke na kufananishwa na shamba la mizabibu.

Angalia Kamusi.

Yaani, Mto Efrati.

Angalia Kamusi.

Inaonekana neno hili linarejelea jiji kuu, Samaria.

Au “majivuno; kiburi.”

Au “majivuno; kiburi.”

Au “Kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia, kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia.”

Tnn., “midomo yenye kigugumizi.”

Au “Kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia, kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia.”

Au labda, “tumetekeleza maono.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “timazi.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au labda, “Watakapoelewa, watashikwa na hofu kubwa.”

Au “nchi tambarare ya chini iliyo.”

Au “kuipata dunia yote.”

Au “humtia nidhamu kwa; humwadhibu kwa.”

Au “kusudi.”

Au “ambaye hekima yake inayotumika ni kuu.”

Huenda jina hili linamaanisha “Jiko la Madhabahu ya Mungu,” inaelekea ni Yerusalemu.

Tnn., “wageni wako.”

Au “nafsi yake ikiwa tupu.”

Au “nafsi yake ikiwa imekauka.”

Au “shauri lao.”

Au “Jinsi mlivyopotoka!”

Tnn., “anayekaripia.”

Yaani, kwa sababu ya aibu na kukata tamaa.

Tnn., “wanaomwaga sadaka ya kinywaji,” inaonekana inarejelea kufanya mapatano.

Au “bila kutafuta ushauri kutoka katika kinywa changu.”

Tnn., “katika ngome ya Farao.”

Au “nyoka mwenye sumu anayerukaruka.”

Au “mafundisho.”

Tnn., “mambo laini.”

Au labda, “tangi la maji.”

Au “anaendelea kuwatarajia.”

Au “wanaomngoja kwa hamu.”

Au “sanamu za kuyeyushwa.”

Au labda, “na kuziita uchafu.”

Au “mkate.”

Tnn., “mnono na wenye mafuta.”

Au “jeraha la kuvunjika.”

Au “Pumzi.”

Tnn., “chujio la ubatili.”

Au “mnapojitakasa.”

Au “akisikia sauti ya.”

Hapa neno “Tofethi” linatumiwa kurejelea mahali pa mfano pa kuteketezea vitu, panafananisha maangamizi.

Au “wapanda farasi.”

Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”

Au “moto wake uko.”

Au “kibanda cha kujificha.”

Au “mahali pa kukimbilia.”

Au “kutenda kwa kutomwogopa Mungu.”

Au “matendo mema.”

Au “Mnaowafungua.”

Au “nguvu zetu.”

Yaani, adui.

Au labda, “inakauka.”

Au “kilele salama.”

Au “utatafakari.”

Tnn., “ina kina kirefu isiweze kueleweka.”

Au “mwenyeji.”

Au “itatiririka.”

Inaonekana vinarejelea Bosra, jiji kuu la Edomu.

Tnn., “mawe.”

Au labda, “Na roho waovu walio kama mbuzi.”

Tnn., “umewagawia kwa kamba ya kupimia.”

Au “msimamizi mkuu wa vinywaji vya mfalme.”

Au “jumba la mfalme.”

Au “Kisiria.”

Tnn., “Fanyeni baraka pamoja nami na mtoke nje na kuja kwangu.”

Au “jumba la mfalme.”

Au “jumba la mfalme.”

Au “matusi.”

Tnn., “wamefika kwenye mlango wa tumbo la uzazi.”

Tnn., “ninatia roho fulani ndani yake.”

Tnn., “akaitandaza.”

Au labda, “katikati ya.”

Au “Nitaikausha mifereji ya Nile ya.”

Tnn., “lilifanywa.”

Au “nimelitengeneza.”

Yaani, Hezekia.

Au “nafaka zilizoanguka na kuota zenyewe.”

Au “hekalu la.”

Tnn., “katika siku zako.”

Labda hatua hizo za ngazi zilitumiwa kuhesabu muda, kama saa ya kivuli.

Au “Huu ni utungo wa.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au labda, “korongo.”

Tnn., “Uwe dhamana yangu.”

Au “kimyakimya.”

Au “uchungu wa nafsi yangu.”

Yaani, maneno na matendo ya Mungu.

Au “uliipenda sana nafsi yangu.”

Au “Umeziondoa dhambi zangu zote kutoka mbele ya macho yako.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Tnn., “akawashangilia.”

Au “jumba lake mwenyewe la mfalme.”

Au “jumba lako la mfalme?”

Au “jumba langu la mfalme.”

Au “jumba lako la mfalme.”

Au “ukweli.”

Tnn., “katika siku zangu.”

Au “Lifarijini.”

Au “malipo maradufu.”

Au “Tayarisheni.”

Au “wanadamu wote.”

Au “Wanadamu wote.”

Au “roho.”

Au “Atalichunga.”

Au “ukubwa wa.”

Ni urefu kuanzia kidole gumba hadi kidole kidogo, kiganja kikiwa kimepanuliwa. Angalia Nyongeza B14.

Au labda, “ameielewa.”

Au “haiwezi kuandaa kuni za kutosha.”

Au “sanamu ya kuyeyushwa.”

Au “tufe la.”

Au “watawala.”

Au “hauwezi kueleweka.”

Au “nguvu zenye msukumo.”

Au “Nyamazeni mbele zangu.”

Au “upande wa mapambazuko ya jua.”

Yaani, ili amtumikie Yeye.

Tnn., “Mbegu ya.”

Yaani, mtu wa hali ya chini asiye na ulinzi.

Tnn., “kwanza.”

Au “tuyaelekezee moyo wetu.”

Au “mashariki.”

Au “watawala wasaidizi.”

Au “kitu kisichokuwepo.”

Au “Sanamu zao za kuyeyushwa.”

Au “nafsi yangu imemkubali.”

Au “mafundisho.”

Au “Sishiriki utukufu wangu na yeyote.”

Au “maeneo ya pwani.”

Au “sanamu za kuyeyushwa.”

Au “mafundisho.”

Au “mafundisho.”

Au “nafsi yako.”

Tnn., “Nitaileta mbegu yako.”

Labda ni mambo yatakayotokea kwanza wakati ujao.

Au “na kunitumaini.”

Au “matendo yako ya uasi.”

Labda hawa ni walimu wa Sheria.

Au “tangu ulipozaliwa.”

Maana yake “Mnyoofu,” jina la heshima la Israeli.

Au “nitaimiminia maji nchi yenye kiu.”

Tnn., “mbegu yako.”

Yaani, sanamu.

Au “sanamu ya kuyeyushwa.”

Au “tezo yake.”

Au “madhabahu.”

Au “ubao uliokauka.”

Au “kuiokoa nafsi yake.”

Au “manabii wa uwongo.”

Tnn., “Kuvifungua viuno vya.”

Tnn., “Nitakufunga kiuno kwa nguvu.”

Au “Kutoka mawio hadi machweo.”

Au “anayebishana.”

Au “na yule aliyemtengeneza.”

Au “yule aliyeutengeneza.”

Au labda, “Je, udongo unapaswa kusema: ‘Kazi yako haina vishikio’?”

Au “Una uchungu wa kuzaa nini?”

Au labda, “Wafanyakazi wa.”

Au labda, “wafanyabiashara wa.”

Au labda, “ili iwe tupu.”

Tnn., “Sikuiambia mbegu ya.”

Au “Nitafuteni bure.”

Tnn., “mbegu.”

Yaani, sanamu zilizobebwa na wanyama.

Tnn., “wanaiinamia.”

Au “awali.”

Au “kusudi; shauri.”

Au “upande wa mapambazuko ya jua.”

Au “kusudi; shauri.”

Tnn., “moyo wenye nguvu.”

Au labda, “sitakutana na yeyote kwa fadhili.”

Au “Malkia.”

Au “Malkia.”

Au labda, “Licha ya.”

Au “Nawe hutajua jinsi ya kuuzuia kwa hirizi.”

Au labda, “Wale wanaozigawa mbingu; Wanajimu.”

Au “kuziokoa nafsi zao.”

Tnn., “kuelekea eneo lake.”

Au labda, “mnaotoka Yuda.”

Au “awali.”

Au “sanamu yangu ya kuyeyushwa.”

Au “Nimekuchunguza.” Au labda, “Nimekuchagua.”

Au “Sishiriki utukufu wangu na yeyote.”

Au “pamoja na.”

Au “kwa faida yako.”

Tnn., “Mbegu yako ingekuwa nyingi.”

Tnn., “kutoka katika tumbo la uzazi.”

Au “uliong’arishwa.”

Au “Yehova atanitendea kwa haki.”

Au “thawabu yangu iko.”

Au “nia njema.”

Au labda, “vilima visivyo na kitu.”

Au “nguzo yangu ya ishara.”

Tnn., “kifuani.”

Tnn., “wote wenye mwili.”

Au “ulimi uliozoezwa vizuri.”

Au labda, “kumwimarisha.”

Tnn., “kwa neno.”

Au “kushindana nami?”

Au “tutazamane.”

Aina fulani ya mdudu mharibifu.

Au “kumtegemea.”

Au “aliyewazaa kwa uchungu wa kuzaa.”

Au “vitangojea nguvu zangu.”

Aina ya mbu anayeitwa hak·kin·namʹ katika Kiebrania.

Au “hautavunjwa.”

Au “mafundisho.”

Au labda, “Mnyoo.”

Angalia Kamusi.

Tnn., “juu ya vichwa vyao.”

Au “yule anayekubana.”

Au “jicho kwa jicho.”

Au “itaona ushindi wa.”

Au “hawatakuwa na la kusema.”

Au labda, “jambo ambalo tulisikia?”

Maneno “mbele yake” huenda yanarejelea mtazamaji yeyote au Mungu.

Au “hana sura ya pekee hivi kwamba tumtamani.”

Au “aliyeelewa.”

Au labda, “Alikuwa kama mtu ambaye watu waligeuza mbali nyuso zao ili wasimtazame.”

Au “alichomwa kwa silaha.”

Au “ukandamizaji.”

Au “njia yake ya maisha.”

Au “Aliuawa.”

Au “Na mtu atatoa kaburi lake.”

Tnn., “mtu tajiri.”

Au “ukatili.”

Au “Yehova alifurahia.”

Au “nafsi yake.”

Tnn., “Ataiona mbegu yake.”

Au “mapendezi.”

Au “maumivu ya nafsi.”

Au “aliimwaga nafsi yake.”

Au “watoto.”

Au “bwana mkubwa.”

Au “Mtengenezaji.”

Au “bwana mkubwa.”

Tnn., “aliyeumizwa rohoni.”

Au “mawe ya moto.”

Au “watoto.”

Au “watoto.”

Au “pesa mlizopata kwa shida.”

Tnn., “mtafurahia sana unono.”

Au “nafsi yenu itaendelea.”

Au “yenye kuaminika; kutegemeka.”

Au “kwa hiari.”

Au “litathibitika kuwa.”

Au “mapenzi yangu.”

Au “litamjengea jina Yehova.”

Au “wenye nafsi yenye nguvu.”

Yaani, katika kifo.

Au labda, “Kutokana na.”

Yaani, kaburini.

Au “makorongo.”

Au “korongoni.”

Au “Je, nijifariji.”

Huenda maneno hayo yanarejelea ibada ya sanamu.

Au labda, “mfalme.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Tnn., “huchoki.”

Au “kuficha mambo.”

Au “Anayekaa.”

Au “kufidia kwa kumpa.”

Au “tunapozitesa nafsi zetu?”

Au “mambo mnayofurahia.”

Au “kuitesa nafsi yake.”

Au “tamaa za nafsi yako.”

Au “kuzishibisha nafsi zinazoteseka.”

Au “kuishibisha nafsi yako.”

Tnn., “wa mashimo yaliyo katika ukuta.”

Tnn., “unaugeuza mguu wako usifuatilie.”

Au “mambo unayofurahia.”

Au “ufurahie.”

Au “ubatili.”

Au “unyoofu.”

Au “Unyoofu.”

Tnn., “na jambo hilo lilikuwa baya machoni pake.”

Au “ukamletea ushindi.”

Au “ushindi.”

Au “koti lisilo na mikono.”

Tnn., “mbegu yako.”

Tnn., “mbegu ya mbegu yako.”

Au “kwenye mwangaza wa mapambazuko yako.”

Tnn., “yatakufunika.”

Au “nyumba yangu ya urembo.”

Au “matundu katika nyumba ya ndege?”

Au “kama zilivyokuwa awali.”

Au “atakurembesha.”

Au “kwa nia yangu njema.”

Au “kibali cha.”

Au “kumrembesha.”

Au “utajiri.”

Tnn., “Mbegu yao itajulikana.”

Tnn., “mbegu ambayo.”

Au “joho lisilo na mikono.”

Au “nguzo ya ishara.”

Au labda, “nyekundu nyangavu.”

Au “ushindi.”

Au “ambao hawatakuwa waongo.”

Au “malaika wa uwepo wake.”

Au “maji yenye kina kirefu.”

Au “nyikani.”

Au “zuri.”

Au “uzuri.”

Tnn., “Msukosuko wa sehemu zako za ndani.”

Au “unatufanya.”

Tnn., “unafanya.”

Au “kumngojea kwa subira.”

Tnn., “tuyeyuke.”

Tnn., “kwa mkono wa.”

Au “Muumba wetu.”

Au “Hekalu letu la.”

Au “uzuri.”

Au labda, “katika vibanda vya kukesha.”

Au “visivyo safi.”

Au labda, “Kwa maana nitakupa utakatifu wangu.”

Tnn., “katika vifua vyao.”

Tnn., “katika vifua vyao.”

Tnn., “kina baraka.”

Tnn., “mbegu.”

Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”

Au “uaminifu.” Tnn., “Amina.”

Au “uaminifu.” Tnn., “Amina.”

Au “matatizo ya zamani yatasahauliwa.”

Au “hayatakumbukwa.”

Au labda, “Na mtu yeyote asiyetimiza miaka mia moja ataonwa kuwa amelaaniwa.”

Au “kazi ngumu.”

Tnn., “mbegu ya.”

Au “anayelihangaikia.”

Au labda, “yule anayeisifu sanamu.”

Au “Na nafsi zao zinapenda.”

Au “mnaolihangaikia.”

Au “nguvu za Yehova zitajulikana.”

Au “wanadamu wote.”

Yaani, bustani za pekee zilizotumiwa kwa ajili ya ibada ya sanamu.

Tnn., “mbegu yenu.”

Au “Wanadamu wote.”

Au “kuabudu.”

Tnn., “wote wenye mwili.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki