Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • nwt Zaburi 1:1-150:6
  • Zaburi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Zaburi
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Zaburi

ZABURI

KITABU CHA KWANZA

(Zaburi 1-41)

1 Mwenye furaha ni mtu ambaye hatembei katika mashauri ya waovu

Na hasimami katika njia ya watenda dhambi+

Naye haketi katika kiti cha wenye dhihaka.+

 2 Lakini anapendezwa na sheria ya Yehova,+

Naye huisoma sheria Yake kwa sauti ya chini* mchana na usiku.+

 3 Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji,

Mti unaozaa matunda katika majira yake,

Na majani yake hayanyauki.

Na kila jambo analofanya litafanikiwa.+

 4 Waovu hawako hivyo;

Wao ni kama makapi yanayopeperushwa mbali na upepo.

 5 Ndiyo sababu waovu hawataendelea kusimama katika hukumu;+

Wala watenda dhambi hawataendelea kusimama katika kusanyiko la waadilifu.+

 6 Kwa maana Yehova anaijua njia ya waadilifu,+

Lakini njia ya waovu itaangamia.+

2 Kwa nini mataifa yana msukosuko

Na watu wananong’ona* kuhusu jambo lisilo na maana?+

 2 Wafalme wa dunia wanajipanga

Na maofisa wakuu wanakusanyika* pamoja kama kitu kimoja+

Dhidi ya Yehova na dhidi ya mtiwa-mafuta* wake.+

 3 Wanasema: “Na tuzikate pingu zao

Na kuzitupa kamba zao!”

 4 Yule anayeketi kwenye kiti cha ufalme mbinguni atacheka;

Yehova atawadhihaki.

 5 Wakati huo ataongea nao kwa hasira yake

Na kuwatisha kwa hasira yake inayowaka,

 6 Akisema: “Mimi mwenyewe nimemweka mfalme wangu+

Juu ya Sayuni,+ mlima wangu mtakatifu.”

 7 Acheni nitangaze agizo la Yehova;

Aliniambia: “Wewe ni mwanangu;+

Leo nimekuwa baba yako.+

 8 Niombe, nami nitakupa mataifa kuwa urithi wako

Na miisho ya dunia kuwa miliki yako.+

 9 Utawavunja kwa fimbo ya mfalme ya chuma,+

Nawe utawavunjavunja kama chombo cha udongo.”+

10 Basi sasa, enyi wafalme, onyesheni ufahamu;

Kubalini kurekebishwa,* enyi waamuzi wa dunia.

11 Mtumikieni Yehova kwa woga,

Na mshangilie mkitetemeka.

12 Mheshimuni* mwana,+ la sivyo Mungu atawaka hasira

Nanyi mtaangamia kutoka njiani,+

Kwa maana hasira Yake huwaka upesi.

Wenye furaha ni wale wote wanaomkimbilia Yeye.

Muziki wa Daudi alipokuwa akimkimbia Absalomu mwanawe.+

3 Ee Yehova, kwa nini maadui wangu wamekuwa wengi sana?+

Kwa nini watu wengi sana wanainuka dhidi yangu?+

 2 Wengi wanasema hivi kunihusu:*

“Mungu hatamwokoa.”+ (Sela)*

 3 Lakini wewe, Ee Yehova, ni ngao kunizunguka,+

Utukufu wangu+ na Yule anayekiinua kichwa changu.+

 4 Nitamlilia Yehova kwa sauti kubwa,

Naye atanijibu kutoka kwenye mlima wake mtakatifu.+ (Sela)

 5 Nitajilaza chini na kulala usingizi;

Nami nitaamka nikiwa salama,

Kwa maana Yehova anaendelea kunitegemeza.+

 6 Siogopi makumi ya maelfu

Waliojipanga dhidi yangu kila upande.+

 7 Inuka, Ee Yehova! Niokoe,+ Ee Mungu wangu!

Kwa maana utawapiga maadui wangu wote kwenye utaya;

Utayavunja meno ya waovu.+

 8 Wokovu ni wa Yehova.+

Baraka yako iko juu ya watu wako. (Sela)

Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Muziki wa Daudi.

4 Ninapokuita, unijibu, Ee Mungu wangu mwadilifu.+

Nitengenezee njia ya kutoroka* taabu yangu.

Nionyeshe kibali na usikie sala yangu.

 2 Enyi wanadamu, mtaendelea mpaka lini kuibadili heshima yangu kuwa aibu?

Mtaendelea mpaka lini kupenda mambo yasiyo na faida na kutafuta mambo ya uwongo? (Sela)

 3 Jueni kwamba Yehova atamtendea mshikamanifu wake kwa njia ya pekee;*

Yehova atasikia ninapomlilia.

 4 Kasirika, lakini usitende dhambi.+

Zungumza moyoni mwako, kitandani mwako, na unyamaze kimya. (Sela)

 5 Toa dhabihu za uadilifu,

Na umtumaini Yehova.+

 6 Kuna wengi wanaosema: “Ni nani atakayetuonyesha jambo lolote jema?”

Acha nuru ya uso wako ituangazie, Ee Yehova.+

 7 Umeujaza moyo wangu shangwe nyingi sana

Kuliko wale walio na mavuno mengi sana ya nafaka na divai mpya.

 8 Nitajilaza chini na kulala usingizi kwa amani,+

Kwa maana wewe peke yako, Ee Yehova, hunifanya niishi kwa usalama.+

Kwa kiongozi wa Nehilothi.* Muziki wa Daudi.

5 Sikiliza maneno yangu, Ee Yehova;+

Sikiliza kwa makini kilio changu cha uchungu.

 2 Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada,

Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa sababu ninasali kwako.

 3 Ee Yehova, utasikia sauti yangu asubuhi;+

Asubuhi nitakueleza mahangaiko yangu+ na kusubiri kwa hamu.

 4 Kwa maana wewe si Mungu anayefurahia uovu;+

Hakuna mtu yeyote mwovu anayeweza kukaa nawe.+

 5 Hakuna mtu yeyote mwenye kiburi anayeweza kusimama mbele zako.*

Unawachukia wale wote wanaotenda maovu;+

 6 Utawaangamiza wale wanaosema uwongo.+

Yehova anawachukia kabisa watu wakatili na wadanganyifu.*+

 7 Lakini nitaingia katika nyumba yako+ kwa sababu ya upendo wako mwingi mshikamanifu;+

Nitainama chini kuelekea hekalu lako takatifu* nikiwa na heshima na woga kukuelekea.+

 8 Niongoze, Ee Yehova, katika uadilifu wako kwa sababu ya maadui wangu;

Ifanye njia yako iwe wazi kwangu.+

 9 Kwa maana hakuna lolote wanalosema linaloweza kutumainiwa;

Ndani yao hamna lolote isipokuwa nia ya kudhuru.

Koo lao ni kaburi lililo wazi;

Wanasifusifu kwa ulimi wao.*+

10 Lakini Mungu atawatangaza kuwa na hatia;

Njama zao wenyewe zitasababisha waanguke.+

Na wafukuzwe kwa sababu ya dhambi zao nyingi,

Kwa maana wamekuasi wewe.

11 Lakini wale wote wanaokukimbilia watashangilia;+

Watapaza sauti kwa shangwe daima.

Nawe utawakinga wasifikiwe,

Na wale wanaolipenda jina lako watashangilia kwa sababu yako.

12 Kwa maana utambariki yeyote aliye mwadilifu, Ee Yehova;

Utawazunguka kwa kibali kana kwamba kwa ngao kubwa.+

Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda vilivyopatanishwa na sauti ya Sheminithi.* Muziki wa Daudi.

6 Ee Yehova, usinikaripie katika hasira yako,

Na usinirekebishe katika ghadhabu yako.+

 2 Nionyeshe kibali,* Ee Yehova, kwa maana ninadhoofika.

Niponye, Ee Yehova,+ kwa maana mifupa yangu inatetemeka.

 3 Naam, ninasumbuka* sana,+

Nami nakuuliza, Ee Yehova—nitasumbuka mpaka lini?+

 4 Rudi, Ee Yehova, uniokoe;*+

Niokoe kwa ajili ya upendo wako mshikamanifu.+

 5 Kwa maana waliokufa hawakutaji;*

Katika kaburi,* ni nani atakayekusifu?+

 6 Nimechoka kwa sababu ya kulia kwa uchungu;+

Usiku kucha ninakilowesha kitanda changu kwa machozi;*

Kochi langu nalifanya lifurike kwa machozi.+

 7 Jicho langu limedhoofika kwa sababu ya huzuni yangu;+

Limeingia giza* kwa sababu ya wote wanaoninyanyasa.

 8 Niondokeeni, ninyi nyote mnaotenda maovu,

Kwa maana Yehova atasikia sauti ya kilio changu.+

 9 Yehova atasikia ombi langu la kutaka kibali;+

Yehova ataikubali sala yangu.

10 Maadui wangu wote wataaibishwa na kutamaushwa;

Watarudi nyuma ghafla kwa aibu.+

Wimbo wa huzuni* wa Daudi ambao alimwimbia Yehova kwa sababu ya maneno ya Kushi Mbenjamini.

7 Ee Yehova Mungu wangu, nimekukimbilia wewe.+

Niokoe kutoka kwa wale wote wanaonitesa na unifanye nisalimike.+

 2 La sivyo watanirarua* vipandevipande kama simba anavyofanya,+

Watanibeba na kwenda nami pasipo na yeyote wa kuniokoa.

 3 Ee Yehova Mungu wangu, ikiwa nimekosea katika jambo hili,

Ikiwa nimetenda isivyo haki,

 4 Ikiwa nimemkosea anayenitendea wema,+

Au ikiwa nimempora adui yangu bila sababu,*

 5 Basi acha adui anikimbize na kunipita;*

Acha aukanyagie uhai wangu ardhini

Na kuufanya utukufu wangu utokomee mavumbini. (Sela)

 6 Inuka katika hasira yako, Ee Yehova;

Simama ukabiliane na hasira kali ya maadui wangu;+

Amka kwa ajili yangu, na uamuru kwamba haki itendeke.+

 7 Acha mataifa yakuzingire;

Nawe utachukua hatua dhidi yao kutoka juu.

 8 Yehova atayahukumu mataifa.+

Nihukumu, Ee Yehova, kulingana na uadilifu wangu

Na kulingana na utimilifu wangu.+

 9 Tafadhali, yakomeshe matendo maovu ya waovu.

Lakini umwimarishe mwadilifu,+

Kwa kuwa wewe ni Mungu mwadilifu+ anayechunguza mioyo+ na hisia zilizo ndani kabisa.*+

10 Mungu ni ngao yangu,+ Mwokozi wa wale walio wanyoofu moyoni.+

11 Mungu ni Mwamuzi mwadilifu,+

Na Mungu huzitangaza hukumu zake* kila siku.

12 Mtu yeyote asipotubu,+ Yeye huunoa upanga wake;+

Huukunja upinde wake na kuuweka tayari.+

13 Hutayarisha silaha zake zinazoua;

Huweka tayari mishale yake inayowaka moto.+

14 Mtazame yule aliye na mimba ya uovu;

Hutunga mimba ya matatizo na kuzaa uwongo.+

15 Huchimba shimo na kuzidisha kina chake,

Lakini huanguka katika shimo hilohilo alilolichimba.+

16 Matatizo anayosababisha yatarudi juu ya kichwa chake mwenyewe;+

Ukatili wake utaanguka juu ya utosi wa kichwa chake.

17 Nitamsifu Yehova kwa sababu ya haki yake;+

Nitaliimbia sifa* jina la Yehova+ Aliye Juu Zaidi.+

Kwa kiongozi; juu ya Gitithi.* Muziki wa Daudi.

8 Ee Yehova Bwana wetu, jinsi jina lako lilivyo kuu katika dunia yote;

Umeweka fahari yako juu zaidi hata kuliko mbingu!*+

 2 Kutoka katika vinywa vya watoto wadogo na wanaonyonya+ umeimarisha nguvu

Kwa sababu ya maadui wako,

Ili kumnyamazisha adui na yule anayelipiza kisasi.

 3 Ninapoziona mbingu zako, kazi za vidole vyako,

Mwezi na nyota ambazo umetayarisha,+

 4 Mwanadamu anayeweza kufa ni nini hivi kwamba unamweka akilini,

Na mwana wa mtu hivi kwamba unamtunza?+

 5 Ulimfanya awe mdogo kidogo kuliko wale walio kama Mungu,*

Nawe ukamvika taji la utukufu na fahari.

 6 Ulimpa mamlaka juu ya kazi za mikono yako;+

Umeweka kila kitu chini ya miguu yake:

 7 Kondoo wote na ng’ombe wote,

Na pia wanyama wa mwituni,+

 8 Ndege wa angani na samaki wa baharini,

Kitu chochote kinachopita katika njia za baharini.

 9 Ee Yehova Bwana wetu, jinsi jina lako lilivyo kuu katika dunia yote!

Kwa kiongozi; juu ya Muth-labeni.* Muziki wa Daudi.

א [Aleph]

9 Nitakusifu, Ee Yehova, kwa moyo wangu wote;

Nitasimulia kuhusu kazi zako zote zinazostaajabisha.+

 2 Nitafurahi na kushangilia kwa sababu yako;

Nitaliimbia sifa* jina lako, Ee Uliye Juu Zaidi.+

ב [Beth]

 3 Maadui wangu wanapokimbia,+

Watajikwaa na kuangamia kutoka mbele zako.

 4 Kwa maana unatetea njia yangu ya haki;

Unaketi kwenye kiti chako cha ufalme ukihukumu kwa uadilifu.+

ג [Gimel]

 5 Umeyakemea mataifa+ na kuwaangamiza waovu,

Na hivyo kulifuta jina lao milele na milele.

 6 Maadui wameangamizwa milele;

Uliyang’oa majiji yao,

Na kumbukumbu lote kuwahusu litatoweka.+

ה [He]

 7 Lakini Yehova ameketi kwenye kiti cha ufalme milele;+

Amekiimarisha kabisa kiti chake cha ufalme kwa ajili ya haki.+

 8 Ataihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa;+

Atayahukumu mataifa kwa kutoa maamuzi ya uadilifu.+

ו [Waw]

 9 Yehova atakuwa kimbilio salama* kwa wanaokandamizwa,+

Kimbilio salama katika nyakati za taabu.+

10 Wale wanaolijua jina lako watakutumaini wewe;+

Hutawaacha kamwe wale wanaokutafuta, Ee Yehova.+

ז [Zayin]

11 Mwimbieni sifa Yehova, anayekaa Sayuni;

Tangazeni matendo yake miongoni mwa mataifa.+

12 Kwa maana Yule anayelipiza kisasi kwa ajili ya damu yao anawakumbuka;+

Hatasahau kilio cha wanaoteseka.+

ח [Heth]

13 Nionyeshe kibali, Ee Yehova; angalia ninavyoteswa na wale wanaonichukia,

Wewe unayeniinua kutoka katika malango ya kifo,+

14 Ili nitangaze katika malango ya binti ya Sayuni matendo yako yanayostahili sifa,+

Na kushangilia kwa sababu ya matendo yako ya wokovu.+

ט [Teth]

15 Mataifa yamezama chini katika shimo walilochimba;

Mguu wao wenyewe umenaswa katika wavu waliouficha.+

16 Yehova anajulikana kwa hukumu anazotekeleza.+

Mwovu amenaswa katika kazi za mikono yake mwenyewe.+

Higayoni.* (Sela)

י [Yod]

17 Waovu watageuka na kuelekea Kaburini,*

Mataifa yote yanayomsahau Mungu.

18 Lakini maskini hawatasahauliwa daima;+

Wala tumaini la wapole halitapotea kamwe.+

כ [Kaph]

19 Inuka, Ee Yehova! Usiache mwanadamu anayeweza kufa ashinde.

Mataifa na yahukumiwe mbele zako.*+

20 Wapige kwa woga, Ee Yehova,+

Acha mataifa yajue kwamba wao ni wanadamu tu wanaoweza kufa. (Sela)

ל [Lamed]

10 Ee Yehova, kwa nini unasimama mbali?

Kwa nini unajificha nyakati za taabu?+

 2 Mwovu humfuatia kwa kiburi mtu asiye na uwezo,+

Lakini atanaswa katika njama anazopanga.+

 3 Kwa maana mwovu hujigamba kuhusu tamaa zake za kichoyo*+

Naye humbariki mwenye pupa;*

נ [Nun]

Humkosea heshima Yehova.

 4 Kwa sababu ya kiburi chake, mwovu hafanyi uchunguzi wowote;

Mawazo yake yote ni: “Hakuna Mungu.”+

 5 Njia zake huendelea kufanikiwa,+

Lakini hukumu zako zimepita uelewaji wake;+

Huwadhihaki* maadui wake wote.

 6 Anasema moyoni mwake: “Sitatikiswa kamwe;*

Kizazi baada ya kizazi

Sitaona msiba kamwe.”+

פ [Pe]

 7 Kinywa chake kimejaa laana, uwongo, na vitisho;+

Chini ya ulimi wake kuna taabu na madhara.+

 8 Huvizia karibu na makao;

Kutoka mahali anapojificha humuua mtu asiye na hatia.+

ע [Ayin]

Macho yake yanamtafuta mtu asiye na kosa.+

 9 Hungojea mahali alipojificha kama simba katika pango* lake.+

Hungojea ili amkamate asiye na uwezo.

Humkamata asiye na uwezo anapouvuta wavu wake na kuufunga.+

10 Mtu huyo hupondwa na kuangushwa chini;

Watu wasio na kosa huanguka mikononi mwake.*

11 Yeye husema moyoni mwake: “Mungu amesahau.+

Ameugeuzia mbali uso wake.

Haoni kamwe.”+

ק [Qoph]

12 Inuka, Ee Yehova.+ Ee Mungu, inua mkono wako.+

Usiwasahau wasio na uwezo.+

13 Kwa nini mwovu amemkosea Mungu heshima?

Husema moyoni mwake: “Hutanifanya niwajibike.”

ר [Resh]

14 Lakini unaona mateso na taabu.

Wewe huendelea kutazama na kuchukua hatua.+

Mtu huyo asiye na kosa hukugeukia wewe;+

Wewe ndiye msaidizi wa yatima.+

ש [Shin]

15 Uvunje mkono wa mtu mwovu na mbaya,+

Ili utakapoutafuta uovu wake,

Hutaupata tena.

16 Yehova ni Mfalme milele na milele.+

Mataifa yameangamia kutoka duniani.+

ת [Taw]

17 Lakini utasikia ombi la wapole, Ee Yehova.+

Utaiimarisha mioyo yao+ na kuwasikiliza kwa makini.+

18 Utawatendea haki mayatima na wale wanaopondwa,+

Ili mwanadamu anayeweza kufa ambaye ni mavumbi asiwaogopeshe tena.+

Kwa kiongozi. Wa Daudi.

11 Nimemkimbilia Yehova.+

Basi mnawezaje kuniambia:*

“Kimbilia kwenye mlima wako kama ndege!

 2 Tazama jinsi waovu wanavyoukunja upinde;

Huutia mshale wao kwenye kamba ya upinde,

Ili wawapige kutoka gizani wale walio wanyoofu moyoni.

 3 Misingi* inapobomolewa,

Mtu mwadilifu anaweza kufanya nini?”

 4 Yehova yumo katika hekalu lake takatifu.+

Kiti cha ufalme cha Yehova kiko mbinguni.+

Macho yake mwenyewe yanatazama, macho yake yaliyo makini* yanawachunguza wanadamu.+

 5 Yehova humchunguza mwadilifu na pia mwovu;+

Humchukia* mtu yeyote anayependa ukatili.+

 6 Atawanyeshea waovu mitego;*

Moto na kiberiti+ na upepo unaounguza vitakuwa fungu la kikombe chao.

 7 Kwa maana Yehova ni mwadilifu;+ yeye hupenda matendo ya uadilifu.+

Wanyoofu watauona uso wake.*+

Kwa kiongozi; umepatanishwa na sauti ya Sheminithi.* Muziki wa Daudi.

12 Niokoe, Ee Yehova, kwa maana mtu mshikamanifu hayupo tena;

Watu waaminifu wametoweka kutoka miongoni mwa wanadamu.

 2 Wanaambiana uwongo;

Wanasifusifu kwa midomo yao* na kuzungumza kwa mioyo midanganyifu.*+

 3 Yehova ataikata kabisa midomo yote inayosifusifu

Na ulimi unaojigamba kupindukia,+

 4 Wale wanaosema: “Tutashinda kwa ndimi zetu.

Tunatumia midomo yetu tupendavyo;

Ni nani atakayekuwa bwana mkubwa wetu?”+

 5 “Kwa sababu wale wanaoteswa wanakandamizwa,

Kwa sababu ya kilio cha uchungu cha maskini,+

Nitainuka na kutenda,” asema Yehova.

“Nitawaokoa kutoka kwa wale wanaowatendea kwa dharau.”*

 6 Maneno ya Yehova ni safi;+

Ni kama fedha iliyosafishwa katika tanuru la udongo,* iliyosafishwa mara saba.

 7 Utawalinda, Ee Yehova;+

Utamlinda kila mmoja wao milele kutokana na kizazi hiki.

 8 Waovu wanatembea huku na huku kwa uhuru

Kwa sababu wanadamu wanaendeleza upotovu.+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

13 Ee Yehova, utanisahau mpaka lini? Milele?

Utanificha uso wako mpaka lini?+

 2 Nitahangaika kwa wasiwasi mpaka lini,

Nikiwa na huzuni moyoni mwangu kila siku?

Adui yangu atanishinda mpaka lini?+

 3 Nitazame na unijibu, Ee Yehova Mungu wangu.

Yatie nuru macho yangu, ili nisilale usingizi katika kifo,

 4 Ili adui yangu asiseme: “Nimemshinda!”

Usiruhusu wapinzani wangu washangilie kuanguka kwangu.+

 5 Lakini mimi, ninautumaini upendo wako mshikamanifu;+

Moyo wangu utashangilia kwa sababu ya matendo yako ya wokovu.+

 6 Nitamwimbia Yehova, kwa maana amenithawabisha kwelikweli.*+

Kwa kiongozi. Wa Daudi.

14 Mpumbavu* husema moyoni mwake:

“Hakuna Yehova.”+

Matendo yao yamepotoka, na shughuli zao zinachukiza;

Hakuna yeyote anayetenda mema.+

 2 Lakini Yehova anawatazama wanadamu kutoka mbinguni

Ili aone ikiwa kuna yeyote aliye na ufahamu, ikiwa kuna yeyote anayemtafuta Yehova.+

 3 Wote wamegeuka kando;+

Wote wamepotoka.

Hakuna yeyote anayetenda mema,

Hakuna hata mmoja.

 4 Je, hakuna mtenda maovu yeyote anayeelewa?

Wanawala watu wangu kana kwamba wanakula mkate.

Hawamwiti Yehova.

 5 Lakini watajawa na hofu kubwa,+

Kwa maana Yehova yuko pamoja na kizazi cha waadilifu.

 6 Ninyi waovu hujaribu kuharibu mipango ya mtu wa hali ya chini,

Lakini Yehova ni kimbilio lake.+

 7 Laiti wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+

Yehova anapowakusanya tena watu wake waliotekwa,

Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi.

Muziki wa Daudi.

15 Ee Yehova, ni nani anayeweza kuwa mgeni katika hema lako?

Ni nani anayeweza kukaa katika mlima wako mtakatifu?+

 2 Yule anayetembea bila kosa,*+

Anayezoea kutenda yaliyo sawa+

Na kusema ukweli moyoni mwake.+

 3 Hachongei kwa ulimi wake,+

Hamtendei jirani yake jambo lolote ovu,+

Naye hawaharibii sifa* rafiki zake.+

 4 Humkataa mtu yeyote anayedharauliwa,+

Lakini huwaheshimu wale wanaomwogopa Yehova.

Havunji ahadi yake, hata ikimletea hasara.*+

 5 Hakopeshi pesa zake kwa faida,+

Naye hakubali rushwa ili kumkandamiza asiye na hatia.+

Yeyote anayefanya mambo hayo hatatikiswa kamwe.*+

Miktamu* ya Daudi.

16 Nilinde, Ee Mungu, kwa maana nimekukimbilia wewe.+

 2 Nimemwambia Yehova: “Wewe ni Yehova, Chanzo changu cha wema.

 3 Na watakatifu walio duniani,

Watukufu, ndio ninaopendezwa nao sana.”+

 4 Wale wanaoifuatia miungu mingine huzidisha huzuni yao.+

Sitamimina kamwe matoleo yao ya vinywaji ya damu,

Wala midomo yangu haitataja majina yao.+

 5 Yehova ni fungu langu, sehemu niliyogawiwa,+ na kikombe changu.+

Unaulinda urithi wangu.

 6 Nimepimiwa sehemu zinazopendeza.

Naam, nimeridhika na urithi wangu.+

 7 Nitamsifu Yehova, ambaye amenipa ushauri.+

Hata wakati wa usiku, mawazo yangu ya ndani kabisa* hunirekebisha.+

 8 Ninamweka Yehova mbele yangu daima.+

Kwa sababu yuko mkono wangu wa kulia, sitatikiswa kamwe.*+

 9 Kwa hiyo moyo wangu unashangilia, nafsi yangu yote ina* shangwe.

Nami ninaishi* kwa usalama.

10 Kwa maana hutaniacha* Kaburini.*+

Hutamruhusu mshikamanifu wako aone shimo.*+

11 Unanijulisha njia ya uzima.+

Shangwe tele iko mbele zako;*+

Kuna furaha* kwenye mkono wako wa kuume milele.

Sala ya Daudi.

17 Sikia sihi yangu ya kuomba haki, Ee Yehova;

Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada;

Sikiliza sala yangu ninayosema bila udanganyifu.+

 2 Nawe ufanye uamuzi wa haki kwa niaba yangu;+

Macho yako na yaone yaliyo sawa.

 3 Umeuchunguza moyo wangu, umenikagua wakati wa usiku;+

Umenisafisha;+

Utagundua kwamba sijapanga njama ya kutenda uovu wowote,

Na kinywa changu hakijatenda dhambi.

 4 Kuhusiana na shughuli za wanadamu,

Kulingana na neno la midomo yako, ninaepuka njia za mnyang’anyi.+

 5 Acha hatua zangu zibaki kwenye njia zako

Ili miguu yangu isijikwae.+

 6 Ninakuita wewe, kwa sababu utanijibu,+ Ee Mungu.

Nitegee sikio lako.* Sikia maneno yangu.+

 7 Onyesha upendo wako mshikamanifu kwa njia yenye kustaajabisha,+

Ee Mwokozi wa wale wanaokimbilia mkono wako wa kuume

Kutoka kwa wale wanaokuasi.

 8 Nilinde kama mboni ya jicho lako;+

Nifiche katika kivuli cha mabawa yako.+

 9 Nilinde kutokana na waovu wanaonishambulia,

Kutokana na maadui wangu* wanaoweza kufa ambao wananizingira.+

10 Wamekufa ganzi;*

Kwa kinywa chao wanaongea kwa kiburi;

11 Sasa wanatuzingira;+

Wanatafuta nafasi ya kutuangusha.*

12 Yeye ni kama simba anayetamani kurarua windo lake vipandevipande,

Kama mwanasimba anayenyemelea mafichoni.

13 Inuka, Ee Yehova, ukabiliane naye+ na kumwangusha chini;

Niokoe* kutoka kwa mwovu kwa kutumia upanga wako;

14 Niokoe kwa mkono wako, Ee Yehova,

Kutoka kwa watu wa ulimwengu huu,* ambao fungu lao liko katika maisha haya,+

Wale ambao unawajaza kwa vitu vizuri unavyoandaa+

Na ambao huwaachia urithi wana wao wengi.

15 Lakini mimi, nitauona uso wako kwa sababu ya uadilifu wangu;

Ninaridhika kuamka mbele zako.*+

Kwa kiongozi. Wa Daudi mtumishi wa Yehova, aliyemwambia Yehova maneno ya wimbo huu siku ambayo Yehova alimwokoa kutoka mikononi mwa maadui wake wote na kutoka mikononi mwa Sauli. Alisema:+

18 Ninakupenda, Ee Yehova, nguvu zangu.+

 2 Yehova ni jabali langu na ngome yangu na Mwokozi wangu.+

Mungu wangu ni mwamba wangu,+ ninayemkimbilia,

Ngao yangu na pembe* yangu ya wokovu,* kimbilio langu salama.*+

 3 Ninamlilia Yehova, anayestahili kusifiwa,

Nami nitaokolewa kutoka kwa maadui wangu.+

 4 Kamba za kifo zilinizunguka;+

Mafuriko ya ghafla ya watu wasiofaa kitu yaliniogopesha.+

 5 Kamba za Kaburi* zilinizunguka;

Mitego ya kifo ilinikabili.+

 6 Katika taabu yangu nilimwita Yehova,

Niliendelea kumlilia Mungu wangu anisaidie.

Akiwa katika hekalu lake aliisikia sauti yangu,+

Na kilio changu cha kumwomba msaada kilifika masikioni mwake.+

 7 Kisha dunia ikaanza kutetemeka na kutikisika;+

Misingi ya milima ikasukasuka

Nayo ikatikisika huku na huku kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+

 8 Moshi ulipanda kutoka katika mianzi ya pua yake,

Na moto unaoteketeza kabisa ukatoka kinywani mwake;+

Makaa ya mawe yanayowaka moto mkali yakatoka kwake.

 9 Alizifanya mbingu zijikunje alipokuwa akishuka,+

Na giza zito lilikuwa chini ya miguu yake.+

10 Alipanda juu ya kerubi, akaja akiruka.+

Akashuka chini kwa ghafla juu ya mabawa ya kiumbe wa roho.*+

11 Kisha akajifunika giza,+

Pande zote kama banda,

Maji yenye giza na mawingu mazito.+

12 Kutoka katika mwangaza ulio mbele zake

Mvua ya mawe na makaa ya mawe yanayowaka moto yakapasua mawingu.

13 Kisha Yehova akaanza kunguruma mbinguni;+

Aliye Juu Zaidi aliifanya sauti yake isikike+

Kwa mvua ya mawe na makaa ya mawe yanayowaka moto.

14 Alipiga mishale yake akawatawanya;+

Alivurumisha radi yake akawavuruga.+

15 Sakafu za vijito zikaonekana;*+

Misingi ya nchi ikafunuliwa kwa kemeo lako, Ee Yehova,

Kwa mlipuko wa pumzi kutoka katika mianzi ya pua yako.+

16 Aliunyoosha mkono wake kutoka juu;

Alinishika na kunivuta kutoka katika maji yenye kina.+

17 Aliniokoa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+

Kutoka kwa wale wanaonichukia, waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.+

18 Walinikabili katika siku ya msiba wangu,+

Lakini Yehova alikuwa tegemeo langu.

19 Alinitoa nje na kunileta mahali penye usalama;*

Aliniokoa kwa sababu alipendezwa nami.+

20 Yehova hunithawabisha kulingana na uadilifu wangu;+

Hunilipa kulingana na usafi* wa mikono yangu.+

21 Kwa maana nimezishika njia za Yehova,

Nami sijamwacha kwa uovu Mungu wangu.

22 Hukumu zake zote ziko mbele yangu;

Sitazipuuza sheria zake.

23 Nitabaki bila lawama mbele zake,+

Nami nitajiepusha na uovu.+

24 Yehova na anilipe kulingana na uadilifu wangu,+

Kulingana na usafi* wa mikono yangu mbele zake.+

25 Kwa mtu mshikamanifu unatenda kwa ushikamanifu;+

Kwa mtu asiye na lawama unatenda bila lawama;+

26 Kwa walio safi unajidhihirisha mwenyewe kuwa safi,+

Lakini kwa waliopotoka unajidhihirisha mwenyewe kuwa mwenye busara.+

27 Kwa maana wewe huwaokoa watu wa hali ya chini*+

Lakini unawashusha wenye kiburi.*+

28 Kwa maana ni wewe unayeiwasha taa yangu, Ee Yehova,

Mungu wangu ambaye hulifanya giza langu liangaze.+

29 Kwa msaada wako ninaweza kukabiliana na kundi la wavamizi;+

Kwa nguvu za Mungu ninaweza kuupanda ukuta.+

30 Njia ya Mungu wa kweli ni kamilifu;+

Neno la Yehova ni safi.+

Yeye ni ngao kwa wote wanaomkimbilia.+

31 Kwa maana ni nani aliye Mungu ila Yehova?+

Na ni nani aliye mwamba isipokuwa Mungu wetu?+

32 Mungu wa kweli ndiye anayenivisha nguvu,+

Naye ataifanya njia yangu iwe kamilifu.+

33 Huifanya miguu yangu iwe kama ya paa;

Hunifanya nisimame mahali palipo juu.+

34 Huizoeza mikono yangu kupigana vita;

Mikono yangu inaweza kuukunja upinde wa shaba.

35 Wewe hunipa ngao yako ya wokovu,+

Mkono wako wa kuume hunitegemeza,*

Na unyenyekevu wako hunifanya niwe mkuu.+

36 Unapanua njia kwa ajili ya hatua zangu;

Miguu yangu haitateleza.*+

37 Nitawafuatia maadui wangu na kuwapita;

Sitarudi mpaka watakapoangamizwa kabisa.

38 Nitawaponda wasiweze kuinuka;+

Wataanguka chini ya miguu yangu.

39 Utanipa nguvu kwa ajili ya vita;

Utawafanya maadui wangu waanguke chini yangu.+

40 Utawafanya maadui wangu wanikimbie,*

Nami nitawakomesha* wale wanaonichukia.+

41 Wanalilia msaada, lakini hakuna mtu wa kuwaokoa;

Hata wanamlilia Yehova, lakini yeye hawajibu.

42 Nitawaponda wawe laini kama mavumbi katika upepo;

Nitawatupa nje kama matope barabarani.

43 Utaniokoa kutoka kwa watu wanaotafuta makosa.+

Utaniweka kuwa kiongozi wa mataifa.+

Watu ambao siwajui watanitumikia.+

44 Watanitii watakaposikia fununu tu;

Wageni watakuja wakijikunyata mbele zangu.+

45 Wageni watakosa ujasiri;*

Watakuja wakitetemeka kutoka katika ngome zao.

46 Yehova yuko hai! Mwamba wangu na asifiwe!+

Mungu wa wokovu wangu na akwezwe.+

47 Mungu wa kweli hunilipizia kisasi;+

Huyatiisha mataifa chini yangu.

48 Yeye huniokoa kutoka kwa maadui wangu wenye hasira;

Unaniinua juu ya wale wanaonishambulia;+

Unaniokoa kutoka kwa mtu mkatili.

49 Ndiyo sababu nitakutukuza wewe miongoni mwa mataifa, Ee Yehova,+

Nami nitaliimbia sifa* jina lako.+

50 Yeye hutenda matendo makuu ya wokovu kwa ajili ya mfalme wake;*+

Humtendea mtiwa-mafuta wake kwa upendo mshikamanifu,+

Kwa Daudi na kwa uzao wake* milele.+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

19 Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu;+

Na anga lililo juu linatangaza kazi ya mikono yake.+

 2 Siku baada ya siku zinabubujisha maneno yake,

Na usiku baada ya usiku zinafunua ujuzi.

 3 Hakuna usemi, wala hakuna maneno;

Sauti zake hazisikiki.

 4 Lakini sauti zake zimefika* katika dunia yote,

Na ujumbe wake umefika mpaka kwenye miisho ya dunia inayokaliwa.+

Amepiga hema mbinguni kwa ajili ya jua;

 5 Ni kama bwana harusi anayetoka katika chumba chake;

Linashangilia kama mwanamume hodari anayekimbia kwenye njia yake.

 6 Linachomoza kutoka mwisho mmoja wa mbingu,

Nalo huzunguka mpaka mwisho mwingine;+

Na hakuna chochote kinachojificha joto lake.

 7 Sheria ya Yehova ni kamilifu,+ hurudisha nguvu.*+

Kikumbusho cha Yehova kinategemeka,+ humfanya asiye na uzoefu awe na hekima.+

 8 Maagizo kutoka kwa Yehova ni ya uadilifu, huufanya moyo ushangilie;+

Amri ya Yehova ni safi, huyafanya macho yang’ae.+

 9 Kumwogopa Yehova ni jambo safi,+ hudumu milele.

Hukumu za Yehova ni za kweli; zote ni za uadilifu.+

10 Zinatamanika kuliko dhahabu,

Kuliko dhahabu nyingi bora,*+

Na tamu zaidi kuliko asali,+ asali inayodondoka kutoka katika sega.

11 Mtumishi wako ameonywa kupitia hizo;+

Anapozishika anapata thawabu kubwa.+

12 Ni nani anayeweza kutambua makosa?+

Nitangaze kuwa sina hatia ya dhambi nisizojua.

13 Na unizuie mimi mtumishi wako nisitende matendo ya kimbelembele;+

Usiruhusu yanitawale.+

Ndipo nitakapokuwa kamili,+

Na sitakuwa na hatia ya dhambi zilizo wazi.*

14 Maneno ya kinywa changu na kutafakari kwa moyo wangu

Na yakupendeze wewe,+ Ee Yehova, Mwamba wangu+ na Mkombozi wangu.+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

20 Yehova na akujibu katika siku ya taabu.

Jina la Mungu wa Yakobo na likulinde.+

 2 Na akuletee msaada kutoka mahali patakatifu+

Na kukutegemeza kutoka Sayuni.+

 3 Na akumbuke matoleo yako yote ya zawadi;

Na aikubali kwa upendeleo* dhabihu yako ya kuteketezwa. (Sela)

 4 Na atosheleze tamaa za moyo wako+

Na kufanikisha mipango yako yote.*

 5 Tutapaza sauti kwa shangwe kwa sababu ya matendo yako ya wokovu;+

Tutainua bendera zetu katika jina la Mungu wetu.+

Yehova na atimize maombi yako yote.

 6 Sasa ninajua kwamba Yehova humwokoa mtiwa-mafuta wake.+

Humjibu kutoka katika mbingu zake takatifu

Kwa wokovu* mkubwa kupitia mkono wake wa kuume.+

 7 Wengine hutegemea magari ya vita na wengine farasi,+

Lakini sisi tunaliitia jina la Yehova Mungu wetu.+

 8 Wamedondoka na kuanguka,

Lakini sisi tumeinuka na kurudishwa.+

 9 Ee Yehova, mwokoe mfalme!+

Atatujibu siku ambayo tutaomba msaada.+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

21 Ee Yehova, mfalme hushangilia kwa sababu ya nguvu zako;+

Jinsi anavyoshangilia sana kwa sababu ya matendo yako ya wokovu!+

 2 Umetosheleza tamaa ya moyo wake,+

Nawe hujamnyima ombi la midomo yake. (Sela)

 3 Kwa maana unamlaki kwa baraka tele;

Unamvika taji la dhahabu bora* kichwani.+

 4 Alikuomba uhai, nawe ukampa,+

Maisha marefu,* milele na milele.

 5 Matendo yako ya wokovu humletea utukufu mkubwa.+

Unamtunukia adhama na fahari.

 6 Unamfanya awe na baraka milele;+

Unamfanya afurahi kwa shangwe ya kuwa mbele zako.*+

 7 Kwa maana mfalme anamtumaini Yehova;+

Kwa sababu ya upendo mshikamanifu wa Aliye Juu Zaidi, hatatikiswa kamwe.*+

 8 Mkono wako utawapata maadui wako wote;

Mkono wako wa kuume utawapata wale wanaokuchukia.

 9 Utawafanya wawe kama tanuru lenye moto mkali utakapofika wakati ulioweka wa kuwakazia uangalifu.

Yehova atawameza kwa hasira yake, na moto utawateketeza kabisa.+

10 Utawaangamiza wazao wao kutoka duniani,

Na uzao wao kutoka kati ya wanadamu.

11 Kwa maana walikusudia kukutendea maovu;+

Wamepanga njama ambazo hazitafanikiwa.+

12 Kwa maana utawafanya wakimbie+

Kwa kuwalenga* kwa upinde wako.*

13 Inuka, Ee Yehova, katika nguvu zako.

Tutauimbia sifa* uwezo wako.

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Paa Jike wa Mapambazuko.”* Muziki wa Daudi.

22 Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?+

Kwa nini uko mbali usiweze kuniokoa,

Mbali na vilio vyangu vya maumivu makali?+

 2 Mungu wangu, ninaendelea kukuita wakati wa mchana, nawe hunijibu;+

Na wakati wa usiku sinyamazi.

 3 Lakini wewe ni mtakatifu,+

Umezungukwa na* sifa za Israeli.

 4 Baba zetu walikutumaini wewe;+

Walikutumaini, nawe ulikuwa ukiwaokoa.+

 5 Walikulilia kwa sauti, wakaokolewa;

Walikutumaini, nao hawakukatishwa tamaa.*+

 6 Lakini mimi ni mnyoo wala si mwanadamu,

Ninadhihakiwa na wanadamu na kudharauliwa na watu.*+

 7 Wote wanaoniona hunikejeli;+

Wanafyonya midomo na kutikisa vichwa vyao kwa dharau:+

 8 “Alijikabidhi mwenyewe kwa Yehova. Acha Yeye amwokoe!

Acha Yeye amwokoe, kwa sababu Yeye anampenda sana!”+

 9 Wewe ndiye uliyenitoa tumboni,+

Ni Wewe uliyenifanya nihisi nikiwa salama kwenye matiti ya mama yangu.

10 Nimewekwa chini ya utunzaji wako* tangu nilipozaliwa;

Tangu nilipokuwa katika tumbo la mama yangu, umekuwa Mungu wangu.

11 Usikae mbali nami, kwa maana taabu iko karibu+

Nami sina msaidizi mwingine.+

12 Ng’ombe dume wengi wachanga wananizunguka;+

Ng’ombe dume wenye nguvu wa Bashani wananizingira.+

13 Wanafungua vinywa vyao wazi dhidi yangu,+

Kama simba anayenguruma ambaye anararua windo lake vipandevipande.+

14 Nimemwagwa kama maji;

Mifupa yangu yote imeteguka.

Moyo wangu umekuwa kama nta;+

Unayeyuka katika sehemu zangu za ndani kabisa.+

15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae;+

Ulimi wangu unashikamana na fizi zangu;+

Unanishusha chini kwenye mavumbi ya kifo.+

16 Kwa maana mbwa wananizunguka;+

Wananizingira kama kundi la watenda maovu,+

Kama simba, wanaishambulia mikono yangu na miguu yangu.+

17 Ninaweza kuhesabu mifupa yangu yote.+

Wananitazama na kunikodolea macho.

18 Wanagawana mavazi yangu,

Nao wanalipigia kura vazi langu.+

19 Lakini wewe, Ee Yehova, usiendelee kukaa mbali.+

Wewe ni nguvu zangu; njoo haraka unisaidie.+

20 Niokoe* kutoka kwa upanga,

Uhai wangu wenye thamani* kutoka katika makucha ya* mbwa;+

21 Niokoe kutoka katika kinywa cha simba+ na pembe za ng’ombe dume wa mwituni;

Nijibu na uniokoe.

22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu;+

Katikati ya kutaniko nitakusifu.+

23 Ninyi mnaomwogopa Yehova, msifuni!

Enyi nyote uzao wa* Yakobo, mtukuzeni!+

Mwogopeni yeye, enyi nyote uzao wa* Israeli.

24 Kwa maana hajadharau wala kuchukizwa na mateso ya yule anayekandamizwa;+

Hajauficha uso wake kutoka kwake.+

Alipomlilia amsaidie, alisikia.+

25 Nitakusifu katika kutaniko kubwa;+

Nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanaomwogopa.

26 Wapole watakula na kushiba;+

Wale wanaomtafuta Yehova watamsifu.+

Na ufurahie maisha* milele.

27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Yehova.

Familia zote za mataifa zitainama chini mbele zako.+

28 Kwa maana ufalme ni wa Yehova;+

Anayatawala mataifa.

29 Watu wote wenye ufanisi* duniani watakula na kumwinamia;

Wote wanaoshuka mavumbini watapiga magoti mbele zake;

Hakuna yeyote kati yao anayeweza kuokoa uhai wao.*

30 Wazao wao watamtumikia;*

Kizazi kitakachokuja kitaambiwa kumhusu Yehova.

31 Watakuja na kusimulia uadilifu wake.

Watawaambia watu ambao bado hawajazaliwa mambo aliyofanya.

Muziki wa Daudi.

23 Yehova ni Mchungaji wangu.+

Sitakosa chochote.+

 2 Hunilaza katika malisho yenye majani mengi;

Huniongoza kwenye sehemu za kupumzika zenye maji mengi.*+

 3 Huniburudisha.*+

Huniongoza katika njia za* uadilifu kwa ajili ya jina lake.+

 4 Hata nikitembea katika bonde lenye kivuli kizito,+

Siogopi madhara yoyote,+

Kwa maana wewe uko pamoja nami;+

Fimbo yako na gongo lako hunipa uhakika.*

 5 Wewe huniandalia meza mbele ya maadui wangu.+

Unakiburudisha* kichwa changu kwa mafuta;+

Kikombe changu kimejazwa vizuri.+

 6 Kwa hakika wema na upendo mshikamanifu utanifuatia sikuzote za maisha yangu,+

Nami nitakaa katika nyumba ya Yehova siku zangu zote.+

Muziki wa Daudi.

24 Dunia na vyote vilivyomo ni vya Yehova,+

Nchi inayozaa na wale wanaokaa ndani yake.

 2 Kwa maana ameiweka imara kabisa juu ya bahari+

Na kuiweka imara kabisa juu ya mito.

 3 Ni nani anayeweza kuupanda mlima wa Yehova,+

Na ni nani anayeweza kusimama mahali pake patakatifu?

 4 Yeyote mwenye mikono isiyo na hatia na mwenye moyo safi,+

Ambaye hajaapa kwa uwongo kwa uhai Wangu,*

Wala kuapa kwa udanganyifu.+

 5 Atapokea baraka kutoka kwa Yehova+

Na uadilifu* kutoka kwa Mungu wa wokovu wake.+

 6 Hiki ndicho kizazi cha wale wanaomtafuta,

Cha wale wanaoutafuta uso wako, Ee Mungu wa Yakobo. (Sela)

 7 Inueni vichwa vyenu, enyi malango;+

Fungukeni,* enyi milango ya kale,

Ili Mfalme mtukufu aingie!+

 8 Mfalme huyu mtukufu ni nani?

Yehova, mwenye nguvu na hodari,+

Yehova, hodari katika vita.+

 9 Inueni vichwa vyenu, enyi malango;+

Fungukeni, enyi milango ya kale,

Ili Mfalme mtukufu aingie!

10 Mfalme huyu mtukufu ni nani?

Yehova wa majeshi—yeye ndiye Mfalme mtukufu.+ (Sela)

Wa Daudi.

א [Aleph]

25 Nakugeukia wewe,* Ee Yehova.

ב [Beth]

 2 Mungu wangu, ninakutumaini wewe;+

Usiruhusu niaibishwe.+

Usiruhusu maadui wangu wanicheke.+

ג [Gimel]

 3 Kwa hakika hakuna yeyote anayekutumaini atakayeaibishwa,+

Lakini aibu inawangoja wale wanaotenda kwa hila bila sababu.+

ד [Daleth]

 4 Nijulishe njia zako, Ee Yehova;+

Nifundishe vijia vyako.+

ה [He]

 5 Nitembeze katika kweli yako na kunifundisha,+

Kwa maana wewe ni Mungu wa wokovu wangu.

ו [Waw]

Ninakutumaini mchana kutwa.

ז [Zayin]

 6 Kumbuka rehema zako, Ee Yehova, na upendo wako mshikamanifu,+

Ambazo umedhihirisha sikuzote.*+

ח [Heth]

 7 Usikumbuke dhambi na makosa niliyotenda nilipokuwa kijana.

Nikumbuke kulingana na upendo wako mshikamanifu,+

Kwa ajili ya wema wako, Ee Yehova.+

ט [Teth]

 8 Yehova ni mwema na mnyoofu.+

Ndiyo sababu yeye huwafundisha watenda dhambi njia wanayopaswa kuishi.+

י [Yod]

 9 Atawaongoza wapole katika yaliyo sawa,*+

Naye atawafundisha wapole njia yake.+

כ [Kaph]

10 Njia zote za Yehova ni upendo mshikamanifu na uaminifu

Kwa wale wanaoshika agano lake+ na vikumbusho vyake.+

ל [Lamed]

11 Kwa ajili ya jina lako, Ee Yehova,+

Nisamehe kosa langu, ingawa ni kubwa.

מ [Mem]

12 Ni nani anayemwogopa Yehova?+

Atamfundisha kuhusu njia anayopaswa kuchagua.+

נ [Nun]

13 Atajionea* yaliyo mema,+

Na wazao wake wataimiliki* dunia.+

ס [Samekh]

14 Urafiki wa karibu pamoja na Yehova ni wa wale wanaomwogopa,+

Naye huwajulisha agano lake.+

ע [Ayin]

15 Macho yangu humtazama Yehova daima,+

Kwa maana ataiweka huru miguu yangu kutoka katika wavu.+

פ [Pe]

16 Nielekezee uso wako na kunionyesha kibali,

Kwa maana niko peke yangu na sina uwezo.

צ [Tsade]

17 Taabu za moyo wangu zimeongezeka;+

Niondolee maumivu yangu makali.

ר [Resh]

18 Yaone mateso yangu na shida yangu,+

Nawe unisamehe dhambi zangu zote.+

19 Tazama jinsi maadui wangu walivyo wengi

Na jinsi wanavyonichukia vikali.

ש [Shin]

20 Ulinde uhai wangu* na uniokoe.+

Usiruhusu niaibishwe, kwa maana nimekukimbilia wewe.

ת [Taw]

21 Utimilifu na unyoofu na vinilinde,+

Kwa maana ninakutumaini wewe.+

22 Ee Mungu, mwokoe* Israeli kutoka katika taabu zake zote.

Wa Daudi.

26 Unihukumu, Ee Yehova, kwa maana nimetembea katika utimilifu wangu;+

Nimemtumaini Yehova bila kuyumbayumba.+

 2 Nichunguze, Ee Yehova, na unijaribu;

Safisha mawazo yangu ya ndani kabisa* na pia moyo wangu.+

 3 Kwa maana upendo wako mshikamanifu uko mbele yangu daima,

Nami ninatembea katika kweli yako.+

 4 Sishirikiani* na watu wadanganyifu,+

Nami huwaepuka wale wanaoficha jinsi walivyo.*

 5 Ninachukia kundi la waovu,+

Nami ninakataa kushirikiana* na waovu.+

 6 Nitanawa mikono yangu katika ukosefu wa hatia,

Nami nitapiga mwendo kuzunguka madhabahu yako, Ee Yehova,

 7 Ili niifanye sauti ya utoaji shukrani isikike+

Na kutangaza kazi zako zote zinazostaajabisha.

 8 Yehova, ninaipenda nyumba ambamo unakaa,+

Mahali ambapo utukufu wako hukaa.+

 9 Usinifagilie mbali* pamoja na watenda dhambi+

Wala kuniua pamoja na watu wakatili,*

10 Ambao mikono yao hutenda matendo ya* aibu,

Na ambao mkono wao wa kulia umejaa rushwa.

11 Lakini mimi, nitatembea katika utimilifu wangu.

Niokoe* na kunionyesha kibali.

12 Mguu wangu umesimama mahali tambarare;+

Katika kutaniko kubwa,* nitamsifu Yehova.+

Wa Daudi.

27 Yehova ni nuru yangu+ na wokovu wangu.

Nimwogope nani?+

Yehova ni ngome ya uhai wangu.+

Nimhofu nani?

 2 Waovu waliponishambulia ili waunyafue mwili wangu,+

Wapinzani wangu na maadui wangu ndio waliojikwaa na kuanguka.

 3 Hata jeshi likipiga kambi ili kunishambulia,

Moyo wangu hautaogopa.+

Hata vita vikizuka dhidi yangu,

Bado nitaendelea kuwa jasiri.

 4 Nimemwomba Yehova jambo moja

—Ndilo nitakalolitafuta—

Kwamba nikae katika nyumba ya Yehova sikuzote za maisha yangu,+

Ili kuutazama uzuri wa Yehova

Na kutazama kwa uthamini* hekalu lake.*+

 5 Kwa maana atanificha katika banda lake siku ya msiba;+

Atanificha mahali pa siri katika hema lake;+

Ataniweka juu kwenye mwamba.+

 6 Sasa kichwa changu kiko juu sana ya maadui wangu wanaonizingira;

Nitatoa dhabihu katika hema lake kwa kelele za shangwe;

Nitamwimbia sifa* Yehova.

 7 Nisikie, Ee Yehova, ninapolia kwa sauti;+

Nionyeshe kibali na kunijibu.+

 8 Moyo wangu umesema hivi kwa niaba yako:

“Utafute uso wangu.”

Nitautafuta uso wako, Ee Yehova.+

 9 Usinifiche uso wako.+

Usimfukuze kwa hasira mtumishi wako.

Wewe ni msaidizi wangu;+

Usinitupe wala usiniache, Mungu wa wokovu wangu.

10 Hata baba yangu na mama yangu wakiniacha,+

Yehova mwenyewe atanichukua.+

11 Nifundishe njia yako, Ee Yehova,+

Niongoze katika kijia cha unyoofu kwa sababu ya maadui wangu.

12 Usinitie mikononi mwa maadui wangu,+

Kwa maana mashahidi wa uwongo wameinuka dhidi yangu,+

Nao wanatoa vitisho vya kunitendea kwa ukatili.

13 Ningekuwa wapi ikiwa singekuwa na imani

Kwamba nitauona wema wa Yehova katika nchi ya walio hai?*+

14 Mtumaini Yehova;+

Uwe jasiri na uwe na moyo mkuu.+

Naam, mtumaini Yehova.

Wa Daudi.

28 Ninaendelea kukulilia wewe, Ee Yehova Mwamba wangu;+

Usiwe kama kiziwi kwangu.

Ukininyamazia,

Nitakuwa kama wale wanaoshuka shimoni.*+

 2 Sikia sihi zangu ninapokulilia unisaidie

Ninapoinua mikono yangu kuelekea chumba cha ndani zaidi cha mahali pako patakatifu.+

 3 Usinikokote pamoja na waovu, pamoja na wale wanaotenda mambo yanayodhuru,+

Wale wanaoongea na jirani yao maneno ya amani lakini uovu uko mioyoni mwao.+

 4 Walipe kulingana na matendo yao,+

Kulingana na mazoea yao maovu.

Walipe kulingana na kazi ya mikono yao,

Kulingana na mambo waliyotenda.+

 5 Kwa maana hawazingatii utendaji wa Yehova,+

Wala kazi ya mikono yake.+

Atawabomoa kabisa naye hatawajenga.

 6 Yehova na asifiwe,

Kwa maana amesikia sihi zangu za kuomba msaada.

 7 Yehova ni nguvu zangu+ na ngao yangu;+

Moyo wangu unamtumaini yeye.+

Amenisaidia, na moyo wangu unashangilia,

Kwa hiyo nitamsifu kwa wimbo wangu.

 8 Yehova ni nguvu kwa watu wake;

Yeye ni ngome, anamletea mtiwa-mafuta wake wokovu mkubwa.+

 9 Waokoe watu wako, na uubariki urithi wako.+

Wachunge na kuwabeba mikononi mwako milele.+

Muziki wa Daudi.

29 Mpeni Yehova anachostahili, enyi wana wa watu hodari,

Mpeni Yehova anachostahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+

 2 Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili.

Mwinamieni* Yehova katika mapambo matakatifu.*

 3 Sauti ya Yehova husikika juu ya maji;

Mungu mtukufu hunguruma.+

Yehova yuko juu ya maji mengi.+

 4 Sauti ya Yehova ina nguvu;+

Sauti ya Yehova ina fahari.

 5 Sauti ya Yehova inavunja mierezi;

Naam, Yehova anaipasua-pasua mierezi ya Lebanoni.+

 6 Hufanya Lebanoni* irukeruke kama ndama,

Na Sirioni+ kama ng’ombe dume mchanga wa mwituni.

 7 Sauti ya Yehova hupiga kwa miali ya moto;+

 8 Sauti ya Yehova huifanya nyika itetemeke;+

Yehova huifanya nyika ya Kadeshi+ itetemeke.

 9 Sauti ya Yehova humfanya paa atetemeke na kuzaa

Nayo huivua kabisa misitu.+

Na wote walio katika hekalu lake husema: “Utukufu!”

10 Yehova huketi kwenye kiti cha ufalme juu ya mafuriko ya maji;*+

Yehova huketi kwenye kiti cha ufalme akiwa Mfalme milele.+

11 Yehova atawapa nguvu watu wake.+

Yehova atawabariki watu wake kwa amani.+

Muziki. Wimbo wa kuizindua nyumba. Wa Daudi.

30 Nitakukweza, Ee Yehova, kwa maana umeniinua* juu;

Hukuruhusu maadui wangu washangilie juu yangu.+

 2 Ee Yehova Mungu wangu, nilikulilia unisaidie, nawe ukaniponya.+

 3 Ee Yehova, umeniinua* kutoka Kaburini.*+

Ulifanya niendelee kuwa hai; uliniokoa nisizame shimoni.*+

 4 Mwimbieni sifa* Yehova, enyi washikamanifu wake,+

Lishukuruni jina lake takatifu;*+

 5 Kwa sababu hasira yake ni ya muda mfupi tu,+

Lakini kibali chake* hudumu maisha yote.+

Huenda kukawa na kilio jioni, lakini asubuhi, kuna kilio cha shangwe.+

 6 Nilipokuwa na amani, nilisema:

“Sitatikiswa kamwe.”*

 7 Ee Yehova, nilipokuwa na kibali chako,* ulinifanya niwe imara kama mlima.+

Lakini ulipouficha uso wako, niliogopa.+

 8 Niliendelea kukulilia wewe, Ee Yehova;+

Nami niliendelea kukusihi wewe, Ee Yehova, unionyeshe kibali.

 9 Kuna faida gani nikifa,* nikishuka shimoni?*+

Je, mavumbi yatakusifu?+ Je, yatasimulia kuhusu uaminifu wako?+

10 Sikia, Ee Yehova, na unionyeshe kibali.+

Ee Yehova, uwe msaidizi wangu.+

11 Umebadili maombolezo yangu kuwa dansi;

Umenivua nguo zangu za magunia, nawe unanivisha shangwe,

12 Ili niimbe* sifa yako, nisinyamaze.

Ee Yehova Mungu wangu, nitakusifu milele.

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

31 Nimekukimbilia wewe, Ee Yehova.+

Acha nisiaibishwe kamwe.+

Niokoe kwa sababu ya uadilifu wako.+

 2 Nitegee sikio lako.*

Njoo haraka uniokoe.+

Uwe kwangu mlima ambao ni ngome,

Ngome ya kuniokoa.+

 3 Kwa maana wewe ni jabali langu na ngome yangu;+

Kwa ajili ya jina lako,+ utaniongoza na kunielekeza.+

 4 Utanitoa katika wavu walionitegea kwa siri,+

Kwa maana wewe ni ngome yangu.+

 5 Naiweka roho yangu mikononi mwako.+

Umenikomboa, Ee Yehova, Mungu wa ukweli.*+

 6 Ninawachukia wale wanaoabudu sanamu zisizo na faida, za ubatili,

Lakini mimi, ninamtumaini Yehova.

 7 Nitashangilia sana kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu,

Kwa maana umeona dhiki yangu;+

Unajua mateso makali yaliyo ndani yangu.*

 8 Hujanitia mikononi mwa adui,

Lakini unanifanya nisimame mahali salama.*

 9 Nionyeshe kibali, Ee Yehova, kwa maana niko katika dhiki.

Maumivu makali yamefanya macho yangu yadhoofike,+ na pia mwili wangu wote.*+

10 Maisha yangu yamejaa huzuni+

Na miaka yangu kilio cha maumivu makali.+

Nguvu zangu zinapungua kwa sababu ya dhambi yangu;

Mifupa yangu inadhoofika.+

11 Ninadhihakiwa na maadui wangu wote,+

Hasa majirani wangu.

Na rafiki zangu wananiogopa;

Wanaponiona hadharani, wananikimbia.+

12 Wameniondoa moyoni* mwao na kunisahau, kana kwamba nimekufa;

Mimi ni kama gudulia lililovunjika.

13 Nimesikia uvumi mwingi wa uovu;

Nimezungukwa na hofu.+

Wanapokusanyika pamoja kama kitu kimoja dhidi yangu,

Wanapanga njama ya kuniua.*+

14 Lakini ninakutumaini wewe, Ee Yehova.+

Ninatangaza: “Wewe ni Mungu wangu.”+

15 Siku* zangu zimo mkononi mwako.

Niokoe kutoka mikononi mwa maadui wangu na kutoka kwa wale wanaonitesa.+

16 Ifanye nuru ya uso wako imwangazie mtumishi wako.+

Niokoe kwa upendo wako mshikamanifu.

17 Ee Yehova, naomba nisiaibishwe ninapokulilia wewe.+

Waovu na waaibishwe;+

Na wanyamazishwe Kaburini.*+

18 Midomo inayosema uwongo na iwe bubu,+

Midomo inayoongea kwa kiburi dhidi ya mwadilifu, kwa majivuno na dharau.

19 Jinsi wema wako ulivyo mwingi sana!+

Umewahifadhia wale wanaokuogopa,+

Nawe umeuonyesha mbele ya wanadamu wote, kwa niaba ya wale wanaokukimbilia wewe.+

20 Utawaficha mahali pa siri mbele zako*+

Mbali na njama za wanadamu;

Utawaficha katika banda lako

Dhidi ya mashambulizi ya watu wenye nia mbaya.*+

21 Yehova na asifiwe,

Kwa maana kwa njia yenye kustaajabisha, amenionyesha upendo wake mshikamanifu+ katika jiji lililozingirwa.+

22 Lakini mimi nilishikwa na wasiwasi nikasema:

“Nitaangamia kutoka mbele zako.”+

Lakini ulisikia sihi zangu za kuomba msaada nilipokulilia kwa sauti.+

23 Mpendeni Yehova, enyi nyote mlio washikamanifu kwake!+

Yehova huwalinda waaminifu,+

Lakini humlipa vilivyo yeyote anayeonyesha kiburi.+

24 Iweni jasiri, na muwe na moyo mkuu,+

Ninyi nyote mnaomngojea Yehova.+

Wa Daudi. Maskili.*

32 Mwenye furaha ni mtu ambaye amesamehewa kosa lake, ambaye dhambi yake imefunikwa.*+

 2 Mwenye furaha ni mtu ambaye Yehova hamwoni kuwa mwenye hatia,+

Asiye na udanganyifu katika roho yake.

 3 Niliponyamaza, mifupa yangu ilidhoofika kwa sababu ya kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.+

 4 Kwa maana usiku na mchana mkono wako ulinilemea.*+

Nguvu zangu zilitoweka* kama mvuke katika joto kavu la kiangazi. (Sela)

 5 Mwishowe nikaungama dhambi yangu kwako;

Sikufunika kosa langu.+

Nilisema: “Nitaungama makosa yangu kwa Yehova.”+

Nawe ukanisamehe kosa la dhambi zangu.+ (Sela)

 6 Ndiyo sababu kila mtu aliye mshikamanifu atasali kwako+

Maadamu unapatikana.+

Ndipo hata mafuriko hayatamfikia.

 7 Wewe ni mahali pangu pa kujificha;

Utanilinda nisipatwe na taabu.+

Utanizunguka kwa kelele za shangwe za ukombozi.+ (Sela)

 8 “Nitakupa ufahamu na kukufundisha njia unayopaswa kufuata.+

Nitakupa ushauri jicho langu likikutazama.+

 9 Usiwe kama farasi au nyumbu, asiye na uelewaji,+

Ambaye ni lazima msisimko wake udhibitiwe kwa hatamu au lijamu

Kabla hajakukaribia.”

10 Mwovu ana maumivu mengi;

Lakini mtu anayemtumaini Yehova amezungukwa na upendo Wake mshikamanifu.+

11 Furahini kwa sababu ya Yehova na kushangilia, enyi waadilifu;

Pazeni sauti kwa shangwe, ninyi nyote mlio wanyoofu moyoni.

33 Pazeni sauti kwa shangwe, enyi waadilifu, kwa sababu ya Yehova.+

Ni jambo linalofaa kwa wanyoofu kumsifu yeye.

 2 Mshukuruni Yehova kwa kinubi;

Mwimbieni sifa* kwa kinanda chenye nyuzi kumi.

 3 Mwimbieni wimbo mpya;+

Pigeni nyuzi kwa ustadi, na kupaza sauti kwa shangwe.

 4 Kwa maana neno la Yehova limenyooka,+

Na kila jambo analofanya linategemeka.

 5 Anapenda uadilifu na haki.+

Dunia imejaa upendo mshikamanifu wa Yehova.+

 6 Kwa neno la Yehova mbingu ziliumbwa,+

Na kwa roho ya* kinywa chake kila kitu kilichomo kiliumbwa.*

 7 Huyakusanya maji ya bahari kana kwamba ni bwawa;+

Huyaweka mawimbi makubwa ya maji katika maghala.

 8 Dunia yote na imwogope Yehova.+

Wakaaji wa nchi* na wamhofu.

 9 Kwa maana alisema, ikawa;+

Aliamuru, ikasimama imara.+

10 Yehova amevuruga njama za* mataifa;+

Ameharibu mipango* ya mataifa.+

11 Lakini maamuzi* ya Yehova yatasimama milele;+

Mawazo ya moyo wake ni ya kizazi baada ya kizazi.

12 Lenye furaha ni taifa ambalo Mungu wake ni Yehova,+

Watu ambao amewachagua kuwa miliki yake mwenyewe.+

13 Yehova anatazama chini kutoka mbinguni;

Anawaona wanadamu wote.+

14 Kutoka katika makao yake,

Anawakazia macho wakaaji wa dunia.

15 Yeye ndiye anayeumba mioyo ya wote;

Huchunguza kazi zao zote.+

16 Hakuna mfalme anayeokolewa na jeshi kubwa;+

Mtu hodari haokolewi na nguvu zake nyingi.+

17 Farasi ni tumaini la uwongo la wokovu;*+

Nguvu zake nyingi hazimhakikishii mtu kwamba ataponyoka.

18 Tazama! Jicho la Yehova linawalinda wale wanaomwogopa,+

Wale wanaongojea upendo wake mshikamanifu,

19 Ili awaokoe* kutoka katika kifo

Na kuwahifadhi hai wakati wa njaa kali.+

20 Tunamtarajia Yehova.

Yeye ni msaidizi wetu na ngao yetu.+

21 Mioyo yetu hushangilia kwa sababu yake,

Kwa maana tunalitumaini jina lake takatifu.+

22 Upendo wako mshikamanifu na ukae juu yetu, Ee Yehova,+

Tunapoendelea kukungojea.+

Wa Daudi, alipojifanya mwenda wazimu+ mbele ya Abimeleki, hivi kwamba akamfukuza, naye akaenda zake.

א [Aleph]

34 Nitamsifu Yehova nyakati zote;

Sifa yake itakuwa midomoni mwangu daima.

ב [Beth]

 2 Nitajigamba* kwa sababu ya Yehova;+

Wapole watasikia na kushangilia.

ג [Gimel]

 3 Mtukuzeni Yehova pamoja nami;+

Na tulikweze jina lake pamoja.

ד [Daleth]

 4 Nilimwomba Yehova ushauri, naye akanijibu.+

Aliniokoa kutoka katika mambo yote yanayoniogopesha.+

ה [He]

 5 Wale waliomtazama waling’aa;

Nyuso zao hazingeweza kuona aibu.

ז [Zayin]

 6 Mtu huyo wa hali ya chini aliita, na Yehova akasikia.

Alimwokoa kutoka katika taabu zake zote.+

ח [Heth]

 7 Malaika wa Yehova hupiga kambi pande zote kuwazunguka wanaomwogopa Yeye,+

Naye huwaokoa.+

ט [Teth]

 8 Onjeni mwone kwamba Yehova ni mwema;+

Mwenye furaha ni mtu anayemkimbilia.

י [Yod]

 9 Mwogopeni Yehova, ninyi nyote watakatifu wake,

Kwa maana wale wanaomwogopa hawakosi chochote.+

כ [Kaph]

10 Hata wanasimba* wenye nguvu wamelemewa na njaa,

Lakini wale wanaomtafuta Yehova hawatakosa chochote chema.+

ל [Lamed]

11 Njooni, wanangu, nisikilizeni;

Nitawafundisha kumwogopa Yehova.+

מ [Mem]

12 Ni nani miongoni mwenu anayependa uzima

Na angependa kuishi siku nyingi njema?+

נ [Nun]

13 Basi ulinde ulimi wako usiseme mabaya,+

Midomo yako isiseme uwongo.+

ס [Samekh]

14 Acha uovu, utende mema;+

Tafuta amani na uifuatie.+

ע [Ayin]

15 Macho ya Yehova yanawatazama waadilifu,+

Na masikio yake yanasikiliza kilio chao cha kuomba msaada.+

פ [Pe]

16 Lakini uso wa Yehova uko dhidi ya wale wanaotenda maovu,

Ili afutilie mbali kumbukumbu lao lote kutoka duniani.+

צ [Tsade]

17 Walilia kwa sauti, na Yehova akasikia;+

Aliwaokoa kutoka katika taabu zao zote.+

ק [Qoph]

18 Yehova yuko karibu na wale waliovunjika moyo;+

Huwaokoa waliopondeka roho.*+

ר [Resh]

19 Mwadilifu ana matatizo mengi,*+

Lakini Yehova humwokoa kutoka katika matatizo hayo yote.+

ש [Shin]

20 Anailinda mifupa yake yote;

Haujavunjwa hata mmoja.+

ת [Taw]

21 Msiba utamuua mwovu;

Wale wanaomchukia mwadilifu watahesabiwa kuwa na hatia.

22 Yehova anaukomboa uhai wa* watumishi wake;

Hakuna yeyote anayemkimbilia atakayepatikana na hatia.+

Wa Daudi.

35 Ee Yehova, itetee kesi yangu dhidi ya wapinzani wangu;+

Pigana na wale wanaopigana nami.+

 2 Chukua ngao yako ndogo* na ngao yako kubwa,+

Inuka unitetee.+

 3 Inua mkuki wako na shoka lako la vita* dhidi ya wale wanaonifuatia.+

Niambie:* “Mimi ni wokovu wako.”+

 4 Wale wanaowinda uhai wangu* na waaibishwe na kufedheheshwa.+

Acha wale wanaopanga njama ya kuniangamiza wakimbie kwa aibu.

 5 Na wawe kama makapi katika upepo;

Malaika wa Yehova na awafukuze.+

 6 Njia yao na iwe na giza na utelezi

Malaika wa Yehova anapowafuatia.

 7 Kwa maana bila sababu wameficha wavu wa kunitega;

Na bila sababu wamenichimbia shimo.

 8 Msiba na umjie kwa ghafla;

Wavu aliouficha na umnase;

Na aanguke ndani yake na kuangamizwa.+

 9 Lakini mimi nitashangilia kwa sababu ya Yehova;

Nitakuwa na shangwe kwa sababu ya matendo yake ya wokovu.

10 Mifupa yangu yote itasema:

“Ee Yehova, ni nani aliye kama wewe?

Unawaokoa wasio na uwezo kutoka kwa wale wanaowazidi nguvu,+

Wasio na uwezo na maskini kutoka kwa wale wanaowanyang’anya.”+

11 Mashahidi wenye nia mbaya hunikabili,+

Na kuniuliza mambo nisiyoyajua.

12 Wananilipa uovu kwa mema niliyotenda,+

Na kunifanya nihisi kama mtu aliyefiwa.

13 Lakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo za magunia;

Nilijitesa kwa kufunga,

Na sala yangu ilipokosa kujibiwa,*

14 Nilitembea huku na huku nikiomboleza kana kwamba ninamwombolezea rafiki au ndugu yangu;

Niliinama chini kwa huzuni, kama mtu anayemwombolezea mama yake.

15 Lakini nilipojikwaa, walishangilia na kukusanyika pamoja;

Walikusanyika pamoja ili wanivizie na kuniua;

Walinirarua vipandevipande nao hawakunyamaza.

16 Wasiomwogopa Mungu wananidhihaki kwa dharau,*

Wananisagia meno yao.+

17 Ee Yehova, utatazama tu mpaka lini?+

Niokoe dhidi ya mashambulizi yao,+

Uhai wangu wenye thamani* kutoka kwa wanasimba.*+

18 Kisha nitakushukuru katika kutaniko kubwa;+

Nitakusifu katikati ya umati wa watu.

19 Usiruhusu wale ambao ni maadui wangu bila sababu wanicheke;

Usiruhusu wale wanaonichukia bila sababu+ wakonyeze macho yao kwa hila.+

20 Kwa maana hawasemi maneno ya amani,

Lakini wanapanga njama kwa hila dhidi ya watu wenye amani nchini.+

21 Wanafungua kinywa chao wazi ili wanishtaki,

Wakisema: “Aha! Aha! Macho yetu yameliona.”

22 Ee Yehova, umeona jambo hilo. Usinyamaze.+

Ee Yehova, usikae mbali nami.+

23 Amka, inuka unitetee,

Mungu wangu, Yehova, nitetee katika kesi yangu.

24 Nihukumu kulingana na uadilifu wako,+ Ee Yehova Mungu wangu;

Usiruhusu wanicheke.

25 Wasiseme kamwe moyoni mwao: “Aha! Tulipata tulichotaka!”*

Wasiseme kamwe: “Tumemmeza.”+

26 Acha wote waaibishwe na kufedheheshwa,

Wale wanaonicheka kwa sababu ya msiba wangu.

Acha wale wanaojikweza juu yangu wavishwe aibu na fedheha.

27 Lakini acha wale wanaofurahia uadilifu wangu wapaze sauti kwa shangwe;

Na waseme daima:

“Yehova na atukuzwe, anayefurahia amani ya mtumishi wake.”+

28 Kisha ulimi wangu utasimulia* uadilifu wako+

Na kukusifu mchana kutwa.+

Kwa kiongozi. Wa Daudi, mtumishi wa Yehova.

36 Dhambi huzungumza na mwovu ndani kabisa ya moyo wake;

Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.+

 2 Kwa maana hujisifusifu sana machoni pake mwenyewe

Hivi kwamba hawezi kutambua kosa lake na kulichukia.+

 3 Maneno ya kinywa chake yanadhuru na ni ya udanganyifu;

Haonyeshi ufahamu wowote wa kutenda mema.

 4 Hupanga njama zinazodhuru hata kitandani mwake.

Hufuatia njia isiyo njema;

Hakatai lililo baya.

 5 Ee Yehova, upendo wako mshikamanifu unafika mpaka mbinguni,+

Uaminifu wako mpaka mawinguni.

 6 Uadilifu wako ni kama milima mikubwa;*+

Hukumu zako ni kama maji mengi yenye kina.+

Unawahifadhi* wanadamu na wanyama, Ee Yehova.+

 7 Jinsi upendo wako mshikamanifu ulivyo na thamani sana, Ee Mungu!+

Katika kivuli cha mabawa yako,

Wanadamu hukimbilia.+

 8 Wanakunywa na kushiba vitu vinono vya* nyumba yako,+

Nawe huwanywesha kwenye kijito cha vitu vyako vinavyofurahisha.+

 9 Wewe ndiye chanzo cha uhai;+

Kwa nuru yako tunaweza kuona nuru.+

10 Endelea kuwatendea kwa upendo wako mshikamanifu wale wanaokujua,+

Na kuwaonyesha uadilifu wako walio wanyoofu moyoni.+

11 Usiruhusu mguu wa mwenye kiburi unikanyage

Wala mkono wa mwovu unifukuze.

12 Watenda maovu wameanguka huko;

Wamepigwa na kuangushwa chini na hawawezi kusimama.+

Wa Daudi.

א [Aleph]

37 Usikasirike* kwa sababu ya waovu

Wala usiwaonee wivu watenda dhambi.+

 2 Watanyauka haraka kama majani+

Na kusinyaa kama majani yaliyochipuka ya kijani kibichi.

ב [Beth]

 3 Mtumaini Yehova na utende mema;+

Kaa duniani,* na utende kwa uaminifu.+

 4 Pata furaha tele* katika Yehova,

Naye atatosheleza tamaa za moyo wako.

ג [Gimel]

 5 Mkabidhi* Yehova njia yako;+

Mtegemee yeye, naye atatenda kwa niaba yako.+

 6 Ataufanya uadilifu wako ung’ae kama mapambazuko,

Na haki yako kama jua la adhuhuri.

ד [Daleth]

 7 Nyamaza mbele za Yehova+

Na umngojee kwa matumaini.*

Usikasirishwe na mtu

Anayefanikiwa kutekeleza njama zake.+

ה [He]

 8 Acha hasira na uache ghadhabu;+

Usikasirike na kuanza kutenda uovu.*

 9 Kwa maana waovu wataangamizwa,+

Lakini wale wanaomtumaini Yehova wataimiliki dunia.+

ו [Waw]

10 Bado muda mfupi tu, na watu waovu hawatakuwepo tena;+

Utapaangalia mahali walipokuwa,

Nao hawatakuwepo.+

11 Lakini wapole wataimiliki dunia,+

Nao watafurahia kwelikweli wingi wa amani.+

ז [Zayin]

12 Mtu mwovu hupanga njama dhidi ya mwadilifu;+

Humsagia meno yake.

13 Lakini Yehova atamcheka,

Kwa maana Anajua kwamba siku yake itakuja.+

ח [Heth]

14 Waovu huchomoa panga zao na kuzikunja* pinde zao

Ili kumwangusha chini aliyekandamizwa na pia maskini,

Ili kuwachinja wale ambao njia yao imenyooka.

15 Lakini upanga wao utauchoma moyo wao wenyewe;+

Pinde zao zitavunjwa.

ט [Teth]

16 Kidogo alicho nacho mwadilifu ni bora

Kuliko wingi wa vitu walivyo navyo watu wengi waovu.+

17 Kwa maana mikono ya waovu itavunjwa,

Lakini Yehova atawategemeza waadilifu.

י [Yod]

18 Yehova anajua mambo wanayokabili watu wasio na lawama,*

Na urithi wao utadumu milele.+

19 Hawataaibishwa wakati wa msiba;

Wakati wa njaa kali watakuwa na chakula tele.

כ [Kaph]

20 Lakini waovu wataangamia;+

Maadui wa Yehova watatoweka kama malisho bora kabisa;

Watatoweka kama moshi.

ל [Lamed]

21 Mwovu hukopa lakini halipi,

Lakini mwadilifu ni mkarimu* naye hutoa.+

22 Wale Anaowabariki wataimiliki dunia,

Lakini wale Anaowalaani wataangamizwa.+

מ [Mem]

23 Yehova huongoza* hatua za mtu+

Njia ya mtu huyo inapompendeza Yeye.+

24 Hata akianguka, hataangushwa chini kabisa,+

Kwa maana Yehova anaushika mkono wake na kumtegemeza.*+

נ [Nun]

25 Nilikuwa kijana lakini sasa nimezeeka,

Lakini sijamwona mtu yeyote mwadilifu akiwa ameachwa,+

Wala watoto wake wakitafuta mkate.*+

26 Sikuzote anakopesha bila faida,+

Na watoto wake watapata baraka.

ס [Samekh]

27 Acha uovu, utende mema,+

Nawe utaishi milele.

28 Kwa maana Yehova anapenda haki,

Naye hatawaacha washikamanifu wake.+

ע [Ayin]

Watalindwa sikuzote;+

Lakini wazao wa waovu wataangamizwa.+

29 Waadilifu wataimiliki dunia,+

Nao wataishi humo milele.+

פ [Pe]

30 Kinywa cha mwadilifu hufundisha hekima,*

Na ulimi wake huongea kuhusu haki.+

31 Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake;+

Hatua zake hazitayumbayumba.+

צ [Tsade]

32 Mwovu humtazama mwadilifu,

Akitafuta kumuua.

33 Lakini Yehova hatamwacha mikononi mwa mtu huyo+

Wala hatampata na hatia anapohukumiwa.+

ק [Qoph]

34 Mtumaini Yehova na ufuate njia yake,

Naye atakukweza uimiliki dunia.

Waovu watakapoangamizwa,+ utaona jambo hilo.+

ר [Resh]

35 Nimemwona mtu mkatili, mwovu

Akisambaa kama mti wenye majani mengi katika udongo wake wa asili.+

36 Lakini alikufa ghafla naye akatoweka;+

Niliendelea kumtafuta, lakini sikuweza kumpata.+

ש [Shin]

37 Mwangalie mtu asiye na lawama,*

Na uendelee kumwangalia mnyoofu,+

Kwa maana wakati ujao wa mtu huyo utakuwa na amani.+

38 Lakini watenda dhambi wote wataangamizwa;

Wakati ujao wa watu waovu utakomeshwa.+

ת [Taw]

39 Wokovu wa watu waadilifu unatoka kwa Yehova;+

Yeye ndiye ngome yao wakati wa taabu.+

40 Yehova atawasaidia na kuwaokoa.+

Atawanusuru kutoka kwa waovu na kuwaokoa,

Kwa sababu wanamkimbilia yeye.+

Muziki wa Daudi, wa kukumbusha.

38 Ee Yehova, usinikaripie kwa hasira yako,

Wala usinirekebishe kwa ghadhabu yako.+

 2 Kwa maana mishale yako imenichoma ndani kabisa,

Na mkono wako unanikandamiza chini.+

 3 Mwili wangu wote ni mgonjwa kwa sababu ya hasira yako kali.

Hakuna amani katika mifupa yangu kwa sababu ya dhambi yangu.+

 4 Kwa maana dhambi zangu zimetanda juu ya kichwa changu;+

Kama mzigo mzito, ni nzito sana siwezi kuzibeba.

 5 Vidonda vyangu vinanuka na vina usaha

Kwa sababu ya upumbavu wangu.

 6 Nimesononeka na kushuka moyo kupita kiasi;

Ninatembea huku na huku mchana kutwa kwa huzuni.

 7 Ninaungua ndani ya mwili wangu;*

Mwili wangu wote ni mgonjwa.+

 8 Nimekufa ganzi na kupondeka kabisa;

Moyo wangu wenye maumivu makali unanifanya nilie kwa sauti kubwa.*

 9 Ee Yehova, unajua mambo yote ninayotamani,

Na kilio changu cha maumivu hakijafichwa machoni pako.

10 Moyo wangu unadundadunda, nguvu zangu zimetoweka,

Na nuru ya macho yangu imetoweka.+

11 Rafiki zangu na wenzangu wananiepuka kwa sababu ya pigo langu,

Na rafiki zangu wa karibu wanasimama mbali.

12 Wale wanaotafuta uhai wangu* wanatega mitego;

Wale wanaojaribu kunidhuru wanazungumza kuhusu kuniangamiza;+

Wananong’onezana uwongo mchana kutwa.

13 Lakini kama kiziwi, sikuwasikiliza;+

Na kama bubu, sikufumbua kinywa changu.+

14 Nimekuwa kama mtu asiyeweza kusikia,

Ambaye kinywa chake hakina lolote la kujitetea.

15 Kwa maana nilikungojea wewe, Ee Yehova,+

Nawe ukanijibu, Ee Yehova Mungu wangu.+

16 Kwa maana nilisema: “Acha wasinicheke

Wala kujikweza juu yangu mguu wangu ukiteleza.”

17 Kwa maana nilikuwa karibu kuanguka,

Na maumivu yangu yalikuwa pamoja nami daima.+

18 Niliungama kosa langu;+

Nilihangaishwa na dhambi yangu.+

19 Lakini maadui wangu wana juhudi* na ni hodari,*

Wale wanaonichukia bila sababu wameongezeka sana.

20 Walinilipa uovu kwa mema niliyotenda;

Walinipinga kwa sababu ya kufuatia mambo mema.

21 Usiniache, Ee Yehova.

Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali nami.+

22 Njoo haraka unisaidie,

Ee Yehova, wokovu wangu.+

Kwa kiongozi; wa Yeduthuni.*+ Muziki wa Daudi.

39 Nilisema: “Nitailinda hatua yangu

Ili niepuke kutenda dhambi kwa ulimi wangu.+

Nitakilinda kinywa changu kwa lijamu+

Maadamu mtu yeyote mwovu yuko mbele yangu.”

 2 Nilinyamaza na kukaa kimya;+

Niliendelea kunyamaza hata kuhusu jambo jema,

Lakini maumivu yangu yalikuwa makali.*

 3 Moyo wangu uliteketea polepole* ndani yangu.

Nilipokuwa nikiwaza sana,* moto huo uliendelea kuwaka.

Kisha ulimi wangu ukasema:

 4 “Ee Yehova, nisaidie kujua mwisho wangu,

Na idadi ya siku zangu,+

Ili nijue ufupi wa maisha yangu.*

 5 Kwa kweli, umefanya siku zangu ziwe chache tu;*+

Na urefu wa maisha yangu kuwa si kitu mbele zako.+

Kwa hakika kila mwanadamu, ingawa anaonekana yuko salama, si kitu ila pumzi tu.+ (Sela)

 6 Kwa hakika kila mwanadamu hutembea huku na huku kama kivuli.

Hukimbia huku na huku* bila sababu.

Hurundika mali, bila kujua ni nani atakayeifurahia.+

 7 Sasa basi, ninaweza kutumaini nini, Ee Yehova?

Wewe ndiye tumaini langu pekee.

 8 Niokoe kutoka katika makosa yangu yote.+

Usimruhusu mpumbavu anifanye kuwa kitu cha kudharauliwa.

 9 Niliendelea kunyamaza;

Sikuweza kufumbua kinywa changu,+

Kwa maana wewe ndiye uliyefanya hayo.+

10 Niondolee pigo lako.

Nimedhoofika kabisa kwa sababu mkono wako unanipiga.

11 Unamrekebisha mwanadamu kwa kumwadhibu kwa sababu ya kosa lake;+

Unaharibu kabisa vitu anavyothamini sana kama nondo* anavyoharibu.

Kwa kweli kila mwanadamu ni pumzi tu.+ (Sela)

12 Sikia sala yangu, Ee Yehova,

Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada.+

Usipuuze machozi yangu.

Kwa maana kwako, mimi ni mkaaji mgeni tu,+

Msafiri apitaye,* kama mababu zangu wote.+

13 Usinitazame kwa ukali ili nichangamke

Kabla sijafa* na kutoweka.”

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

40 Nilimtumaini Yehova kwa bidii,*

Naye akanitegea sikio lake na kusikia* kilio changu cha kuomba msaada.+

 2 Akanipandisha kutoka katika shimo linalonguruma,

Kutoka katika matope yenye utelezi.

Akaiweka miguu yangu juu ya jabali;

Akanifanya nisimame mahali palipo imara.

 3 Kisha akaweka wimbo mpya kinywani mwangu,+

Asifiwe Mungu wetu.

Wengi watatazama kwa hofu

Na kumtumaini Yehova.

 4 Mwenye furaha ni mtu anayemtumaini Yehova

Na ambaye hawatumaini wakaidi au watu wadanganyifu.*

 5 Jinsi ulivyotenda mambo mengi sana,

Ee Yehova Mungu wangu,

Kazi zako zinazostaajabisha na mawazo yako kutuelekea.+

Hakuna yeyote anayeweza kulinganishwa nawe;+

Ikiwa ningejaribu kusimulia na kuongea kuzihusu,

Zingekuwa nyingi sana kwangu kusimulia!+

 6 Hukutamani* dhabihu na toleo,+

Lakini ulifungua masikio yangu ili yasikie.+

Hukuomba dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za dhambi.+

 7 Kisha nikasema: “Tazama, nimekuja.

Katika kitabu cha kukunjwa imeandikwa kunihusu.+

 8 Ee Mungu wangu, ninafurahia* kufanya mapenzi yako,+

Na sheria yako imo ndani yangu kabisa.+

 9 Ninatangaza habari njema ya uadilifu katika kutaniko kubwa.+

Tazama! Siizuii midomo yangu,+

Ee Yehova, kama unavyojua vema.

10 Siufuniki uadilifu wako moyoni mwangu.

Ninatangaza uaminifu wako na wokovu wako.

Siufichi upendo wako mshikamanifu na ukweli wako katika kutaniko kubwa.”+

11 Ee Yehova, usininyime rehema yako.

Upendo wako mshikamanifu na ukweli wako na unilinde daima.+

12 Misiba inayonizunguka ni mingi sana haihesabiki.+

Makosa yangu mengi yananilemea hivi kwamba siwezi kuona njia yangu;+

Ni mengi sana kuliko nywele za kichwa changu,

Nami nimevunjika moyo.

13 Tafadhali, Ee Yehova, uwe tayari kuniokoa.+

Ee Yehova, njoo haraka unisaidie.+

14 Wote wanaotaka kuniua*

Na waaibishwe na kufedheheshwa.

Wale wanaofurahia msiba wangu

Na wakimbie kwa aibu.

15 Wale wanaoniambia: “Aha! Aha!”

Na washtuke kwa sababu ya aibu yao.

16 Lakini acha wale wanaokutafuta+

Wafurahi na kushangilia kwa sababu yako.+

Wale wanaopenda matendo yako ya wokovu na waseme daima:

“Yehova na atukuzwe.”+

17 Lakini sina uwezo, nami ni maskini;

Yehova na anitunze.

Wewe ni msaidizi wangu na mwokozi wangu;+

Mungu wangu, usikawie.+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

41 Mwenye furaha ni mtu yeyote anayemjali mtu wa hali ya chini;+

Yehova atamwokoa siku ya msiba.

 2 Yehova atamlinda na kumhifadhi hai.

Atatangazwa kuwa mwenye furaha duniani;+

Hutamtia kamwe mikononi mwa maadui wake ili wamtendee wapendavyo.*+

 3 Yehova atamtegemeza kwenye kitanda chake cha ugonjwa;+

Wakati huo wa ugonjwa utakibadili kabisa kitanda chake.

 4 Kwa maana nilisema: “Ee Yehova, nionyeshe kibali.+

Niponye,*+ kwa maana nimekutendea dhambi.”+

 5 Lakini maadui wangu wanasema mambo maovu kunihusu:

“Atakufa lini jina lake litoweke?”

 6 Mmoja wao akija kuniona, moyo wake husema uwongo.

Hukusanya mambo yenye kudhuru ya kusema;

Kisha hutoka nje na kuyaeneza kotekote.

 7 Wote wanaonichukia wananong’onezana;

Wanapanga njama ya uovu dhidi yangu:

 8 “Amepatwa na jambo linaloogopesha;

Sasa kwa kuwa yuko chini, hatainuka tena.”+

 9 Hata mtu niliyekuwa na amani naye, ambaye nilimwamini,+

Aliyekuwa akila mkate wangu, amekiinua kisigino chake dhidi yangu.*+

10 Lakini wewe, Ee Yehova, nionyeshe kibali na kuniinua,

Ili niwalipize.

11 Kwa njia hii nitajua kwamba unapendezwa nami:

Adui yangu asipoweza kupaza sauti kwa ushindi dhidi yangu.+

12 Lakini mimi, unanitegemeza kwa sababu ya utimilifu wangu;+

Utaniweka mbele zako* milele.+

13 Yehova, Mungu wa Israeli, na asifiwe

Kwa umilele wote.*+

Amina na Amina.

KITABU CHA PILI

(Zaburi 42-72)

Kwa kiongozi. Maskili* ya wana wa Kora.+

42 Kama paa anayetamani vijito vya maji,

Ndivyo ninavyokutamani, Ee Mungu.

 2 Nina kiu kwa ajili ya Mungu, kwa ajili ya Mungu aliye hai.+

Nije lini na kuonekana mbele za Mungu?+

 3 Machozi yangu ni chakula changu usiku na mchana;

Mchana kutwa watu wananidhihaki wakisema: “Mungu wako yuko wapi?”+

 4 Ninayakumbuka mambo haya, nami naimwaga nafsi* yangu,

Kwa maana wakati fulani nilitembea pamoja na umati;

Nilikuwa nikitembea kimyakimya* mbele zao kwenda katika nyumba ya Mungu,

Kwa sauti za shangwe na shukrani,

Za umati unaofanya sherehe.+

 5 Kwa nini nimesononeka?+

Kwa nini msukosuko huu umo ndani yangu?

Mngojee Mungu,+

Kwa maana bado nitamsifu kwa kuwa yeye ni Mwokozi wangu Mtukufu.+

 6 Mungu wangu, nimesononeka.+

Ndiyo sababu ninakukumbuka,+

Kutoka katika nchi ya Yordani na vilele vya Hermoni,

Kutoka Mlima Mizari.*

 7 Vilindi vya maji vinaita vilindi vya maji

Kwa sauti ya maporomoko yako ya maji.

Mawimbi yako makubwa yamenilemea.+

 8 Wakati wa mchana Yehova atanipa upendo wake mshikamanifu,

Na usiku wimbo wake utakuwa pamoja nami—sala kwa Mungu wa uhai wangu.+

 9 Nitamwambia Mungu, jabali langu:

“Kwa nini umenisahau?+

Kwa nini nitembee huku na huku nikiwa na huzuni kwa sababu ya kukandamizwa na adui yangu?”+

10 Maadui wangu wananidhihaki kwa chuki kali sana;**

Mchana kutwa wananidhihaki wakisema: “Mungu wako yuko wapi?”+

11 Kwa nini nimesononeka?

Kwa nini msukosuko huu umo ndani yangu?

Mngojee Mungu,+

Kwa maana bado nitamsifu kwa kuwa yeye ni Mwokozi wangu Mtukufu na Mungu wangu.+

43 Nihukumu, Ee Mungu,+

Itetee kesi yangu+ dhidi ya taifa lisilo na ushikamanifu.

Niokoe kutoka kwa mtu mdanganyifu na asiye mwadilifu.

 2 Kwa maana wewe ni Mungu wangu, ngome yangu.+

Kwa nini umenitupa?

Kwa nini nitembee huku na huku nikiwa na huzuni kwa sababu ya kukandamizwa na adui yangu?+

 3 Itume nuru yako na kweli yako.+

Navyo viniongoze;+

Viniongoze kwenye mlima wako mtakatifu na kwenye hema lako tukufu la ibada.+

 4 Kisha nitakuja kwenye madhabahu ya Mungu,+

Kwa Mungu, shangwe yangu inayofurika.

Nami nitakusifu kwa kinubi,+ Ee Mungu, Mungu wangu.

 5 Kwa nini nimesononeka?

Kwa nini msukosuko huu umo ndani yangu?

Mngojee Mungu,+

Kwa maana bado nitamsifu kwa kuwa yeye ni Mwokozi wangu Mtukufu na Mungu wangu.+

Kwa kiongozi. Wa wana wa Kora.+ Maskili.*

44 Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu wenyewe,

Mababu zetu wametusimulia,+

Mambo uliyotimiza katika siku zao,

Siku za zamani za kale.

 2 Kwa mkono wako uliyafukuza mataifa+

Ukawafanya mababu zetu waishi huko.+

Uliyapondaponda mataifa na kuyafukuza.+

 3 Hawakuimiliki nchi kwa upanga wao wenyewe,+

Na mkono wao wenyewe haukuwaletea ushindi.+

Badala yake, waliimiliki kwa mkono wako wa kuume na uwezo wako+ na nuru ya uso wako,

Kwa maana ulipendezwa nao.+

 4 Wewe ni Mfalme wangu, Ee Mungu;+

Amuru* ushindi kamili* kwa ajili ya Yakobo.

 5 Kwa nguvu zako tutawafukuza maadui wetu;+

Katika jina lako tutawakanyagia chini wale wanaoinuka dhidi yetu.+

 6 Kwa maana siutumaini upinde wangu,

Na upanga wangu hauwezi kuniokoa.+

 7 Ni wewe uliyetuokoa kutoka kwa maadui wetu,+

Wewe uliyewaaibisha wale wanaotuchukia.

 8 Tutamsifu Mungu mchana kutwa,

Nasi tutalishukuru jina lako milele. (Sela)

 9 Lakini sasa umetutupa na kutuaibisha,

Nawe huendi pamoja na majeshi yetu.

10 Unaendelea kutufanya tumkimbie adui yetu;+

Wale wanaotuchukia wanachukua chochote wanachotaka.

11 Unatutia mikononi mwao ili tunyafuliwe kama kondoo;

Umetutawanya miongoni mwa mataifa.+

12 Unawauza watu wako kwa bei ya chini kabisa;+

Hupati faida yoyote kwa kuwauza.*

13 Unatufanya kuwa shutuma kwa majirani wetu,

Kitu cha kudhihakiwa na kufanyiwa mzaha na wale wote wanaotuzunguka.

14 Unatufanya kuwa kitu cha kudharauliwa* miongoni mwa mataifa,+

Kitu cha kutikisiwa kichwa na mataifa.

15 Ninaaibika mchana kutwa,

Nami nimelemewa na aibu yangu,

16 Kwa sababu ya sauti za wale wanaonidhihaki na kunitukana,

Kwa sababu ya adui yetu anayelipiza kisasi.

17 Tumepatwa na mambo haya yote, lakini hatujakusahau,

Wala hatujavunja agano lako.+

18 Moyo wetu haujakengeuka;

Hatua zetu hazitoki katika njia yako.

19 Lakini umetuponda mahali ambapo mbwamwitu wanakaa;

Umetufunika kwa kivuli kizito.

20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu

Au ikiwa tutamnyooshea mungu wa kigeni mikono yetu tunaposali,

21 Je, Mungu hatagundua hilo?

Anajua siri za moyo.+

22 Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa;

Tumehesabiwa kuwa kondoo wa kuchinjwa.+

23 Amka. Kwa nini unaendelea kulala usingizi, Ee Yehova?+

Amka! Usiendelee kututupa milele.+

24 Kwa nini unauficha uso wako?

Kwa nini unasahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?

25 Kwa maana tumeshushwa chini mavumbini;

Miili yetu imegandamizwa ardhini.+

26 Amka utusaidie!+

Tuokoe* kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu.+

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Mayungiyungi.” Wa wana wa Kora.+ Maskili.* Wimbo wa upendo.

45 Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema.

Ninasema: “Wimbo wangu unamhusu* mfalme.”+

Ulimi wangu na uwe kalamu+ ya mnakili* stadi.+

 2 Una sura nzuri kuliko wanadamu wote.

Maneno yenye fadhili hutiririka kutoka katika midomo yako.+

Ndiyo sababu Mungu amekubariki milele.+

 3 Jifunge upanga wako+ pajani, Ee mwenye nguvu,+

Katika heshima na fahari yako.+

 4 Na katika fahari yako endelea mpaka ushinde;*+

Panda utetee kweli na unyenyekevu na uadilifu,+

Na mkono wako wa kulia utatimiza* mambo yanayoogopesha.

 5 Mishale yako ni mikali, inaangusha mataifa mbele yako;+

Inachoma mioyo ya maadui wa mfalme.+

 6 Mungu ni kiti chako cha ufalme milele na milele;+

Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya unyoofu.*+

 7 Ulipenda uadilifu+ na kuchukia uovu.+

Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta+ kwa mafuta ya kushangilia+ kuliko wenzako.

 8 Mavazi yako yote yametiwa manukato ya manemane na udi na kida;

Kutoka katika jumba tukufu la mfalme lililotengenezwa kwa pembe za tembo, vinanda vinakufanya ushangilie.

 9 Mabinti wa wafalme ni miongoni mwa wanawake wako wanaoheshimiwa.

Malkia amesimama mkono wako wa kulia, akiwa amepambwa kwa dhahabu ya Ofiri.+

10 Sikiliza, Ee binti, sikiliza kwa makini na utege sikio lako;

Wasahau watu wako na nyumba ya baba yako.

11 Naye mfalme atautamani urembo wako,

Kwa maana yeye ni bwana wako,

Kwa hiyo mwinamie.

12 Binti ya Tiro ataleta zawadi;

Watu matajiri zaidi watatafuta kibali chako.*

13 Katika jumba la mfalme,* binti ya mfalme ana utukufu mwingi ajabu;

Mavazi yake yamepambwa kwa* dhahabu.

14 Atapelekwa kwa mfalme akiwa na mavazi yaliyofumwa kwa ustadi mkubwa.*

Mabikira wenzake wanaomfuata wanaletwa ndani mbele ya mfalme.

15 Wataletwa kwa furaha na shangwe;

Wataingia katika jumba la mfalme.

16 Wana wako watachukua mahali pa mababu zako.

Utawaweka kuwa wakuu katika dunia yote.+

17 Nitalitangaza jina lako katika vizazi vyote vijavyo.+

Ndiyo sababu mataifa yatakusifu milele na milele.

Kwa kiongozi. Wa wana wa Kora.+ Kulingana na mtindo wa Alamothi.* Wimbo.

46 Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu,+

Msaada unaopatikana kwa urahisi nyakati za taabu.+

 2 Ndiyo sababu hatutaogopa, hata dunia ikibadilika,

Hata milima ikianguka katika vilindi vya bahari,+

 3 Hata maji yake yakinguruma na povu lake kufurika,+

Hata milima ikitikiswa na msukosuko wake. (Sela)

 4 Kuna mto ambao vijito vyake hufanya jiji la Mungu lishangilie,+

Hema la ibada la Aliye Juu Zaidi lililo takatifu na tukufu.

 5 Mungu yuko katika jiji hilo;+ haliwezi kupinduliwa.

Mungu atalisaidia wakati wa mapambazuko.+

 6 Mataifa yalikuwa katika msukosuko, falme zilipinduliwa;

Alipaza sauti yake, dunia ikayeyuka.+

 7 Yehova wa majeshi yuko pamoja nasi;+

Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu salama.* (Sela)

 8 Njooni mtazame matendo ya Yehova,

Jinsi alivyotenda mambo yanayostaajabisha duniani.

 9 Anakomesha vita katika dunia yote.+

Anauvunja upinde na kuuvunja mkuki vipandevipande;

Anayateketeza magari ya vita motoni.*

10 “Salimuni amri na mjue kwamba mimi ni Mungu.

Nitakwezwa miongoni mwa mataifa;+

Nitakwezwa duniani.”+

11 Yehova wa majeshi yuko pamoja nasi;+

Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu salama.+ (Sela)

Kwa kiongozi. Muziki wa wana wa Kora.+

47 Enyi mataifa yote, pigeni makofi.

Mpigieni Mungu kelele za ushindi kwa vigelegele vya shangwe.

 2 Kwa maana Yehova, Aliye Juu Zaidi, ni mwenye kuogopesha;+

Yeye ndiye Mfalme mkuu juu ya dunia yote.+

 3 Huyatiisha mataifa chini yetu;

Huyaweka mataifa chini ya miguu yetu.+

 4 Hutuchagulia urithi wetu,+

Fahari ya Yakobo, ambaye anampenda.+ (Sela)

 5 Mungu amepanda juu kwa kelele za shangwe;

Yehova, kwa sauti ya pembe.*

 6 Mwimbieni Mungu sifa,* mwimbieni sifa.

Mwimbieni sifa Mfalme wetu, mwimbieni sifa.

 7 Kwa maana Mungu ni Mfalme wa dunia yote;+

Mwimbieni sifa, na mwonyeshe ufahamu.

 8 Mungu amekuwa Mfalme juu ya mataifa.+

Mungu huketi kwenye kiti chake kitakatifu cha ufalme.

 9 Viongozi wa mataifa wamekusanyika pamoja

Pamoja na watu wa Mungu wa Abrahamu.

Kwa maana watawala wa dunia ni wa* Mungu.

Amekwezwa sana.+

Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+

48 Yehova ni mkuu na anastahili kabisa kusifiwa

Katika jiji la Mungu wetu, katika mlima wake mtakatifu.

 2 Urefu wake unavutia, shangwe ya dunia yote,+

Ni Mlima Sayuni ulio mbali sana kaskazini,

Jiji la Mfalme Mkuu.+

 3 Katika minara yake yenye ngome,

Mungu ametangaza kwamba yeye ni kimbilio salama.*+

 4 Kwa maana tazama! wafalme wamekusanyika;*

Wamesonga mbele pamoja.

 5 Walipoliona, walishangaa.

Wakashikwa na wasiwasi na kukimbia kwa hofu.

 6 Wakaanza kutetemeka wakiwa huko,

Wakashikwa na uchungu kama wa mwanamke anayezaa.

 7 Kwa upepo wa mashariki unavunjavunja meli za Tarshishi.

 8 Mambo tuliyosikia, tumejionea wenyewe

Katika jiji la Yehova wa majeshi, katika jiji la Mungu wetu.

Mungu ataliimarisha kabisa milele.+ (Sela)

 9 Tunautafakari upendo wako mshikamanifu, Ee Mungu,+

Katika hekalu lako.

10 Kama jina lako, Ee Mungu, sifa yako

Hufika mpaka kwenye miisho ya dunia.+

Mkono wako wa kuume umejaa uadilifu.+

11 Mlima Sayuni+ na ushangilie,

Miji ya Yuda na ishangilie,* kwa sababu ya hukumu zako.+

12 Pigeni mwendo kuzunguka Sayuni; lizungukeni pande zote;

Hesabuni minara yake.+

13 Wekeni mioyo yenu juu ya maboma yake.*+

Kagueni minara yake yenye ngome,

Ili msimulie vizazi vijavyo kulihusu.

14 Kwa maana Mungu huyu ni Mungu wetu+ milele na milele.

Yeye mwenyewe atatuongoza kwa umilele wote.*+

Kwa kiongozi. Muziki wa wana wa Kora.+

49 Sikieni hili, enyi mataifa yote.

Sikilizeni, enyi wakaaji wote wa ulimwengu,*

 2 Wakubwa kwa wadogo,*

Matajiri na pia maskini.

 3 Kinywa changu mwenyewe kitasema maneno ya hekima,

Na kutafakari kwa moyo wangu+ kutaonyesha kwamba nina uelewaji.

 4 Nitasikiliza methali;

Nitategua kitendawili changu kwa kinubi.

 5 Kwa nini niogope nyakati za taabu,+

Ninapozungukwa na uovu wa* wale wanaojaribu kunipindua?

 6 Wale wanaotumaini mali zao+

Na kujigamba kuhusu utajiri wao mwingi,+

 7 Hakuna yeyote kati yao anayeweza kamwe kumkomboa ndugu yake

Wala kumpa Mungu fidia kwa ajili yake,+

 8 (Bei ya fidia* kwa ajili ya uhai wao* ni yenye thamani sana

Hivi kwamba hawawezi kamwe kulipa);

 9 Ili kwamba aishi milele asilione shimo.*+

10 Anaona kwamba hata watu wenye hekima hufa;

Wapumbavu na wasiotumia akili huangamia pamoja,+

Nao hulazimika kuwaachia wengine mali zao.+

11 Ndani yao wanatamani nyumba zao zidumu milele,

Mahema yao kizazi baada ya kizazi.

Wameyaita mashamba yao kwa majina yao.

12 Lakini mwanadamu, ingawa anaheshimiwa, hataendelea kuishi;+

Yeye si bora kuliko wanyama wanaoangamia.+

13 Hiyo ndiyo njia ya wapumbavu+

Na ya wale wanaowafuata, wanaofurahia maneno yao yasiyo na maana. (Sela)

14 Kama kondoo, wamepangiwa kwenda Kaburini.*

Kifo kitawachunga;

Wanyoofu watawatawala+ asubuhi.

Kila sehemu ya mwili wao itatoweka kabisa;+

Kaburi*+ litakuwa makao yao badala ya jumba la mfalme.+

15 Lakini Mungu atanikomboa* kutoka katika nguvu za* Kaburi,*+

Kwa maana atanishika. (Sela)

16 Usiogope mtu anapotajirika,

Fahari ya nyumba yake ikiongezeka,

17 Kwa maana akifa hawezi kwenda na kitu chochote;+

Fahari yake haitashuka shimoni pamoja naye.+

18 Kwa maana wakati wa maisha yake anajipongeza mwenyewe.+

(Watu hukusifu unapopata ufanisi.)+

19 Lakini mwishowe hujiunga na kizazi cha mababu zake.

Hawataona nuru tena kamwe.

20 Mtu ambaye haelewi jambo hili, ingawa anaheshimiwa,+

Yeye si bora kuliko wanyama wanaoangamia.

Muziki wa Asafu.+

50 Mungu wa miungu, Yehova,*+ amesema;

Anaiita dunia

Kutoka mapambazuko ya jua mpaka machweo yake.*

 2 Kutoka Sayuni, ukamilifu wa uzuri,+ Mungu huangaza.

 3 Mungu wetu atakuja na hawezi kunyamaza.+

Mbele zake kuna moto unaoteketeza kabisa,+

Na dhoruba kali inamzunguka pande zote.+

 4 Anaziita mbingu zilizo juu na pia dunia,+

Ili awahukumu watu wake:+

 5 “Nikusanyieni washikamanifu wangu,

Wale wanaofanya agano pamoja nami kwa dhabihu.”+

 6 Mbingu zinatangaza uadilifu wake,

Kwa maana Mungu mwenyewe ni Mwamuzi.+ (Sela)

 7 “Sikilizeni, enyi watu wangu, nami nitaongea;

Israeli, nitatoa ushahidi dhidi yako.+

Mimi ni Mungu, Mungu wako.+

 8 Siwakaripii kwa sababu ya dhabihu zenu,

Wala kwa sababu ya dhabihu zenu nzima za kuteketezwa ambazo daima ziko mbele zangu.+

 9 Sihitaji kuchukua ng’ombe dume katika nyumba yako,

Wala mbuzi* katika mazizi yako.+

10 Kwa maana kila mnyama wa mwituni ni wangu,+

Hata wanyama walio juu ya milima elfu moja.

11 Ninamjua kila ndege wa milimani;+

Wanyama wasio na idadi wa mbugani ni wangu.

12 Ningekuwa na njaa, nisingekwambia,

Kwa maana nchi inayozaa na kila kitu kilichomo ni changu.+

13 Je, nitakula nyama ya ng’ombe dume

Na kunywa damu ya mbuzi?+

14 Toa shukrani zikiwa dhabihu yako kwa Mungu,+

Na utimize nadhiri zako kwa Aliye Juu Zaidi;+

15 Nililie wakati wa taabu.+

Nitakuokoa, nawe utanitukuza.”+

16 Lakini Mungu atamwambia mwovu:

“Una haki gani ya kusimulia masharti yangu+

Au kuongea kuhusu agano langu?+

17 Kwa maana unachukia nidhamu,*

Nawe unaendelea kuyageuzia mgongo maneno yangu.*+

18 Unapomwona mwizi, unapendezwa naye,*+

Nawe unashirikiana na wazinzi.

19 Unatumia kinywa chako kueneza mabaya,

Na udanganyifu umeshikamana na ulimi wako.+

20 Unaketi na kumsema vibaya ndugu yako mwenyewe;+

Unafunua makosa ya* mwana wa mama yako mwenyewe.

21 Ulipofanya mambo hayo, niliendelea kunyamaza,

Kwa hiyo ukafikiri kwamba nitakuwa kama wewe.

Lakini sasa nitakukaripia,

Nami nitatangaza kesi yangu dhidi yako.+

22 Tafadhali, zingatieni jambo hili, ninyi mnaomsahau Mungu,+

Nisije nikawararua vipandevipande asiwepo yeyote wa kuwaokoa.

23 Yule anayetoa shukrani kuwa dhabihu yake ananitukuza,+

Na yule anayefuata njia iliyowekwa,

Nitamfanya aone wokovu wa Mungu.”+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi, nabii Nathani alipokuja kwake baada ya Daudi kulala na Bath-sheba.+

51 Ee Mungu, nionyeshe kibali kulingana na upendo wako mshikamanifu.+

Yafute kabisa makosa yangu kulingana na rehema zako nyingi.+

 2 Nioshe kabisa kutoka katika kosa langu,+

Na unisafishe kutoka katika dhambi yangu.+

 3 Kwa maana ninajua vizuri makosa yangu,

Na dhambi yangu iko mbele yangu* daima.+

 4 Dhidi yako wewe—wewe zaidi ya wote*—nimetenda dhambi;+

Nimetenda yaliyo mabaya machoni pako.+

Kwa hiyo, wewe ni mwadilifu unapoongea,

Wewe ni mwenye haki katika hukumu yako.+

 5 Tazama! Nilizaliwa nikiwa na hatia ya kosa,

Na mama yangu alinichukua mimba katika dhambi.*+

 6 Tazama! Unapendezwa na ukweli katika utu wa ndani;+

Ufundishe utu wangu wa ndani kabisa* hekima ya kweli.

 7 Nisafishe kutoka katika dhambi yangu kwa hisopo, ili niwe safi;+

Nioshe, ili niwe mweupe kuliko theluji.+

 8 Acha nisikie sauti za shangwe na furaha,

Ili mifupa uliyoiponda ishangilie.+

 9 Ugeuze uso wako* mbali na dhambi zangu,+

Na uyafutilie mbali* makosa yangu yote.+

10 Umba moyo safi ndani yangu, Ee Mungu,+

Na uweke roho mpya ndani yangu,+ iliyo imara.

11 Usinitupe kutoka mbele zako;*

Wala usiniondolee roho yako takatifu.

12 Nirudishie shangwe ya wokovu wako;+

Chochea ndani yangu utayari wa kukutii.*

13 Nitawafundisha wakosaji njia zako,+

Ili watenda dhambi wakurudie.

14 Niokoe kutoka katika hatia ya damu,+ Ee Mungu, Mungu wa wokovu wangu,+

Ili ulimi wangu utangaze uadilifu wako kwa shangwe.+

15 Ee Yehova, ifungue midomo yangu,

Ili kinywa changu kitangaze sifa yako.+

16 Kwa maana hutaki dhabihu—la sivyo ningeitoa;+

Hupendezwi na dhabihu nzima ya kuteketezwa.+

17 Dhabihu zinazompendeza Mungu ni roho iliyovunjika;

Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaukataa.*+

18 Kwa nia yako njema litendee jiji la Sayuni jambo jema;

Zijenge kuta za Yerusalemu.

19 Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za uadilifu,

Dhabihu za kuteketezwa na matoleo mazima;

Kisha ng’ombe dume watatolewa kwenye madhabahu yako.+

Kwa kiongozi. Maskili.* Wa Daudi, Doegi Mwedomu alipokuja na kumwambia Sauli kwamba Daudi alikuwa ameenda kwenye nyumba ya Ahimeleki.+

52 Kwa nini unajigamba kuhusu matendo yako maovu, ewe mwenye nguvu?+

Upendo mshikamanifu wa Mungu unadumu mchana kutwa.+

 2 Ulimi wako, wenye makali kama wembe,+

Hupanga madhara na kutunga mambo ya udanganyifu.+

 3 Unapenda uovu kuliko mema,

Kusema uwongo kuliko kusema ukweli. (Sela)

 4 Unapenda kila neno linalodhuru,

Ewe ulimi mdanganyifu!

 5 Ndiyo sababu Mungu atakubomoa milele na milele;+

Atakunyakua na kukurarua kutoka katika hema lako;+

Atakung’oa kutoka katika nchi ya walio hai.+ (Sela)

 6 Waadilifu wataona jambo hilo na kujawa na woga,+

Nao watamcheka.+

 7 “Huyu ndiye mwanamume ambaye hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake,*+

Lakini aliutumaini utajiri wake mwingi+

Na kutegemea* njama zake mwenyewe za uovu.”*

 8 Lakini mimi nitakuwa kama mzeituni wenye majani mengi katika nyumba ya Mungu;

Ninautumaini upendo mshikamanifu wa Mungu,+ milele na milele.

 9 Nitakusifu milele kwa sababu umechukua hatua;+

Mbele ya washikamanifu wako,

Nitalitumaini jina lako,+ kwa maana ni jema.

Kwa kiongozi; katika mtindo wa Mahalathi.* Maskili.* Wa Daudi.

53 Mpumbavu* husema moyoni mwake:

“Hakuna Yehova.”+

Matendo yao maovu yamepotoka na yanachukiza;

Hakuna yeyote anayetenda mema.+

 2 Lakini Mungu anawatazama wanadamu kutoka mbinguni+

Ili aone ikiwa kuna yeyote aliye na ufahamu, ikiwa kuna yeyote anayemtafuta Yehova.+

 3 Wote wamekengeuka;

Wote wamepotoka.

Hakuna yeyote anayetenda mema,

Hakuna hata mmoja.+

 4 Je, hakuna mtenda maovu yeyote anayeelewa?

Wanawala watu wangu kwa pupa kana kwamba wanakula mkate.

Hawamwiti Yehova.+

 5 Lakini watajawa na hofu kubwa,

Hofu ambayo hawajawahi kamwe kuwa nayo,*

Kwa maana Mungu ataitawanya mifupa ya wale wanaowashambulia ninyi.*

Mtawaaibisha, kwa maana Yehova amewakataa wao.

 6 Laiti wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+

Yehova anapowakusanya tena watu wake waliotekwa,

Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi.

Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Maskili.* Wa Daudi, Wazifu walipokuja na kumwambia Sauli: “Daudi anajificha miongoni mwetu.”+

54 Ee Mungu, niokoe kwa jina lako,+

Na unitetee*+ kwa nguvu zako.

 2 Ee Mungu, isikie sala yangu;+

Sikiliza maneno ya kinywa changu.

 3 Kwa maana wageni wanainuka dhidi yangu,

Na wanaume wakatili wanatafuta uhai wangu.*+

Hawamheshimu Mungu.*+ (Sela)

 4 Tazama! Mungu ni msaidizi wangu;+

Yehova yuko pamoja na wale wanaonitegemeza.

 5 Utawalipa maadui wangu+ uovu wao wenyewe;

Katika uaminifu wako, waangamize.*+

 6 Nitakutolea dhabihu+ kwa hiari.

Nitalisifu jina lako, Ee Yehova, kwa maana ni jema.+

 7 Kwa maana wewe huniokoa kutoka katika kila taabu,+

Nami nitawatazama maadui wangu wakishindwa.+

Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Maskili.* Wa Daudi.

55 Sikiliza sala yangu, Ee Mungu,+

Na usiipuuze sala yangu ya kuomba rehema.*+

 2 Nisikilize na unijibu.+

Hangaiko langu linanisumbua,+

Nami nimefadhaika

 3 Kwa sababu ya mambo ambayo adui anasema

Na mkazo kutoka kwa mwovu.

Kwa maana wananirundikia taabu,

Na kwa hasira wana chuki kali kunielekea.+

 4 Moyo wangu una maumivu makali,+

Na hofu ya kifo inanilemea.+

 5 Hofu na kutetemeka hunijia,

Na woga hunishika.

 6 Daima ninasema: “Laiti ningekuwa na mabawa kama ya njiwa!

Ningeruka mbali na kukaa kwa usalama.

 7 Tazama! Ningekimbia na kwenda mbali sana.+

Ningekaa nyikani.+ (Sela)

 8 Ningeenda haraka mahali pa kujificha

Mbali na upepo mkali, mbali na dhoruba.”

 9 Wavuruge, Ee Yehova, na uvuruge mipango yao,*+

Kwa maana nimeona ukatili na mizozo jijini.

10 Usiku na mchana wanazunguka juu ya kuta zake;

Ndani yake kuna fitina na taabu.+

11 Uharibifu uko ndani yake;

Ukandamizaji na udanganyifu hauondoki kamwe katika uwanja wake.+

12 Kwa maana si adui anayenidhihaki;+

La sivyo ningevumilia.

Si adui aliyeinuka dhidi yangu;

La sivyo ningeweza kujificha.

13 Lakini ni wewe, mwanadamu kama mimi,*+

Rafiki yangu mwenyewe ninayemjua vizuri.+

14 Tulikuwa tukifurahia pamoja urafiki wa karibu sana;

Katika nyumba ya Mungu tulikuwa tukitembea pamoja na umati.

15 Na wapatwe na maangamizi!+

Na washuke Kaburini* wakiwa hai;

Kwa maana uovu hukaa miongoni mwao na ndani yao.

16 Lakini mimi, nitamlilia Mungu,

Na Yehova ataniokoa.+

17 Jioni na asubuhi na adhuhuri, ninahangaika na kulia kwa uchungu,*+

Naye huisikia sauti yangu.+

18 Ataniokoa* na kunipa amani mbali na wale wanaopigana nami,

Kwa maana umati huja kunishambulia.+

19 Mungu atasikia na kukabiliana nao,+

Yule anayeketi kwenye kiti cha ufalme tangu zamani.+ (Sela)

Watakataa kubadilika,

Wale ambao hawajamwogopa Mungu.+

20 Aliwashambulia* walio na amani pamoja naye;+

Alilivunja agano lake.+

21 Maneno yake ni laini kuliko siagi,+

Lakini mzozo umo moyoni mwake.

Maneno yake ni laini kuliko mafuta,

Lakini ni panga zilizochomolewa.+

22 Mtupie Yehova mzigo wako,+

Naye atakutegemeza.+

Hataruhusu kamwe mwadilifu aanguke.*+

23 Lakini wewe, Ee Mungu, utawashusha chini kwenye shimo lenye kina kabisa.+

Watu hao wenye hatia ya damu ambao ni wadanganyifu hawataishi nusu ya siku zao.+

Lakini mimi, nitakutumaini wewe.

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Njiwa Mnyamavu Aliye Mbali.” Wa Daudi. Miktamu.* Wafilisti walipomkamata kule Gathi.+

56 Nionyeshe kibali, Ee Mungu, kwa sababu mwanadamu anayeweza kufa ananishambulia.*

Mchana kutwa wanaendelea kunipiga vita na kunikandamiza.

 2 Maadui wangu wanajaribu mchana kutwa kuning’ata;

Wengi wanapigana nami kwa kiburi.

 3 Ninapoogopa,+ ninakutumaini wewe.+

 4 Katika Mungu—ninayelisifu neno lake—

Katika Mungu ninaweka tumaini langu; siogopi.

Mwanadamu ambaye ni duni tu atanifanya* nini?+

 5 Mchana kutwa wanavuruga mambo yangu;

Jambo pekee wanalowazia ni kunidhuru.+

 6 Wanajificha ili wanishambulie,

Wanachunguza kila hatua yangu,+

Wakikusudia kuuondoa uhai wangu.+

 7 Wakatae kwa sababu ya uovu wao.

Yaangushe mataifa kwa hasira yako, Ee Mungu.+

 8 Unafuatia kutangatanga kwangu.+

Yakusanye machozi yangu katika kiriba chako cha ngozi.+

Je, hayajaandikwa katika kitabu chako?+

 9 Maadui wangu watakimbia siku nitakayoomba msaada.+

Nina hakika kuhusu jambo hili: Mungu yuko upande wangu.+

10 Katika Mungu—ninayelisifu neno lake—

Katika Yehova—ninayelisifu neno lake—

11 Katika Mungu ninaweka tumaini langu; siogopi.+

Mwanadamu ambaye ni duni tu atanifanya nini?+

12 Nimefungwa na nadhiri nilizokuwekea, Ee Mungu;+

Nitakutolea matoleo ya shukrani.+

13 Kwa maana umeniokoa kutoka katika kifo+

Na kuizuia miguu yangu isijikwae,+

Ili nitembee mbele za Mungu katika nuru ya walio hai.+

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Usiharibu.” Wa Daudi. Miktamu.* Alipomkimbia Sauli na kuingia pangoni.+

57 Nionyeshe kibali, Ee Mungu, nionyeshe kibali,

Kwa maana ninakukimbilia,+

Ninakimbilia kivuli cha mabawa yako mpaka matatizo haya yapite.+

 2 Ninamlilia Mungu Aliye Juu Zaidi,

Mungu wa kweli, anayeyakomesha kwa ajili yangu.

 3 Atatuma msaada kutoka mbinguni na kuniokoa.+

Atamtamausha yule anayejaribu kuning’ata. (Sela)

Mungu atatuma upendo wake mshikamanifu na uaminifu wake.+

 4 Nimezungukwa na simba;+

Nimelazimika kulala miongoni mwa watu wanaotaka kuninyafua,

Ambao meno yao ni mikuki na mishale

Na ambao ulimi wao ni upanga mkali.+

 5 Ukwezwe juu ya mbingu, Ee Mungu;

Utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+

 6 Wameutayarisha wavu ili kuinasa miguu yangu;+

Taabu zimenifanya niiname chini.+

Wamechimba shimo mbele yangu,

Lakini wao wenyewe wameanguka ndani yake.+ (Sela)

 7 Moyo wangu uko imara, Ee Mungu,+

Moyo wangu uko imara.

Nitaimba na kupiga muziki.

 8 Amka, utukufu wangu.

Amka, Ee kinanda; nawe pia, Ee kinubi.

Nitayaamsha mapambazuko.+

 9 Nitakusifu miongoni mwa mataifa, Ee Yehova;+

Nitakuimbia sifa* miongoni mwa mataifa.+

10 Kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mkubwa, uko juu kama mbingu,+

Na uaminifu wako, unafika mpaka angani.

11 Ukwezwe juu ya mbingu, Ee Mungu;

Utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Usiharibu.” Wa Daudi. Miktamu.*

58 Je, mnaweza kuzungumza kuhusu uadilifu wakati mmenyamaza?+

Je, mnaweza kuhukumu kwa unyoofu, enyi wanadamu?+

 2 Badala yake, mnatunga uovu moyoni mwenu,+

Na mikono yenu inatawanya ukatili nchini.+

 3 Waovu wanakengeuka* tangu kuzaliwa;

Ni wakaidi, waongo tangu wanapozaliwa.

 4 Sumu yao ni kama sumu ya nyoka;+

Wao ni viziwi kama swila anayeziba sikio lake.

 5 Hataisikiliza sauti ya wanaomchezesha,

Hata wafanye uchawi kwa ustadi kadiri gani.

 6 Ee Mungu, yavunje meno yao vinywani mwao!

Yavunje mataya ya hawa simba,* Ee Yehova!

 7 Na watoweke kama maji yanayotiririka na kwenda zake.

Mungu na aukunje upinde wake na kuwaangusha kwa mishale yake.

 8 Na wawe kama konokono anayeyeyuka anapotembea;

Kama mtoto anayefia tumboni mwa mwanamke, mtoto asiyeona jua kamwe.

 9 Kabla vyungu vyenu vya kupikia havijapata moto wa kuni za mkwamba,

Atazifagilia mbali kuni zenye unyevu na zinazowaka moto, kama kwa kimbunga.+

10 Mwadilifu atashangilia kwa sababu ameona kisasi;+

Miguu yake italowa damu ya waovu.+

11 Kisha watu watasema: “Kwa hakika kuna thawabu kwa ajili ya mwadilifu.+

Kwa hakika kuna Mungu anayehukumu duniani.”+

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Usiharibu.” Wa Daudi. Miktamu.* Sauli alipowatuma watu waichunguze nyumba ya Daudi* ili wamuue.+

59 Niokoe kutoka kwa maadui wangu, Ee Mungu wangu;+

Nilinde kutoka kwa wale wanaoinuka dhidi yangu.+

 2 Niokoe kutoka kwa wale wanaotenda uovu,

Na uniokoe kutoka kwa watu wakatili.*

 3 Tazama! Wananivizia;+

Wanaume wenye nguvu wananishambulia

Lakini si kwa sababu nimeasi au kutenda dhambi,+ Ee Yehova.

 4 Ingawa sikutenda kosa lolote, wanakimbia na kujitayarisha kunishambulia.

Inuka ninapokuita, uone.

 5 Kwa maana wewe, Ee Yehova Mungu wa majeshi, ni Mungu wa Israeli.+

Amka uyakazie uangalifu mataifa yote.

Usiwaonyeshe rehema wasaliti wowote wenye nia ya kudhuru.+ (Sela)

 6 Wanarudi kila jioni;+

Wanabweka* kama mbwa+ na kuzungukazunguka jijini.+

 7 Tazama kinachomwagika* kutoka katika kinywa chao;

Midomo yao ni kama panga,+

Kwa maana wanauliza: “Ni nani anayesikiliza?”+

 8 Lakini wewe, Ee Yehova, utawacheka;+

Utayadhihaki mataifa yote.+

 9 Ee Nguvu zangu, nitaendelea kukutarajia;+

Kwa maana Mungu ni kimbilio langu salama.*+

10 Mungu anayenitendea kwa upendo mshikamanifu atanisaidia;+

Mungu ataniwezesha niwatazame maadui wangu wakishindwa.+

11 Usiwaue, ili watu wangu wasisahau.

Kwa nguvu zako wafanye watangetange;

Waangushe, Ee Yehova, ngao yetu.+

12 Kwa sababu ya dhambi ya kinywa chao, neno la midomo yao,

Kiburi chao na kiwanase,+

Kwa sababu ya matusi na udanganyifu wanaosema.

13 Waangamize kwa hasira yako kali;+

Waangamize kabisa, ili wasiwepo tena;

Wafanye wajue kwamba Mungu anatawala katika Yakobo na mpaka kwenye miisho ya dunia.+ (Sela)

14 Acha warudi jioni;

Acha wabweke* kama mbwa na kuzungukazunguka jijini.+

15 Acha watangetange wakitafuta chakula;+

Usiwaruhusu washibe au kupata makao.

16 Lakini mimi, nitaimba kuhusu nguvu zako;+

Asubuhi nitatangaza kwa shangwe kuhusu upendo wako mshikamanifu.

Kwa maana wewe ni kimbilio langu salama+

Na mahali pangu pa kukimbilia wakati wa taabu.+

17 Ee Nguvu zangu, nitakuimbia sifa,*+

Kwa maana wewe Mungu ni kimbilio langu salama, Mungu unayenitendea kwa upendo mshikamanifu.+

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Yungiyungi la Kikumbusho.” Miktamu.* Wa Daudi. Wa kufundisha. Alipopigana na Aram-naharaimu na Aram-Soba, kisha Yoabu akarudi na kuwaua Waedomu 12,000 katika Bonde la Chumvi.+

60 Ee Mungu, ulitukataa; ulipenya katika vikosi vyetu vya ulinzi.+

Ulitukasirikia; lakini sasa tupokee tena!

 2 Uliifanya dunia itetemeke; uliipasua ikafunguka.

Ziba nyufa zake, kwa maana inaporomoka.

 3 Uliwafanya watu wako wateseke.

Ulitufanya tunywe divai inayosababisha tuyumbeyumbe.+

 4 Wape* ishara wale wanaokuogopa

Wakimbie na kuukwepa upinde. (Sela)

 5 Ili wapendwa wako waokolewe,

Tuokoe kwa mkono wako wa kuume na utujibu.+

 6 Mungu ameongea katika utakatifu wake:*

“Nitashangilia, nitawagawia Shekemu kuwa urithi,+

Nami nitawapimia Bonde la* Sukothi.+

 7 Gileadi ni yangu, na Manase ni yangu,+

Na Efraimu ni kofia ya kukinga* kichwa changu;

Yuda ni fimbo yangu ya kiongozi.+

 8 Moabu ni beseni langu la kuogea.+

Nitatupa kiatu changu juu ya Edomu.+

Nitapaza sauti kwa ushindi juu ya Ufilisti.”+

 9 Ni nani atakayenipeleka kwenye jiji lililozingirwa?*

Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?+

10 Je, si wewe, Ee Mungu, ambaye umetukataa,

Mungu wetu, ambaye haendi tena na majeshi yetu?+

11 Tusaidie katika taabu yetu,

Kwa maana wokovu kutoka kwa wanadamu hauna faida yoyote.+

12 Kwa msaada wa Mungu tutapata nguvu,+

Naye atawakanyagia chini maadui wetu.+

Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Wa Daudi.

61 Ee Mungu, sikia kilio changu cha kuomba msaada.

Sikiliza sala yangu.+

 2 Nitakulilia kwa sauti kutoka katika miisho ya dunia

Ninapovunjika moyo.*+

Niongoze kwenye mwamba ulio juu kuliko mimi.+

 3 Kwa maana wewe ni kimbilio langu,

Mnara ulio imara unaonilinda dhidi ya adui.+

 4 Nitakuwa mgeni katika hema lako milele;+

Nitakimbilia katika kivuli cha mabawa yako.+ (Sela)

 5 Kwa maana wewe, Ee Mungu, umesikia nadhiri zangu.

Umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.+

 6 Utamwongezea mfalme siku za maisha yake,+

Na miaka yake itatoka kizazi hadi kizazi.

 7 Ataketi kwenye kiti cha ufalme* milele mbele za Mungu;+

Mpe upendo wako mshikamanifu na uaminifu, ili vimlinde.+

 8 Kisha nitaliimbia sifa* jina lako milele+

Ninapotimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.+

Kwa kiongozi; wa Yeduthuni.* Muziki wa Daudi.

62 Kwa kweli, ninamngojea Mungu kimyakimya.

Wokovu wangu unatoka kwake.+

 2 Kwa kweli, yeye ni mwamba wangu na wokovu wangu, kimbilio langu salama;*+

Kamwe, sitatikiswa sana.+

 3 Mtaendelea mpaka lini kumshambulia mtu ili kumuua?+

Ninyi nyote ni hatari kama ukuta ulioinama, ukuta wa mawe unaokaribia kuanguka.*

 4 Kwa maana wanashauriana ili kumwangusha kutoka katika cheo chake cha juu;*

Wanafurahia kusema uwongo.

Kwa kinywa chao wanabariki, lakini ndani yao wanalaani.+ (Sela)

 5 Kwa kweli, ninamngojea* Mungu kimyakimya+

Kwa sababu tumaini langu linatoka kwake.+

 6 Kwa kweli, yeye ni mwamba wangu na wokovu wangu, kimbilio langu salama;

Sitatikiswa kamwe.+

 7 Wokovu wangu na utukufu wangu unamtegemea Mungu.

Mwamba wangu imara, kimbilio langu, ni Mungu.+

 8 Mtumainini nyakati zote, enyi watu.

Mwageni mioyo yenu mbele zake.+

Mungu ni kimbilio letu.+ (Sela)

 9 Wanadamu ni pumzi tu,

Wana wa binadamu ni njozi ya uwongo.+

Wanapowekwa pamoja kwenye mizani, ni wepesi kuliko pumzi.+

10 Msitegemee upunjaji

Wala kuwa na matumaini ya uwongo katika unyang’anyi.

Mali zako zikiongezeka, usizikazie moyoni mwako.+

11 Mungu ameongea mara moja, mara mbili nimelisikia jambo hili:

Kwamba nguvu ni za Mungu.+

12 Pia upendo mshikamanifu ni wako, Ee Yehova,+

Kwa maana unamlipa kila mtu kulingana na matendo yake.+

Muziki wa Daudi, alipokuwa katika nyika ya Yuda.+

63 Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, ninaendelea kukutafuta.+

Nina kiu kwa ajili yako.+

Ninazimia* kwa sababu ninakutamani

Katika nchi kame iliyokauka, ambayo haina maji.+

 2 Kwa hiyo nimekutazama mahali patakatifu;

Nimeziona nguvu zako na utukufu wako.+

 3 Kwa sababu upendo wako mshikamanifu ni bora kuliko uhai,+

Midomo yangu mwenyewe itakutukuza.+

 4 Basi nitakusifu maisha yangu yote;

Katika jina lako nitaiinua mikono yangu.

 5 Nimeridhika na fungu bora ambalo ni zuri kabisa,*

Kwa hiyo kinywa changu kitakusifu kwa midomo yenye shangwe.+

 6 Ninakukumbuka wewe nikiwa kitandani mwangu;

Ninatafakari kukuhusu katika makesha ya usiku.+

 7 Kwa maana wewe ni msaidizi wangu,+

Nami ninapaza sauti kwa shangwe katika kivuli cha mabawa yako.+

 8 Ninashikamana nawe;

Mkono wako wa kuume hunishika kwa nguvu.+

 9 Lakini wale wanaotaka kuniua*

Watashuka katika sehemu zenye kina zaidi za dunia.

10 Watatiwa katika nguvu za upanga;

Watakuwa chakula cha mbwamwitu.*

11 Lakini mfalme atashangilia kwa sababu ya Mungu.

Kila mtu anayeapa katika jina la Mungu atashangilia,*

Kwa maana kinywa cha wale wanaosema uwongo kitanyamazishwa.

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

64 Ee Mungu, sikia sauti yangu ninapokusihi.+

Ulinde uhai wangu kutokana na hofu ya adui.

 2 Nikinge kutokana na njama za siri za waovu,+

Kutoka kwa umati wa watenda maovu.

 3 Wanaunoa ulimi wao kama upanga;

Wanayalenga maneno yao ya ukatili kama mishale,

 4 Ili wampige mtu asiye na hatia wakiwa mafichoni;

Wanampiga ghafla, bila kuogopa.

 5 Wanashikamana sana na kusudi lao ovu;*

Wanazungumzia jinsi ya kuficha mitego yao.

Wanasema: “Ni nani atakayeiona?”+

 6 Wanatafuta njia mpya za kutenda uovu;

Wanatunga kwa siri mbinu zao za ujanja;+

Fikira zilizo ndani ya moyo wa kila mmoja wao hazieleweki kamwe.

 7 Lakini Mungu atawapiga mishale;+

Watajeruhiwa kwa ghafla na mshale.

 8 Ulimi wao wenyewe utasababisha waanguke;+

Wote wanaowatazama watatikisa kichwa.

 9 Ndipo watu wote wataogopa,

Nao watatangaza mambo ambayo Mungu ametenda,

Nao watayafahamu matendo yake.+

10 Mwadilifu atashangilia kwa sababu ya Yehova na kumkimbilia;+

Wote walio wanyoofu moyoni watashangilia.*

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. Wimbo.

65 Ee Mungu, sifa inakungojea Sayuni;+

Tutatimiza nadhiri zetu kwako.+

 2 Ee Msikiaji wa sala, watu wa kila aina* watakujia.+

 3 Dhambi zangu zimenilemea,+

Lakini unafunika makosa yetu.+

 4 Mwenye furaha ni yule unayemchagua na kumleta karibu

Ili akae katika nyua zako.+

Tutaridhika na wema wa nyumba yako,+

Hekalu lako takatifu.*+

 5 Utatujibu kwa matendo ya uadilifu yanayoogopesha,+

Ee Mungu wa wokovu wetu;

Wewe ndiye Tegemeo la miisho yote ya dunia+

Na wa wale walio mbali ng’ambo ya bahari.

 6 Uliimarisha kabisa milima kwa nguvu zako;

Umevaa uwezo.+

 7 Unazituliza bahari zilizochafuka,+

Kishindo cha mawimbi yake na msukosuko wa mataifa.+

 8 Wale wanaokaa sehemu za mbali wataogopeshwa na ishara zako;+

Utawafanya wale wanaoishi upande wa mashariki mpaka upande wa magharibi wapaze sauti kwa shangwe.

 9 Unaitunza dunia,

Unaifanya izae kwa wingi* na kuitajirisha sana.+

Kijito kinachotoka kwa Mungu kimejaa maji;

Unawapa nafaka,+

Kwa maana hivyo ndivyo ulivyoitayarisha dunia.

10 Unajaza maji katika mitaro yake na kusawazisha udongo wake uliolimwa;*

Unailainisha kwa manyunyu ya mvua; unabariki mimea yake.+

11 Unauvika mwaka taji kwa wema wako;

Vijia vyako vinafurika kwa wingi wa vitu.*+

12 Malisho ya nyikani yanaendelea kufurika,*+

Na vilima vimevishwa shangwe.+

13 Malisho yamefunikwa na makundi ya kondoo,

Na mabonde yamefunikwa* na nafaka.+

Yanapaza sauti kwa ushindi, naam, yanaimba.+

Kwa kiongozi. Wimbo. Muziki.

66 Mpazieni Mungu sauti ya ushindi, dunia yote.+

 2 Liimbieni sifa* jina lake tukufu.

Tukuzeni sifa yake.+

 3 Mwambieni Mungu: “Kazi zako zinaogopesha kwelikweli!+

Kwa sababu ya nguvu zako nyingi,

Maadui wako watajikunyata mbele zako.+

 4 Dunia yote itakuinamia;+

Watakuimbia sifa;

Wataliimbia sifa jina lako.”+ (Sela)

 5 Njooni mwone kazi za Mungu.

Mambo aliyowatendea wanadamu yanaogopesha.+

 6 Aliigeuza bahari kuwa nchi kavu;+

Walivuka mto kwa miguu.+

Huko tulishangilia kwa sababu yake.+

 7 Anatawala milele+ kwa nguvu zake.

Macho yake yanachunguza mataifa.+

Wale ambao ni wakaidi hawapaswi kujikweza.+ (Sela)

 8 Msifuni Mungu wetu, enyi mataifa,+

Sauti ya sifa yake na isikiwe.

 9 Yeye hutuhifadhi hai;*+

Haruhusu miguu yetu ijikwae.*+

10 Kwa maana umetuchunguza, Ee Mungu;+

Umetusafisha kama fedha inavyosafishwa.

11 Ulituingiza katika wavu wa kuwindia;

Ulitutwika mzigo mzito.*

12 Ulimruhusu mwanadamu anayeweza kufa apande juu yetu;*

Tulipita motoni na katika maji;

Kisha ukatuleta mahali penye kitulizo.

13 Nitaingia katika nyumba yako nikiwa na dhabihu nzima za kuteketezwa;+

Nitatimiza nadhiri zangu kwako+

14 Ambazo midomo yangu iliahidi+

Na kinywa changu kilisema nilipokuwa katika taabu.

15 Nitakutolea dhabihu za kuteketezwa za wanyama waliononeshwa

Pamoja na moshi wa dhabihu za kondoo dume.

Nitatoa ng’ombe dume pamoja na mbuzi dume. (Sela)

16 Njooni msikilize, ninyi nyote mnaomwogopa Mungu,

Nami nitawaambia mambo aliyonitendea.+

17 Nilimwita kwa kinywa changu

Na kumtukuza kwa ulimi wangu.

18 Ikiwa nilihifadhi moyoni mwangu jambo lolote linalodhuru,

Yehova hangenisikia.+

19 Lakini Mungu alinisikia;+

Aliisikiliza sala yangu.+

20 Asifiwe Mungu, ambaye hakukataa sala yangu

Wala kuninyima upendo wake mshikamanifu.

Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Muziki. Wimbo.

67 Mungu atatuonyesha kibali na kutubariki;

Atatuangazia nuru ya uso wake+ (Sela)

 2 Ili njia yako ijulikane duniani kote,+

Matendo yako ya wokovu miongoni mwa mataifa yote.+

 3 Mataifa na yakusifu wewe, Ee Mungu;

Mataifa yote na yakusifu.

 4 Mataifa na yashangilie na kupaza sauti kwa shangwe,+

Kwa maana utayahukumu mataifa kwa haki.+

Utayaongoza mataifa ya dunia. (Sela)

 5 Mataifa na yakusifu, Ee Mungu;

Mataifa yote na yakusifu wewe.

 6 Dunia itatoa mazao yake;+

Mungu, Mungu wetu, atatubariki.+

 7 Mungu atatubariki,

Na miisho yote ya dunia itamwogopa* yeye.+

Kwa kiongozi. Wa Daudi. Muziki. Wimbo.

68 Mungu na ainuke, maadui wake na watawanyike,

Wale wanaomchukia na wakimbie kutoka mbele zake.+

 2 Wapeperushe mbali kama moshi unavyopeperushwa;

Kama nta inavyoyeyuka karibu na moto,

Waovu na waangamie vivyo hivyo kutoka mbele za Mungu.+

 3 Lakini waadilifu na washangilie;+

Na wafurikwe na shangwe mbele za Mungu;

Na wafurahi na kushangilia.

 4 Mwimbieni Mungu; liimbieni sifa* jina lake.+

Mwimbieni Yule anayepanda kupitia jangwa tambarare.*

Jina lake ni Yah!*+ Shangilieni mbele zake!

 5 Baba wa mayatima na mlinzi* wa wajane+

Ni Mungu katika makao yake matakatifu.+

 6 Mungu huwapa makao walio peke yao;+

Huwaachilia huru wafungwa na kuwafanikisha.+

Lakini ni lazima watu wakaidi* waishi katika nchi iliyokauka.+

 7 Ee Mungu, ulipowaongoza* watu wako,+

Ulipopiga mwendo jangwani, (Sela)

 8 Dunia ilitetemeka;+

Mbingu zilinyesha* mvua kwa sababu ya Mungu;

Huu Mlima Sinai ulitetemeka kwa sababu ya Mungu, Mungu wa Israeli.+

 9 Ulisababisha mvua kubwa inyeshe, Ee Mungu;

Uliwatia nguvu tena watu wako waliochoka.*

10 Walikaa katika kambi yako yenye mahema;+

Kwa wema wako, uliwaandalia maskini, Ee Mungu.

11 Yehova anatoa amri;

Wanawake wanaotangaza habari njema ni jeshi kubwa.+

12 Wafalme na majeshi yao wanakimbia,+ wanakimbia!

Mwanamke anayebaki nyumbani anagawiwa nyara.+

13 Ingawa ninyi wanaume mlikuwa mkilala katikati ya mioto kambini,*

Kutakuwa na mabawa ya njiwa yaliyofunikwa kwa fedha,

Yenye manyoya ya dhahabu bora.*

14 Mweza-Yote alipowatawanya wafalme waliokuwa nchini,+

Theluji ilianguka Salmoni.*

15 Mlima wa Bashani+ ni mlima wa Mungu;*

Mlima wa Bashani ni mlima wenye vilele.

16 Enyi milima yenye vilele, kwa nini mnautazama kwa wivu,

Mlima ambao Mungu ameuchagua kuwa* makao yake?+

Kwa kweli, Yehova atakaa huko milele.+

17 Magari ya Mungu ya vita ni makumi ya maelfu, maelfu kwa maelfu.+

Yehova ametoka Sinai na kuingia mahali patakatifu.+

18 Ulipanda juu;+

Ulichukua mateka;

Ulichukua wanaume kuwa zawadi,+

Naam, hata walio wakaidi,+ ili ukae miongoni mwao, Ee Yah Mungu.

19 Na asifiwe Yehova, anayetubebea mzigo wetu kila siku,+

Mungu wa kweli wa wokovu wetu. (Sela)

20 Kwetu, Mungu wa kweli ni Mungu anayeokoa;+

Na Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu huokoa kutoka katika kifo.+

21 Naam, Mungu atapondaponda vichwa vya maadui wake,

Utosi wenye nywele wa mtu yeyote anayeendelea kuwa na* hatia.+

22 Yehova amesema: “Nitawarudisha kutoka Bashani;+

Nitawarudisha kutoka katika vilindi vya bahari,

23 Ili mguu wako ufunikwe na damu+

Na ulimi wa mbwa wako upate fungu lake kutoka kwa maadui.”

24 Wanaona misafara yako, Ee Mungu,

Misafara ya Mungu wangu, Mfalme wangu, inayoingia mahali patakatifu.+

25 Waimbaji wanatangulia mbele, wanamuziki wanaopiga vinanda wanawafuata;+

Katikati yao kuna wanawake vijana wakipiga matari.+

26 Katika umati uliokutanika,* msifuni Mungu;

Msifuni Yehova, enyi mnaotoka katika Chemchemi ya Israeli.+

27 Huko Benjamini,+ aliye mdogo zaidi, anawatiisha,

Pia wakuu wa Yuda pamoja na umati wao wenye kelele,

Wakuu wa Zabuloni, wakuu wa Naftali.

28 Mungu wako ameamuru kwamba utakuwa na nguvu.

Onyesha nguvu zako, Ee Mungu, wewe ambaye umetenda kwa niaba yetu.+

29 Kwa sababu ya hekalu lako lililo Yerusalemu,+

Wafalme watakuletea zawadi.+

30 Wakemee wanyama wa mwituni walio kwenye matete,

Kusanyiko la ng’ombe dume+ na ndama wao,

Mpaka mataifa yatakapoinama chini yakileta* vipande vya fedha.

Lakini anayatawanya mataifa yanayopenda vita.

31 Vitu vya shaba nyekundu vitaletwa kutoka* Misri;+

Kushi itafanya haraka kumpa Mungu zawadi.

32 Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu,+

Mwimbieni sifa* Yehova, (Sela)

33 Yule anayepanda mbingu ya kale kati ya mbingu.+

Tazama! Hunguruma kwa sauti yake, sauti yake yenye nguvu.

34 Tambueni nguvu za Mungu.+

Fahari yake iko juu ya Israeli,

Na nguvu zake ziko angani.*

35 Mungu anaogopesha kutoka katika mahali pake patakatifu penye utukufu.+

Yeye ni Mungu wa Israeli,

Anayewapa watu uwezo na nguvu.+

Asifiwe Mungu.

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Mayungiyungi.” Wa Daudi.

69 Niokoe, Ee Mungu, kwa maana maji yanahatarisha uhai wangu.*+

 2 Nimezama chini katika matope yenye kina, mahali pasipo na udongo mgumu.+

Nimefika katika maji yenye kina,

Na kijito kinachotiririka haraka kimenifagilia mbali.+

 3 Nimechoka kupaza sauti;+

Koo langu limekauka.

Macho yangu yamechoka nikimngojea Mungu wangu.+

 4 Wale wanaonichukia bila sababu+

Ni wengi sana kuliko nywele za kichwa changu.

Wale wanaotaka kuniangamiza,

Maadui wangu wenye hila,* wamekuwa wengi.

Nililazimishwa kurudisha kitu ambacho sikuiba.

 5 Ee Mungu, unajua upumbavu wangu,

Na hatia yangu haijafichika mbele zako.

 6 Acha wale wanaokutumaini wasiaibishwe kwa sababu yangu,

Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi.

Wale wanaokutafuta na wasifedheheshwe kwa sababu yangu,

Ee Mungu wa Israeli.

 7 Ninashutumiwa kwa sababu yako;+

Aibu imefunika uso wangu.+

 8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu,

Mgeni kwa wana wa mama yangu.+

 9 Bidii kwa ajili ya nyumba yako imenila,+

Na shutuma za wale wanaokushutumu zimeniangukia.+

10 Nilipojinyenyekeza* kwa kufunga,*

Nilishutumiwa kwa sababu hiyo.

11 Nilipoyafanya magunia kuwa mavazi yangu,

Nikawa kitu cha kudharauliwa nao.*

12 Wale wanaoketi kwenye lango la jiji huzungumza kunihusu,

Na walevi huimba juu yangu katika nyimbo zao.

13 Lakini sala yangu na ikufikie,

Ee Yehova, kwa wakati unaofaa.+

Katika upendo wako mwingi mshikamanifu, Ee Mungu,

Nijibu kwa matendo yako hakika ya wokovu.+

14 Niokoe kutoka katika matope;

Usiache nizame.

Niokoe kutoka kwa wale wanaonichukia

Na kutoka katika maji yenye kina.+

15 Usiache mafuriko yenye kasi yanifagilie mbali,+

Wala kilindi kinimeze,

Wala kisima kifumbe* kinywa chake juu yangu.+

16 Nijibu, Ee Yehova, kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mwema.+

Nigeukie kulingana na rehema zako nyingi,+

17 Wala usimfiche mtumishi wako uso wako.+

Nijibu haraka, kwa maana ninataabika.+

18 Nikaribie uniokoe;*

Nikomboe kwa sababu ya maadui wangu.

19 Unajua shutuma yangu na aibu yangu na fedheha yangu.+

Unawaona maadui wangu wote.

20 Shutuma imeuvunja moyo wangu, na jeraha haliwezi kuponywa.*

Nilitarajia kuhurumiwa, lakini sikuhurumiwa hata kidogo,+

Nilitarajia kupata watu wa kunifariji, lakini sikupata yeyote.+

21 Lakini walinipa sumu* kuwa chakula,+

Na wakanipa siki ninywe ili nikate kiu.+

22 Meza yao na iwe mtego kwao,

Na ufanisi wao uwe kitu cha kuwanasa.+

23 Acha macho yao yatiwe giza wasiweze kuona,

Na ufanye viuno vyao vitetemeke daima.

24 Wamwagie ghadhabu yako,*

Na hasira yako inayowaka iwapate.+

25 Kambi yao* na iwe ukiwa;

Mahema yao yasiwe na mkaaji yeyote.+

26 Kwa maana wanamfuatia yule uliyempiga,

Nao huendelea kusimulia kuhusu maumivu ya wale uliowajeruhi.

27 Ongeza hatia zaidi juu ya hatia yao,

Nao wasiwe na fungu lolote katika uadilifu wako.

28 Na wafutwe kutoka katika kitabu cha walio hai,*+

Na wasiorodheshwe miongoni mwa waadilifu.+

29 Lakini ninateseka, nami nina maumivu.+

Ee Mungu, nguvu zako za kuokoa na zinilinde.

30 Nitaliimbia sifa jina la Mungu,

Nami nitamtukuza kwa kutoa shukrani.

31 Jambo hilo litampendeza Yehova kuliko ng’ombe dume,

Kuliko ng’ombe dume mchanga mwenye pembe na kwato.+

32 Wapole wataona jambo hilo na kushangilia.

Mioyo yenu na ihuishwe, ninyi mnaomtafuta Mungu.

33 Kwa maana Yehova anawasikiliza maskini,+

Naye hatawadharau watu wake waliotekwa.+

34 Mbingu na dunia na zimsifu,+

Bahari na kila kitu kinachoogelea ndani yake.

35 Kwa maana Mungu ataliokoa Sayuni+

Naye atayajenga upya majiji ya Yuda,

Nao watakaa humo na kuimiliki.*

36 Wazao wa watumishi wake watairithi,+

Na wale wanaolipenda jina lake+ wataishi humo.

Kwa kiongozi. Wa Daudi, wa kukumbusha.

70 Ee Mungu, niokoe;

Ee Yehova, njoo haraka unisaidie.+

 2 Wale wanaotaka kuniua*

Na waaibishwe na kufedheheshwa.

Wale wanaofurahia msiba wangu

Na wakimbie kwa aibu.

 3 Wale wanaosema: “Aha! Aha!”

Na wakimbizwe kwa aibu.

 4 Lakini acha wale wanaokutafuta

Wafurahi na kushangilia kwa sababu yako.+

Wale wanaopenda matendo yako ya wokovu na waseme daima:

“Mungu na atukuzwe!”

 5 Lakini sina uwezo, nami ni maskini;+

Ee Mungu, tenda haraka kwa niaba yangu.+

Wewe ni msaidizi wangu na mwokozi wangu.+

Ee Yehova, usikawie.+

71 Nimekukimbilia wewe, Ee Yehova.

Usiache niaibishwe kamwe.+

 2 Niokoe na kuninusuru kwa uadilifu wako.

Nitegee sikio lako* na uniokoe.+

 3 Uwe ngome ya mwamba kwangu

Ambamo ninaweza kuingia sikuzote.

Toa amri ya kuniokoa,

Kwa maana wewe ni jabali langu na ngome yangu.+

 4 Ee Mungu wangu, niokoe kutoka mikononi mwa mwovu,+

Kutoka katika makucha ya mkandamizaji asiyetenda haki.

 5 Kwa maana wewe ni tumaini langu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova;

Nimekutumaini wewe* tangu nilipokuwa kijana.+

 6 Nimekutegemea tangu nilipozaliwa;

Wewe ndiye uliyenitoa tumboni mwa mama yangu.+

Ninakusifu daima.

 7 Nimekuwa kama muujiza kwa watu wengi,

Lakini wewe ni kimbilio langu imara.

 8 Kinywa changu kimejaa sifa zako;+

Mchana kutwa ninasimulia kuhusu fahari yako.

 9 Usinitupe wakati wa uzee;+

Usiniache ninapoishiwa na nguvu.+

10 Maadui wangu wanasema mambo mabaya kunihusu,

Na wale wanaotaka kuniua* wanapanga njama pamoja,+

11 Wakisema: “Mungu amemwacha.

Mkimbizeni na kumkamata, kwa maana hakuna yeyote wa kumwokoa.”+

12 Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali nami.

Ee Mungu wangu, njoo haraka unisaidie.+

13 Wale wanaonipinga

Na waaibishwe na kuangamia.+

Wale wanaonitakia msiba

Na wafunikwe na aibu na fedheha.+

14 Lakini mimi, nitaendelea kungoja;

Nitakusifu hata zaidi.

15 Kinywa changu kitasimulia uadilifu wako,+

Mchana kutwa kitasimulia matendo yako ya wokovu,

Ingawa ni mengi sana kwangu kuyajua.*+

16 Nitakuja na kutangaza matendo yako yenye nguvu,

Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova;

Nitatangaza uadilifu wako, wako peke yako.

17 Ee Mungu, umenifundisha tangu nilipokuwa kijana,+

Na mpaka sasa ninaendelea kutangaza kazi zako zinazostaajabisha.+

18 Ee Mungu, hata nikizeeka na kuwa na mvi, usiniache.+

Acha nikiambie kizazi kijacho kuhusu nguvu zako*

Na kuwaambia wote watakaokuja kuhusu uwezo wako.+

19 Uadilifu wako, Ee Mungu, unafika vileleni;+

Umetenda mambo makuu;

Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?+

20 Ingawa umenifanya nipate taabu nyingi na misiba mingi,+

Nihuishe tena;

Niinue kutoka katika sehemu zenye kina za* dunia.+

21 Ongeza ukuu wangu

Nizunguke na kunifariji.

22 Kisha nitakusifu kwa zeze

Kwa sababu ya uaminifu wako, Ee Mungu wangu.+

Nitaimba sifa zako* kwa kinubi,

Ee Mtakatifu wa Israeli.

23 Midomo yangu itapaza sauti kwa shangwe ninapokuimbia sifa,+

Kwa maana umeokoa uhai wangu.*+

24 Ulimi wangu utaongea* kuhusu uadilifu wako mchana kutwa,+

Kwa maana wale wanaotaka kuniangamiza wataaibishwa na kufedheheshwa.+

Zaburi Inayomhusu Sulemani.

72 Ee Mungu, mpe mfalme hukumu zako,

Na umzawadie mwana wa mfalme uadilifu wako.+

 2 Na atetee kesi ya watu wako kwa uadilifu,

Na ya watu wako wa hali ya chini kwa haki.+

 3 Milima na iwaletee watu amani,

Na vilima vilete uadilifu.

 4 Na awalinde* watu wa hali ya chini miongoni mwa mataifa,

Na awaokoe watoto* wa mtu maskini,

Na amponde mpunjaji.+

 5 Watakuogopa maadamu jua lipo

Na maadamu mwezi unadumu,

Kizazi baada ya kizazi.+

 6 Atakuwa kama mvua inayonyeshea majani yaliyofyekwa,

Kama manyunyu ya mvua yanayoinywesha dunia.+

 7 Katika siku zake mwadilifu atasitawi,*+

Na amani itakuwa nyingi+ mpaka mwezi utakapokuwa haupo tena.

 8 Atakuwa na raia* kutoka bahari mpaka bahari

Na kutoka Mto Efrati mpaka kwenye miisho ya dunia.+

 9 Wakaaji wa jangwani watainama chini mbele yake,

Na maadui wake wataramba mavumbi.+

10 Wafalme wa Tarshishi na wa visiwa watalipa ushuru.+

Wafalme wa Sheba na wa Seba watatoa zawadi.+

11 Wafalme wote watainama chini mbele yake,

Na mataifa yote yatamtumikia.

12 Kwa maana atamwokoa maskini anayelilia msaada,

Pia mtu wa hali ya chini na yeyote ambaye hana msaidizi.

13 Atamhurumia mtu wa hali ya chini na maskini,

Naye ataokoa uhai wa* maskini.

14 Atawaokoa* kutoka katika ukandamizaji na ukatili,

Na damu yao itakuwa na thamani machoni pake.

15 Na aishi na kupewa dhahabu ya Sheba.+

Sala na zitolewe daima kwa ajili yake,

Na abarikiwe mchana kutwa.

16 Kutakuwa na nafaka nyingi duniani;+

Itafurika juu ya milima.

Matunda yake yatasitawi kama ya Lebanoni,+

Na katika majiji watu watachanua kama mimea ya dunia.+

17 Jina lake na lidumu milele,+

Na lisitawi maadamu jua lipo.

Watu na wajipatie baraka kupitia yeye;+

Mataifa yote na yamtangaze kuwa mwenye furaha.

18 Na asifiwe Yehova Mungu, Mungu wa Israeli,+

Ambaye peke yake hutenda mambo yanayostaajabisha.+

19 Jina lake tukufu na lisifiwe milele,+

Na utukufu wake ujae duniani pote.+

Amina na Amina.

20 Huo ndio mwisho wa sala za Daudi, mwana wa Yese.+

KITABU CHA TATU

(Zaburi 73-89)

Muziki wa Asafu.+

73 Kwa kweli Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio safi moyoni.+

 2 Lakini mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kukengeuka;

Hatua zangu zilikuwa karibu kuteleza.+

 3 Kwa maana niliwaonea wivu wenye kiburi*

Nilipokuwa nikiona amani ya waovu.+

 4 Kwa maana hawana maumivu wanapokufa;

Miili yao ina afya.*+

 5 Hawataabiki kama wanadamu wengine,+

Wala hawateseki kama watu wengine.+

 6 Kwa hiyo, kiburi ni mkufu wao;+

Ukatili huwafunika kama vazi.

 7 Ufanisi wao* hufanya macho yao yanenepe;

Wamezidi mawazo ya moyo.

 8 Wanadhihaki na kusema mambo maovu.+

Kwa kiburi, wanatoa vitisho vya kuwakandamiza wengine.+

 9 Wanaongea kana kwamba wako juu kama mbingu,

Na ndimi zao hutamba duniani.

10 Kwa hiyo watu wake huwageukia,

Nao hunywa maji yao mengi.

11 Wanasema: “Mungu anajuaje?+

Je, Aliye Juu Zaidi ana ujuzi kweli?”

12 Naam, hivyo ndivyo walivyo waovu, ambao sikuzote wanastarehe.+

Wanaendelea kuongeza mali zao.+

13 Kwa hakika nimeusafisha moyo wangu bure

Na kunawa mikono yangu katika ukosefu wa hatia.+

14 Nami nilitaabika mchana kutwa;+

Niliadhibiwa kila asubuhi.+

15 Lakini kama ningesema mambo hayo,

Ningewasaliti watu wako.*

16 Nilipojaribu kulielewa jambo hilo,

Lilinitaabisha

17 Mpaka nilipoingia mahali patakatifu pa Mungu penye utukufu,

Nami nikatambua wakati wao ujao.

18 Kwa hakika unawaweka kwenye ardhi yenye utelezi.+

Unawafanya waanguke katika uharibifu wao.+

19 Jinsi wanavyoangamizwa kwa ghafla!+

Jinsi wanavyofikia kwa ghafla mwisho wao unaotisha!

20 Kama ndoto wakati wa kuamka, Ee Yehova,

Utakapoinuka, utaitupilia mbali* sanamu yao.

21 Lakini moyo wangu ulikuwa mchungu,+

Na ndani kabisa* nilihisi maumivu makali.

22 Nilikuwa mpumbavu wala sikuwa na uelewaji;

Nilikuwa kama mnyama asiye na akili mbele zako.

23 Lakini sasa niko pamoja nawe sikuzote;

Umeushika mkono wangu wa kulia.+

24 Unaniongoza kwa ushauri wako,+

Na baadaye utaniongoza kwenye utukufu.+

25 Ni nani niliye naye mbinguni?

Isipokuwa wewe tu, sitamani chochote duniani.+

26 Mwili wangu na moyo wangu unaweza kudhoofika,

Lakini Mungu ni mwamba wa moyo wangu na fungu langu milele.+

27 Kwa kweli, wale wanaojitenga mbali nawe wataangamia.

Utamwangamiza* kila mtu anayekuacha kwa upotovu.*+

28 Lakini kwa upande wangu, kumkaribia Mungu ni jambo jema kwangu.+

Nimemfanya Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova kuwa kimbilio langu,

Ili nizitangaze kazi zako zote.+

Maskili.* Wa Asafu.+

74 Ee Mungu, kwa nini umetukataa milele?+

Kwa nini hasira yako inawaka* dhidi ya kundi la malisho yako?+

 2 Wakumbuke watu uliojipatia* zamani za kale,+

Kabila ulilokomboa liwe urithi wako.+

Ukumbuke Mlima Sayuni, mahali unapokaa.+

 3 Zielekeze hatua zako kwenye magofu ya kudumu.+

Adui ameharibu kila kitu mahali patakatifu.+

 4 Maadui wako walinguruma ndani ya mahali pako pa mkutano.*+

Wameweka bendera zao wenyewe ziwe ishara humo.

 5 Walikuwa kama watu wanaotumia mashoka kufyeka msitu wenye miti mingi.

 6 Walivunjavunja michongo yake yote+ kwa mashoka na fito za chuma.

 7 Walichoma moto mahali pako patakatifu.+

Walichafua hema la ibada lenye jina lako, wakaliangusha chini.

 8 Wao pamoja na uzao wao wamesema mioyoni mwao:

“Sehemu zote za Mungu za mikutano* zilizo nchini ni lazima ziteketezwe.”

 9 Hatuoni ishara yoyote;

Hakuna tena nabii yeyote,

Na hakuna yeyote miongoni mwetu anayejua hali hii itaendelea hadi lini.

10 Ee Mungu, mpinzani ataendelea kudhihaki mpaka lini?+

Je, adui ataendelea kulidharau jina lako milele?+

11 Kwa nini unauzuia mkono wako, mkono wako wa kuume?+

Uchomoe kifuani mwako* na kuwaangamiza?

12 Lakini Mungu ni Mfalme wangu tangu zamani za kale,

Yeye anayefanya matendo ya wokovu duniani.+

13 Uliitibua bahari kwa nguvu zako;+

Uliviponda vichwa vya wanyama wakubwa sana wa baharini.

14 Uliviponda vichwa vya Lewiathani;*

Ukawapa watu wamle kama chakula chao, wale wanaokaa jangwani.

15 Ulipasua vijia kwa ajili ya chemchemi na vijito;+

Ulikausha mito inayotiririka daima.+

16 Mchana ni wako, na usiku pia.

Uliumba nuru* na jua.+

17 Uliweka mipaka yote ya dunia;+

Uliumba majira ya kiangazi na majira ya baridi kali.+

18 Kumbuka dhihaka za adui, Ee Yehova,

Jinsi taifa pumbavu linavyodharau jina lako.+

19 Usiwape wanyama wa mwituni uhai wa* njiwa tetere wako.

Usiusahau milele uhai wa watu wako wanaoteseka.

20 Likumbuke lile agano,

Kwa maana sehemu za dunia zenye giza zimejaa makao ya ukatili.

21 Mtu aliyepondwa na asigeuke na kwenda zake akiwa amekata tamaa;+

Watu wa hali ya chini na maskini na walisifu jina lako.+

22 Inuka, Ee Mungu, na utetee kesi yako.

Kumbuka jinsi wapumbavu wanavyokudhihaki mchana kutwa.+

23 Usisahau mambo ambayo maadui wako wanasema.

Kelele za wale wanaokuasi zinapanda juu daima.

Kwa kiongozi. Umepatanishwa na muziki wa “Usiharibu.” Wimbo wa Asafu.+

75 Tunakushukuru, Ee Mungu, tunakushukuru;

Jina lako liko karibu,+

Na watu wanatangaza kazi zako zinazostaajabisha.

 2 Unasema: “Ninapoweka wakati hususa,

Ninahukumu kwa haki.

 3 Dunia na wakaaji wake wote walipoyeyushwa,

Mimi ndiye niliyeziimarisha nguzo zake.” (Sela)

 4 Ninawaambia wenye kujigamba, “Msijigambe,”

Na waovu, “Msikweze nguvu zenu.*

 5 Msikweze nguvu zenu* juu sana

Au kuongea kwa kiburi.

 6 Kwa maana kukwezwa

Hakutoki mashariki wala magharibi wala kusini.

 7 Kwa maana Mungu ni Mwamuzi.+

Humshusha huyu na kumkweza yule.+

 8 Kwa maana kuna kikombe mkononi mwa Yehova;+

Divai inatoa povu nayo imechanganywa kikamili.

Hakika ataimwaga,

Na waovu wote duniani watainywa, mpaka machicha yake.”+

 9 Lakini mimi, nitalitangaza hilo milele;

Nitamwimbia sifa* Mungu wa Yakobo.

10 Kwa maana anasema: “Nitazikata nguvu* zote za waovu.”

Lakini nguvu* za waadilifu zitakwezwa.

Kwa kiongozi; uimbwe kwa ala za nyuzi. Muziki wa Asafu.+ Wimbo.

76 Mungu anajulikana Yuda;+

Jina lake ni kuu katika Israeli.+

 2 Banda lake liko Salemu,+

Na makao yake yako Sayuni.+

 3 Huko aliivunja mishale inayowaka ya upinde,

Ngao na upanga na silaha za vita.+ (Sela)

 4 Unang’aa kwa uangavu;*

Una fahari kuliko milima ya mawindo.

 5 Wenye moyo jasiri wameporwa.+

Wamelala usingizi;

Mashujaa wote hawakuwa na uwezo.+

 6 Kwa sababu ya kemeo lako, Ee Mungu wa Yakobo,

Mwendeshaji wa gari na farasi wote wamelala usingizi mzito.+

 7 Ni wewe peke yako unayeogopesha.+

Na ni nani anayeweza kustahimili hasira yako kali?+

 8 Kutoka mbinguni ulitangaza hukumu;+

Dunia iliogopa na kunyamaza+

 9 Mungu alipoinuka ili kutekeleza hukumu,

Ili kuwaokoa wapole wote walio duniani.+ (Sela)

10 Kwa maana ghadhabu ya mwanadamu itakuletea sifa;+

Nawe utajipamba kwa mabaki ya ghadhabu yao.

11 Wekeni nadhiri zenu kwa Yehova Mungu wenu na kuzitimiza,+

Wote wanaomzunguka na walete zawadi yao kwa woga.+

12 Atakinyenyekeza kiburi cha* viongozi;

Yeye huwaogopesha wafalme wa dunia.

Kwa kiongozi; mtindo wa Yeduthuni.* Muziki wa Asafu.+

77 Kwa sauti yangu nitamlilia Mungu;

Nitamlilia Mungu kwa sauti kubwa, naye atanisikia.+

 2 Katika siku ya taabu yangu ninamtafuta Yehova.+

Usiku ninamnyooshea mikono yangu bila kuacha.*

Siwezi* kufarijiwa.

 3 Ninapomkumbuka Mungu, ninalia kwa maumivu;+

Ninataabika na nguvu zangu zinaniishia.*+ (Sela)

 4 Unazishika kope zangu ili nisifumbe macho;

Nimefadhaika, nami siwezi kuongea.

 5 Mawazo yangu yanarudi katika siku za zamani za kale,+

Miaka mingi iliyopita.

 6 Wakati wa usiku ninaukumbuka wimbo wangu;*+

Ninatafakari moyoni mwangu;+

Ninatafuta* kwa bidii.

 7 Je, Yehova atatutupa mbali milele?+

Je, hatatuonyesha tena kamwe kibali chake?+

 8 Je, upendo wake mshikamanifu utakoma milele?

Je, ahadi yake itakosa kutimia katika vizazi vyote?

 9 Je, Mungu amesahau kuonyesha kibali chake,+

Au je, hasira yake imekomesha rehema yake? (Sela)

10 Je, ni lazima niendelee kusema: “Hili ndilo linalonitaabisha:*+

Aliye Juu Zaidi amebadili msimamo wake kutuelekea”?*

11 Nitazikumbuka kazi za Yah;

Nitayakumbuka matendo yako yanayostaajabisha ya zamani za kale.

12 Nitautafakari utendaji wako wote

Na kutafakari shughuli zako.+

13 Ee Mungu, njia zako ni takatifu.

Ee Mungu, ni mungu gani aliye mkuu kama wewe?+

14 Wewe ndiye Mungu wa kweli, unayetenda mambo yanayostaajabisha.+

Umeyafunulia mataifa nguvu zako.+

15 Kwa nguvu zako* umewaokoa* watu wako,+

Wana wa Yakobo na wa Yosefu. (Sela)

16 Maji yalikuona, Ee Mungu,

Maji yalikuona yakavurugika.+

Na vilindi vya maji vikatibuka.

17 Mawingu yakamwaga maji.

Anga lenye mawingu likanguruma,

Na mishale yako ikaruka huku na kule.+

18 Sauti ya mngurumo+ wako ilikuwa kama magurudumu ya gari la vita;

Mimweko ya radi iliangaza dunia inayokaliwa;*+

Dunia ilitikisika na kutetemeka.+

19 Njia yako ilipita baharini,+

Kijia chako kilipita katika maji mengi;

Lakini nyayo zako hazingeweza kuonekana.

20 Uliwaongoza watu wako kama kundi la kondoo,+

Chini ya uangalizi* wa Musa na Haruni.+

Maskili.* Wa Asafu.+

78 Sikilizeni sheria* yangu, enyi watu wangu;

Tegeni sikio lenu kwa maneno ya kinywa changu.

 2 Nitakifungua kinywa changu kwa methali.

Nitafumbua mafumbo ya zamani za kale.+

 3 Mambo ambayo tumesikia na tunayojua,

Ambayo baba zetu wametusimulia,+

 4 Hatutawaficha wana wao;

Tutakisimulia kizazi kijacho mambo hayo+

Matendo ya Yehova yanayostahili sifa na nguvu zake,+

Mambo yanayostaajabisha aliyotenda.+

 5 Alianzisha kikumbusho katika Yakobo

Na kuweka sheria katika Israeli;

Aliwaamuru mababu zetu

Wawajulishe watoto wao mambo hayo,+

 6 Ili kizazi kijacho,

Watoto ambao hawajazaliwa, wayajue.+

Kisha wao watawasimulia watoto wao.+

 7 Halafu watoto hao watamtumaini Mungu.

Hawatasahau kazi za Mungu+

Lakini watashika amri zake.+

 8 Kisha hawatakuwa kama mababu zao,

Kizazi chenye ukaidi na uasi,+

Kizazi kilichokuwa na moyo unaoyumbayumba*+

Na ambacho hakikuwa na roho ya uaminifu kwa Mungu.

 9 Waefraimu walijihami kwa upinde,

Lakini walikimbia siku ya vita.

10 Hawakushika agano la Mungu+

Nao walikataa kutembea katika sheria yake.+

11 Walisahau pia mambo aliyotenda,+

Kazi zake zinazostaajabisha alizowaonyesha.+

12 Alifanya maajabu mbele ya mababu zao,+

Katika nchi ya Misri, eneo la Soani.+

13 Aliipasua bahari ili kuwaruhusu wavuke,

Naye akayafanya maji yasimame juu kama bwawa.*+

14 Aliwaongoza kwa wingu wakati wa mchana

Na usiku kucha kwa mwangaza wa moto.+

15 Aliipasua miamba nyikani,

Akawanywesha maji ya kutosha kana kwamba yanatoka vilindini.+

16 Alivitoa vijito kutoka kwenye jabali

Na kufanya maji yatiririke chini kama mito.+

17 Lakini waliendelea kumtendea dhambi

Kwa kumwasi jangwani yule Aliye Juu Zaidi;+

18 Walimjaribu* Mungu moyoni mwao+

Walidai wapewe chakula walichotamani.*

19 Kwa hiyo wakalalamika kumhusu Mungu,

Wakisema: “Je, Mungu anaweza kuandaa meza nyikani?”+

20 Tazama! Aliupiga mwamba

Hivi kwamba maji yakatiririka na vijito vikafurika.+

“Je, anaweza pia kutupatia mkate,

Au je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”+

21 Yehova alipowasikia, alikasirika sana;+

Moto+ ukawaka dhidi ya Yakobo,

Na hasira yake ikawaka dhidi ya Israeli+

22 Kwa sababu hawakudhihirisha imani katika Mungu;+

Hawakuutumaini uwezo wake wa kuwaokoa.

23 Basi akaliamuru anga lililo juu lenye mawingu,

Naye akaifungua milango ya mbingu.

24 Akaendelea kuwanyeshea mana ili wale;

Akawapa nafaka ya mbinguni.+

25 Wanadamu wakala mkate wa wenye nguvu;*+

Aliwapa mkate wa kutosha wa kuwashibisha.+

26 Aliuvumisha upepo wa mashariki mbinguni

Na kwa nguvu zake akaufanya upepo wa kusini uvume.+

27 Naye akawanyeshea nyama kama mavumbi,

Ndege kama mchanga kwenye ufuo wa bahari.

28 Aliwaangusha katikati ya kambi yake,

Pande zote kuzunguka mahema yake.

29 Nao wakala na kujilazimisha kula zaidi;

Aliwapa walichotamani.+

30 Lakini kabla hawajatosheleza kikamili tamaa yao,

Chakula kilipokuwa kingali kinywani mwao,

31 Ghadhabu ya Mungu ikawaka dhidi yao.+

Akawaua wanaume wenye nguvu zaidi;+

Aliwaangamiza wanaume vijana wa Israeli.

32 Licha ya hayo walizidi kutenda dhambi+

Nao hawakudhihirisha imani katika kazi zake zinazostaajabisha.+

33 Basi akazikatisha siku zao kana kwamba ni pumzi tu,+

Na miaka yao kwa matukio ya ghafla yenye kutisha.

34 Lakini kila mara alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta;+

Walirudi na kumtafuta Mungu,

35 Wakikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao+

Na kwamba Mungu Aliye Juu Zaidi alikuwa Mkombozi* wao.+

36 Lakini walijaribu kumdanganya kwa kinywa chao

Na kumwambia uwongo kwa ulimi wao.

37 Moyo wao haukuwa imara kumwelekea;+

Nao hawakuwa waaminifu kwa agano lake.+

38 Lakini alikuwa mwenye rehema;+

Alikuwa akiwasamehe* kosa lao, naye hakuwaangamiza.+

Mara nyingi aliizuia hasira yake+

Badala ya kuichochea ghadhabu yake yote.

39 Kwa maana alikumbuka kwamba walikuwa nyama tu,+

Upepo upitao ambao haurudi.*

40 Jinsi walivyomwasi mara nyingi nyikani+

Na kumtia uchungu jangwani!+

41 Walimjaribu Mungu tena na tena,+

Nao wakamhuzunisha* Mtakatifu wa Israeli.

42 Hawakuzikumbuka nguvu zake,*

Siku ambayo aliwaokoa* kutoka kwa adui,+

43 Jinsi alivyoonyesha ishara zake kule Misri+

Na miujiza yake katika eneo la Soani,

44 Na jinsi alivyobadili mifereji ya Nile kuwa damu+

Hivi kwamba hawangeweza kunywa maji kutoka katika vijito vyake.

45 Alituma makundi ya nzi ili yawale+

Na vyura ili kuwaangamiza.+

46 Mazao yao aliwapa parare wanaokula sana,

Matunda ya kazi yao ngumu akayapa makundi ya nzige.+

47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe+

Na mikuyu yao kwa mawe ya mvua.

48 Aliwaua kwa mvua ya mawe wanyama wao wa kubeba mizigo+

Na mifugo yao kwa umeme wa radi.*

49 Aliwamwagia hasira yake inayowaka,

Hasira kali na ghadhabu na taabu,

Makundi ya malaika yanayoleta msiba.

50 Alitayarisha njia kwa ajili ya hasira yake.

Hakuwalinda wasife;*

Naye aliwaua kwa ugonjwa hatari.

51 Mwishowe aliwaangamiza wazaliwa wote wa kwanza wa Misri,+

Mwanzo wa nguvu zao za uzazi katika mahema ya Hamu.

52 Kisha akawatoa nje watu wake kama kundi la kondoo+

Na kuwaongoza nyikani kama kundi la mifugo.

53 Aliwaongoza kwa usalama,

Nao hawakuogopa;+

Bahari iliwafunika maadui wao.+

54 Naye akawaleta katika eneo lake takatifu,+

Eneo hili lenye milima ambalo mkono wake wa kuume ulilitwaa.+

55 Aliyafukuza mataifa kutoka mbele yao;+

Akawagawia urithi kwa kamba ya kupimia;+

Aliyafanya makabila ya Israeli yakae katika makao yao.+

56 Lakini waliendelea kumjaribu* Mungu Aliye Juu Zaidi, na kumwasi;+

Hawakusikiliza vikumbusho vyake.+

57 Pia walipotoka na kutenda kwa hila kama mababu zao.+

Hawakutegemeka kama upinde uliolegea usivyotegemeka.+

58 Waliendelea kumkasirisha kwa mahali pao pa juu,+

Nao wakachochea hasira yake kali* kwa sanamu zao za kuchongwa.+

59 Mungu alisikia na kuwaka hasira,+

Kwa hiyo akaikataa kabisa Israeli.

60 Mwishowe akaliacha hema la ibada lililo Shilo,+

Hema alimokaa miongoni mwa wanadamu.+

61 Aliacha ishara ya nguvu zake ipelekwe utekwani;

Fahari yake itiwe mikononi mwa adui.+

62 Aliwatoa watu wake wauawe kwa upanga+

Naye akaukasirikia vikali urithi wake.

63 Moto uliwateketeza kabisa vijana wake wa kiume,

Na mabikira wake hawakuimbiwa nyimbo za harusi.*

64 Makuhani wake waliuawa kwa upanga,+

Na wajane wao hawakulia.+

65 Kisha Yehova akaamka kana kwamba anatoka usingizini,+

Kama mwanamume hodari+ aamkavyo baada ya divai kumtoka.

66 Naye akawakimbiza maadui wake;+

Akawatia aibu ya kudumu.

67 Alilikataa hema la Yosefu;

Hakulichagua kabila la Efraimu.

68 Lakini alichagua kabila la Yuda,+

Mlima Sayuni, anaoupenda.+

69 Alipafanya mahali pake patakatifu pawe mahali pa kudumu kama mbingu,*+

Kama dunia ambayo ameiimarisha milele.+

70 Alimchagua Daudi+ mtumishi wake

Na kumtoa katika mazizi ya kondoo,+

71 Alimwondoa katika kazi ya kuchunga kondoo wanaonyonyesha;

Akamfanya kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake,+

Na wa Israeli, urithi wake.+

72 Aliwachunga kwa utimilifu wa moyo,+

Na kwa mikono stadi aliwaongoza.+

Muziki wa Asafu.+

79 Ee Mungu, mataifa yamevamia urithi wako;+

Yamelichafua hekalu lako takatifu;+

Yamebadili Yerusalemu kuwa rundo la magofu.+

 2 Wamewapa ndege wa angani maiti za watumishi wako kuwa chakula chao

Na miili ya washikamanifu wako wamewapa wanyama wa mwituni wa dunia.+

 3 Wamemwaga damu yao kama maji kotekote Yerusalemu,

Na hakuna aliyebaki wa kuwazika.+

 4 Tumekuwa kitu cha kushutumiwa na majirani wetu;+

Wale wanaotuzunguka wanatudhihaki na kutufanyia mzaha.

 5 Ee Yehova, utaendelea kuwaka hasira mpaka lini? Milele?+

Ghadhabu yako itaendelea kuwaka kama moto mpaka lini?+

 6 Yamwagie ghadhabu yako mataifa ambayo hayakujui

Na falme ambazo haziliitii jina lako.+

 7 Kwa maana wamemnyafua Yakobo

Nao wameifanya nchi yake ukiwa.+

 8 Usitufanye tuwajibike kwa sababu ya makosa ya mababu zetu.+

Tuonyeshe haraka rehema yako,+

Kwa maana tumeshushwa chini sana.

 9 Tusaidie, Ee Mungu wa wokovu wetu,+

Kwa ajili ya jina lako tukufu;

Tuokoe na kutusamehe* dhambi zetu kwa ajili ya jina lako.+

10 Kwa nini mataifa yaseme: “Mungu wao yuko wapi?”+

Na ijulikane miongoni mwa mataifa mbele ya macho yetu

Kwamba damu iliyomwagwa ya watumishi wako imelipiziwa kisasi.+

11 Na usikie kilio cha maumivu cha mfungwa.+

Tumia nguvu zako kuu* kuwahifadhi* wale waliohukumiwa kifo.*+

12 Walipize majirani wetu mara saba+

Kwa sababu ya shutuma walizotoa dhidi yako, Ee Yehova.+

13 Kisha sisi, watu wako na kondoo wa malisho yako,+

Tutakushukuru milele;

Nasi tutatangaza sifa yako kizazi mpaka kizazi.+

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Mayungiyungi.” Kikumbusho. Muziki wa Asafu.+

80 Ee Mchungaji wa Israeli, sikiliza,

Wewe unayemwongoza Yosefu kama kundi la kondoo.+

Wewe unayeketi kwenye kiti cha ufalme juu ya* makerubi,+

Angaza.*

 2 Mbele ya Efraimu na Benjamini na Manase,

Chochea nguvu zako;+

Njoo utuokoe.+

 3 Ee Mungu, turudishe;+

Uso wako na utuangazie, ili tuokolewe.+

 4 Yehova Mungu wa majeshi, utaendelea mpaka lini kuwa na hasira kali kuelekea* sala ya watu wako?+

 5 Unawalisha machozi kama mkate,

Nawe unawanywesha machozi kupita kiasi.

 6 Unawaruhusu majirani wetu wagombane kwa sababu yetu;

Maadui wetu wanaendelea kutudhihaki wapendavyo.+

 7 Ee Mungu wa majeshi, turudishe;

Uso wako na utuangazie, ili tuokolewe.+

 8 Uliufanya mzabibu+ uondoke Misri.

Uliyafukuza mataifa na kuupanda.+

 9 Ulitayarisha nafasi kwa ajili yake,

Nao ukatia mizizi na kujaa nchini.+

10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake,

Na mierezi ya Mungu kwa matawi yake.

11 Matawi yake yalienea mpaka baharini,

Na machipukizi yake mpaka kwenye Mto Efrati.+

12 Kwa nini umebomoa kuta za mawe za shamba la mzabibu huo,+

Hivi kwamba wote wanaopita karibu nao wanachuma matunda yake?+

13 Nguruwe wa mwituni wanauharibu,

Na wanyama wa porini wanaula.+

14 Ee Mungu wa majeshi, rudi tafadhali.

Tazama chini kutoka mbinguni uone!

Utunze mzabibu huu,+

15 Shina* ambalo mkono wako wa kuume umepanda,+

Na umtazame mwana ambaye umemtia nguvu* kwa ajili yako mwenyewe.+

16 Umechomwa moto,+ umekatwa.

Wanaangamia kwa kemeo lako.*

17 Mkono wako na umtegemeze mwanamume aliye kwenye mkono wako wa kuume,

Mwana wa binadamu uliyemtia nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+

18 Kisha hatutageuka kutoka kwako.

Tuhifadhi hai, ili tuliitie jina lako.

19 Ee Yehova Mungu wa majeshi, turudishe;

Uso wako na utuangazie, ili tuokolewe.+

Kwa kiongozi; juu ya Gitithi.* Wa Asafu.+

81 Mshangilieni Mungu kwa sauti, nguvu zetu.+

Mpazieni sauti kwa ushindi Mungu wa Yakobo.

 2 Anzisheni muziki na kuchukua tari,

Kinubi chenye sauti tamu pamoja na kinanda.

 3 Pigeni pembe wakati wa mwezi mpya,+

Wakati wa mwezi mpevu, kwa ajili ya siku ya sherehe yetu.+

 4 Kwa maana ni agizo kwa Israeli,

Sheria ya Mungu wa Yakobo.+

 5 Aliiweka ili iwe kikumbusho kwa Yosefu+

Alipoenda* kuishambulia nchi ya Misri.+

Nilisikia sauti* ambayo sikuitambua:

 6 “Niliuinua mzigo kutoka begani mwake;+

Mikono yake iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.

 7 Katika taabu uliita, nami nikakuokoa;+

Nilikujibu kutoka katika wingu lenye ngurumo.*+

Nilikujaribu katika maji ya Meriba.*+ (Sela)

 8 Sikieni, watu wangu, nami nitatoa ushahidi dhidi yenu.

Ee Israeli, laiti ungenisikiliza.+

 9 Hakutakuwa na mungu yeyote wa kigeni miongoni mwenu;

Nanyi hamtamwinamia mungu wa kigeni.+

10 Mimi, Yehova, ni Mungu wako,

Niliyekutoa nchini Misri.+

Fungua wazi kinywa chako, nami nitakijaza.+

11 Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu;

Israeli hakujitiisha kwangu.+

12 Kwa hiyo nikawaacha wafuate mioyo yao mikaidi;

Walitenda mambo waliyofikiri yanafaa.*+

13 Laiti watu wangu wangenisikiliza,+

Laiti Israeli angetembea katika njia zangu!+

14 Ningewatiisha haraka maadui wao;

Ningeugeuza mkono wangu dhidi ya wapinzani wao.+

15 Wale wanaomchukia Yehova watajikunyata mbele zake,

Na mwisho* wao utakuwa wa milele.

16 Lakini atakulisha* ngano bora kabisa*+

Na kukushibisha kwa asali kutoka mwambani.”+

Muziki wa Asafu.+

82 Mungu anachukua mahali pake katika kusanyiko la Mungu;+

Anahukumu katikati ya miungu:*+

 2 “Mtaendelea mpaka lini kuhukumu bila haki+

Na kuwapendelea waovu?+ (Sela)

 3 Mteteeni* mtu wa hali ya chini na yatima.+

Mtendeeni kwa haki mtu asiye na uwezo na maskini.+

 4 Mwokoeni mtu wa hali ya chini na maskini;

Waokoeni kutoka mkononi mwa mwovu.”

 5 Hawajui wala hawaelewi;+

Wanatembea huku na huku gizani;

Misingi yote ya dunia inatikiswa.+

 6 “Nimesema, ‘Ninyi ni miungu,*+

Ninyi nyote ni wana wa Aliye Juu Zaidi.

 7 Lakini mtakufa kama wanadamu wanavyokufa;+

Nanyi mtaanguka kama mkuu mwingine yeyote anavyoanguka!’”+

 8 Inuka, Ee Mungu, uihukumu dunia,+

Kwa maana mataifa yote ni yako.

Wimbo. Muziki wa Asafu.+

83 Ee Mungu, usinyamaze;+

Usikae kimya wala kutulia, Ee Mungu.

 2 Kwa maana, tazama! Maadui wako wanafanya fujo;+

Wale wanaokuchukia wanatenda kwa kiburi.*

 3 Kwa hila wanapanga njama kwa siri dhidi ya watu wako;

Wanapanga njama dhidi ya watu wako unaowathamini.*

 4 Wanasema: “Njooni, acheni tuwaangamize wakiwa taifa,+

Ili jina la Israeli lisikumbukwe tena kamwe.”

 5 Kwa umoja wanatunga mbinu;*

Wameungana* dhidi yako+—

 6 Mahema ya Edomu na Waishmaeli, Moabu+ na Wahagri,+

 7 Gebali na Amoni+ na Amaleki,

Ufilisti+ pamoja na wakaaji wa Tiro.+

 8 Pia Ashuru+ imejiunga nao;

Wanawaunga mkono* wana wa Loti.+ (Sela)

 9 Watendee kama ulivyoitendea Midiani,+

Kama ulivyomtendea Sisera na Yabini kwenye kijito cha* Kishoni.+

10 Waliangamizwa kule En-dori;+

Wakawa mbolea juu ya ardhi.

11 Wafanye viongozi wao wawe kama Orebu na Zeebu+

Na wakuu* wao kama Zeba na Zalmuna,+

12 Kwa maana walisema: “Na tuimiliki nchi ambamo Mungu anakaa.”

13 Ee Mungu wangu, wafanye wawe kama mchongoma unaopeperushwa,*+

Kama majani makavu yanayopeperushwa na upepo.

14 Kama moto unaoteketeza kabisa msitu,

Kama mwali wa moto unaounguza milima,+

15 Wafuatie vivyo hivyo kwa tufani yako+

Na kuwaogopesha kwa dhoruba yako ya upepo.+

16 Funika nyuso zao kwa aibu,*

Ili walitafute jina lako, Ee Yehova.

17 Na waaibishwe na kuogopeshwa milele;

Na wafedheheshwe na kuangamia;

18 Na watu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova,+

Wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.+

Kwa kiongozi; juu ya Gitithi.* Muziki wa wana wa Kora.+

84 Jinsi linavyovutia sana* hema lako tukufu la ibada,+

Ee Yehova wa majeshi!

 2 Nafsi yangu yote inatamani,

Naam, ninazimia kwa kutamani,

Nyua za Yehova.+

Moyo wangu na mwili wangu humshangilia kwa sauti Mungu aliye hai.

 3 Hata ndege hupata makao huko

Na mbayuwayu hujipatia kiota,

Ambamo huyatunza makinda wake

Karibu na madhabahu yako tukufu, Ee Yehova wa majeshi,

Mfalme wangu na Mungu wangu!

 4 Wenye furaha ni wale wanaokaa katika nyumba yako!+

Wanaendelea kukusifu.+ (Sela)

 5 Wenye furaha ni watu wanaopata nguvu kutoka kwako,+

Ambao mioyo yao inatamani sana* barabara kuu.

 6 Wanapopita katika Bonde la Mibaka,*

Wanalifanya kuwa mahali penye chemchemi;

Na mvua ya mapema hulivisha* baraka.

 7 Wataendelea kutembea kutoka nguvu hadi nguvu zaidi;+

Kila mmoja wao hufika mbele za Mungu kule Sayuni.

 8 Ee Yehova Mungu wa majeshi, isikie sala yangu;

Sikiliza, Ee Mungu wa Yakobo. (Sela)

 9 Tazama, ngao yetu+ na Mungu wetu,*

Utazame uso wa mtiwa-mafuta wako.+

10 Kwa maana siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu moja kwingineko!+

Ninachagua kusimama kwenye kizingiti cha nyumba ya Mungu wangu

Badala ya kukaa katika mahema ya uovu.

11 Kwa maana Yehova Mungu ni jua+ na ngao;+

Yeye hutoa kibali na utukufu.

Yehova hatawanyima jambo lolote jema

Wale wanaotembea kwa utimilifu.+

12 Ee Yehova wa majeshi,

Mwenye furaha ni mtu anayekutumaini.+

Kwa kiongozi. Muziki wa wana wa Kora.+

85 Ee Yehova, umeionyesha kibali nchi yako;+

Uliwarudisha watu wa Yakobo waliokuwa wametekwa.+

 2 Umelisamehe kosa la watu wako;

Ulisamehe* dhambi yao yote.+ (Sela)

 3 Uliizuia ghadhabu yako yote;

Uliiacha hasira yako kali.+

 4 Turudishe,* Ee Mungu wa wokovu wetu,

Na uache kutukasirikia.+

 5 Je, utatughadhibikia milele?+

Je, utaendelea kukasirika kizazi baada ya kizazi?

 6 Je, hutatuhuisha tena

Ili watu wako washangilie kwa sababu yako?+

 7 Ee Yehova, tutendee kwa upendo mshikamanifu,+

Nawe utupe wokovu wako.

 8 Nitasikiliza jambo ambalo Mungu wa kweli Yehova anasema,

Kwa maana atawaambia watu wake kuhusu amani,+ washikamanifu wake,

Lakini wasianze tena kujiamini kupita kiasi.+

 9 Kwa hakika wokovu wake uko karibu na wale wanaomwogopa,+

Ili utukufu wake ukae katika nchi yetu.

10 Upendo mshikamanifu utakutana na uaminifu;

Uadilifu utabusiana na amani.+

11 Uaminifu utachipuka duniani,

Na uadilifu utatazama chini kutoka mbinguni.+

12 Naam, Yehova atatoa kilicho chema,*+

Na nchi yetu itazaa mavuno yake.+

13 Uadilifu utatembea mbele zake+

Na kutengeneza njia kwa ajili ya hatua zake.

Sala ya Daudi.

86 Tega sikio lako,* Ee Yehova, nawe unijibu,

Kwa maana ninateseka nami ni maskini.+

 2 Ulinde uhai wangu,* kwa maana mimi ni mshikamanifu.+

Mwokoe mtumishi wako anayekutumaini,

Kwa maana wewe ni Mungu wangu.+

 3 Nionyeshe kibali, Ee Yehova,+

Kwa maana ninakulilia wewe mchana kutwa.+

 4 Mfanye mtumishi wako ashangilie,

Kwa maana ninakugeukia wewe,* Ee Yehova.

 5 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ni mwema+ na uko tayari kusamehe;+

Una upendo mwingi mshikamanifu kwa wote wanaokuitia.+

 6 Ee Yehova, sikiliza sala yangu;

Na usikilize sihi zangu za kuomba msaada.+

 7 Ninakuitia wewe katika siku ninayotaabika,+

Kwa maana utanijibu.+

 8 Hakuna yeyote aliye kama wewe kati ya miungu, Ee Yehova,+

Hakuna kazi zilizo kama kazi zako.+

 9 Mataifa yote uliyoyaumba

Yatakuja na kuinama mbele zako, Ee Yehova,+

Nayo yatalitukuza jina lako.+

10 Kwa maana wewe ni mkuu, nawe unafanya mambo yanayostaajabisha;+

Wewe ni Mungu, wewe peke yako.+

11 Nifundishe, Ee Yehova, kuhusu njia yako.+

Nitatembea katika kweli yako.+

Unganisha moyo wangu* ili niliogope jina lako.+

12 Ninakusifu, Ee Yehova Mungu wangu, kwa moyo wangu wote,+

Nami nitalitukuza jina lako milele,

13 Kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mkuu kwangu,

Nawe umeuokoa uhai wangu* kutoka katika vina vya Kaburi.*+

14 Ee Mungu, watu wenye kimbelembele wanainuka dhidi yangu;+

Kundi la wanaume wakatili wanataka kuniua,*

Nao hawakuheshimu kamwe.*+

15 Lakini wewe, Ee Yehova, ni Mungu mwenye rehema na huruma,*

Si mwepesi wa hasira, nawe una upendo mwingi mshikamanifu na uaminifu.*+

16 Nigeukie na kunionyesha kibali.+

Mpe mtumishi wako nguvu zako,+

Na umwokoe mwana wa kijakazi wako.

17 Nionyeshe ishara ya* wema wako,

Ili wale wanaonichukia waione na kuaibika.

Kwa maana wewe, Ee Yehova, ni msaidizi wangu na mfariji wangu.

Muziki wa wana wa Kora.+ Wimbo.

87 Msingi wa jiji lake uko katika milima mitakatifu.+

 2 Yehova anapenda malango ya Sayuni+

Kuliko mahema yote ya Yakobo.

 3 Mambo matukufu yanasemwa kukuhusu, Ee jiji la Mungu wa kweli.+ (Sela)

 4 Nitamhesabu Rahabu+ na Babiloni kuwa kati ya wale wanaonijua* mimi;

Tazama, Ufilisti na Tiro, pamoja na Kushi.

Itasemwa hivi: “Huyu alizaliwa humo.”

 5 Na kuhusu Sayuni itasemwa:

“Kila mtu alizaliwa humo.”

Na Aliye Juu Zaidi atamwimarisha kabisa.

 6 Yehova atatangaza hivi atakapoyaandikisha mataifa:

“Huyu alizaliwa humo.” (Sela)

 7 Waimbaji+ na wale wanaocheza dansi za mzunguko+ watasema:

“Chemchemi zangu zote zimo ndani yako.”*+

Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+ Kwa kiongozi; kwa mtindo wa Mahalathi,* uimbwe kwa zamu. Maskili* ya Hemani+ Mwezra.

88 Ee Yehova, Mungu wa wokovu wangu,+

Wakati wa mchana ninalia kwa sauti,

Na usiku ninakuja mbele zako.+

 2 Sala yangu na ikufikie,+

Tega sikio lako* usikie kilio changu cha kuomba msaada.+

 3 Kwa maana nafsi* yangu imejaa msiba,+

Na uhai wangu uko kwenye kingo za Kaburi.*+

 4 Tayari nimehesabiwa miongoni mwa wale wanaoshuka shimoni;*+

Nimekuwa mtu asiye na uwezo wowote,*+

 5 Aliyeachwa kati ya watu waliokufa

Kama waliouawa wanaolala kaburini,

Ambao huwakumbuki tena

Na ambao wametengwa mbali na utunzaji* wako.

 6 Umeniweka katika shimo lenye kina kirefu sana,

Sehemu zenye giza, shimo kubwa.*

 7 Ghadhabu yako inanilemea sana,+

Nawe unanilemea kwa mawimbi yako yenye nguvu. (Sela)

 8 Umewafukuza rafiki zangu mbali sana nami;+

Umenifanya niwe kitu kinachowachukiza.

Nimenaswa na siwezi kutoroka.

 9 Jicho langu limedhoofika kwa sababu ya mateso yangu.+

Ee Yehova, ninakulilia mchana kutwa;+

Ninakunyooshea mikono yangu.

10 Je, utawatendea maajabu waliokufa?

Je, wale waliokufa ambao hawana uwezo wanaweza kuinuka na kukusifu?+ (Sela)

11 Je, upendo wako mshikamanifu utatangazwa kaburini,

Na uaminifu wako mahali pa maangamizi?*

12 Je, maajabu yako yatajulikana gizani

Au uadilifu wako katika nchi ya waliosahauliwa?+

13 Lakini bado ninakulilia unisaidie, Ee Yehova,+

Kila asubuhi sala yangu inakufikia.+

14 Kwa nini, Ee Yehova, unanikataa?*+

Kwa nini unanificha uso wako?+

15 Tangu nilipokuwa kijana,

Nimeteseka nami niko karibu kuangamia;+

Nimekufa ganzi kwa sababu ya mambo yanayotisha unayoruhusu yanipate.

16 Hasira yako inayowaka inanilemea;+

Vitisho vyako vinaniangamiza.

17 Vinanizunguka mchana kutwa kama maji;

Vinanizingira ili kunibana pande zote.*

18 Umewafukuza rafiki zangu na wenzangu mbali sana nami;+

Giza limekuwa mwenzangu.

Maskili.* Wa Ethani+ Mwezra.

89 Nitaimba kuhusu jinsi Yehova anavyoonyesha upendo mshikamanifu milele.

Kwa kinywa changu ninavitangazia vizazi vyote uaminifu wako.

 2 Kwa maana nimesema: “Upendo mshikamanifu utajengwa* milele,+

Nawe umeuimarisha kabisa uaminifu wako mbinguni.”

 3 “Nimefanya agano pamoja na yule niliyemchagua;+

Nimemwapia Daudi mtumishi wangu:+

 4 ‘Nitauimarisha kabisa uzao wako*+ milele,

Nami nitakijenga kiti chako cha ufalme kwa vizazi vyote.’”+ (Sela)

 5 Mbingu zinasifu maajabu yako, Ee Yehova,

Naam, uaminifu wako katika kutaniko la watakatifu.

 6 Kwa maana ni nani mbinguni anayeweza kulinganishwa na Yehova?+

Ni nani miongoni mwa wana wa Mungu+ aliye kama Yehova?

 7 Mungu anaogopwa katika baraza* la watakatifu;+

Yeye ni mtukufu na mwenye kuogopesha kwa wote wanaomzunguka.+

 8 Ee Yehova Mungu wa majeshi,

Ni nani aliye na nguvu kama wewe, Ee Yah?+

Uaminifu wako unakuzunguka.+

 9 Unautawala msukosuko wa bahari;+

Mawimbi yake yanapoinuka, unayatuliza.+

10 Umemponda Rahabu+ kama mtu aliyeuawa.+

Kwa mkono wako wenye nguvu umewatawanya maadui wako.+

11 Mbingu ni zako, na dunia ni yako;+

Nchi inayozaa na vinavyoijaza+—umeviumba.

12 Kaskazini na kusini—uliziumba;

Tabori+ na Hermoni+ hulisifu kwa shangwe jina lako.

13 Mkono wako una uwezo;+

Mkono wako una nguvu;+

Mkono wako wa kuume umekwezwa.+

14 Uadilifu na haki ndio msingi wa kiti chako cha ufalme;+

Upendo mshikamanifu na uaminifu husimama mbele zako.+

15 Wenye furaha ni watu wanaojua kelele za shangwe.+

Ee Yehova, wanatembea katika nuru ya uso wako.

16 Wanashangilia mchana kutwa kwa sababu ya jina lako,

Na kwa sababu ya uadilifu wako wanakwezwa.

17 Kwa maana wewe ni utukufu wa nguvu zao,+

Na kwa kibali chako nguvu zetu zinakwezwa.*+

18 Kwa maana ngao yetu ni ya Yehova,

Mfalme wetu ni wa Mtakatifu wa Israeli.+

19 Wakati huo uliwaambia hivi washikamanifu wako katika maono:

“Nimempa nguvu aliye hodari;+

Nimemkweza aliyechaguliwa kutoka miongoni mwa watu.+

20 Nimempata Daudi mtumishi wangu;+

Kwa mafuta yangu matakatifu nimemtia mafuta.+

21 Mkono wangu utamtegemeza,+

Na mkono wangu utamwimarisha.

22 Hakuna adui atakayemtoza ushuru,

Na hakuna mwovu atakayemkandamiza.+

23 Nitawavunja maadui wake vipandevipande kutoka mbele yake+

Na kuwaangamiza wale wanaomchukia.+

24 Uaminifu wangu na upendo wangu mshikamanifu uko pamoja naye,+

Na katika jina langu nguvu zake zitakwezwa.*

25 Nitauweka mkono wake* juu ya bahari

Na mkono wake wa kulia juu ya mito.+

26 Atasema kwa sauti: ‘Wewe ni Baba yangu,

Mungu wangu na Mwamba wa wokovu wangu.’+

27 Nami nitamfanya kuwa mzaliwa wa kwanza,+

Aliye juu zaidi kati ya wafalme wa dunia.+

28 Nitadumisha upendo wangu mshikamanifu kumwelekea milele,+

Na agano langu nililofanya pamoja naye halitavunjika kamwe.+

29 Nitauimarisha uzao wake* milele

Na kukifanya kiti chake cha ufalme kidumu kama mbingu.+

30 Wanawe wakiiacha sheria yangu

Na wasipotembea kulingana na maagizo yangu,*

31 Wakizivunja sheria zangu

Na wasiposhika amri zangu,

32 Basi nitaadhibu uasi wao* kwa fimbo+

Na kosa lao kwa viboko.

33 Lakini sitaacha kamwe kumtendea kwa upendo wangu mshikamanifu+

Wala sitakosa kutimiza ahadi yangu.*

34 Sitavunja agano langu+

Wala kubadili maneno yaliyosemwa na midomo yangu.+

35 Nimeapa katika utakatifu wangu, mara moja kwa wakati wote;

Sitamwambia Daudi uwongo.+

36 Uzao wake utadumu* milele;+

Kiti chake cha ufalme kitadumu kama jua mbele zangu.+

37 Kama mwezi, kitaimarishwa kabisa milele

Kama shahidi mwaminifu angani.” (Sela)

38 Lakini wewe mwenyewe umemtupa mbali na kumkataa;+

Umemkasirikia sana mtiwa-mafuta wako.

39 Umelikataa kwa dharau agano ulilofanya na mtumishi wako;

Umelichafua* taji lake kwa kulitupa ardhini.

40 Umezivunja kuta zake zote za mawe;*

Umezifanya ngome zake kuwa magofu.

41 Wote wanaopita karibu naye wamempora;

Yeye ni shutuma kwa jirani zake.+

42 Umewapa ushindi wapinzani wake;*+

Umewafanya maadui wake wote washangilie.

43 Pia umeusukuma nyuma upanga wake,

Na kumfanya ashindwe vitani.

44 Umekomesha fahari yake

Na kukitupa ardhini kiti chake cha ufalme.

45 Umefupisha siku zake za ujana;

Umemvisha aibu. (Sela)

46 Ee Yehova, utaendelea kujificha mpaka lini? Utajificha milele?+

Je, ghadhabu yako itaendelea kuwaka kama moto?

47 Kumbuka jinsi maisha yangu yalivyo mafupi!+

Je, uliwaumba wanadamu wote bila kusudi?

48 Ni mwanadamu gani anayeweza kuishi na asione kifo kamwe?+

Je, anaweza kujiokoa mwenyewe* kutoka katika nguvu za Kaburi?* (Sela)

49 Yako wapi matendo yako ya zamani ya upendo mshikamanifu, Ee Yehova,

Ambayo ulimwapia Daudi katika uaminifu wako?+

50 Kumbuka, Ee Yehova, dhihaka ambazo watumishi wako wanavurumishiwa;

Jinsi ninavyolazimika kuvumilia* dhihaka za mataifa yote;

51 Jinsi ambavyo maadui wako wamevurumisha matusi, Ee Yehova;

Jinsi ambavyo wameitukana kila hatua ya mtiwa-mafuta wako.

52 Yehova na asifiwe milele. Amina na Amina.+

KITABU CHA NNE

(Zaburi 90-106)

Sala ya Musa, mtu wa Mungu wa kweli.+

90 Ee Yehova, umekuwa makao yetu*+ katika vizazi vyote.

 2 Kabla milima haijazaliwa

Au kabla hujaiumba* dunia na nchi inayozaa,+

Tangu milele hadi milele, wewe ni Mungu.+

 3 Unamfanya mwanadamu anayeweza kufa arudi mavumbini;

Unasema: “Rudini, enyi wanadamu.”+

 4 Kwa maana miaka elfu moja machoni pako ni kama siku ya jana ambayo tayari imepita,+

Kama kesha moja tu la usiku.

 5 Unawafagilia mbali;+ wanakuwa kama usingizi tu;

Asubuhi, wao ni kama majani yanayochipuka.+

 6 Asubuhi yanachanua maua na kusitawi,

Lakini ifikapo jioni yamenyauka na kukauka.+

 7 Kwa maana tumemezwa na hasira yako+

Na kutishwa na ghadhabu yako.

 8 Unayaweka makosa yetu mbele zako;*+

Siri zetu zinafichuliwa na nuru ya uso wako.+

 9 Siku zetu zinadidimia* kwa sababu ya ghadhabu yako;

Na miaka yetu hufikia kikomo kama mnong’ono.*

10 Urefu wa maisha yetu ni miaka 70,

Au miaka 80+ ikiwa mtu ana nguvu za pekee.*

Lakini imejaa taabu na huzuni;

Nayo hupita haraka, nasi hutokomea.+

11 Ni nani anayeweza kuelewa nguvu za hasira yako?

Ghadhabu yako ni kubwa kama hofu unayostahili kuonyeshwa.+

12 Tufundishe jinsi ya kuhesabu siku zetu+

Ili tupate moyo wa hekima.

13 Rudi, Ee Yehova!+ Hali hiyo itadumu mpaka lini?+

Wahurumie watumishi wako.+

14 Tushibishe asubuhi kwa upendo wako mshikamanifu,+

Ili tupaze sauti kwa shangwe na kushangilia+ siku zetu zote.

15 Tufanye tushangilie kulingana na siku ambazo umetutesa,+

Kwa kadiri ya miaka mingi tuliyopata msiba.+

16 Watumishi wako na waone utendaji wako,

Na wana wao waone fahari yako.+

17 Kibali chako, Ee Yehova Mungu wetu, na kiwe juu yetu;

Na uifanikishe* kazi ya mikono yetu.

Naam, ifanikishe* kazi ya mikono yetu.+

91 Yeyote anayekaa mahali pa siri pa Aliye Juu Zaidi+

Ataishi katika kivuli cha Mweza-Yote.+

 2 Nitamwambia Yehova: “Wewe ni kimbilio langu na ngome yangu,+

Mungu wangu ninayemtumaini.”+

 3 Kwa maana atakuokoa usinaswe na mtego wa mwindaji wa ndege,

Kutoka kwa ugonjwa wa kuambukiza unaoangamiza.

 4 Kwa manyoya yake atakufunika,

Nawe utapata kimbilio chini ya mabawa yake.+

Uaminifu wake+ utakuwa ngao kubwa+ na ukuta wa ulinzi.*

 5 Hutaogopa vitisho vya usiku,+

Wala mshale unaoruka mchana,+

 6 Wala ugonjwa wa kuambukiza unaonyemelea gizani,

Wala maangamizi yanayoharibu wakati wa adhuhuri.

 7 Elfu moja wataanguka kando yako

Na elfu kumi mkono wako wa kulia,

Lakini hayatakukaribia wewe.+

 8 Utayaona tu kwa macho yako

Unaposhuhudia adhabu* ya waovu.

 9 Kwa sababu ulisema: “Yehova ni kimbilio langu,”

Umemfanya Aliye Juu Zaidi kuwa makao* yako;+

10 Hutapatwa na msiba,+

Na hakuna pigo litakalokaribia hema lako.

11 Kwa maana atawaagiza malaika zake+ kukuhusu wewe,

Ili kukulinda katika njia zako zote.+

12 Watakubeba mikononi mwao,+

Ili mguu wako usigonge jiwe.+

13 Utamkanyaga mwanasimba na swila;

Utamkanyagia chini simba mwenye manyoya marefu shingoni na nyoka mkubwa.+

14 Mungu alisema: “Kwa sababu ananipenda,* nitamwokoa.+

Nitamlinda kwa sababu analijua* jina langu.+

15 Ataniita, nami nitamjibu.+

Nitakuwa pamoja naye katika taabu.+

Nitamwokoa na kumtukuza.

16 Nitamshibisha kwa maisha marefu,+

Nami nitamfanya aone matendo yangu ya wokovu.”*+

Muziki. Wimbo wa siku ya Sabato.

92 Ni vema kukushukuru, Ee Yehova+

Na kuliimbia sifa* jina lako, Ee Uliye Juu Zaidi,

 2 Kutangaza upendo wako mshikamanifu+ asubuhi

Na uaminifu wako nyakati za usiku,

 3 Kwa kinanda cha nyuzi kumi na kwa udi,

Kwa sauti tamu ya kinubi.+

 4 Kwa maana umenifanya nishangilie, Ee Yehova, kwa sababu ya matendo yako;

Kwa sababu ya kazi za mikono yako ninapaza sauti kwa shangwe.

 5 Jinsi kazi zako zilivyo kuu, Ee Yehova!+

Jinsi mawazo yako yalivyo na kina sana!+

 6 Mtu yeyote asiyetumia akili hawezi kuyajua;

Na hakuna mtu yeyote mjinga anayeweza kuelewa hili:+

 7 Waovu wanapochipuka kama magugu*

Na watenda mabaya wote wanapositawi,

Ni ili waangamizwe milele.+

 8 Lakini wewe umekwezwa milele, Ee Yehova.

 9 Kwa kweli, watazame maadui wako wakishindwa, Ee Yehova,

Tazama jinsi maadui wako watakavyoangamia;

Watenda maovu wote watatawanywa.+

10 Lakini utazikweza nguvu zangu kama za* fahali mwitu;

Nitailainisha ngozi yangu kwa mafuta mapya.+

11 Macho yangu yatawaangalia maadui wangu wakishindwa;+

Masikio yangu yatasikia kuhusu kuangamia kwa watu waovu wanaonishambulia.

12 Lakini waadilifu watasitawi kama mtende

Na kuwa wakubwa kama mwerezi kule Lebanoni.+

13 Wamepandwa katika nyumba ya Yehova;

Wanasitawi katika nyua za Mungu wetu.+

14 Hata wakati wa uzeeni* wataendelea kunawiri;+

Wataendelea kuwa na nguvu* na kuwa wabichi,+

15 Wakitangaza kwamba Yehova ni mnyoofu.

Yeye ni Mwamba wangu,+ ambaye hana ukosefu wowote wa uadilifu.

93 Yehova amekuwa Mfalme!+

Amevaa adhama;

Yehova amevaa nguvu;

Huzivaa kama mshipi.

Dunia imeimarishwa kabisa;

Haiwezi kusogezwa.*

 2 Kiti chako cha ufalme kiliimarishwa kabisa zamani za kale;+

Umekuwapo tangu milele.+

 3 Mito imefurika, Ee Yehova,

Mito imefurika na kunguruma;

Mito inaendelea kufurika na kugonga kwa kishindo.

 4 Ana nguvu kuliko sauti ya maji mengi,

Ana nguvu kuliko mawimbi makubwa ya bahari,+

Yehova ni mwenye fahari mbinguni.+

 5 Vikumbusho vyako vinategemeka sana.+

Utakatifu unaipamba* nyumba yako nyakati zote,+ Ee Yehova.

94 Ee Mungu wa kisasi, Yehova,+

Ee Mungu wa kisasi, angaza!

 2 Inuka, Ee Mwamuzi wa dunia.+

Walipe wanachostahili watu wenye kiburi.+

 3 Waovu wataendelea mpaka lini, Ee Yehova,

Waovu wataendelea mpaka lini kushangilia?+

 4 Wanaropoka na kuongea kwa kiburi;

Watenda dhambi wote wanajigamba kujihusu.

 5 Wanawaponda watu wako, Ee Yehova,+

Na kuukandamiza urithi wako.

 6 Wanamuua mjane na mkaaji mgeni,

Na kuwaua mayatima.

 7 Wanasema: “Yah haoni;+

Mungu wa Yakobo hatambui jambo hilo.”+

 8 Eleweni jambo hili, ninyi msiotumia akili;

Ninyi wajinga, ni lini mtakapoonyesha ufahamu?+

 9 Yule aliyetengeneza* sikio, je, hawezi kusikia?

Yule aliyeumba jicho, je, hawezi kuona?+

10 Yule anayeyarekebisha mataifa, je, hawezi kukaripia?+

Yeye Ndiye anayewafundisha watu ujuzi!+

11 Yehova anajua mawazo ya wanadamu,

Ya kwamba ni pumzi tu.+

12 Mwenye furaha ni mtu unayemrekebisha, Ee Yah,+

Unayemfundisha kwa sheria yako,+

13 Ili kumpa utulivu katika siku za msiba,

Mpaka shimo litakapochimbwa kwa ajili ya mwovu.+

14 Kwa maana Yehova hatawaacha watu wake,+

Wala hatautupa urithi wake.+

15 Kwa maana kwa mara nyingine tena hukumu itakuwa ya uadilifu,

Na wote walio wanyoofu moyoni wataifuata.

16 Ni nani atakayeinuka dhidi ya waovu kwa ajili yangu?

Ni nani atakayenitetea dhidi ya watenda maovu?

17 Ikiwa Yehova hangekuwa msaidizi wangu,

Ningekuwa nimeangamia upesi.*+

18 Niliposema: “Mguu wangu unateleza,”

Upendo wako mshikamanifu, Ee Yehova, uliendelea kunitegemeza.+

19 Mahangaiko* yaliponilemea,*

Ulinifariji na kunibembeleza.*+

20 Je, kiti cha ufalme* chenye ufisadi kinaweza kuungana nawe

Wakati kinapotunga matatizo kwa kutumia sheria?*+

21 Wanamshambulia vikali mwadilifu+

Na kumhukumu asiye na hatia auawe.*+

22 Lakini Yehova atakuwa kimbilio langu salama,*

Mungu wangu ni mwamba wangu ninaokimbilia.+

23 Atafanya matendo yao maovu yawarudie.+

Atawaangamiza* kwa uovu wao wenyewe.

Yehova Mungu wetu atawaangamiza.*+

95 Njooni, na tumshangilie Yehova kwa sauti!

Na tumpazie sauti kwa ushindi Mwamba wetu wa wokovu.+

 2 Twendeni mbele zake* tukiwa na shukrani;+

Na tuimbe na kumpazia sauti kwa ushindi.

 3 Kwa maana Yehova ni Mungu mkuu,

Mfalme mkuu juu ya miungu mingine yote.+

 4 Sehemu zenye kina za dunia zimo mkononi mwake;

Vilele vya milima ni vyake.+

 5 Bahari, ambayo aliiumba, ni yake,+

Na mikono yake ilitengeneza nchi kavu.+

 6 Njooni, tuabudu na kuinama;

Na tupige magoti mbele za Yehova Muumba wetu.+

 7 Kwa maana yeye ni Mungu wetu,

Na sisi ni watu wa malisho yake,

Kondoo anaowatunza.*+

Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake,+

 8 Msiufanye moyo wenu kuwa mgumu kama mlivyofanya kule Meriba,*+

Kama katika siku ya Masa* kule nyikani,+

 9 Mababu zenu waliponijaribu;+

Walinipima, ingawa walikuwa wameona matendo yangu.+

10 Kwa miaka 40 nilichukizwa na kizazi hicho, nikasema:

“Wao ni watu wanaopotoka sikuzote katika mioyo yao;

Hawajazijua njia zangu.”

11 Kwa hiyo niliapa kwa hasira yangu:

“Hawataingia katika pumziko langu.”+

96 Mwimbieni Yehova wimbo mpya.+

Mwimbieni Yehova, dunia yote!+

 2 Mwimbieni Yehova; lisifuni jina lake.

Tangazeni habari njema za wokovu wake siku baada ya siku.+

 3 Tangazeni utukufu wake miongoni mwa mataifa,

Kazi zake zinazostaajabisha miongoni mwa mataifa yote.+

 4 Yehova ni mkuu na anastahili kusifiwa kuliko wote.

Anaogopesha kuliko miungu mingine yote.

 5 Miungu yote ya mataifa ni miungu ya ubatili,+

Lakini Yehova ndiye aliyeziumba mbingu.+

 6 Mbele zake kuna utukufu* na fahari;+

Nguvu na uzuri umo mahali pake patakatifu.+

 7 Mpeni Yehova anachostahili, enyi familia za mataifa,

Mpeni Yehova anachostahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+

 8 Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili;+

Leteni zawadi na mwingie katika nyua zake.

 9 Mwinamieni* Yehova katika mapambo matakatifu;*

Tetemekeni mbele zake, dunia yote!

10 Tangazeni miongoni mwa mataifa: “Yehova amekuwa Mfalme!+

Dunia imeimarishwa kabisa, haiwezi kusogezwa.*

Atayahukumu* mataifa kwa haki.”+

11 Mbingu na zishangilie, dunia na iwe na shangwe;

Bahari na ingurume na vitu vyote vinavyoijaza;+

12 Mashamba na vitu vyote vilivyomo na vishangilie.+

Wakati uleule miti yote ya msituni na ishangilie kwa sauti+

13 Mbele za Yehova, kwa maana anakuja,*

Anakuja kuihukumu dunia.

Ataihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa+

Na mataifa kwa uaminifu wake.+

97 Yehova amekuwa Mfalme!+

Dunia na iwe na shangwe.+

Na visiwa vyake vingi vishangilie.+

 2 Mawingu na giza zito vinamzunguka;+

Uadilifu na haki ndio msingi wa kiti chake cha ufalme.+

 3 Moto hutangulia mbele zake+

Na kuwateketeza kabisa maadui wake pande zote.+

 4 Umeme wake wa radi huiangazia nchi;

Dunia huona na kutetemeka.+

 5 Milima huyeyuka kama nta mbele za Yehova,+

Mbele za Bwana wa dunia yote.

 6 Mbingu hutangaza uadilifu wake,

Na mataifa yote huona utukufu wake.+

 7 Wote wanaoabudu sanamu yoyote ya kuchongwa na waaibishwe,+

Wale wanaojigamba kuhusu miungu yao ya ubatili.+

Mwinamieni,* enyi miungu yote.+

 8 Sayuni husikia na kufurahi;+

Miji ya Yuda ina* shangwe

Kwa sababu ya hukumu zako, Ee Yehova.+

 9 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote;

Umekwezwa juu zaidi ya miungu mingine yote.+

10 Enyi mnaompenda Yehova, chukieni maovu.+

Anaulinda uhai wa* washikamanifu wake;+

Huwaokoa kutoka katika mkono wa* mwovu.+

11 Nuru imemwangazia mwadilifu+

Na shangwe walio wanyoofu moyoni.

12 Shangilieni kwa sababu ya Yehova, enyi waadilifu,

Na mlishukuru jina lake takatifu.*

Muziki.

98 Mwimbieni Yehova wimbo mpya,+

Kwa maana ametenda mambo yanayostaajabisha.+

Mkono wake wa kuume, mkono wake mtakatifu, umeleta wokovu.*+

 2 Yehova ameutangaza wokovu wake;+

Amefunua uadilifu wake mbele ya mataifa.+

 3 Amekumbuka upendo wake mshikamanifu na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli.+

Miisho yote ya dunia imeona wokovu kutoka kwa* Mungu wetu.+

 4 Mpazieni Yehova sauti ya ushindi, dunia yote.

Changamkeni na kupaza sauti kwa shangwe na kuimba sifa.*+

 5 Mwimbieni sifa* Yehova kwa kinubi,

Kwa kinubi na wimbo mtamu.

 6 Kwa tarumbeta na mlio wa pembe,+

Pazeni sauti kwa ushindi mbele za Mfalme, Yehova.

 7 Bahari na ingurume na vitu vyote vinavyoijaza,

Dunia na wote wanaokaa humo.

 8 Mito na ipige makofi;

Milima na ipaze sauti pamoja kwa shangwe+

 9 Mbele za Yehova, kwa maana anakuja* kuihukumu dunia.

Ataihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa+

Na mataifa kwa haki.+

99 Yehova amekuwa Mfalme.+ Mataifa na yatetemeke.

Anaketi kwenye kiti cha ufalme juu ya* makerubi.+ Dunia na itikisike.

 2 Yehova ni mkuu Sayuni,

Naye yuko juu ya mataifa yote.+

 3 Na walisifu jina lako kuu,+

Kwa maana linaogopesha, nalo ni takatifu.

 4 Yeye ni mfalme hodari anayependa haki.+

Umeimarisha kabisa mambo manyoofu.

Umetekeleza haki na uadilifu+ katika Yakobo.

 5 Mkwezeni Yehova Mungu wetu+ na kuinama chini* mbele ya kiti cha miguu yake;+

Yeye ni mtakatifu.+

 6 Musa na Haruni walikuwa miongoni mwa makuhani wake,+

Na Samweli alikuwa miongoni mwa wale walioliita jina lake.+

Walikuwa wakimwita Yehova,

Naye alikuwa akiwajibu.+

 7 Alikuwa akiongea nao kutoka katika nguzo ya wingu.+

Walishika vikumbusho vyake na amri aliyowapa.+

 8 Ee Yehova Mungu wetu, uliwajibu.+

Ulikuwa Mungu uliyewasamehe,+

Lakini uliwaadhibu* kwa sababu ya dhambi walizotenda.+

 9 Mkwezeni Yehova Mungu wetu+

Na mwiname chini* mbele ya mlima wake mtakatifu,+

Kwa maana Yehova Mungu wetu ni mtakatifu.+

Muziki wa shukrani.

100 Mpazieni Yehova sauti ya ushindi, dunia yote.+

 2 Mtumikieni Yehova kwa kushangilia.+

Njooni mbele zake kwa kelele za shangwe.

 3 Jueni* kwamba Yehova ni Mungu.+

Yeye ndiye aliyetuumba, na sisi ni mali yake.*+

Sisi ni watu wake na kondoo wa malisho yake.+

 4 Ingieni katika malango yake kwa shukrani,+

Katika nyua zake kwa sifa.+

Mshukuruni yeye; lisifuni jina lake.+

 5 Kwa maana Yehova ni mwema;+

Upendo wake mshikamanifu unadumu milele,

Na uaminifu wake katika vizazi vyote.+

Muziki wa Daudi.

101 Nitaimba kuhusu upendo mshikamanifu na haki.

Nitakuimbia sifa,* Ee Yehova.

 2 Nitatenda kwa busara na bila lawama.*

Utanijia lini?

Nitatembea kwa utimilifu wa moyo+ ndani ya nyumba yangu.

 3 Sitaweka kitu chochote kisichofaa* mbele ya macho yangu.

Ninachukia matendo ya wale wanaokengeuka kutoka kwa jambo lililo sawa;+

Sitashirikiana nao kamwe.*

 4 Moyo uliopotoka uko mbali nami;

Sitakubali* jambo lililo ovu.

 5 Yeyote anayemchongea jirani yake kwa siri,+

Nitamnyamazisha.*

Yeyote aliye na macho ya kiburi na moyo wenye majivuno,

Sitamvumilia.

 6 Nitawatazama waaminifu wa dunia,

Ili wakae nami.

Yule anayetembea bila lawama* atanihudumia.

 7 Hakuna mtu yeyote mdanganyifu atakayekaa katika nyumba yangu,

Na hakuna mwongo atakayesimama mbele yangu.*

 8 Kila asubuhi nitawanyamazisha* waovu wote wa dunia,

Nitawaangamiza waovu wote kutoka katika jiji la Yehova.+

Sala ya mtu aliyekandamizwa, anapokuwa amekata tamaa* na kummwagia Yehova mahangaiko yake.+

102 Ee Yehova, sikia sala yangu;+

Kilio changu cha kuomba msaada na kikufikie.+

 2 Usinifiche uso wako ninapokuwa katika taabu.+

Nitegee sikio lako;*

Nijibu haraka ninapokuita.+

 3 Kwa maana siku zangu zinatoweka kama moshi,

Na mifupa yangu imeungua na kuwa myeusi kama tanuru.+

 4 Moyo wangu umepigwa kama majani na umenyauka,+

Kwa maana ninasahau kula chakula changu.

 5 Kwa sababu ya kilio changu kikubwa cha maumivu,+

Mifupa yangu inashikamana na nyama yangu.+

 6 Mimi ni kama mwari wa nyikani;

Mimi ni kama bundi mdogo katikati ya magofu.

 7 Nikilala sipati usingizi;*

Mimi ni kama ndege aliye peke yake juu ya paa.+

 8 Mchana kutwa maadui wangu wananidhihaki.+

Wale wanaonidhihaki* wanatumia jina langu kama laana.

 9 Kwa maana ninakula majivu kama mkate,+

Na kinywaji changu kimechanganyika na machozi,+

10 Kwa sababu ya hasira yako na ghadhabu yako,

Kwa maana uliniinua juu ili unitupe tu pembeni.

11 Siku zangu zinafifia kama kivuli,*+

Nami ninanyauka kama majani.+

12 Lakini wewe unadumu milele, Ee Yehova,+

Na umaarufu wako utadumu* katika vizazi vyote.+

13 Kwa hakika utainuka na kulionyesha rehema Sayuni,+

Kwa maana ni wakati wa kulionyesha kibali chako;+

Wakati uliowekwa umefika.+

14 Kwa maana watumishi wako wanayathamini mawe yake+

Nao wanayapenda hata mavumbi yake.+

15 Mataifa yataliogopa jina la Yehova,

Na wafalme wote wa dunia utukufu wako.+

16 Kwa maana Yehova atalijenga upya Sayuni;+

Atatokea katika utukufu wake.+

17 Ataisikiliza sala ya maskini;+

Hataidharau sala yao.+

18 Hili limeandikwa kwa ajili ya kizazi cha wakati ujao,+

Ili watu watakaozaliwa* baadaye wamsifu Yah.

19 Kwa maana yeye hutazama chini kutoka katika makao yake matakatifu yaliyo juu,+

Kutoka mbinguni Yehova huitazama dunia,

20 Ili asikie kilio cha maumivu cha mfungwa,+

Ili awaweke huru wale waliohukumiwa kifo,+

21 Ili jina la Yehova litangazwe Sayuni+

Na sifa yake Yerusalemu,

22 Mataifa na falme

Zinapokusanyika pamoja ili kumtumikia Yehova.+

23 Alininyang’anya nguvu zangu kabla ya wakati;

Alifupisha siku zangu.

24 Nikasema: “Ee Mungu wangu,

Usiniangamize nikiwa katikati ya maisha yangu,

Wewe ambaye miaka yako inadumu katika vizazi vyote.+

25 Zamani za kale uliiweka misingi ya dunia,

Na mbingu ni kazi ya mikono yako.+

26 Zitaangamia, lakini wewe utadumu;

Zote zitachakaa kama vazi.

Na kama nguo utazibadili, nazo zitatokomea.

27 Lakini wewe ni yuleyule, na miaka yako haitaisha kamwe.+

28 Watoto wa watumishi wako watakaa kwa usalama,

Na uzao wao utaimarishwa kabisa mbele zako.”+

Wa Daudi.

103 Nafsi yangu na imsifu Yehova;

Kila kitu kilicho ndani yangu na kilisifu jina lake takatifu.

 2 Nafsi yangu na imsifu Yehova;

Nami nisisahau kamwe mambo yote aliyotenda.+

 3 Husamehe makosa yako yote+

Na kuyaponya magonjwa yako yote;+

 4 Huukomboa uhai wako kutoka shimoni*+

Na kukuvika taji la upendo wake mshikamanifu na rehema.+

 5 Hukushibisha kwa vitu vyema+ maisha yako yote,

Hivi kwamba ujana wako unarudishwa upya kama ule wa tai.+

 6 Yehova hutenda kwa uadilifu+ na haki

Kwa ajili ya wote wanaokandamizwa.+

 7 Alimjulisha Musa njia zake,+

Na wana wa Israeli matendo yake.+

 8 Yehova ni mwenye rehema na mwenye huruma,*+

Si mwepesi wa hasira naye ana upendo mwingi mshikamanifu.*+

 9 Hatatafuta makosa sikuzote,+

Wala hataendelea kuwa na hasira milele.+

10 Hajatutendea kulingana na dhambi zetu,+

Wala hajatupa adhabu tuliyostahili kulingana na makosa yetu.+

11 Kwa maana kama mbingu zilivyo juu kuliko dunia,

Ndivyo upendo wake mshikamanifu ulivyo mkubwa kuelekea wale wanaomwogopa.+

12 Kama mashariki ilivyo mbali sana na magharibi,

Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali sana na sisi.+

13 Kama baba anavyowaonyesha wanawe rehema,

Ndivyo ambavyo Yehova amewaonyesha rehema wale wanaomwogopa.+

14 Kwa maana anajua vema umbo letu,+

Akikumbuka kwamba sisi ni mavumbi.+

15 Siku za mwanadamu anayeweza kufa ni kama za majani;+

Yeye huchanua kama ua la shambani.+

16 Lakini upepo unapovuma, linatoweka,

Kana kwamba halikuwahi kuwepo.*

17 Lakini upendo mshikamanifu wa Yehova ni wa milele na milele*

Kuelekea wale wanaomwogopa,+

Na uadilifu wake kuelekea watoto wa watoto wao,+

18 Kuelekea wale wanaolishika agano lake+

Na wale walio waangalifu ili kuyashika maagizo yake.

19 Yehova amekiimarisha kabisa kiti chake cha ufalme mbinguni;+

Nao ufalme wake unatawala kila kitu.+

20 Msifuni Yehova, enyi malaika wake wote,+ mlio na nguvu nyingi,

Mnaotekeleza neno lake,+ mkitii sauti yake.*

21 Msifuni Yehova, enyi majeshi yake yote,+

Ninyi wahudumu wake mnaofanya mapenzi yake.+

22 Msifuni Yehova, kazi zake zote,

Kila mahali anapotawala.*

Nafsi yangu yote na imsifu Yehova.

104 Nafsi yangu na imsifu Yehova.+

Ee Yehova Mungu wangu, wewe ni mkuu sana.+

Umevaa utukufu* na fahari.+

 2 Umejifunika nuru+ kama vazi;

Unazitandaza mbingu kama kitambaa cha hema.+

 3 Hujenga boriti za vyumba vyake vya juu katika maji yaliyo juu,*+

Akiyafanya mawingu kuwa gari lake,+

Akienda juu ya mabawa ya upepo.+

 4 Huwafanya malaika wake kuwa roho,

Wahudumu wake kuwa moto unaoteketeza kabisa.+

 5 Ameiimarisha dunia juu ya misingi yake;+

Haitasogezwa kutoka mahali pake* milele na milele.+

 6 Uliifunika kwa vilindi vya maji kama kwa vazi.+

Maji yalisimama juu ya milima.

 7 Kwa kemeo lako yalikimbia;+

Kwa sauti ya mngurumo wako yalikimbia kwa wasiwasi

 8 —Milima ilipanda+ na mabonde yakashuka—

Mahali ulipokusudia yawepo.

 9 Uliweka mpaka ambao hayapaswi kuvuka,+

Ili yasiifunike dunia tena kamwe.

10 Wewe hupeleka chemchemi katika mabonde;*

Kati ya milima zinatiririka.

11 Zinawapa maji wanyama wote wa mwituni;

Punda mwitu hukata kiu yake.

12 Juu yake ndege wa angani hukaa;

Wanaimba katikati ya majani mengi.

13 Anainywesha milima maji kutoka katika vyumba vyake vya juu.+

Dunia hushibishwa kwa matunda ya kazi zako.+

14 Anaotesha majani kwa ajili ya ng’ombe

Na mimea kwa ajili ya matumizi ya wanadamu,+

Ili chakula kikue ardhini

15 Na divai inayofanya moyo wa mwanadamu ushangilie,+

Mafuta yanayofanya uso ung’ae,

Na mkate unaotegemeza moyo wa mwanadamu anayeweza kufa.+

16 Miti ya Yehova imetosheka,

Mierezi ya Lebanoni aliyopanda,

17 Ambamo ndege hutengeneza viota.

Makao ya korongo+ ni miberoshi.

18 Milima mirefu ni ya mbuzi wa milimani;+

Majabali ni kimbilio la wibari.+

19 Ameuumba mwezi ili upime nyakati zilizowekwa;

Jua linajua vizuri wakati wa kutua.+

20 Wewe unaleta giza, usiku unaingia,+

Wakati ambapo wanyama wote wa mwituni wanazunguka-zunguka.

21 Wanasimba* hunguruma ili wapate mawindo+

Na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.+

22 Jua linapochomoza,

Wanarudi na kulala katika mapango yao.

23 Mwanadamu huenda kwenye kazi yake,

Naye hufanya kazi kwa jasho mpaka jioni.

24 Jinsi kazi zako zilivyo nyingi sana, Ee Yehova!+

Umezifanya zote kwa hekima.+

Dunia imejaa vitu ulivyoumba.

25 Kisha kuna bahari, ni kubwa sana na pana,

Imejaa viumbe walio hai wasio na idadi, wadogo kwa wakubwa.+

26 Humo meli husafiri,

Na Lewiathani,*+ uliyemuumba ili acheze humo.

27 Wote wanakungojea wewe

Uwape chakula chao kwa wakati wake.+

28 Wanakusanya unachowapa.+

Unapofumbua mkono wako, wanashiba vitu vyema.+

29 Ukiuficha uso wako, wanahangaika.

Ukiiondoa roho yao, wanakufa na kurudi mavumbini.+

30 Ukiituma roho yako, wanaumbwa,+

Nawe unaifanya ardhi iwe na sura mpya.

31 Utukufu wa Yehova utadumu milele.

Yehova atashangilia kwa sababu ya kazi zake.+

32 Huitazama dunia, inatetemeka;

Huigusa milima, inafuka moshi.+

33 Nitamwimbia Yehova+ maisha yangu yote;

Nitamwimbia sifa* Mungu wangu maadamu ninaishi.+

34 Mawazo yangu na yampendeze.*

Nitashangilia kwa sababu ya Yehova.

35 Watenda dhambi watatoweka duniani,

Na waovu hawatakuwapo tena.+

Nafsi yangu na imsifu Yehova. Msifuni Yah!*

105 Mshukuruni Yehova,+ liitieni jina lake,

Yajulisheni mataifa matendo yake!+

 2 Mwimbieni, mwimbieni sifa,*

Tafakarini* kazi zake zote zinazostaajabisha.+

 3 Jivunieni jina lake takatifu.+

Mioyo ya wale wanaomtafuta Yehova na ishangilie.+

 4 Mtafuteni Yehova+ na nguvu zake.

Utafuteni uso* wake daima.

 5 Kumbukeni kazi zinazostaajabisha alizofanya,

Miujiza yake na hukumu alizotangaza,+

 6 Enyi uzao wa* Abrahamu mtumishi wake,+

Enyi wana wa Yakobo, watu wake aliowachagua.+

 7 Yeye ni Yehova Mungu wetu.+

Hukumu zake ziko duniani kote.+

 8 Anakumbuka agano lake milele,+

Ahadi aliyotoa,* hata kufikia vizazi elfu,+

 9 Agano alilofanya na Abrahamu,+

Na kiapo alichomwapia Isaka,+

10 Alichotoa kama amri kwa Yakobo

Na kama agano la kudumu kwa Israeli,

11 Akisema, “Nitakupa nchi ya Kanaani+

Kuwa urithi wako uliogawiwa.”+

12 Wakati walipokuwa wachache,+

Naam, wachache sana, nao walikuwa wageni nchini.+

13 Walitembeatembea kutoka taifa moja hadi taifa lingine,

Kutoka ufalme mmoja hadi ufalme mwingine.+

14 Hakumruhusu mtu yeyote awakandamize,+

Lakini kwa sababu yao aliwakaripia wafalme,+

15 Akisema, “Msiwaguse watiwa-mafuta wangu,

Wala msiwatendee manabii wangu jambo lolote baya.”+

16 Alileta njaa kali nchini;+

Alifanya wakose mikate.*

17 Alimtuma mtu awatangulie

Ambaye aliuzwa kuwa mtumwa, Yosefu.+

18 Waliifunga* miguu yake kwa pingu,+

Shingo yake ilitiwa katika vyuma;*

19 Mpaka wakati ambapo neno lake lilitimia,+

Neno la Yehova ndilo lililomsafisha.

20 Mfalme aliamuru afunguliwe,+

Mtawala wa mataifa akamweka huru.

21 Akamweka kuwa bwana mkubwa wa nyumba yake,

Mtawala wa mali zake zote,+

22 Ili awe na mamlaka juu ya* wakuu wake kama alivyopenda*

Na kuwafundisha wazee wake hekima.+

23 Kisha Israeli akaja Misri,+

Na Yakobo akakaa akiwa mgeni katika nchi ya Hamu.

24 Mungu aliwafanya watu wake waongezeke sana;+

Aliwafanya wawe na nguvu kuliko maadui wao,+

25 Akaruhusu mioyo yao ibadilike ili wawachukie watu wake,

Ili wapange njama dhidi ya watumishi wake.+

26 Alimtuma Musa mtumishi wake,+

Na Haruni,+ aliyekuwa amemchagua.

27 Walifanya ishara zake kati yao,

Miujiza yake katika nchi ya Hamu.+

28 Alilituma giza na nchi ikawa giza;+

Hawakuasi maneno yake.

29 Alibadili maji yao yakawa damu

Na kuwaua samaki wao.+

30 Nchi yao ikajaa vyura,+

Hata katika vyumba vya mfalme.

31 Aliagiza nzi wavamie

Na mbu* katika maeneo yao yote.+

32 Aliibadili mvua yao ikawa mvua ya mawe

Naye akatuma radi* katika nchi yao.+

33 Aliipiga mizabibu yao na mitini yao

Na kuivunjavunja miti ya eneo lao.

34 Aliagiza nzige wavamie,

Nzige wachanga wasio na idadi.+

35 Walikula kabisa mimea yote nchini,

Nao wakala kabisa mazao ya ardhi.

36 Kisha akamuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi yao,+

Mwanzo wa nguvu zao za uzazi.

37 Aliwatoa nje watu wake wakiwa na fedha na dhahabu;+

Na hakuna yeyote katika makabila yake aliyejikwaa.

38 Misri ilishangilia walipoondoka,

Kwa maana hofu ya Israeli* ilikuwa imewashika.+

39 Alitandaza wingu ili liwafunike+

Na moto uangaze wakati wa usiku.+

40 Waliomba, naye akaleta kware;+

Aliendelea kuwashibisha mkate kutoka mbinguni.+

41 Alifungua mwamba, maji yakatiririka kutoka humo;+

Maji hayo yalitiririka jangwani kama mto.+

42 Kwa maana aliikumbuka ahadi takatifu aliyompa Abrahamu mtumishi wake.+

43 Kwa hiyo akawatoa watu wake wakishangilia,+

Watu wake aliowachagua aliwatoa kwa kilio cha shangwe.

44 Aliwapa nchi za mataifa;+

Walirithi vitu ambavyo mataifa mengine yalikuwa yametaabika kuvipata,+

45 Ili waweze kutii maagizo yake+

Na kushika sheria zake.

Msifuni Yah!*

106 Msifuni Yah!*

Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+

Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+

 2 Ni nani anayeweza kutangaza kikamili matendo ya Yehova yenye nguvu

Au kutangaza matendo yake yote yanayostahili sifa?+

 3 Wenye furaha ni wale wanaotenda haki,

Ambao sikuzote wanatenda yaliyo sawa.+

 4 Nikumbuke, Ee Yehova, unapowaonyesha kibali* watu wako.+

Nitunze kwa matendo yako ya wokovu,

 5 Ili nifurahie wema unaowaonyesha watu wako uliowachagua,+

Ili nishangilie pamoja na taifa lako,

Ili nikusifu kwa fahari* pamoja na urithi wako.

 6 Tumetenda dhambi kama mababu zetu;+

Tumetenda kosa; tumetenda uovu.+

 7 Mababu zetu kule Misri hawakuthamini* kazi zako zinazostaajabisha.

Hawakukumbuka upendo wako mwingi mshikamanifu,

Bali waliasi baharini, kando ya Bahari Nyekundu.+

 8 Lakini aliwaokoa kwa ajili ya jina lake,+

Ili kufanya nguvu zake zijulikane.+

 9 Aliikemea Bahari Nyekundu, ikakauka;

Aliwaongoza katika vilindi vyake kana kwamba wanapitia jangwani;*+

10 Aliwaokoa kutoka mikononi mwa adui yao+

Na kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.+

11 Maji yaliwafunika maadui wao;

Hakuna hata mmoja wao aliyeokoka.*+

12 Kisha wakawa na imani katika ahadi yake;+

Wakaanza kuimba sifa yake.+

13 Lakini walisahau haraka mambo aliyotenda;+

Hawakungojea ushauri wake.

14 Walifuata tamaa zao za kichoyo nyikani;+

Walimjaribu Mungu jangwani.+

15 Aliwapa walichoomba,

Lakini akawapiga kwa ugonjwa uliowadhoofisha.+

16 Walimwonea wivu Musa kambini

Na Haruni,+ mtakatifu wa Yehova.+

17 Kisha dunia ikafunguka na kummeza Dathani

Na kuwafunika wale waliokusanyika pamoja na Abiramu.+

18 Moto uliwaka katika kundi lao;

Mwali wa moto ukawateketeza kabisa waovu.+

19 Walitengeneza ndama kule Horebu

Na kuiinamia sanamu ya chuma;*+

20 Waliubadili utukufu wangu

Kwa mfano wa ng’ombe dume anayekula nyasi.+

21 Walimsahau Mungu+ Mwokozi wao,

Aliyetenda mambo makuu nchini Misri,+

22 Kazi zinazostaajabisha katika nchi ya Hamu,+

Mambo yanayoogopesha kwenye Bahari Nyekundu.+

23 Alikuwa karibu kuamuru waangamizwe,

Lakini Musa, mchaguliwa wake, akaingilia kati*

Ili kuzuia hasira yake inayoangamiza.+

24 Kisha wakaidharau ile nchi inayotamanika;+

Hawakuwa na imani katika ahadi yake.+

25 Waliendelea kunung’unika katika mahema yao;+

Hawakuisikiliza sauti ya Yehova.+

26 Kwa hiyo akainua mkono wake na kuapa kuwahusu

Kwamba angewaangusha nyikani;+

27 Angewaangusha wazao wao miongoni mwa mataifa,

Naye angewatawanya katika nchi mbalimbali.+

28 Kisha wakajiunga* na ibada ya Baali wa Peori,+

Nao wakala dhabihu zilizotolewa kwa waliokufa.*

29 Walimkasirisha kwa matendo yao,+

Na pigo likazuka miongoni mwao.+

30 Lakini Finehasi alipoinuka na kuingilia kati,

Pigo hilo lilikomeshwa.+

31 Na jambo hilo likahesabiwa kwake kuwa uadilifu

Katika vizazi vyote milele.+

32 Walimkasirisha kwenye maji ya Meriba,*

Na mambo yakamwendea Musa vibaya kwa sababu yao.+

33 Waliitia uchungu roho yake,

Naye akaongea bila kufikiri kwa midomo yake.+

34 Hawakuyaangamiza mataifa,+

Kama Yehova alivyokuwa amewaamuru.+

35 Lakini walichangamana na mataifa hayo+

Na kuzikubali* njia zao.+

36 Waliendelea kuabudu sanamu zao,+

Nazo zikawa mtego kwao.+

37 Waliwatoa dhabihu wana wao

Na mabinti wao kwa roho waovu.+

38 Waliendelea kumwaga damu isiyo na hatia,+

Damu ya wana wao na mabinti wao wenyewe

Ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani;+

Na nchi ikachafuliwa kwa umwagaji wa damu.

39 Wakawa wachafu kwa sababu ya kazi zao;

Walifanya ukahaba wa kiroho kwa matendo yao.+

40 Kwa hiyo hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya watu wake,

Naye akauchukia sana urithi wake.

41 Aliwatia tena na tena mikononi mwa mataifa,+

Ili wale waliowachukia waweze kuwatawala.+

42 Maadui wao waliwakandamiza,

Nao wakatiishwa chini ya nguvu zao.*

43 Aliwaokoa mara nyingi,+

Lakini walikuwa wakiasi na kukosa kutii,+

Nao walikuwa wakifedheheshwa kwa sababu ya makosa yao.+

44 Lakini alikuwa akiona taabu yao+

Na kusikia kilio chao cha kuomba msaada.+

45 Na kwa ajili yao alikuwa akikumbuka agano lake,

Naye alikuwa akiwahurumia,* akichochewa na upendo wake mwingi* mshikamanifu.+

46 Alikuwa akisababisha wahurumiwe

Na wote waliowachukua mateka.+

47 Tuokoe, Ee Yehova Mungu wetu,+

Na kutukusanya kutoka katika mataifa+

Ili tulishukuru jina lako takatifu

Na tushangilie kukusifu wewe.*+

48 Yehova, Mungu wa Israeli, na asifiwe

Kwa umilele wote.*+

Na watu wote waseme, “Amina!”*

Msifuni Yah!*

KITABU CHA TANO

(Zaburi 107-150)

107 Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+

Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+

 2 Wale waliokombolewa* na Yehova na waseme jambo hilo,

Wale aliowakomboa kutoka mikononi mwa* adui,+

 3 Wale aliowakusanya pamoja kutoka katika nchi mbalimbali,+

Kutoka mashariki na kutoka magharibi,*

Kutoka kaskazini na kutoka kusini.+

 4 Walitangatanga nyikani, jangwani;

Hawakupata njia ya kwenda katika jiji ambamo wangeweza kuishi.

 5 Walikuwa na njaa na kiu;

Walidhoofika kwa sababu ya uchovu.

 6 Waliendelea kumlilia Yehova walipokuwa wakitaabika;+

Aliwaokoa kutoka katika dhiki yao.+

 7 Aliwaongoza kutembea katika njia inayofaa+

Ili wafike katika jiji ambamo wangeweza kuishi.+

 8 Watu na wamshukuru Yehova+ kwa sababu ya upendo wake mshikamanifu

Na kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu.+

 9 Kwa maana amewatosheleza wenye kiu*

Na kuwashibisha wenye njaa* kwa vitu vyema.+

10 Baadhi yao walikuwa wakiishi katika giza zito sana,

Wafungwa walioteseka na kufungwa kwa vyuma.

11 Kwa maana walikuwa wameliasi neno la Mungu;

Waliudharau ushauri wa Aliye Juu Zaidi.+

12 Kwa hiyo aliinyenyekeza mioyo yao kupitia taabu;+

Walijikwaa, na hakukuwa na yeyote wa kuwasaidia.

13 Walimlilia Yehova awasaidie walipokuwa wakitaabika;

Akawaokoa kutoka katika dhiki yao.

14 Aliwatoa katika giza zito sana,

Na kuzikata pingu zao.+

15 Watu na wamshukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mshikamanifu+

Na kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu.

16 Kwa maana ameivunja milango ya shaba

Na kuyakata makomeo ya chuma.+

17 Walikuwa wapumbavu, nao wakateseka+

Kwa sababu ya makosa yao na dhambi zao.+

18 Walipoteza hamu ya kula kila aina ya chakula;*

Waliyakaribia malango ya kifo.

19 Walikuwa wakimlilia Yehova awasaidie walipokuwa wakitaabika;

Naye alikuwa akiwaokoa kutoka katika dhiki yao.

20 Alikuwa akituma neno lake na kuwaponya+

Na kuwaokoa kutoka katika mashimo ambamo walikuwa wamenaswa.

21 Watu na wamshukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mshikamanifu

Na kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu.

22 Na watoe dhabihu za shukrani+

Na kutangaza kazi zake kwa kilio cha shangwe.

23 Wale wanaosafiri kwa meli baharini,

Wanaofanya biashara yao kwenye maji mengi,+

24 Wameziona kazi za Yehova

Na kazi zake zinazostaajabisha zilizo vilindini;+

25 Jinsi dhoruba ya upepo inavyoinuka kwa neno lake,+

Na kuyainua mawimbi ya bahari.

26 Hayo huinuka juu angani;

Hushuka chini kwa nguvu vilindini.

Ujasiri wao* huyeyuka kwa sababu ya msiba unaokaribia.

27 Wao hugaagaa na kupepesuka kama mlevi,

Na ustadi wao wote unakosa manufaa kabisa.+

28 Kisha wanamlilia Yehova kwa sauti wanapotaabika,+

Naye huwaokoa kutoka katika dhiki yao.

29 Yeye huituliza dhoruba ya upepo;

Mawimbi ya bahari hunyamaza.+

30 Wanashangilia yanapotulia,

Naye huwaongoza kwenda kwenye bandari wanayotamani.

31 Watu na wamshukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mshikamanifu

Na kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu.+

32 Na wamkweze katika kutaniko la watu,+

Na wamsifu katika baraza la* wazee.

33 Yeye hubadili mito kuwa jangwa,

Na chemchemi za maji kuwa ardhi iliyokauka,+

34 Nchi inayozaa kuwa nchi iliyoharibika yenye chumvi,+

Kwa sababu ya uovu wa wale wanaokaa humo.

35 Yeye hulibadili jangwa kuwa madimbwi ya maji yenye matete,

Na nchi kavu kuwa chemchemi za maji.+

36 Huwafanya wenye njaa wakae humo,+

Ili wajenge jiji ambamo wanaweza kuishi.+

37 Wanapanda mbegu mashambani na kupanda mashamba ya mizabibu+

Yanayozaa mazao mengi.+

38 Huwabariki, nao huongezeka sana;

Haachi ng’ombe wao wapungue.+

39 Kisha wanakuwa wachache tena na kuaibishwa

Kwa sababu ya ukandamizaji, msiba, na huzuni.

40 Huwamwagia wakuu dharau

Na kuwafanya watangetange jangwani kusiko na njia.+

41 Lakini huwalinda* maskini ili wasikandamizwe+

Na kufanya familia zao ziwe nyingi kama kundi la kondoo.

42 Wanyoofu huona hilo na kushangilia;+

Lakini waovu wote hufunga vinywa vyao.+

43 Yeyote aliye na hekima atayachunguza mambo hayo+

Naye atatafakari kwa makini matendo ya Yehova ya upendo mshikamanifu.+

Wimbo. Muziki wa Daudi.

108 Moyo wangu uko imara, Ee Mungu.

Nitaimba na kupiga muziki kwa nafsi yangu yote.*+

 2 Amka, Ee kinanda; nawe pia, Ee kinubi.+

Nitayaamsha mapambazuko.

 3 Nitakusifu miongoni mwa mataifa, Ee Yehova,

Nami nitakuimbia sifa* miongoni mwa mataifa.

 4 Kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mkubwa, uko juu kama mbingu,+

Na uaminifu wako, unafika mpaka angani.

 5 Ukwezwe juu ya mbingu, Ee Mungu;

Utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+

 6 Ili wapendwa wako waokolewe,

Tuokoe kwa mkono wako wa kuume na unijibu.+

 7 Mungu ameongea katika utakatifu wake:*

“Nitashangilia, nitawagawia Shekemu+ kuwa urithi,

Nami nitawapimia Bonde la* Sukothi.+

 8 Gileadi+ ni yangu, na Manase ni yangu,

Na Efraimu ni kofia ya kukinga* kichwa changu;+

Yuda ni fimbo yangu ya kiongozi.+

 9 Moabu ni beseni langu la kuogea.+

Nitatupa kiatu changu juu ya Edomu.+

Nitapaza sauti kwa ushindi juu ya Ufilisti.”+

10 Ni nani atakayenipeleka kwenye lile jiji lenye ngome?

Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?+

11 Je, si wewe, Ee Mungu, ambaye umetukataa,

Mungu wetu, ambaye haendi tena na majeshi yetu?+

12 Tusaidie katika taabu yetu,+

Kwa maana wokovu kutoka kwa wanadamu hauna faida yoyote.+

13 Kwa msaada wa Mungu tutapata nguvu,+

Naye atawakanyagia chini maadui wetu.+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

109 Ee Mungu ninayekusifu,+ usinyamaze.

 2 Kwa maana waovu na wadanganyifu hufumbua vinywa vyao dhidi yangu.

Wanaongea kunihusu kwa ndimi za uwongo;+

 3 Wananizingira kwa maneno ya chuki,

Na kunishambulia bila sababu.+

 4 Wananipinga licha ya kwamba ninawapenda;+

Lakini ninaendelea kusali.

 5 Wananilipa uovu kwa mema niliyotenda+

Na chuki kwa upendo wangu.+

 6 Mweke mtu mwovu amhukumu;

Mpinzani* na asimame mkono wake wa kulia.

 7 Anapohukumiwa, na apatikane kuwa na hatia;*

Hata sala yake ihesabiwe kuwa dhambi.+

 8 Siku zake na ziwe chache;+

Mtu mwingine na achukue cheo chake cha uangalizi.+

 9 Watoto wake* na wawe mayatima,

Na mke wake awe mjane.

10 Watoto wake* na watangetange wakiombaomba,

Wakitafuta chakula katika nyumba zao zilizoharibiwa.

11 Anayemdai na achukue kwa nguvu* vitu vyote alivyo navyo,

Wageni na wapore mali zake.

12 Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea kwa fadhili,*

Na asiwepo mtu yeyote wa kuwahurumia watoto wake mayatima.

13 Wazao wake na waangamizwe;*+

Jina lao na lifutwe katika kizazi kilekile.

14 Kosa la mababu zake na likumbukwe na Yehova,+

Na dhambi ya mama yake isifutwe.

15 Yehova na akumbuke daima waliyotenda;

Na afutilie mbali kumbukumbu lao kutoka duniani.+

16 Kwa maana hakukumbuka kutenda kwa fadhili,*+

Bali aliendelea kumfuatia mtu aliyekandamizwa,+ maskini, na aliyevunjika moyo

Ili amuue.+

17 Alipenda kulaani, kwa hiyo laana hiyo ikampata;

Hakupenda kubariki, kwa hiyo hakupata baraka yoyote.

18 Alivishwa laana kama vazi lake.

Nazo zikamwagwa mwilini mwake kama maji,

Mifupani mwake kama mafuta.

19 Laana zake na ziwe kama vazi analojifunika+

Na kama mshipi anaovaa daima.

20 Hayo ndiyo malipo yanayotoka kwa Yehova ya mtu anayenipinga+

Na ya wale wanaosema mambo maovu dhidi yangu.

21 Lakini wewe, Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu,

Tenda kwa niaba yangu kwa ajili ya jina lako.+

Niokoe, kwa sababu upendo wako mshikamanifu ni mwema.+

22 Kwa maana sina uwezo, nami ni maskini,+

Na moyo wangu umechomwa ndani yangu.+

23 Ninapitilia mbali kama kivuli kinachofifia;

Nimekung’utwa kama nzige.

24 Magoti yangu yanalegea kwa sababu ya kufunga;

Mwili wangu umekonda, unazidi kupungua.*

25 Nimekuwa kitu cha kudhihakiwa nao.+

Wanaponiona, wanatikisa vichwa vyao.+

26 Nisaidie, Ee Yehova Mungu wangu;

Niokoe kwa upendo wako mshikamanifu.

27 Na wajue kwamba mkono wako ndio uliotenda hili;

Kwamba wewe, Ee Yehova, umetenda hili.

28 Waache watangaze laana, lakini wewe toa baraka.

Na waaibishwe wanapoinuka dhidi yangu,

Lakini acha mtumishi wako ashangilie.

29 Wale wanaonipinga na wavishwe aibu;

Na wafunikwe na aibu yao kama joho.*+

30 Kinywa changu kitamsifu Yehova kwa bidii;

Nitamsifu yeye mbele ya watu wengi.+

31 Kwa maana atasimama mkono wa kulia wa maskini

Ili amwokoe kutoka kwa wale wanaomhukumu.

Muziki wa Daudi.

110 Yehova alimtangazia hivi Bwana wangu:

“Keti kwenye mkono wangu wa kuume+

Mpaka nitakapowaweka maadui wako kuwa kiti cha miguu yako.”+

 2 Yehova atainyoosha fimbo ya ufalme ya nguvu zako kutoka Sayuni, akisema:

“Nenda ukitiisha kati ya maadui wako.”+

 3 Watu wako watajitoa kwa hiari katika siku ya jeshi lako.*

Katika utakatifu wenye fahari, kutoka katika tumbo la uzazi la mapambazuko,

Una kundi lako la vijana kama matone ya umande.

 4 Yehova ameapa naye hatabadili nia yake:*

“Wewe ni kuhani milele+

Kwa mfano wa Melkizedeki!”+

 5 Yehova atakuwa kwenye mkono wako wa kulia;+

Atawaponda wafalme katika siku ya hasira yake.+

 6 Atatekeleza hukumu dhidi ya* mataifa;+

Atajaza maiti nchini.+

Atamponda kiongozi wa* nchi kubwa sana.*

 7 Atakunywa* maji ya kijito kilicho kando ya barabara.

Kwa hiyo, atakiinua juu kichwa chake.

111 Msifuni Yah!*+

א [Aleph]

Nitamsifu Yehova kwa moyo wangu wote+

ב [Beth]

Katika kikundi kilichokusanyika cha watu wanyoofu na katika kutaniko.

ג [Gimel]

 2 Kazi za Yehova ni kuu;+

ד [Daleth]

Wale wote wanaopendezwa nazo hujifunza kuzihusu.+

ה [He]

 3 Utendaji wake ni wenye utukufu na fahari,

ו [Waw]

Na uadilifu wake unadumu milele.+

ז [Zayin]

 4 Hufanya kazi zake zinazostaajabisha zikumbukwe.+

ח [Heth]

Yehova ni mwenye huruma* na mwenye rehema.+

ט [Teth]

 5 Huwapa chakula wale wanaomwogopa.+

י [Yod]

Hukumbuka agano lake milele.+

כ [Kaph]

 6 Amewafunulia watu wake kazi zake zenye nguvu

ל [Lamed]

Kwa kuwapa urithi wa mataifa.+

מ [Mem]

 7 Kazi za mikono yake ni kweli na haki;+

נ [Nun]

Maagizo yake yote yanategemeka.+

ס [Samekh]

 8 Yanategemeka* sikuzote, sasa na milele;

ע [Ayin]

Msingi wake ni kweli na uadilifu.+

פ [Pe]

 9 Amewakomboa watu wake.+

צ [Tsade]

Aliamuru kwamba agano lake linapaswa kudumu milele.

ק [Qoph]

Jina lake ni takatifu na linaogopesha.+

ר [Resh]

10 Kumwogopa Yehova ni mwanzo wa hekima.+

ש [Sin]

Wale wote wanaotii maagizo yake wana ufahamu mzuri.+

ת [Taw]

Sifa yake hudumu milele.

112 Msifuni Yah!*+

א [Aleph]

Mwenye furaha ni mtu anayemwogopa Yehova,+

ב [Beth]

Anayependezwa sana na amri zake.+

ג [Gimel]

 2 Wazao wake watakuwa wenye nguvu duniani,

ד [Daleth]

Na kizazi cha mtu mnyoofu kitabarikiwa.+

ה [He]

 3 Nyumbani mwake mna mali na utajiri,

ו [Waw]

Na uadilifu wake unadumu milele.

ז [Zayin]

 4 Yeye humwangazia mnyoofu kama nuru gizani.+

ח [Heth]

Ni mwenye huruma* na mwenye rehema+ na ni mwadilifu.

ט [Teth]

 5 Mambo humwendea vema mtu anayekopesha kwa ukarimu.*+

י [Yod]

Hufanya mambo yake kwa haki.

כ [Kaph]

 6 Hatatikiswa kamwe.+

ל [Lamed]

Mwadilifu atakumbukwa milele.+

מ [Mem]

 7 Hataogopa habari mbaya.+

נ [Nun]

Moyo wake ni imara, unamtumaini Yehova.+

ס [Samekh]

 8 Moyo wake hauwezi kutikiswa;* haogopi;+

ע [Ayin]

Hatimaye atawatazama maadui wake wakishindwa.+

פ [Pe]

 9 Amegawa kwa wingi;* amewapa maskini.+

צ [Tsade]

Uadilifu wake unadumu milele.+

ק [Qoph]

Nguvu zake mwenyewe zitakwezwa* kwa utukufu.

ר [Resh]

10 Mwovu ataona na kukasirika.

ש [Shin]

Atasaga meno yake na kuyeyuka.

ת [Taw]

Tamaa za mwovu zitaangamia.+

113 Msifuni Yah!*

Msifuni, enyi watumishi wa Yehova,

Lisifuni jina la Yehova.

 2 Jina la Yehova na lisifiwe

Kuanzia sasa mpaka milele.+

 3 Kuanzia jua linapochomoza mpaka linapotua,

Jina la Yehova na lisifiwe.+

 4 Yehova yuko juu zaidi ya mataifa yote;+

Utukufu wake uko juu ya mbingu.+

 5 Ni nani aliye kama Yehova Mungu wetu,+

Anayekaa juu?*

 6 Huinama chini ili atazame mbingu na dunia,+

 7 Akimwinua mtu wa hali ya chini kutoka mavumbini.

Humwinua juu maskini kutoka kwenye rundo la majivu*+

 8 Ili amketishe pamoja na viongozi,

Pamoja na viongozi wa watu wake.

 9 Humpa makao mwanamke tasa

Kama mama mwenye furaha aliye na watoto.*+

Msifuni Yah!*

114 Israeli alipotoka Misri,+

Nyumba ya Yakobo ilipotoka kati ya watu waliozungumza lugha ya kigeni,

 2 Yuda ikawa mahali pake patakatifu,

Israeli, miliki yake.+

 3 Bahari iliona hilo na kukimbia;+

Mto Yordani ukarudi nyuma.+

 4 Milima ilirukaruka kama kondoo dume,+

Vilima, kama wanakondoo.

 5 Ee bahari, ni nini kilichofanya ukimbie?+

Ee Yordani, kwa nini ulirudi nyuma?+

 6 Enyi milima, kwa nini mlirukaruka kama kondoo dume,

Kama wanakondoo, enyi vilima?

 7 Tetemeka, Ee dunia, kwa sababu ya Bwana,

Kwa sababu ya Mungu wa Yakobo,+

 8 Anayeubadili mwamba kuwa dimbwi la maji lenye matete,

Mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.+

115 Usitutukuze sisi, Ee Yehova, usitutukuze sisi,*

Bali litukuze jina lako+

Kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu na uaminifu wako.+

 2 Kwa nini mataifa yaseme:

“Yuko wapi Mungu wao?”+

 3 Mungu wetu yuko mbinguni;

Hufanya lolote apendalo.

 4 Sanamu zao ni fedha na dhahabu,

Kazi ya mikono ya mwanadamu.+

 5 Zina kinywa, lakini haziwezi kuongea;+

Zina macho, lakini haziwezi kuona;

 6 Zina masikio, lakini haziwezi kusikia;

Zina pua, lakini haziwezi kunusa;

 7 Zina mikono, lakini haziwezi kugusa;

Zina miguu, lakini haziwezi kutembea;+

Hazitoi sauti yoyote kwa koo zake.+

 8 Watu wanaozitengeneza watakuwa kama sanamu hizo,+

Na pia wote wanaozitumaini.+

 9 Ee Israeli, mtumainini Yehova+

—Yeye ndiye msaada wenu na ngao yenu.+

10 Ee nyumba ya Haruni,+ mtumainini Yehova;

—Yeye ndiye msaada wenu na ngao yenu.

11 Ninyi mnaomwogopa Yehova, mtumainini Yehova+

—Yeye ndiye msaada wenu na ngao yenu.+

12 Yehova anatukumbuka na atatubariki;

Ataibariki nyumba ya Israeli;+

Ataibariki nyumba ya Haruni.

13 Atawabariki wale wanaomwogopa Yehova,

Wadogo kwa wakubwa.

14 Yehova atawapa ongezeko,

Ninyi na watoto* wenu.+

15 Yehova na awabariki,+

Muumba wa mbingu na dunia.+

16 Mbingu ni za Yehova,+

Lakini dunia amewapa wanadamu.+

17 Watu waliokufa hawamsifu Yah;+

Wala yeyote anayeshuka kwenye ukimya wa kifo.*+

18 Lakini sisi tutamsifu Yah

Kuanzia sasa mpaka milele.

Msifuni Yah!*

116 Ninampenda Yehova

Kwa sababu yeye huisikia* sauti yangu, sihi zangu za kuomba msaada.+

 2 Kwa maana yeye hunitegea sikio lake,*+

Nami nitamlilia maadamu ninaishi.*

 3 Kamba za kifo zilinizunguka;

Kaburi lilinishika kwa nguvu.*+

Nililemewa na taabu na huzuni.+

 4 Lakini nikaliita jina la Yehova:+

“Ee, Yehova, niokoe!”*

 5 Yehova ni mwenye huruma* na ni mwadilifu;+

Mungu wetu ni mwenye rehema.+

 6 Yehova anawalinda wasio na uzoefu.+

Nilishushwa chini, akaniokoa.

 7 Acha nafsi* yangu ipumzike tena,

Kwa maana Yehova amenitendea kwa fadhili.

 8 Umeniokoa* kutoka katika kifo,

Jicho langu kutokana na machozi, mguu wangu usijikwae.+

 9 Nitatembea mbele za Yehova katika nchi ya walio hai.

10 Nilikuwa na imani, ndio maana niliongea;+

Niliteseka sana.

11 Basi nikashikwa na hofu na kusema:

“Kila mwanadamu ni mwongo.”+

12 Nitamlipa Yehova nini

Kwa mema yote aliyonitendea?

13 Nitakiinua kikombe cha wokovu,*

Nami nitaliitia jina la Yehova.

14 Nitamtimizia Yehova nadhiri zangu

Mbele ya watu wake wote.+

15 Ni chenye thamani sana* machoni pa Yehova

Kifo cha washikamanifu wake.+

16 Ninakusihi, Ee Yehova,

Kwa maana mimi ni mtumishi wako.

Mimi ni mtumishi wako, mwana wa kijakazi wako.

Umezifungua pingu zangu.+

17 Nitakutolea dhabihu ya shukrani;+

Nitaliitia jina la Yehova.

18 Nitamtimizia Yehova nadhiri zangu+

Mbele ya watu wake wote,+

19 Katika nyua za nyumba ya Yehova,+

Kati yako, Ee Yerusalemu.

Msifuni Yah!*+

117 Msifuni Yehova, enyi mataifa yote;+

Mtukuzeni, enyi mataifa yote.*+

 2 Kwa maana upendo wake mshikamanifu kutuelekea ni mkubwa;+

Uaminifu+ wa Yehova unadumu milele.+

Msifuni Yah!*+

118 Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+

Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

 2 Watu wa Israeli na waseme sasa:

“Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.”

 3 Watu wa nyumba ya Haruni na waseme sasa:

“Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.”

 4 Wale wanaomwogopa Yehova na waseme sasa:

“Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.”

 5 Nilimlilia Yah* nilipokuwa nikitaabika;

Yah akanijibu na kunipeleka mahali salama.*+

 6 Yehova yuko upande wangu; sitaogopa.+

Mwanadamu atanifanya nini?+

 7 Yehova yuko upande wangu akiwa msaidizi wangu;*+

Wale wanaonichukia nitawatazama wakishindwa.+

 8 Ni bora kumkimbilia Yehova

Kuliko kuwatumaini wanadamu.+

 9 Ni bora kumkimbilia Yehova

Kuliko kuwatumaini wakuu.+

10 Mataifa yote yalinizingira,

Lakini katika jina la Yehova,

Niliyafukuza.+

11 Yalinizingira, naam, yalinizingira kabisa,

Lakini katika jina la Yehova,

Niliyafukuza.

12 Yalinizingira kama nyuki,

Lakini yalizimwa haraka kama moto unaoteketeza miiba.

Katika jina la Yehova,

Niliyafukuza.+

13 Nilisukumwa kwa nguvu* ili nianguke,

Lakini Yehova alinisaidia.

14 Yah ni mahali pangu pa kujificha na nguvu zangu,

Naye amekuwa wokovu wangu.+

15 Sauti ya shangwe na wokovu*

Imo katika mahema ya waadilifu.

Mkono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu zake.+

16 Mkono wa kuume wa Yehova unajikweza;

Mkono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu zake.+

17 Sitakufa, hapana, nitaishi,

Ili nizitangaze kazi za Yah.+

18 Yah aliniadhibu vikali,+

Lakini hakunitia mikononi mwa kifo.+

19 Nifungulieni malango ya uadilifu;+

Nitaingia humo na kumsifu Yah.

20 Hili ndilo lango la Yehova.

Waadilifu wataingia humo.+

21 Nitakusifu, kwa maana ulinijibu+

Nawe ukawa wokovu wangu.

22 Jiwe ambalo wajenzi walilikataa

Limekuwa jiwe kuu la pembeni.*+

23 Hili limetoka kwa Yehova;+

Linastaajabisha machoni petu.+

24 Hii ndiyo siku ambayo Yehova ameifanya;

Tutaishangilia na kuifurahia.

25 Yehova, tuokoe, tafadhali, tunakusihi!

Yehova, tupe ushindi, tafadhali!

26 Amebarikiwa yule anayekuja katika jina la Yehova;+

Tunakubariki kutoka katika nyumba ya Yehova.

27 Yehova ni Mungu;

Hutupatia nuru.+

Mkiwa na matawi mikononi jiungeni na maandamano ya sherehe,+

Mpaka kwenye pembe za madhabahu.+

28 Wewe ni Mungu wangu, nami nitakusifu;

Mungu wangu, nitakukweza.+

29 Mshukuruni Yehova,+ kwa maana yeye ni mwema;

Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+

א [Aleph]

119 Wenye furaha ni wale wasio na lawama* katika njia yao,

Wanaotembea katika sheria ya Yehova.+

 2 Wenye furaha ni wale wanaoshika vikumbusho vyake,+

Wanaomtafuta kwa moyo wao wote.+

 3 Hawatendi uovu wowote;

Wanatembea katika njia zake.+

 4 Umeamuru

Kwamba maagizo yako yafuatwe kwa uangalifu.+

 5 Laiti ningeweza kubaki imara*+

Ili niyashike masharti yako!

 6 Ndipo sitaaibishwa+

Ninapokazia uangalifu amri zako zote.

 7 Nitakusifu kwa moyo mnyoofu

Ninapojifunza hukumu zako za uadilifu.

 8 Nitayashika masharti yako.

Kamwe usiniache kabisa.

ב [Beth]

 9 Kijana anaweza kuisafishaje njia yake?

Kwa kujilinda kulingana na neno lako.+

10 Ninakutafuta kwa moyo wangu wote.

Usiache nikengeuke kutoka katika amri zako.+

11 Ninaweka neno lako moyoni mwangu kama hazina+

Ili nisikutendee dhambi.+

12 Na usifiwe, Ee Yehova;

Nifundishe masharti yako.

13 Kwa midomo yangu ninatangaza

Hukumu zote ulizonena.

14 Ninashangilia kwa sababu ya vikumbusho vyako+

Kuliko vitu vingine vyote vyenye thamani.+

15 Nitatafakari* maagizo yako+

Na kuzikazia macho njia zako.+

16 Ninazipenda sana sheria zako.

Sitalisahau neno lako.+

ג [Gimel]

17 Nitendee kwa fadhili mimi mtumishi wako,

Ili niishi na kulishika neno lako.+

18 Yafumbue macho yangu ili nione wazi

Mambo yanayostaajabisha katika sheria yako.

19 Mimi ni mgeni tu nchini.+

Usinifiche amri zako.

20 Ninapondeka* kwa kutamani sana

Hukumu zako nyakati zote.

21 Unawakemea wenye kimbelembele,

Watu waliolaaniwa wanaokengeuka kutoka katika amri zako.+

22 Niondolee* dhihaka na dharau,

Kwa maana nimeshika vikumbusho vyako.

23 Hata wakuu wanapoketi pamoja na kusema mambo mabaya kunihusu,

Mimi mtumishi wako ninatafakari* masharti yako.

24 Ninavipenda sana vikumbusho vyako;+

Navyo ni washauri wangu.+

ד [Daleth]

25 Ninalala kifudifudi mavumbini.+

Nihifadhi hai kulingana na neno lako.+

26 Nilikwambia kuhusu njia zangu, nawe ukanijibu;

Nifundishe masharti yako.+

27 Nifanye nielewe maana* ya maagizo yako,

Ili niweze kutafakari* kazi zako zinazostaajabisha.+

28 Nimekosa usingizi kwa sababu ya huzuni.

Nitie nguvu kulingana na neno lako.

29 Niondolee njia ya udanganyifu,+

Na unionyeshe kibali kwa kunipa sheria yako.

30 Nimechagua njia ya uaminifu.+

Ninatambua kwamba hukumu zako zinafaa.

31 Ninashikamana na vikumbusho vyako.+

Ee Yehova, usiache nikatishwe tamaa.*+

32 Nitaifuata kwa bidii* njia ya amri zako

Kwa sababu wewe huufanya moyo wangu uwe na nafasi kwa ajili yake.*

ה [He]

33 Nifundishe, Ee Yehova,+ njia ya masharti yako,

Nami nitaifuata mpaka mwisho.+

34 Nipe uelewaji,

Ili niweze kushika sheria yako

Na kuitii kwa moyo wangu wote.

35 Niongoze* katika njia ya amri zako,+

Kwa maana ninapendezwa nayo.

36 Uelekeze moyo wangu kwenye vikumbusho vyako,

Wala si kwa tamaa ya* kichoyo.+

37 Yageuzie mbali macho yangu yasitazame mambo yasiyofaa;+

Nihifadhi hai katika njia yako.

38 Nitimizie mimi mtumishi wako ahadi yako,*

Ili uogopwe.*

39 Niondolee aibu ninayoogopa sana,

Kwa maana hukumu zako ni njema.+

40 Tazama jinsi ninavyoyatamani sana maagizo yako!

Nihifadhi hai katika uadilifu wako.

ו [Waw]

41 Acha nijionee upendo wako mshikamanifu, Ee Yehova,+

Wokovu wako kulingana na ahadi yako;*+

42 Kisha nitamjibu yule anayenidhihaki,

Kwa maana ninalitumaini neno lako.

43 Usiondoe kabisa neno la kweli kutoka kinywani mwangu,

Kwa maana nimetumaini* hukumu yako.

44 Nitaishika sheria yako daima,

Milele na milele.+

45 Nami nitatembeatembea mahali salama,*+

Kwa maana ninayatafuta maagizo yako.

46 Nitaongea kuhusu vikumbusho vyako mbele ya wafalme,

Nami sitaaibika.+

47 Ninazipenda sana amri zako,

Naam, ninazipenda.+

48 Nitainua mikono yangu kuelekea amri zako, ambazo ninazipenda,+

Nami nitayatafakari* masharti yako.+

ז [Zayin]

49 Likumbuke neno lako ulilomwambia* mtumishi wako,

Ambalo kupitia hilo unanipa tumaini.*

50 Hilo ndilo faraja yangu katika mateso yangu,+

Kwa maana neno lako limenihifadhi hai.

51 Wenye kimbelembele wananidhihaki sana,

Lakini sikengeuki kutoka kwenye sheria yako.+

52 Ninazikumbuka hukumu zako za tangu zamani,+ Ee Yehova,

Nazo zinanifariji.+

53 Nimeshikwa na hasira kali kwa sababu ya waovu,

Wanaoiacha sheria yako.+

54 Masharti yako ni nyimbo kwangu

Popote ninapoishi.*

55 Wakati wa usiku ninalikumbuka jina lako, Ee Yehova,+

Ili niweze kuishika sheria yako.

56 Nimezoea kufanya hivyo

Kwa sababu nimeyatii maagizo yako.

ח [Heth]

57 Yehova ni fungu langu;+

Nimeahidi kuyashika maneno yako.+

58 Ninakusihi* kwa moyo wangu wote;+

Nionyeshe kibali+ kulingana na ahadi yako.*

59 Nimezichunguza njia zangu,

Ili niirudishe miguu yangu kwenye vikumbusho vyako.+

60 Ninafanya haraka wala sikawii

Kuzishika amri zako.+

61 Kamba za waovu zinanizunguka,

Lakini siisahau sheria yako.+

62 Katikati ya usiku ninaamka ili kukushukuru+

Kwa sababu ya hukumu zako za uadilifu.

63 Mimi ni rafiki ya wote wanaokuogopa wewe

Na ya wale wanaoyatii maagizo yako.+

64 Upendo wako mshikamanifu, Ee Yehova, umeijaza dunia;+

Nifundishe masharti yako.

ט [Teth]

65 Umenitendea mema mimi mtumishi wako,

Ee Yehova, kulingana na neno lako.

66 Nifundishe busara na ujuzi,+

Kwa maana nimezitumaini amri zako.

67 Kabla ya kuteswa, nilikuwa nikikengeuka,*

Lakini sasa ninalishika neno lako.+

68 Wewe ni mwema+ na kazi zako ni njema.

Nifundishe masharti yako.+

69 Wenye kimbelembele hunipaka uwongo,

Lakini ninayatii maagizo yako kwa moyo wangu wote.

70 Moyo wao umekufa ganzi,*+

Lakini ninaipenda sana sheria yako.+

71 Ni vema kwamba nimeteswa,+

Ili nijifunze masharti yako.

72 Sheria uliyotangaza ni njema kwangu,+

Kuliko maelfu ya vipande vya dhahabu na fedha.+

י [Yod]

73 Mikono yako iliniumba na kunifinyanga.

Nipe uelewaji,

Ili nijifunze amri zako.+

74 Wale wanaokuogopa huniona na kushangilia,

Kwa maana neno lako ni tumaini langu.*+

75 Ninajua, Ee Yehova, kwamba hukumu zako ni za uadilifu+

Na kwamba umenitesa kwa uaminifu wako.+

76 Tafadhali, upendo wako mshikamanifu+ na unifariji,

Kulingana na ahadi yako uliyonipa* mimi mtumishi wako.

77 Nionyeshe rehema ili niendelee kuishi,+

Kwa maana ninaipenda sana sheria yako.+

78 Wenye kimbelembele na waaibishwe,

Kwa maana wananikosea bila sababu.*

Lakini nitayatafakari* maagizo yako.+

79 Acha wale wanaokuogopa warudi kwangu,

Wale wanaojua vikumbusho vyako.

80 Moyo wangu na uwe bila lawama katika kufuata masharti yako,+

Ili nisiaibishwe.+

כ [Kaph]

81 Ninautamani sana wokovu wako,+

Kwa maana neno lako ni tumaini langu.*

82 Macho yangu yanatamani sana neno lako+

Huku nikisema: “Utanifariji lini?”+

83 Kwa maana mimi ni kama kiriba cha ngozi kilichokaushwa na moshi,

Lakini siyasahau masharti yako.+

84 Mimi mtumishi wako nisubiri kwa siku ngapi?

Ni lini utakapowahukumu wale wanaonitesa?+

85 Wenye kimbelembele wananichimbia mashimo,

Wale wanaoasi sheria yako.

86 Amri zako zote zinategemeka.

Watu wananitesa bila sababu; nisaidie!+

87 Karibu waniangamize kutoka duniani,

Lakini sikuyaacha maagizo yako.

88 Nihifadhi hai kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu,

Ili nishike vikumbusho ulivyosema.

ל [Lamed]

89 Milele, Ee Yehova,

Neno lako litadumu mbinguni.+

90 Uaminifu wako umekuwepo kwa vizazi vyote.+

Umeiimarisha kabisa dunia, ili idumu.+

91 Kwa sababu ya hukumu zako zinadumu* mpaka leo,

Kwa maana zote ni watumishi wako.

92 Kama singeipenda sana sheria yako,

Ningekuwa nimeangamia katika mateso yangu.+

93 Sitayasahau kamwe maagizo yako,

Kwa sababu kupitia hayo umenihifadhi hai.+

94 Mimi ni wako; niokoe,+

Kwa sababu nimeyatafuta maagizo yako.+

95 Waovu wanasubiri kuniangamiza,

Lakini ninavikazia sana fikira vikumbusho vyako.

96 Nimeona mwisho wa ukamilifu wote,

Lakini amri yako haina mpaka.*

מ [Mem]

97 Jinsi ninavyoipenda sana sheria yako!+

Ninaitafakari* mchana kutwa.+

98 Amri yako hunifanya niwe na hekima kuliko maadui wangu,+

Kwa sababu ninayo milele.

99 Nina ufahamu mwingi kuliko walimu wangu wote,+

Kwa sababu ninavitafakari* vikumbusho vyako.

100 Ninatenda kwa uelewaji mwingi kuliko wanaume wazee,

Kwa sababu ninayatii maagizo yako.

101 Ninakataa kutembea kwenye njia yoyote ya uovu,+

Ili nishike neno lako.

102 Sigeuki kando kutoka katika hukumu zako,

Kwa maana umenifundisha.

103 Jinsi maneno yako yalivyo matamu kwenye kaakaa langu,

Kuliko asali kinywani mwangu!+

104 Kwa sababu ya maagizo yako ninatenda kwa uelewaji.+

Ndiyo sababu ninaichukia kila njia ya uwongo.+

נ [Nun]

105 Neno lako ni taa ya mguu wangu,

Na nuru ya njia yangu.+

106 Nimeweka kiapo, nami nitakitimiza,

Kwamba nitazishika hukumu zako za uadilifu.

107 Nimeteseka sana.+

Ee Yehova, nihifadhi hai kulingana na neno lako.+

108 Tafadhali yafurahie matoleo yangu ya hiari ya kukusifu,*+ Ee Yehova,

Na unifundishe hukumu zako.+

109 Uhai wangu umo hatarini daima,*

Lakini sijaisahau sheria yako.+

110 Waovu wamenitegea mtego,

Lakini sijakengeuka kutoka katika maagizo yako.+

111 Ninavichukua vikumbusho vyako kuwa mali yangu ya kudumu,*

Kwa maana hivyo ni shangwe ya moyo wangu.+

112 Nimeazimia* kuyatii masharti yako

Nyakati zote, mpaka mwisho.

ס [Samekh]

113 Ninawachukia watu wenye moyo nusunusu,*+

Lakini ninaipenda sheria yako.+

114 Wewe ni mahali pangu pa kujificha na ngao yangu,+

Kwa maana neno lako ni tumaini langu.*+

115 Kaeni mbali nami, enyi waovu,+

Ili nizishike amri za Mungu wangu.

116 Nitegemeze kama ulivyoahidi,*+

Ili niendelee kuishi;

Usiache tumaini langu libadilike na kunikatisha tamaa.*+

117 Nitegemeze ili niokolewe;+

Kisha nitayakazia uangalifu daima masharti yako.+

118 Unawakataa wote wanaokengeuka kutoka katika masharti yako,+

Kwa maana ni waongo na wadanganyifu.

119 Unawatupilia mbali waovu wote walio duniani kana kwamba ni takataka.*+

Ndiyo sababu ninavipenda vikumbusho vyako.

120 Mwili wangu unatetemeka kwa sababu ya kukuhofu;

Ninaogopa hukumu zako.

ע [Ayin]

121 Nimetenda yaliyo ya haki na uadilifu.

Usiniache mikononi mwa wale wanaonikandamiza!

122 Nihakikishie hali njema mimi mtumishi wako;

Wenye kimbelembele wasinikandamize.

123 Macho yangu yamechoka nikiungojea wokovu wako+

Na ahadi yako ya* uadilifu.+

124 Nitendee mimi mtumishi wako kwa upendo mshikamanifu,+

Na unifundishe masharti yako.+

125 Mimi ni mtumishi wako; nipe uelewaji,+

Ili nijue vikumbusho vyako.

126 Wakati umefika wa Yehova kutenda,+

Kwa maana wameivunja sheria yako.

127 Ndiyo sababu ninazipenda amri zako

Kuliko dhahabu, hata dhahabu bora.*+

128 Kwa hiyo, ninayaona mafundisho* yote yanayotoka kwako kuwa yanafaa;+

Ninaichukia kila njia ya uwongo.+

פ [Pe]

129 Vikumbusho vyako ni vizuri sana.

Ndiyo sababu ninavishika.

130 Kufunuliwa kwa maneno yako huleta nuru,+

Na humpa uelewaji mtu asiye na uzoefu.+

131 Ninakifumbua wazi kinywa changu na kutweta,*

Kwa sababu ninazitamani sana amri zako.+

132 Nigeukie na kunionyesha kibali,+

Kama unavyowatendea* wale wanaolipenda jina lako.+

133 Ziongoze hatua zangu kwa usalama* kupitia neno lako;

Jambo lolote ovu lisinitawale.+

134 Niokoe* kutoka kwa wanadamu wanaokandamiza,

Nami nitayatii maagizo yako.

135 Ufanye uso wako uniangazie* mimi mtumishi wako,+

Na unifundishe masharti yako.

136 Macho yangu yanatiririkwa na machozi

Kwa sababu watu hawatii sheria yako.+

צ [Tsade]

137 Wewe ni mwadilifu, Ee Yehova,+

Na hukumu zako ni za haki.+

138 Vikumbusho unavyotoa ni vya uadilifu

Navyo vinategemeka kabisa.

139 Bidii yangu inanila,+

Kwa sababu maadui wangu wameyasahau maneno yako.

140 Neno lako ni safi kabisa,+

Nami mtumishi wako ninalipenda.+

141 Mimi ni duni na mwenye kudharauliwa;+

Hata hivyo, sijayasahau maagizo yako.

142 Uadilifu wako ni uadilifu wa milele,+

Na sheria yako ni kweli.+

143 Hata nikipatwa na taabu na shida,

Nitaendelea kuzipenda sana amri zako.

144 Uadilifu wa vikumbusho vyako ni wa milele.

Nipe uelewaji,+ ili niendelee kuishi.

ק [Qoph]

145 Ninakuita kwa moyo wangu wote. Nijibu, Ee Yehova.

Nitayashika masharti yako.

146 Ninakulilia wewe; niokoe!

Nitashika vikumbusho vyako.

147 Nimeamka kabla ya mapambazuko* ili nililie msaada,+

Kwa maana maneno yako ni tumaini langu.*

148 Macho yangu hufunguka kabla ya makesha ya usiku,

Ili nitafakari* neno lako.+

149 Isikie sauti yangu kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu.+

Ee Yehova, nihifadhi hai kulingana na haki yako.

150 Watu wenye mwenendo wa aibu* hunikaribia;

Wako mbali sana na sheria yako.

151 Wewe uko karibu nami, Ee Yehova,+

Na amri zako zote ni kweli.+

152 Zamani za kale nilijifunza kuhusu vikumbusho vyako,

Ambavyo umeviweka vidumu milele.+

ר [Resh]

153 Yatazame mateso yangu na uniokoe,+

Kwa maana sijaisahau sheria yako.

154 Nitetee* na uniokoe;+

Nihifadhi hai kulingana na ahadi yako.*

155 Wokovu uko mbali sana na waovu,

Kwa maana hawajayatafuta masharti yako.+

156 Rehema zako ni nyingi, Ee Yehova.+

Nihifadhi hai kulingana na haki yako.

157 Wanaonitesa na pia maadui wangu ni wengi;+

Lakini sijakengeuka kutoka katika vikumbusho vyako.

158 Ninawatazama wenye hila kwa chuki kali,

Kwa sababu hawalishiki neno lako.+

159 Tazama jinsi ninavyoyapenda sana maagizo yako!

Ee Yehova, nihifadhi hai kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu.+

160 Kiini hasa cha neno lako ni kweli,+

Na hukumu zako zote za uadilifu zinadumu milele.

ש [Sin] au [Shin]

161 Wakuu wananitesa+ bila sababu,

Lakini moyo wangu unayahofu maneno yako.+

162 Ninashangilia kwa sababu ya neno lako+

Kama mtu anayepata nyara nyingi.

163 Nauchukia uwongo—nauchukia sana+—

Ninaipenda sheria yako.+

164 Mara saba kwa siku ninakusifu wewe

Kwa sababu ya hukumu zako za uadilifu.

165 Wale wanaoipenda sheria yako wana amani nyingi;+

Hakuna chochote kinachoweza kuwakwaza.*

166 Ninayatazamia matendo yako ya wokovu, Ee Yehova,

Nami ninazishika amri zako.

167 Ninavishika vikumbusho vyako,

Nami navipenda sana.+

168 Ninayatii maagizo yako na vikumbusho vyako,

Kwa maana unajua mambo yote ninayotenda.+

ת [Taw]

169 Kilio changu cha kuomba msaada na kikufikie wewe, Ee Yehova.+

Nifanye nielewe, kulingana na neno lako.+

170 Ombi langu la kutaka kibali na lifike mbele zako.

Niokoe, kama ulivyoahidi.*

171 Midomo yangu na ifurikwe na sifa,+

Kwa maana wewe hunifundisha masharti yako.

172 Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako,+

Kwa maana amri zako zote ni za uadilifu.

173 Mkono wako na uwe tayari kunisaidia,+

Kwa sababu nimechagua kutii maagizo yako.+

174 Ninautamani sana wokovu wako, Ee Yehova,

Nami ninaipenda sana sheria yako.+

175 Acha niishi ili nikusifu;+

Hukumu zako na ziwe msaada wangu.

176 Nimetangatanga kama kondoo aliyepotea.+ Nitafute mimi mtumishi wako,

Kwa maana sijazisahau amri zako.+

Wimbo wa Safari za Kupanda.*

120 Nilimwita Yehova nilipokuwa nikitaabika,+

Naye akanijibu.+

 2 Ee Yehova, niokoe kutoka kwa midomo inayosema uwongo

Na kutoka kwa ulimi mdanganyifu.

 3 Mungu atakufanya nini, Naye atakuadhibu jinsi gani,*

Ewe ulimi mdanganyifu?+

 4 Kwa mishale mikali+ ya shujaa

Na makaa yanayowaka moto+ ya miretemu.

 5 Ole wangu, kwa maana nimeishi kama mgeni Mesheki!+

Nimekuwa nikiishi kati ya mahema ya Kedari.+

 6 Nimekuwa nikiishi mbali kwa muda mrefu

Pamoja na watu wanaochukia amani.+

 7 Mimi ni mtu wa amani, lakini ninapoongea,

Wao wanataka vita.

Wimbo wa Safari za Kupanda.

121 Ninayainua macho yangu nitazame milimani.+

Msaada wangu utatoka wapi?

 2 Msaada wangu hutoka kwa Yehova,+

Muumba wa mbingu na dunia.

 3 Hataruhusu kamwe mguu wako uteleze.*+

Yeye anayekulinda hatasinzia kamwe.

 4 Tazama! Hatasinzia kamwe wala kulala usingizi,

Yeye anayelinda Israeli.+

 5 Yehova anakulinda.

Yehova ni kivuli+ kwenye mkono wako wa kulia.+

 6 Mchana, jua halitakuchoma,+

Wala mwezi usiku.+

 7 Yehova atakulinda dhidi ya madhara yote.+

Ataulinda uhai wako.*+

 8 Yehova atakulinda katika mambo yote unayofanya*

Kuanzia sasa mpaka milele.

Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.

122 Nilishangilia waliponiambia:

“Na twende katika nyumba ya Yehova.”+

 2 Na sasa miguu yetu imesimama

Ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu.+

 3 Yerusalemu limejengwa kama jiji

Ambalo limeunganishwa pamoja kama kitu kimoja.+

 4 Makabila yamepanda kwenda humo,

Makabila ya Yah,*

Kulingana na kikumbusho walichopewa Waisraeli,

Ili walishukuru jina la Yehova.+

 5 Kwa maana viti vya ufalme vya hukumu viliwekwa huko,+

Viti vya ufalme vya nyumba ya Daudi.+

 6 Ombeni ili Yerusalemu liwe na amani.+

Wale wanaokupenda, Ee jiji, watakuwa salama.

 7 Amani na idumu ndani ya maboma yako,*

Usalama ndani ya minara yako yenye ngome.

 8 Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu nitasema:

“Amani na iwe ndani yako.”

 9 Kwa ajili ya nyumba ya Yehova Mungu wetu,+

Nitakutakia mema.

Wimbo wa Safari za Kupanda.

123 Nayainua macho yangu kukuelekea wewe,+

Wewe unayeketi kwenye kiti cha ufalme mbinguni.

 2 Kama macho ya watumishi yanavyoutazama mkono wa bwana wao,

Na macho ya kijakazi yanavyoutazama mkono wa bimkubwa wake,

Ndivyo macho yetu yanavyokutazama wewe, Ee Yehova Mungu wetu+

Mpaka utakapotuonyesha kibali.+

 3 Tuonyeshe kibali, Ee Yehova, tuonyeshe kibali,

Kwa maana tumedharauliwa vya kutosha.+

 4 Tumedhihakiwa vya kutosha na* watu wanaojitumaini

Na kudharauliwa na wenye kiburi.

Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.

124 “Kama Yehova hangekuwa pamoja nasi”+

—Watu wa Israeli na waseme sasa—

 2 “Kama Yehova hangekuwa pamoja nasi+

Watu walipokuja kutushambulia,+

 3 Basi wangetumeza tukiwa hai+

Hasira yao ilipokuwa ikiwaka dhidi yetu.+

 4 Kisha maji yangetufagilia mbali,

Mafuriko yangetufunika.+

 5 Maji yenye nguvu yangetulemea.

 6 Yehova na asifiwe,

Kwa maana hakututia katika meno yao kama mawindo.

 7 Sisi* ni kama ndege aliyeponyoka

Kutoka katika mtego wa mwindaji;+

Mtego ulivunjika,

Nasi tukaponyoka.+

 8 Msaada wetu uko katika jina la Yehova,+

Muumba wa mbingu na dunia.”

Wimbo wa Safari za Kupanda.

125 Wale wanaomtumaini Yehova+

Ni kama Mlima Sayuni, ambao hauwezi kutikiswa

Bali hudumu milele.+

 2 Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,+

Ndivyo Yehova anavyowazunguka watu wake+

Kuanzia sasa mpaka milele.

 3 Fimbo ya ufalme ya uovu haitadumu katika nchi waliyogawiwa waadilifu,+

Ili waadilifu wasije wakatenda* jambo baya.+

 4 Ee Yehova, watendee mema walio wema,+

Walio wanyoofu moyoni mwao.+

 5 Lakini wale wanaogeuka na kufuata njia zao zilizopotoka,

Yehova atawaondoa pamoja na watenda maovu.+

Amani na iwe juu ya Israeli.

Wimbo wa Safari za Kupanda.

126 Yehova alipowakusanya na kuwarudisha mateka wa Sayuni,+

Tulifikiri tunaota ndoto.

 2 Wakati huo kinywa chetu kilijaa kicheko

Na ulimi wetu kelele za shangwe.+

Wakati huo ilisemwa miongoni mwa mataifa:

“Yehova amewatendea mambo makuu.”+

 3 Yehova ametutendea mambo makuu,+

Nasi tuna shangwe nyingi sana.

 4 Wakusanye na kuwarudisha watu wetu waliotekwa, Ee Yehova,

Kama vijito vya Negebu.*

 5 Wale wanaopanda mbegu kwa machozi

Watavuna kwa kelele za shangwe.

 6 Yule anayetoka kwenda nje, ingawa analia,

Akiwa amebeba mfuko wake uliojaa mbegu,

Kwa hakika atarudi kwa kelele za shangwe,+

Akiwa amebeba masuke yake.+

Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Sulemani.

127 Yehova asipoijenga nyumba,

Wale wanaoijenga wanafanya kazi ngumu ya bure.+

Yehova asipolilinda jiji,+

Mlinzi anakesha bure.

 2 Mnajisumbua bure kuamka mapema,

Na kuchelewa kulala,

Mkitaabika kupata chakula,

Kwa maana yeye huwaandalia anaowapenda na kuwapa usingizi.+

 3 Tazama! Watoto* ni urithi kutoka kwa Yehova;+

Uzao wa tumbo ni thawabu.+

 4 Kama mishale mkononi mwa mwanamume hodari,

Ndivyo walivyo watoto ambao mtu anawazaa akiwa kijana.+

 5 Mwenye furaha ni mwanamume anayelijaza podo lake watoto.+

Hawataaibishwa,

Kwa maana watazungumza na maadui katika lango la jiji.

Wimbo wa Safari za Kupanda.

128 Mwenye furaha ni kila mtu anayemwogopa Yehova,+

Anayetembea katika njia Zake.+

 2 Utakula mazao ambayo mkono wako ulifanya kazi ngumu kuyapata.

Utakuwa na furaha na kufurahia ufanisi.+

 3 Mke wako atakuwa kama mzabibu unaozaa matunda mengi nyumbani mwako;+

Watoto wako watakuwa kama machipukizi ya mzeituni kuzunguka meza yako.

 4 Tazama! Hivyo ndivyo mwanamume anayemwogopa Yehova

Atakavyobarikiwa.+

 5 Yehova atakubariki kutoka Sayuni.

Na uone Yerusalemu likipata ufanisi sikuzote za maisha yako+

 6 Na uone watoto wa watoto wako.

Na amani iwe juu ya Israeli.

Wimbo wa Safari za Kupanda.

129 “Wamenishambulia daima tangu nilipokuwa kijana”+

—Watu wa Israeli na waseme sasa—

 2 “Wamenishambulia daima tangu nilipokuwa kijana;+

Lakini hawajanishinda.+

 3 Wale wanaolima kwa jembe la plau wamelima mgongoni mwangu;+

Wameirefusha mitaro yao.”

 4 Lakini Yehova ni mwadilifu;+

Amezikatakata kamba za waovu.+

 5 Wataaibishwa na kukimbia kwa fedheha,

Wale wote wanaolichukia Sayuni.+

 6 Watakuwa kama majani juu ya paa

Yanayonyauka kabla hayajang’olewa,

 7 Ambayo hayawezi kujaa mkononi mwa mvunaji

Wala mikononi mwa yule anayekusanya masuke.

 8 Wale wanaopita karibu nao hawatasema:

“Baraka ya Yehova na iwe juu yenu;

Tunawabariki katika jina la Yehova.”

Wimbo wa Safari za Kupanda.

130 Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Yehova.+

 2 Ee Yehova, isikie sauti yangu.

Masikio yako na yasikilize sihi zangu za kuomba msaada.

 3 Ikiwa ungekuwa unatazama* tu makosa, Ee Yah,*

Basi ni nani, Ee Yehova, angeweza kusimama?+

 4 Kwa maana wewe hutoa msamaha wa kweli,+

Ili watu wakuhofu.*+

 5 Ninamtumaini Yehova, nafsi yangu yote inamtumaini;

Ninangoja neno lake.

 6 Ninamngojea Yehova kwa hamu,+

Kuliko walinzi wanavyoingojea asubuhi,+

Naam, kuliko walinzi wanavyoingojea asubuhi.

 7 Watu wa Israeli na waendelee kumngojea Yehova,

Kwa maana Yehova ni mshikamanifu katika upendo wake,+

Naye ana nguvu nyingi za kukomboa.

 8 Atawakomboa watu wa Israeli kutoka katika makosa yao yote.

Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.

131 Ee Yehova, moyo wangu hauna kiburi,

Wala macho yangu hayana majivuno;+

Wala sijitafutii mambo makubwa sana,+

Wala mambo yanayopita uwezo wangu.

 2 Hasha, badala yake nimeituliza na kuinyamazisha nafsi yangu*+

Kama mtoto aliyeachishwa kunyonya aliye na mama yake;

Nimeridhika kama mtoto aliyeachishwa kunyonya.

 3 Watu wa Israeli na wamngojee Yehova+

Kuanzia sasa mpaka milele.

Wimbo wa Safari za Kupanda.

132 Ee Yehova, mkumbuke Daudi

Na mateso yake yote;+

 2 Jinsi alivyomwapia Yehova,

Jinsi alivyomwekea nadhiri hii Mwenye Nguvu wa Yakobo:+

 3 “Sitaingia katika hema langu, nyumbani mwangu.+

Sitalala kwenye kochi langu, kitandani mwangu;

 4 Sitayaruhusu macho yangu yalale usingizi,

Wala kope zangu kusinzia

 5 Mpaka nitakapopata mahali kwa ajili ya Yehova,

Makao bora* kwa ajili ya Mwenye Nguvu wa Yakobo.”+

 6 Tazama! Tulisikia habari hizo huko Efratha;+

Tulizipata katika mashamba yaliyo msituni.+

 7 Na tuingie katika makao yake;*+

Na tuiname chini kwenye kiti cha miguu yake.+

 8 Inuka, Ee Yehova, uje mahali pako pa kupumzikia,+

Wewe na Sanduku la nguvu zako.+

 9 Makuhani wako na wavae uadilifu,

Washikamanifu wako na wapaze sauti kwa shangwe.

10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako,

Usimkatae* mtiwa-mafuta wako.+

11 Yehova amemwapia Daudi;

Kwa hakika hatakosa kutimiza neno lake:

“Mmoja wa wazao wako,*

Nitamfanya aketi kwenye kiti chako cha ufalme.+

12 Wana wako wakilishika agano langu

Na vikumbusho vyangu ninavyowafundisha,+

Wana wao pia

Wataketi kwenye kiti chako cha ufalme milele.”+

13 Kwa maana Yehova amelichagua Sayuni;+

Amelitamani liwe makao yake:+

14 “Hapa ndipo mahali pangu pa kupumzikia milele;

Nitakaa hapa,+ kwa maana nimepatamani.

15 Nitapabariki sana kwa vyakula;

Nitawashibisha maskini wake kwa mikate.+

16 Makuhani wake nitawavisha wokovu,+

Na washikamanifu wake watapaza sauti kwa shangwe.+

17 Huko nitazifanya nguvu za Daudi zikue.*

Nimemtayarishia taa mtiwa-mafuta wangu.+

18 Nitawavisha aibu maadui wake,

Lakini taji lililo kwenye kichwa chake litasitawi.”+

Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.

133 Tazama! Jinsi ilivyo vema na jinsi inavyopendeza

Ndugu kukaa pamoja kwa umoja!+

 2 Ni kama mafuta bora yanayomiminwa kichwani+

Yanayotiririka kwenye ndevu,

Ndevu za Haruni,+

Na kutiririka mpaka kwenye ukosi wa mavazi yake.

 3 Ni kama umande wa Hermoni+

Unaoshuka kwenye milima ya Sayuni.+

Huko ndiko Yehova alikoamuru baraka yake

—Uzima wa milele.

Wimbo wa Safari za Kupanda.

134 Msifuni Yehova,

Enyi nyote watumishi wa Yehova,+

Ninyi mnaosimama katika nyumba ya Yehova nyakati za usiku.+

 2 Inueni mikono yenu+ katika utakatifu*

Na mumsifu Yehova.

 3 Yehova, Muumba wa mbingu na dunia,

Na awabariki kutoka Sayuni.

135 Msifuni Yah!*

Lisifuni jina la Yehova;

Msifuni, enyi watumishi wa Yehova,+

 2 Ninyi mnaosimama katika nyumba ya Yehova,

Katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.+

 3 Msifuni Yah, kwa maana Yehova ni mwema.+

Liimbieni sifa* jina lake, kwa maana linapendeza.

 4 Kwa maana Yah amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe,

Israeli awe mali yake ya pekee.*+

 5 Kwa maana ninajua vizuri kwamba Yehova ni mkuu;

Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu mingine yote.+

 6 Yehova hufanya kila jambo apendalo+

Mbinguni na duniani, baharini na katika vilindi vyote.

 7 Huyafanya mawingu yapande* kutoka kwenye miisho ya dunia;

Hutengeneza radi* kwa ajili ya mvua;

Huutoa upepo katika maghala yake.+

 8 Aliwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri,

Wanadamu na wanyama pia.+

 9 Alipeleka ishara na miujiza kati yako, Ee Misri,+

Dhidi ya Farao na watumishi wake wote.+

10 Aliyaangamiza mataifa mengi+

Na kuwaua wafalme hodari+

11 —Sihoni mfalme wa Waamori,+

Ogu mfalme wa Bashani,+

Na falme zote za Kanaani.

12 Aliitoa nchi yao kuwa urithi,

Urithi kwa watu wake Waisraeli.+

13 Ee Yehova, jina lako linadumu milele.

Ee Yehova, umaarufu wako unadumu* katika vizazi vyote.+

14 Kwa maana Yehova atawatetea* watu wake,+

Naye atawahurumia* watumishi wake.+

15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu,

Kazi ya mikono ya mwanadamu.+

16 Zina kinywa, lakini haziwezi kuongea;+

Zina macho, lakini haziwezi kuona;

17 Zina masikio, lakini haziwezi kusikia.

Hazina pumzi vinywani mwake.+

18 Watu wanaozitengeneza watakuwa kama sanamu hizo,+

Na pia wote wanaozitumaini.+

19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Yehova.

Ee nyumba ya Haruni, msifuni Yehova.

20 Ee nyumba ya Lawi, msifuni Yehova.+

Enyi mnaomwogopa Yehova, msifuni Yehova.

21 Yehova na asifiwe kutoka Sayuni,+

Yeye anayekaa Yerusalemu.+

Msifuni Yah!+

136 Mshukuruni Yehova, kwa maana ni mwema;+

Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+

 2 Mshukuruni Mungu wa miungu,+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

 3 Mshukuruni Bwana wa mabwana,

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

 4 Yeye peke yake ndiye anayetenda mambo makuu yanayostaajabisha,+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+

 5 Aliziumba mbingu kwa ustadi,*+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

 6 Aliitandaza dunia juu ya maji,+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

 7 Aliiumba ile mianga mikubwa,+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,

 8 Jua litawale mchana,+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,

 9 Mwezi na nyota zitawale usiku,+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

10 Aliwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri,+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

11 Aliwatoa Waisraeli kutoka kati yao,+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,

12 Kwa mkono wenye nguvu+ na mkono ulionyooshwa,

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

13 Aliigawa Bahari Nyekundu sehemu mbili,*+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

14 Aliwavusha Waisraeli katikati yake,+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

15 Alimkung’uta Farao na jeshi lake ndani ya Bahari Nyekundu,+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

16 Aliwaongoza watu wake kupitia nyikani,+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

17 Aliwaua wafalme wakuu,+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

18 Aliwaua wafalme hodari,

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

19 Sihoni+ mfalme wa Waamori,

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,

20 Na Ogu+ mfalme wa Bashani,

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

21 Aliitoa nchi yao kuwa urithi,+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

22 Urithi kwa Israeli mtumishi wake,

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

23 Alitukumbuka tulipokuwa wanyonge,+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+

24 Alituokoa tena na tena kutoka kwa maadui wetu,+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

25 Huwapa chakula viumbe wote walio hai,*+

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

26 Mshukuruni Mungu wa mbinguni,

Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

137 Kando ya mito ya Babiloni,+ hapo ndipo tulipoketi.

Tulilia tulipokumbuka Sayuni.+

 2 Juu ya miti ya mierebi iliyo ndani yake,*

Tulitundika vinubi vyetu.+

 3 Kwa maana huko, waliotuteka walitaka tuwaimbie,+

Waliotudhihaki walitaka tuwatumbuize:

“Tuimbieni mojawapo ya nyimbo za Sayuni.”

 4 Tunawezaje kuimba wimbo wa Yehova

Katika nchi ya kigeni?

 5 Ikiwa nitakusahau wewe, Ee Yerusalemu,

Mkono wangu wa kulia na uwe msahaulifu.*+

 6 Ulimi wangu na ushikamane na kaakaa langu

Nisipokukumbuka,

Nisipoliweka Yerusalemu juu ya

Sababu zangu kuu zaidi za kushangilia.+

 7 Kumbuka, Ee Yehova,

Mambo ambayo Waedomu walisema siku ambayo Yerusalemu lilianguka:

“Libomoeni! Libomoeni mpaka kwenye misingi yake!”+

 8 Ee binti ya Babiloni, uliye karibu kuangamizwa,+

Mwenye furaha ni yule atakayekupa thawabu yako

Kwa maovu uliyotutendea.+

 9 Mwenye furaha ni yule atakayewakamata kwa nguvu watoto wako

Na kuwaponda juu ya miamba.+

Wa Daudi.

138 Nitakusifu kwa moyo wangu wote.+

Mbele ya miungu mingine,

Nitaimba sifa.*

 2 Nitainama chini kuelekea hekalu lako takatifu,*+

Nami nitalisifu jina lako+

Kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu na uaminifu wako.

Kwa maana umelitukuza neno lako na jina lako juu ya vitu vingine vyote.*

 3 Siku niliyokuita, ulinijibu;+

Ulinifanya niwe jasiri* na mwenye nguvu.+

 4 Wafalme wote wa dunia watakusifu wewe, Ee Yehova,+

Kwa maana watakuwa wamesikia ahadi ulizotoa.

 5 Wataimba kuhusu njia za Yehova,

Kwa maana utukufu wa Yehova ni mkuu.+

 6 Ingawa Yehova yuko juu, yeye huwaona wanyenyekevu,+

Lakini anajitenga mbali na wenye kiburi.+

 7 Hata nikitembea katikati ya hatari, utanihifadhi hai.+

Unaunyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya maadui wangu;

Mkono wako wa kuume utaniokoa.

 8 Yehova atayatimiza mambo yote kwa niaba yangu.

Ee Yehova, upendo wako mshikamanifu unadumu milele;+

Usiziache kazi za mikono yako.+

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

139 Ee Yehova, umenichunguza kabisa, nawe unanijua.+

 2 Unajua wakati ninapoketi na wakati ninaposimama.+

Unatambua mawazo yangu kutoka mbali.+

 3 Unanichunguza* ninaposafiri na ninapolala;

Unazijua njia zangu zote.+

 4 Kabla sijatamka neno lolote kwa ulimi wangu,

Tazama! Ee Yehova, tayari unalijua vizuri.+

 5 Unanizingira nyuma na mbele;

Nawe unauweka mkono wako juu yangu.

 6 Ujuzi huo unazidi ufahamu wangu.*

Uko juu sana nisiweze kuufikia.*+

 7 Ninaweza kujificha wapi mbali na roho yako,

Na ni wapi ninapoweza kukimbia mbali na uso wako?+

 8 Kama ningepanda mbinguni, ungekuwa huko,

Na kama ningetandika kitanda changu Kaburini,* tazama! ungekuwa huko.+

 9 Kama ningeruka kwa mabawa ya mapambazuko

Ili niishi kando ya bahari iliyo mbali zaidi,

10 Hata huko mkono wako ungeniongoza

Na mkono wako wa kuume ungenishika.+

11 Nikisema: “Hakika giza litanificha!”

Basi usiku unaonizunguka utakuwa nuru.

12 Hata giza halitakuwa zito mno kwako,

Lakini usiku utakuwa mwangavu kama mchana;+

Kwako giza ni sawa na nuru.+

13 Kwa maana uliziumba figo zangu;

Ulinisitiri* katika tumbo la mama yangu.+

14 Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa njia inayoogopesha na kustaajabisha.+

Kazi zako zinastaajabisha,+

Ninajua* vizuri sana jambo hilo.

15 Mifupa yangu haikufichwa kwako

Nilipoumbwa sirini,

Nilipofumwa katika sehemu zenye kina za dunia.+

16 Macho yako hata yaliniona nikiwa kiinitete;

Sehemu zake zote ziliandikwa katika kitabu chako

Kuhusiana na siku ambazo zingeumbwa,

Kabla sehemu yoyote haijakuwepo.

17 Kwa hiyo kwangu mimi, mawazo yako ni yenye thamani sana!+

Ee Mungu, jinsi jumla yake ilivyo kubwa sana!+

18 Nikijaribu kuyahesabu, ni mengi kuliko chembe za mchanga.+

Nikiamka, bado nipo pamoja nawe.*+

19 Ee Mungu, laiti ungewaua waovu!+

Ndipo watu wakatili* wangeniondokea,

20 Wale wanaosema mambo mabaya kukuhusu kwa nia ovu;*

Wao ni maadui wako wanaolitumia jina lako kwa njia isiyofaa.+

21 Je, siwachukii wale wanaokuchukia wewe, Ee Yehova,+

Na kuwachukia kabisa wale wanaokuasi?+

22 Ninawachukia kwelikweli;+

Hakika wamekuwa maadui wangu.

23 Nichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu.+

Nipime, uyajue mawazo yangu yanayonihangaisha.*+

24 Angalia ikiwa kuna njia yoyote yenye madhara ndani yangu,+

Uniongoze+ katika njia ya milele.

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.

140 Niokoe, Ee Yehova, kutoka kwa watu waovu;

Nilinde kutoka kwa watu wakatili,+

 2 Wale wanaopanga njama za uovu mioyoni mwao+

Na kuchochea vita mchana kutwa.

 3 Wanaunoa ulimi wao kama wa nyoka;+

Sumu ya nyoka vipiri iko nyuma ya midomo yao.+ (Sela)

 4 Nilinde, Ee Yehova, kutoka mikononi mwa waovu;+

Nilinde kutoka kwa watu wakatili,

Wale wanaopanga njama ya kunitega miguu.

 5 Wenye kiburi huuficha mtego ili uninase;

Kwa kamba wanautandaza wavu kando ya njia.+

Wanatega mitego ya kuninasa.+ (Sela)

 6 Ninamwambia Yehova: “Wewe ni Mungu wangu.

Sikiliza, Ee Yehova, sihi zangu za kuomba msaada.”+

 7 Ee Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu, Mwokozi wangu mwenye nguvu,

Wewe hukinga kichwa changu katika siku ya vita.+

 8 Ee Yehova, usitosheleze tamaa za waovu.

Usiruhusu njama zao zifanikiwe, ili wasijikweze. (Sela)+

 9 Vichwa vya wale wanaonizingira

Na vifunikwe na uovu unaosemwa na midomo yao.+

10 Makaa ya mawe yanayowaka na yawanyeshee kama mvua.+

Na watupwe motoni,

Ndani ya mashimo yenye kina,*+ wasiinuke tena kamwe.

11 Mchongezi na asipate makao duniani.*+

Uovu na uwafuatie watu wakatili na kuwaangamiza.

12 Ninajua kwamba Yehova atawatetea watu wa hali ya chini

Na kuwatendea haki maskini.+

13 Hakika waadilifu watalishukuru jina lako;

Wanyoofu watakaa mbele za uso wako.*+

Muziki wa Daudi.

141 Ee Yehova, ninakulilia wewe.+

Njoo haraka unisaidie.+

Sikiliza ninapokulilia.+

 2 Sala yangu na itayarishwe kama uvumba+ mbele zako,+

Mikono yangu iliyoinuliwa na iwe kama toleo la jioni la nafaka.+

 3 Weka mlinzi wa kinywa changu, Ee Yehova,

Weka ulinzi kwenye mlango wa midomo yangu.+

 4 Usiache moyo wangu uelekee kwenye jambo lolote ovu,+

Nisishirikiane na watu waovu kutenda mambo mapotovu;

Nisile kamwe vyakula vyao vitamu.

 5 Mwadilifu akinipiga, hilo litakuwa tendo la upendo mshikamanifu;+

Akinikaripia, hilo litakuwa kama mafuta kwenye kichwa changu,+

Ambayo kichwa changu hakiwezi kamwe kukataa.+

Nitaendelea kusali hata wanapopatwa na misiba.

 6 Ingawa waamuzi wao wanatupwa chini kutoka kwenye jabali,

Watu watayasikiliza maneno yangu, kwa maana yanapendeza.

 7 Kama mtu anavyolima na kuuvunja-vunja udongo,

Ndivyo mifupa yetu ilivyotawanywa kwenye mlango wa Kaburi.*

 8 Lakini macho yangu yanakutazama wewe, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+

Nimekukimbilia wewe.

Usiniue.*

 9 Nilinde dhidi ya mataya ya mtego walionitegea,

Dhidi ya mitego ya watenda maovu.

10 Waovu wote wataanguka pamoja ndani ya nyavu zao wenyewe+

Huku nikipitia karibu nazo kwa usalama.

Maskili.* Wa Daudi, alipokuwa pangoni.+ Sala.

142 Kwa sauti yangu ninamlilia Yehova anisaidie;+

Kwa sauti yangu ninamsihi Yehova anionyeshe kibali.

 2 Ninamwaga mahangaiko yangu mbele zake;

Mbele zake ninaeleza taabu yangu+

 3 Roho yangu inapozimia ndani yangu.*

Ndipo unapoitazama barabara yangu.+

Katika njia ninayotembea,

Wanaficha mtego wa kuninasa.

 4 Tazama upande wa mkono wangu wa kulia uone+

Kwamba hakuna yeyote anayenijali.*

Sina mahali popote pa kukimbilia;+

Hakuna yeyote anayenihangaikia.

 5 Ninakulilia unisaidie, Ee Yehova.

Ninasema: “Wewe ni kimbilio langu,+

Ni wewe tu niliye nawe* katika nchi ya walio hai.”

 6 Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada,

Kwa maana nimeshushwa chini sana.

Niokoe kutoka kwa wale wanaonitesa,+

Kwa maana wana nguvu kuliko mimi.

 7 Nitoe katika gereza lililo chini ya ardhi

Ili nilisifu jina lako.

Waadilifu na wakusanyike kunizunguka

Kwa sababu unanitendea kwa fadhili.

Muziki wa Daudi.

143 Ee Yehova, isikie sala yangu;+

Sikiliza sihi yangu ya kuomba msaada.

Nijibu katika uaminifu wako na katika uadilifu wako.

 2 Usinihukumu mimi mtumishi wako,

Kwa maana hakuna yeyote aliye hai anayeweza kuwa mwadilifu mbele zako.+

 3 Kwa maana adui ananifuatia;

Ameuponda uhai wangu ardhini.

Amenifanya nikae gizani kama wale waliokufa zamani za kale.

 4 Roho yangu inazimia;*+

Moyo wangu umekufa ganzi.+

 5 Ninazikumbuka siku za kale;

Ninatafakari utendaji wako wote;+

Ninatafakari* kwa bidii kazi ya mikono yako.

 6 Ninakunyooshea mikono yangu;

Mimi ni kama nchi iliyokauka yenye kiu kwa ajili yako.+ (Sela)

 7 Nijibu haraka, Ee Yehova;+

Nguvu zangu zimefikia* mwisho.+

Usinifiche uso wako,+

La sivyo nitakuwa kama wale wanaoshuka shimoni.*+

 8 Acha nisikie upendo wako mshikamanifu asubuhi,

Kwa maana ninakutumaini wewe.

Nijulishe njia ninayopaswa kutembea ndani yake,+

Kwa maana ninakugeukia wewe.*

 9 Niokoe kutoka kwa maadui wangu, Ee Yehova.

Ninatafuta ulinzi wako.+

10 Nifundishe kufanya mapenzi yako,+

Kwa maana wewe ni Mungu wangu.

Roho yako ni nzuri;

Na iniongoze kwenye nchi tambarare.*

11 Ee Yehova, nihifadhi hai kwa ajili ya jina lako.

Katika uadilifu wako, niokoe kutoka katika taabu.+

12 Katika upendo wako mshikamanifu, waangamize* maadui wangu;+

Waangamize wote wanaoninyanyasa,+

Kwa maana mimi ni mtumishi wako.+

Wa Daudi.

144 Yehova, Mwamba wangu,+ na asifiwe,

Anayeizoeza mikono yangu kwa ajili ya vita,

Vidole vyangu kwa ajili ya kupigana.+

 2 Yeye ni upendo wangu mshikamanifu na ngome yangu,

Kimbilio langu salama* na mwokozi wangu,

Ngao yangu na Yule ambaye nimejificha ndani yake,+

Yule anayeyatiisha mataifa chini yangu.+

 3 Ee Yehova, mwanadamu ni nini hata umtambue,

Mwana wa mtu anayeweza kufa ni nini hata umkazie uangalifu?+

 4 Mwanadamu ni kama pumzi tu;+

Siku zake ni kama kivuli kinachopita.+

 5 Ee Yehova, shusha* mbingu zako uteremke;+

Iguse milima na uifanye ifuke moshi.+

 6 Ifanye radi imweke na kuwatawanya maadui;+

Piga mishale yako uwavuruge.+

 7 Inyooshe mikono yako kutoka juu;

Niokoe na kuninusuru kutoka katika maji mengi,

Kutoka katika mkono* wa wageni,+

 8 Ambao kinywa chao kinasema uwongo

Na ambao wanainua juu mkono wao wa kulia ili kuapa kwa uwongo.*

 9 Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya.+

Nitakuimbia sifa* kwa kinanda cha nyuzi kumi,

10 Wewe unayewapa wafalme ushindi,*+

Wewe unayemwokoa mtumishi wako Daudi kutokana na upanga hatari.+

11 Niokoe na kuninusuru kutoka katika mkono wa wageni,

Ambao vinywa vyao husema uwongo

Na ambao wanainua mkono wao wa kulia ili kuapa kwa uwongo.

12 Ndipo wana wetu watakuwa kama mimea michanga inayokua haraka,

Mabinti wetu kama nguzo za pembeni zilizochongwa kwa ajili ya jumba la mfalme.

13 Maghala yetu yatafurika mazao ya kila aina;

Makundi yetu ya kondoo yataongezeka kwa maelfu, kwa makumi ya maelfu.

14 Ng’ombe wetu, wakiwa na mimba, hawatapatwa na jambo baya* wala mimba kuharibika,

Hakutakuwa na kilio cha kuteseka katika viwanja vyetu vya mji.

15 Wenye furaha ni watu wenye hali hizo!

Wenye furaha ni watu ambao Mungu wao ni Yehova!+

Sifa ya Daudi.

א [Aleph]

145 Nitakukweza, Ee Mungu wangu Mfalme,+

Nitalisifu jina lako milele na milele.+

ב [Beth]

 2 Nitakusifu mchana kutwa;+

Nitalisifu jina lako milele na milele.+

ג [Gimel]

 3 Yehova ni mkuu na anastahili kabisa kusifiwa;+

Ukuu wake hauchunguziki.*+

ד [Daleth]

 4 Kizazi baada ya kizazi kitasifu kazi zako;

Watasimulia matendo yako yenye nguvu.+

ה [He]

 5 Watasema kuhusu fahari tukufu ya ukuu wako+

Nami nitatafakari kazi zako zinazostaajabisha.

ו [Waw]

 6 Watasema kuhusu matendo yako yanayoogopesha,*

Nami nitautangaza ukuu wako.

ז [Zayin]

 7 Watabubujikwa na maneno wanapokumbuka wema wako mwingi,+

Nao watapaza sauti kwa shangwe kwa sababu ya uadilifu wako.+

ח [Heth]

 8 Yehova ni mwenye huruma* na rehema,+

Si mwepesi wa hasira, naye ana upendo mwingi mshikamanifu.+

ט [Teth]

 9 Yehova ni mwema kwa wote,+

Na rehema zake zinaonekana katika kazi zake zote.

י [Yod]

10 Kazi zako zote zitakutukuza, Ee Yehova,+

Na washikamanifu wako watakusifu.+

כ [Kaph]

11 Watatangaza utukufu wa ufalme wako+

Na kusema kuhusu nguvu zako,+

ל [Lamed]

12 Ili kuwajulisha wanadamu matendo yako yenye nguvu+

Na fahari yenye utukufu ya ufalme wako.+

מ [Mem]

13 Ufalme wako ni ufalme wa milele,

Na mamlaka yako hudumu katika vizazi vyote.+

ס [Samekh]

14 Yehova huwategemeza wote wanaoanguka+

Na kuwainua juu wote walioinama chini.+

ע [Ayin]

15 Macho yote yanakutazama yakiwa na tumaini;

Unawapa chakula chao katika majira yake.+

פ [Pe]

16 Unaufumbua mkono wako

Na kutosheleza tamaa ya kila kitu kilicho hai.+

צ [Tsade]

17 Yehova ni mwadilifu katika njia zake zote+

Na mshikamanifu katika kila jambo analotenda.+

ק [Qoph]

18 Yehova yuko karibu na wote wanaomwitia,+

Wote wanaomwitia yeye katika ukweli.*+

ר [Resh]

19 Hutosheleza tamaa ya wale wanaomwogopa;+

Husikia kilio chao cha kuomba msaada, naye huwaokoa.+

ש [Shin]

20 Yehova huwalinda wale wote wanaompenda,+

Lakini atawaangamiza waovu wote.+

ת [Taw]

21 Kinywa changu kitatangaza sifa za Yehova;+

Kila kitu kilicho hai na kilisifu* jina lake takatifu milele na milele.+

146 Msifuni Yah!*+

Nafsi yangu yote na imsifu Yehova.+

 2 Nitamsifu Yehova maisha yangu yote.

Nitamwimbia sifa* Mungu wangu maadamu ninaishi.

 3 Msiwatumaini wakuu*

Wala mwanadamu, ambaye hawezi kuleta wokovu.+

 4 Roho* yake hutoka, naye hurudi ardhini;+

Siku hiyohiyo mawazo yake hupotea.+

 5 Mwenye furaha ni yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaidizi wake,+

Ambaye anamtumaini Yehova Mungu wake,+

 6 Muumba wa mbingu na dunia,

Wa bahari, na vyote vilivyomo,+

Yeye ambaye ni mwaminifu daima,+

 7 Yeye anayetekeleza haki kwa ajili ya waliopunjwa,

Yeye anayewapa chakula* wenye njaa.+

Yehova anawaachilia huru wafungwa.*+

 8 Yehova anafungua macho ya vipofu;+

Yehova anawainua juu wale walioinama chini;+

Yehova anawapenda waadilifu.

 9 Yehova anawalinda wakaaji wageni;

Humtegemeza yatima na mjane,+

Lakini huivuruga mipango ya waovu.*+

10 Yehova atakuwa Mfalme milele,+

Mungu wako, Ee Sayuni, kizazi baada ya kizazi.

Msifuni Yah!*

147 Msifuni Yah!*

Ni vema kumwimbia sifa* Mungu wetu;

Jinsi inavyopendeza na jinsi inavyofaa sana kumsifu yeye!+

 2 Yehova analijenga Yerusalemu;+

Huwakusanya pamoja watu wa Israeli waliotawanywa.+

 3 Huwaponya waliovunjika moyo;

Huyafunga majeraha yao.

 4 Huhesabu idadi ya nyota;

Zote anaziita kwa majina.+

 5 Bwana wetu ni mkuu naye ana nguvu nyingi;+

Uelewaji wake haupimiki.+

 6 Yehova huwainua wapole,+

Lakini huwatupa chini waovu.

 7 Mwimbieni Yehova kwa shukrani;

Mwimbieni sifa Mungu wetu kwa kinubi,

 8 Yeye anayezifunika mbingu kwa mawingu,

Yeye anayeiletea dunia mvua,+

Yeye anayechipusha majani+ milimani.

 9 Anawapa wanyama chakula,+

Kunguru wachanga wanaokililia.+

10 Hapendezwi na nguvu za farasi;+

Wala havutiwi na miguu yenye nguvu ya mwanamume.+

11 Yehova anafurahishwa na wale wanaomwogopa,+

Wale wanaongojea upendo wake mshikamanifu.+

12 Mtukuze Yehova, Ee Yerusalemu.

Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.

13 Huyafanya makomeo ya malango ya jiji lako yawe imara;

Huwabariki wana wako walio ndani yako.

14 Huleta amani katika eneo lako;+

Hukushibisha kwa ngano bora kabisa.*+

15 Huituma amri yake duniani;

Neno lake hukimbia upesi sana.

16 Hutoa theluji kama sufu;+

Hutawanya theluji nyembamba kama majivu tu.+

17 Huyatupa chini mawe yake ya mvua* kama chembe za mkate.+

Ni nani anayeweza kustahimili baridi yake?+

18 Hulituma neno lake, nayo inayeyuka.

Huufanya upepo wake uvume,+ maji yanatiririka.

19 Anamtangazia Yakobo neno lake,

Na Israeli masharti yake na hukumu zake.+

20 Hajalifanyia hivyo taifa lingine lolote;+

Hawajui lolote kuhusu hukumu zake.

Msifuni Yah!*+

148 Msifuni Yah!*

Msifuni Yehova kutoka mbinguni,+

Msifuni katika vilele.

 2 Msifuni, enyi malaika wake wote.+

Msifuni, enyi jeshi lake lote.+

 3 Msifuni, enyi jua na mwezi.

Msifuni, enyi nyota zote zinazong’aa.+

 4 Msifuni, enyi mbingu zilizo juu kabisa*

Na maji yaliyo juu ya mbingu.

 5 Na vilisifu jina la Yehova,

Kwa maana aliamuru, navyo vikaumbwa.+

 6 Huvifanya viendelee kuwa imara milele na milele;+

Ametoa agizo ambalo halitapitilia mbali.+

 7 Msifuni Yehova kutoka duniani,

Enyi viumbe wakubwa wa baharini na pia vilindi vyote vya maji,

 8 Enyi radi na mvua ya mawe, theluji na mawingu mazito,

Ewe kimbunga, unayetekeleza neno lake,+

 9 Enyi milima na vilima vyote,+

Enyi miti ya matunda na mierezi yote,+

10 Enyi wanyama wa mwituni+ na wanyama wote wa kufugwa,

Enyi viumbe mnaotambaa na ndege wenye mabawa,

11 Enyi wafalme wa dunia, nanyi mataifa yote,

Enyi wakuu na waamuzi wote wa dunia,+

12 Enyi vijana wa kiume na wa kike,*

Wazee pamoja na watoto.*

13 Na walisifu jina la Yehova,

Kwa maana jina lake peke yake liko juu sana lisiweze kufikiwa.+

Ukuu wake uko juu ya dunia na mbingu.+

14 Ataikweza nguvu* ya watu wake,

Kwa sifa ya washikamanifu wake wote,

Ya wana wa Israeli, watu walio karibu naye.

Msifuni Yah!*

149 Msifuni Yah!*

Mwimbieni Yehova wimbo mpya;+

Msifuni katika kutaniko la washikamanifu.+

 2 Watu wa Israeli na washangilie kwa sababu ya Muumba wao Mkuu;+

Wana wa Sayuni na washangilie kwa sababu ya Mfalme wao.

 3 Na walisifu jina lake kwa kucheza dansi+

Na wamwimbie sifa* kwa tari na kinubi.+

 4 Kwa maana Yehova anawafurahia watu wake.+

Anawapamba wapole kwa wokovu.+

 5 Washikamanifu na washangilie kwa utukufu;

Na wapaze sauti kwa shangwe vitandani mwao.+

 6 Nyimbo zinazomsifu Mungu na ziwe kooni mwao,

Na upanga wenye makali pande mbili uwe mkononi mwao,

 7 Ili kuyalipiza kisasi mataifa

Na kuyaadhibu mataifa,

 8 Ili kuwafunga wafalme wao kwa pingu

Na viongozi wao kwa pingu za chuma,

 9 Ili kutekeleza hukumu iliyoandikwa kuwahusu.+

Heshima hii ni ya washikamanifu wake wote.

Msifuni Yah!*

150 Msifuni Yah!*+

Msifuni Mungu katika mahali pake patakatifu.+

Msifuni katika anga la* nguvu zake.+

 2 Msifuni kwa kazi zake zenye nguvu.+

Msifuni kwa ukuu wake usio na kifani.+

 3 Msifuni kwa kupiga pembe.+

Msifuni kwa kinanda na kinubi.+

 4 Msifuni kwa tari+ na kwa dansi ya mzunguko.

Msifuni kwa nyuzi+ na filimbi.*+

 5 Msifuni kwa matoazi yanayolia.

Msifuni kwa matoazi yanayogonganishwa.+

 6 Kila kitu kinachopumua—na kimsifu Yah.

Msifuni Yah!*+

Au “huitafakari sheria Yake.”

Au “wanatafakari kuhusu.”

Au “wanashauriana.”

Au “Kristo.”

Au “onyo.”

Tnn., “Mbusuni.”

Au “kuihusu nafsi yangu.”

Angalia Kamusi.

Tnn., “Nitengenezee nafasi pana katika.”

Au “atamfanya mshikamanifu wake aonekane kuwa tofauti; atamtenga kando mshikamanifu wake kwa ajili yake mwenyewe.”

Angalia Kamusi.

Tnn., “katika uwepo wako.”

Au “anamchukia mtu anayemwaga damu na ambaye ni mdanganyifu.”

Au “mahali pako patakatifu.”

Au “Wanatumia ulimi laini.”

Angalia Kamusi.

Au “rehema.”

Au “nafsi yangu inasumbuka.”

Au “uiokoe nafsi yangu.”

Au “hawakukumbuki.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Tnn., “ninakifanya kitanda changu kiogelee.”

Au “Limezeeka.”

Au “Wimbo wa maombolezo.

Au “watairarua nafsi yangu.”

Au labda, “Nilipomwacha hai yule anayenipinga bila sababu.”

Au “na kuipita nafsi yangu.”

Au “anayejaribu mioyo na figo.”

Au “huvurumisha shutuma zake.”

Au “Nitalipigia muziki.”

Angalia Kamusi.

Au labda, “Wewe ambaye fahari yako inasimuliwa juu ya mbingu!”

Au “kuliko malaika.”

Angalia Kamusi.

Au “Nitalipigia muziki.”

Au “kilele salama.”

Angalia Kamusi.

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Tnn., “mbele za uwepo wako.”

Au “tamaa ya nafsi yake.”

Au labda, “Mwenye pupa hujibariki mwenyewe.”

Au “Hujitutumua kwa.”

Au “Sitapepesuka (Sitayumbayumba) kamwe.”

Au “pori.”

Au “katika makucha yake.”

Au “kuiambia nafsi yangu.”

Au “Misingi ya haki.”

Au “yanayong’aa.”

Au “Nafsi yake inamchukia; Yeye binafsi anamchukia.”

Au labda, “makaa ya mawe yanayowaka.”

Au “watajionea kibali chake.”

Angalia Kamusi.

Tnn., “Wanaongea kwa mdomo laini.”

Tnn., “kwa moyo na moyo.”

Au “wanaojitutumua mbele yao.”

Au labda, “tanuru la kuyeyusha lililowekwa ardhini.”

Au “ameshughulika nami kwa njia inayothawabisha.”

Au “Asiyetumia akili.”

Au “kwa utimilifu.”

Au “hawaaibishi.”

Tnn., “Havunji kiapo chake, hata kinapomletea hasara.”

Au “hatapepesuka (hatayumbayumba) kamwe.”

Angalia Kamusi.

Au “hisia zangu za ndani kabisa.” Tnn., “figo zangu.”

Au “sitapepesuka (sitayumbayumba) kamwe.”

Tnn., “utukufu wangu una.”

Au “Mwili wangu huishi.”

Au “hutaiacha nafsi yangu.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au labda, “aone uharibifu.”

Tnn., “pamoja na uso wako.”

Au “uzuri.”

Au “Inama chini na unisikilize.”

Au “maadui wangu walio dhidi ya nafsi.”

Au “Wamefunikwa na mafuta yao wenyewe.”

Au “kututupa chini.”

Au “Iokoe nafsi yangu.”

Au “mfumo huu wa mambo.”

Au “kuona sura yako.”

Angalia Kamusi.

Au “mwokozi wangu mwenye nguvu.”

Au “kilele changu salama.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “upepo.”

Au “Mifereji ya maji ikaonekana.”

Au “mahali penye nafasi kubwa.”

Au “ukosefu wa hatia.”

Au “ukosefu wa hatia.”

Au “wanaoteseka.”

Tnn., “unayashusha macho ya kiburi.”

Au “hunidumisha.”

Au “Vifundo vya miguu yangu havitateleza.”

Au “Utanionyesha migongo ya maadui wangu.”

Au “nitawanyamazisha.”

Au “watafifia.”

Au “nitalipigia muziki.”

Au “humpa ushindi mkubwa mfalme wake.”

Tnn., “mbegu yake.”

Au labda, “kamba yake ya kupimia imefika.”

Au “huirudisha nafsi.”

Au “iliyosafishwa.”

Au “dhambi nyingi.”

Tnn., “aione kuwa mafuta.”

Au “ushauri wako wote.”

Au “ushindi.”

Au “iliyosafishwa.”

Tnn., “Urefu wa siku.”

Tnn., “mbele za uso wako.”

Au “hatapepesuka (hatayumbayumba) kamwe.”

Tnn., “kulenga nyuso zao.”

Tnn., “kamba zako za upinde.”

Tnn., “Tutauimbia na kuupigia muziki.”

Labda ni sauti au mtindo wa muziki.

Au “Umeketi kwenye kiti cha ufalme kati ya (juu ya).”

Au “hawakuaibishwa.”

Au “Mimi ni fedheha kwa wanadamu na ninadharauliwa na watu.”

Tnn., “Nimetupwa kwako.”

Au “Iokoe nafsi yangu.”

Tnn., “Uhai pekee nilio nao,” yaani, nafsi yake.

Tnn., “mkono wa.”

Tnn., “mbegu ya.”

Tnn., “mbegu ya.”

Tnn., “Moyo wako na uishi.”

Tnn., “wanene.”

Au “nafsi zao.”

Tnn., “Mbegu itamtumikia.”

Au labda, “maji matulivu.”

Au “Huiburudisha nafsi yangu.”

Tnn., “mapito ya; vijia vya.”

Au “hunifariji.”

Au “Unakipaka.”

Au “nafsi Yangu,” ikirejelea mtu kuapa kwa uhai wa Yehova.

Au “haki.”

Au “Inukeni.”

Au “Nainua nafsi yangu kwako.”

Au “Ambazo ni za tangu nyakati za kale.”

Tnn., “katika hukumu.”

Au “Nafsi yake itajionea.”

Tnn., “mbegu yake itamiliki.”

Au “Ilinde nafsi yangu.”

Tnn., “mkomboe.”

Au “hisia zangu za ndani kabisa.” Tnn., “figo zangu.”

Tnn., “Siketi.”

Au “sichangamani na wanafiki.”

Tnn., “kuketi.”

Tnn., “Usiifagilie mbali nafsi yangu.”

Au “watu wanaomwaga damu.”

Au “mwenendo wa.”

Tnn., “Nikomboe.”

Tnn., “makusanyiko.”

Au “kutazama kwa kutafakari.”

Au “mahali pake patakatifu.”

Au “Nitampigia muziki.”

Au labda, “Kwa hakika nina imani kwamba nitauona wema wa Yehova katika nchi ya walio hai.”

Au “kaburini.”

Au “Mwabuduni.”

Au labda, “kwa sababu ya fahari ya utakatifu wake.”

Inaonekana ni safu ya milima ya Lebanoni.

Au “bahari ya mbinguni.”

Au “umenivuta.”

Au “umeiinua nafsi yangu.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “kaburini.”

Au “Mpigieni muziki.”

Tnn., “Ushukuruni ukumbusho wake.”

Au “nia yake njema.”

Au “Sitapepesuka (sitayumbayumba) kamwe.”

Au “nia yako njema.”

Tnn., “Damu yangu ina faida gani.”

Au “kaburini.”

Au “Ili utukufu wangu uimbe.”

Au “Inama chini na unisikilize.”

Au “Mungu mwaminifu.”

Au “mateso ya nafsi yangu.”

Au “penye nafasi kubwa.”

Au “nafsi yangu na tumbo langu.”

Au “akilini.”

Au “kuiondoa nafsi yangu.”

Tnn., “Nyakati.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “katika uwepo wako.”

Tnn., “Kutoka kwa ugomvi wa ndimi.”

Angalia Kamusi.

Au “imesamehewa.”

Au “hasira yako ilinilemea.”

Au “Unyevunyevu wa uhai wangu ulibadilika.”

Au “Mpigieni muziki.”

Au “pumzi ya.”

Au “jeshi lote la mbinguni liliumbwa.”

Au “ardhi inayozaa.”

Au “mashauri ya.”

Au “mawazo.”

Au “mashauri.”

Au “la ushindi.”

Au “aokoe nafsi zao.”

Au “Nafsi yangu itajigamba.”

Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni ambao ni.”

Au “waliovunjika moyo.”

Au “misiba mingi.”

Au “anaikomboa nafsi ya.”

Kwa kawaida ilibebwa na wapiga mishale.

Au “shoka lenye makali pande zote mbili.”

Au “Iambie nafsi yangu.”

Au “wanaowinda nafsi yangu.”

Au “iliporudi kwenye kifua changu.”

Au labda, “Wasiomwogopa Mungu wanadhihaki ili wapate keki.”

Tnn., “Uhai pekee nilio nao,” yaani, nafsi yake.

Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”

Au “Aha! Nafsi yetu.”

Au “utatafakari.”

Tnn., “kama milima ya Mungu.”

Au “Unawaokoa.”

Tnn., “mafuta ya.”

Au “Usiwake hasira.”

Au “nchini.”

Au “Pata shangwe nyingi sana.”

Tnn., “Mvingirishie.”

Au “subira.”

Au labda, “Usikasirike, kwa maana hasira itakuongoza tu kwenye madhara.”

Au “kuzitia nyuzi.”

Tnn., “siku za wasio na lawama.”

Au “hufadhili.”

Au “huimarisha.”

Au “anamtegemeza kwa mkono Wake.”

Au “chakula.”

Au “huzungumza hekima kwa sauti ya chini.”

Au “mtu anayeshika utimilifu.”

Tnn., “Viuno vyangu vimejaa moto.”

Au “ningurume.”

Au “nafsi yangu.”

Tnn., “wako hai.”

Au labda, “Lakini wale ambao ni maadui wangu bila sababu ni wengi.”

Angalia Kamusi.

Au “yalichochewa.”

Tnn., “uliwaka moto.”

Au “nikipiga kite.”

Au “nijue jinsi ninavyopita upesi.”

Tnn., “ziwe vipimo vya mkono.”

Tnn., “Hupiga kelele.”

Aina fulani ya wadudu waharibifu.

Au “Mlowezi.”

Tnn., “sijapita.”

Au “Nilimngojea Yehova kwa subira.”

Au “akainama chini ili kunisikiliza, akasikia.”

Au “waongo.”

Au “Hukupendezwa na.”

Au “ninatamani.”

Au “wanaoitafuta nafsi yangu.”

Au “Hutamtia kamwe katika tamaa ya maadui wake; au katika nafsi ya maadui wake.” Angalia Kamusi.

Au “Iponye nafsi yangu.”

Au “amenigeuka.”

Tnn., “mbele za uwepo wako.”

Au “Milele na milele.”

Angalia Kamusi.

Angalia Kamusi.

Au “polepole.”

Au “ule mlima mdogo.”

Yaani, inayoweza kusababisha mauaji.

Au labda, “kana kwamba wanaiponda mifupa yangu.”

Angalia Kamusi.

Au “Toa.”

Au “wokovu mkuu.”

Au “kutokana na bei yao.”

Tnn., “methali.”

Tnn., “Tukomboe.”

Angalia Kamusi.

Tnn., “Kazi zangu zinamhusu.”

Au “mwandishi.”

Au “ufanikiwe.”

Tnn., “utakufundisha.”

Au “haki.”

Au “watautuliza uso wako.”

Tnn., “Ndani.”

Tnn., “yametiwa mapambo ya.”

Au labda, “kwa majoho yaliyotariziwa.”

Angalia Kamusi.

Au “kilele chetu salama.”

Au labda, “Anaziteketeza ngao motoni.”

Au “pembe ya kondoo dume; tarumbeta.”

Au “Mpigieni Mungu muziki.”

Tnn., “ngao za dunia ni za.”

Au “kilele salama.”

Au “wamekutana kama walivyokubaliana.”

Tnn., “Mabinti wa Yuda na washangilie.”

Au “kuta zake zenye ngome.”

Au labda, “mpaka tufe.”

Au “wa mfumo wa mambo.”

Tnn., “Wana wa wanadamu na pia wana wa mtu.”

Tnn., “kosa la.”

Au “ukombozi.”

Au “nafsi yao.”

Au “kaburi.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “ataikomboa nafsi yangu.”

Tnn., “mkono wa.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “Yule Mungu, Yehova.”

Au “Kutoka mashariki mpaka magharibi.”

Tnn., “mbuzi dume.”

Au “mafundisho.”

Tnn., “kuyatupa maneno yangu nyuma yako.”

Au labda, “unaungana naye.”

Au “Unamharibia sifa.”

Au “akilini mwangu.”

Tnn., “wewe peke yako.”

Au “Na nilikuwa na dhambi tangu mama yangu aliponichukua mimba.”

Au “utu wangu wa sirini.”

Au “Ufiche uso wako.”

Au “uyafute kabisa.”

Tnn., “mbele za uwepo wako.”

Tnn., “Nitegemeze kwa kunipa roho ya utayari.”

Au “hutaudharau.”

Angalia Kamusi.

Au “ngome yake.”

Au “kujificha katika.”

Tnn., “taabu anazosababisha.”

Angalia Kamusi.

Angalia Kamusi.

Au “Asiye na akili.”

Au labda, “Hofu mahali pasipo na chochote cha kuhofu.”

Tnn., “wanaopiga kambi dhidi yenu.”

Angalia Kamusi.

Au “uamue kesi yangu.”

Au “nafsi yangu.”

Au “Hawamweki Mungu mbele yao.”

Tnn., “wanyamazishe.”

Angalia Kamusi.

Au “Na usijifiche ninaposali kukuomba msaada.”

Tnn., “ugawanye ndimi zao.”

Au “mwanadamu, mtu tunayelingana.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “nimevurugika.”

Tnn., “Atanikomboa.”

Yaani, rafiki yake wa zamani anayetajwa katika mstari wa 13 na 14.

Au “ayumbeyumbe; apepesuke.”

Angalia Kamusi.

Au “anataka kuning’ata.”

Tnn., “Mwili wa nyama utanifanya.”

Angalia Kamusi.

Au “Nitakupigia muziki.”

Angalia Kamusi.

Au “wamepotoka.”

Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”

Angalia Kamusi.

Tnn., “waichunguze ile nyumba.”

Au “wenye kiu ya damu.”

Au “Wananguruma.”

Au “kinachobubujika.”

Au “kilele changu salama.”

Au “wangurume.”

Au “nitakupigia muziki.”

Angalia Kamusi.

Au labda, “Umewapa.”

Au labda, “mahali pake patakatifu.”

Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”

Tnn., “ngome ya.”

Au labda, “lenye ngome.”

Au “Moyo wangu unapodhoofika.”

Au “Atakaa.”

Au “nitalipigia muziki.”

Angalia Kamusi.

Au “kilele changu salama.”

Au labda, “Ninyi nyote, kana kwamba alikuwa ukuta ulioinama, ukuta wa mawe unaokaribia kuanguka.”

Au “heshima yake.”

Au “Kwa kweli, Ee nafsi yangu, mngojee.”

Tnn., “Mwili wangu unazimia.”

Tnn., “Nimeridhika kana kwamba nina mafuta na nimejaa mafuta.”

Au “kuiangamiza nafsi yangu.”

Au “mbweha.”

Au “atajigamba.”

Au “Wanatiana moyo kutenda uovu.”

Au “watajigamba.”

Tnn., “watu wote wenye mwili.”

Au “Mahali pako patakatifu.”

Tnn., “ifurike.”

Au “matuta yake.”

Tnn., “vinadondosha mafuta.”

Tnn., “kudondosha.”

Au “nchi tambarare za chini zimefunikwa.”

Au “Lipigieni muziki.”

Au “Hufanya nafsi zetu kuwa hai.”

Au “iyumbeyumbe; itetemeke.”

Tnn., “Uliweka mzigo mzito kwenye viuno vyetu.”

Tnn., “juu ya vichwa vyetu.”

Au “itamheshimu.”

Au “lipigieni muziki.”

Au labda, “juu ya mawingu.”

“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Tnn., “mwamuzi.”

Au “waasi.”

Tnn., “ulipotangulia mbele ya.”

Tnn., “zilidondosha.”

Tnn., “Uliutia nguvu tena urithi wako.”

Au labda, “katikati ya mazizi ya kondoo.”

Au “yenye mchanganyiko wa rangi ya manjano na kijani kibichi.”

Au “Ni kana kwamba theluji ilianguka Salmoni.”

Au “ni mlima mrefu.”

Au “anatamani uwe.”

Au “anayetembeatembea katika.”

Tnn., “Katika makusanyiko.”

Au labda, “yakikanyagia chini.”

Au labda, “Mabalozi watatoka.”

Au “Mpigieni muziki.”

Tnn., “mawinguni.”

Au “nafsi yangu.”

Au “Wale ambao ni maadui wangu bila sababu.”

Au “Nilipoinyenyekeza nafsi yangu.”

Au labda, “Nilipolia na kufunga.”

Tnn., “Nilikuwa methali kwao.”

Au “shimo lifumbe.”

Au “Ikaribie nafsi yangu uikomboe.”

Au “nami nimefikia hatua ya kukata tamaa.”

Au “mmea wenye sumu.”

Au “hasira yako kali.”

Au “Kambi yao iliyozingirwa na ukuta.”

Au “kitabu cha uzima.”

Yaani, ile nchi.

Au “wanaoitafuta nafsi yangu.”

Au “Inama chini na unisikilize.”

Au “Wewe ni tegemeo langu.”

Au “wanaoitafuta nafsi yangu.”

Au “kuyahesabu.”

Tnn., “mkono wako.”

Au “vilindi vya.”

Au “Nitakupigia muziki.”

Au “umeikomboa nafsi yangu.”

Au “utatafakari.”

Tnn., “awahukumu.”

Au “wana.”

Tnn., “atachipuka.”

Au “Atatawala.”

Au “nafsi za.”

Au “Atazikomboa nafsi zao.”

Au “wanaojigamba.”

Au “Kitambi chao kimenenepa.”

Tnn., “Mafuta yao.”

Tnn., “Ningekisaliti kizazi cha wana wako.”

Tnn., “utaidharau.”

Tnn., “katika figo zangu.”

Tnn., “Utamnyamazisha.”

Au “kukosa uaminifu.”

Angalia Kamusi.

Tnn., “inafuka moshi.”

Tnn., “Likumbuke kusanyiko lako ulilojipatia.”

Au “kusanyiko.”

Au “Sehemu zote ambazo Mungu anaabudiwa.”

Au “Uchomoe kutoka katika makunjo ya vazi lako.”

Angalia Kamusi.

Au “mwanga.”

Au “nafsi ya.”

Tnn., “pembe yenu.”

Tnn., “pembe yenu.”

Au “Nitampigia muziki.”

Tnn., “pembe.”

Tnn., “pembe.”

Au “Umefunikwa na nuru.”

Tnn., “Atainyenyekeza roho ya.”

Angalia Kamusi.

Tnn., “bila kufa ganzi.”

Au “Nafsi yangu haiwezi.”

Tnn., “roho yangu inazimia.”

Au “muziki wangu wa nyuzi.”

Tnn., “Roho yangu inatafuta.”

Au “linalonichoma.”

Tnn., “amebadili mkono wake wa kuume dhidi yetu.”

Tnn., “mkono wako.”

Tnn., “umewakomboa.”

Au “ardhi inayozaa.”

Tnn., “Kwa mkono.”

Angalia Kamusi.

Au “mafundisho.”

Tnn., “ambao haujatayarishwa.”

Au “ukuta.”

Tnn., “Walimtahini.”

Au “chakula kwa ajili ya nafsi yao.”

Au “wa malaika.”

Au “Mlipiza-Kisasi.”

Tnn., “akifunika.”

Au labda, “Kwamba roho inaenda nayo hairudi.”

Au “wakamtia uchungu.”

Tnn., “Hawakuukumbuka mkono wake.”

Tnn., “aliwakomboa.”

Au labda, “homa kali.”

Au “Hakulinda nafsi zao zisife.”

Tnn., “kumtahini.”

Au “wivu wake.”

Tnn., “hawakusifiwa.”

Tnn., “Alipajenga mahali pake patakatifu kama vilele.”

Tnn., “ufunike.”

Tnn., “mkono wako.”

Au labda, “kuwaweka huru.”

Tnn., “wana wa kifo.”

Au labda, “katikati ya.”

Au “Funua uangavu wako.”

Tnn., “kuwaka hasira dhidi ya.”

Au “Shina kuu la mzabibu.”

Au “ulitazame tawi ambalo umelitia nguvu.”

Tnn., “kwa kemeo la uso wako.”

Angalia Kamusi.

Yaani, Mungu.

Au “lugha.”

Tnn., “katika mahali palipofichika pa ngurumo.”

Maana yake “Kugombana.”

Tnn., “Walitembea katika mashauri yao.”

Tnn., “wakati.”

Tnn., “atamlisha,” yaani, watu wa Mungu.

Tnn., “mafuta ya ngano.”

Au “walio kama miungu.”

Au “Hukumuni kwa ajili ya.”

Au “ni kama miungu.”

Au “wanainua vichwa vyao.”

Tnn., “waliofichwa.”

Tnn., “Wanashauriana kwa moyo mmoja.”

Au “Wamefanya agano.”

Tnn., “Wamekuwa mkono kwa.”

Au “korongo la.”

Au “viongozi.”

Au “kama mbaruti.”

Tnn., “Jaza nyuso zao aibu.”

Angalia Kamusi.

Au “linavyopendwa sana.”

Tnn., “inakazia.”

Au “bonde lenye vichaka vya mibaka.”

Au labda, “Na mfundishaji hujifunika mwenyewe.”

Au labda, “Itazame ngao yetu, Ee Mungu.”

Tnn., “Uliifunika.”

Au “Tukusanye tena.”

Au “ufanisi.”

Au “Inama chini na unisikilize.”

Au “Ilinde nafsi yangu.”

Au “ninakuinulia wewe nafsi yangu.”

Au “Nipe moyo ambao haujagawanyika.”

Au “umeiokoa nafsi yangu.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “wanaitafuta nafsi yangu.”

Au “hawajakuweka mbele yao.”

Au “neema.”

Au “kweli.”

Au “uthibitisho wa.”

Au “wanaonitambua.”

Au “Kwangu mimi, wewe ni chanzo cha vitu vyote.”

Angalia Kamusi.

Angalia Kamusi.

Au “Inama chini na unisikilize.”

Angalia Kamusi.

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “kaburini.”

Au “mtu asiye na nguvu.”

Tnn., “mkono.”

Au “abiso.” Angalia Kamusi.

Au “katika Abadoni.”

Au “unaikataa nafsi yangu.”

Au labda, “Vinanizingira vyote kwa pamoja.”

Angalia Kamusi.

Au “utadumu.”

Tnn., “Nitaiimarisha kabisa mbegu yako.”

Au “kusanyiko.”

Tnn., “pembe yetu inakwezwa.”

Tnn., “pembe yake itakwezwa.”

Au “Nitaweka mamlaka yake.”

Tnn., “Nitaiimarisha mbegu yake.”

Au “hukumu zangu.”

Au “kutotii kwao.”

Tnn., “Wala kuwa mwongo kuhusu uaminifu wangu.”

Tnn., “Mbegu yake itadumu.”

Au “Umelitia unajisi.”

Au “Umeyavunja mabanda yake yote ya mawe.”

Tnn., “Umeuinua juu mkono wa kulia wa maadui wake.”

Au “kuiokoa nafsi yake.”

Tnn., “mkono wa Sheoli.” Angalia Kamusi.

Tnn., “kubeba kifuani mwangu.”

Au labda, “kimbilio letu.”

Au “hujatokeza kama kwa uchungu wa kuzaa.”

Au “Unajua makosa yetu.”

Au “Maisha yetu yanadidimia.”

Au “kupiga kite.”

Au “kwa sababu ya uwezo wa pekee.”

Au “uimarishe kabisa.”

Au “iimarishe kabisa.”

Au “boma.”

Tnn., “malipo.”

Au labda, “ngome; kimbilio.”

Tnn., “amejiunga nami.”

Au “analitambua.”

Au “aone wokovu kutoka kwangu.”

Au “kulipigia muziki.”

Au “majani.”

Tnn., “utaikweza pembe yangu kama ya.”

Au “wakiwa na mvi.”

Tnn., “kuwa wanene.”

Au “kutikiswa.”

Au “unaifaa.”

Tnn., “aliyelipanda.”

Tnn., “nimekaa katika ukimya.”

Au “Mawazo yenye kufadhaisha.”

Au “yalipokuwa mengi ndani yangu.”

Au “Faraja zako ziliibembeleza nafsi yangu.”

Au “watawala; mahakimu.”

Au “kwa kutoa amri.”

Tnn., “Na damu ya asiye na hatia wanaitangaza kuwa na hatia (ovu).”

Au “kilele changu salama.”

Tnn., “Atawanyamazisha.”

Tnn., “atawanyamazisha.”

Tnn., “mbele za uso wake.”

Tnn., “wa mkono wake.”

Maana yake “Kugombana.”

Maana yake “Kujaribu; Jaribu.”

Au “adhama.”

Au “Mwabuduni.”

Au labda, “kwa sababu ya fahari ya utakatifu wake.”

Au “kutikiswa.”

Au “Ataamua kesi ya.”

Au “amekuja.”

Au “Mwabuduni.”

Tnn., “Mabinti wa Yuda wana.”

Au “nafsi za.”

Tnn., “nguvu za.”

Tnn., “muushukuru ukumbusho wake.”

Au “umemletea ushindi.”

Au “ushindi wa.”

Au “kupiga muziki.”

Au “Mpigieni muziki.”

Au “amekuja.”

Au labda, “katikati ya.”

Au “kuabudu.”

Tnn., “ulilipiza kisasi.”

Au “mwabudu.”

Au “Tambueni.”

Au labda, “hatukujiumba wenyewe.”

Au “Nitakupigia muziki.”

Au “utimilifu.”

Au “cha ubatili.”

Au “Matendo yao hayashikamani nami.”

Tnn., “Sitajua.”

Au “Nitamwangamiza.”

Au “kwa utimilifu.”

Tnn., “mbele ya macho yangu.”

Au “nitawaangamiza.”

Au “anapokuwa dhaifu.”

Au “Inama chini na unisikilize.”

Au labda, “Nimekonda sana.”

Au “wanaonifanya nionekane mpumbavu.”

Au “ni kama kivuli kinachorefuka.”

Au “jina lako litadumu.” Tnn., “ukumbusho wako utadumu.”

Tnn., “watakaoumbwa.”

Au “kaburini.”

Au “neema.”

Au “fadhili nyingi zenye upendo.”

Tnn., “Na mahali pake hapalijui tena.”

Au “tangu milele hadi milele.”

Tnn., “mkiisikia sauti ya neno lake.”

Au “Kila mahali pa enzi yake kuu.”

Au “adhama.”

Tnn., “katika maji.”

Au “Haitatikiswa.”

Au “makorongo.”

Au “Wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”

Angalia Kamusi.

Au “Nitampigia muziki.”

Au labda, “Kutafakari kwangu kumhusu na kupendeze.”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “mpigieni muziki.”

Au labda, “Zungumzieni.”

Au “uwepo.”

Au “wazao wa.” Tnn., “mbegu ya.”

Tnn., “Neno aliloamuru.”

Tnn., “Aliuvunja kila ufito wa mikate.” Labda ni fito zilizotumiwa kuhifadhia mikate.

Tnn., “Waliitesa.”

Au “Nafsi yake iliingia katika chuma.”

Tnn., “Ili awafunge.”

Au “kama nafsi ilivyotaka.”

Aina ya mbu anayeitwa hak·kin·namʹ katika Kiebrania.

Au “miali ya moto.”

Tnn., “hofu yao.”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “nia njema.”

Au “nijigambe kukuhusu.”

Au “hawakuelewa maana ya.”

Au “nyikani.”

Au “aliyebaki.”

Au “sanamu ya kuyeyushwa.”

Tnn., “akasimama kwenye pengo hilo mbele zake.”

Au “wakashikamana.”

Yaani, dhabihu zilizotolewa kwa watu waliokufa au kwa miungu ambayo haina uhai.

Maana yake “Kugombana.”

Au “kujifunza.”

Tnn., “mkono wao.”

Au “akighairi.”

Au “mkubwa; mkuu.”

Au “tupate shangwe kwa kukusifu.”

Au “Milele na milele.”

Au “Na iwe hivyo!”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “walionunuliwa.”

Au “katika nguvu za.”

Au “Kutoka mapambazuko ya jua na kutoka machweo ya jua.”

Au “amezitosheleza nafsi zilizokauka.”

Au “kuzishibisha nafsi zenye njaa.”

Au “Walichukia kabisa vyakula vyote.”

Au “Nafsi yao.”

Tnn., “kwenye kiti cha.”

Au “huwainua juu,” yaani, ili wasifikiwe.

Tnn., “hata kwa utukufu wangu.”

Au “nitakupigia muziki.”

Au labda, “mahali pake patakatifu.”

Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”

Tnn., “ngome ya.”

Au “Mshtaki.”

Au “mwovu.”

Tnn., “Wanawe.”

Au “Wanawe.”

Au “Wala riba na waviwekee mitego.”

Au “upendo mshikamanifu.”

Au “Kizazi chake kijacho na kiangamizwe.”

Au “upendo mshikamanifu.”

Tnn., “Mwili wangu umekuwa mwembamba, hauna mafuta.”

Au “joho lisilo na mikono.”

Au “siku ambayo jeshi lako litakusanyika.”

Au “hataghairi.”

Au “miongoni mwa.”

Tnn., “Ataponda kichwa cha.”

Au “dunia nzima.”

Anayerejelewa ni “Bwana wangu” anayetajwa katika mstari wa 1.

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “neema.”

Au “Yana msingi mzuri.”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “neema.”

Au “fadhili.”

Au “ni thabiti; ni imara.”

Au “kwa ukarimu.”

Tnn., “Pembe yake mwenyewe itakwezwa.”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “Anayeketi juu kwenye kiti cha ufalme?”

Au labda, “jaa la takataka.”

Tnn., “wana.”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “Hatustahili chochote, Ee Yehova, hatustahili chochote.”

Tnn., “wana.”

Tnn., “kwenye kimya.”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au labda, “Ninapenda kwa sababu Yehova huisikia.”

Au “huinama chini ili kunisikiliza.”

Tnn., “katika siku zangu.”

Tnn., “Nilipatwa na taabu za Sheoli.”

Au “iokoe nafsi yangu.”

Au “neema.”

Angalia Kamusi.

Au “Umeiokoa nafsi yangu.”

Au “wokovu mkuu.”

Au “Ni cha bei kubwa sana.”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “koo zote.”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “mahali penye nafasi kubwa.”

Au labda, “pamoja na wale wanaonisaidia.”

Au labda, “Ulinisukuma kwa nguvu.”

Au “ushindi.”

Tnn., “kichwa cha pembeni.”

Au “wanaoshika utimilifu.”

Tnn., “Laiti njia zangu zingekuwa zimeimarishwa kabisa.”

Au “Nitajifunza.”

Au “Nafsi yangu inapondeka.”

Tnn., “Vingirisha mbali nami.”

Au “ninajifunza.”

Tnn., “njia.”

Au “kujifunza.”

Au “niaibishwe.”

Tnn., “Nitakimbia katika.”

Au labda, “huufanya moyo wangu uwe na ujasiri.”

Au “Nitembeze.”

Au “kwa faida za.”

Au “neno lako.”

Au labda, “Ambayo hutolewa kwa wale wanaokuogopa.”

Au “neno lako.”

Au “ninangojea.”

Au “mahali penye nafasi kubwa.”

Au “nitajifunza.”

Au “Kumbuka ahadi yako uliyompa.”

Au “Ambalo ulinifanya nisubiri.”

Au “Katika nyumba ninamoishi kama mgeni.”

Au “Ninautuliza (ninatafuta tabasamu ya) uso wako.”

Au “neno lako.”

Au “nilikuwa nikitenda dhambi bila kukusudia.”

Tnn., “hauna hisia, ni kama mafuta.”

Au “ninalingojea neno lako.”

Au “neno lako ulilonipa.”

Au labda, “kwa kusema uwongo.”

Au “nitajifunza.”

Au “ninalingojea neno lako.”

Yaani, kazi zake zote za uumbaji.

Tnn., “ni pana sana.”

Au “Ninajifunza kuihusu.”

Au “ninajifunza.”

Tnn., “matoleo ya hiari ya kinywa changu.”

Au “Nafsi yangu imo mikononi mwangu daima.”

Au “urithi wangu wa milele.”

Tnn., “Nimeuelekeza moyo wangu.”

Au “moyo uliogawanyika.”

Au “Ninalingojea neno lako.”

Au “kulingana na neno lako.”

Au “liaibishwe.”

Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “takataka” katika mstari huu linarejelea uchafu unaotoka katika fedha au dhahabu inapoyeyushwa.

Au “neno lako la.”

Au “iliyosafishwa.”

Au “maagizo.”

Tnn., “kuhemahema.”

Tnn., “Kulingana na uamuzi wako kuwaelekea.”

Au “Zifanye hatua zangu ziwe imara.”

Tnn., “Nikomboe.”

Au “utabasamu kunielekea.”

Au “alfajiri.”

Au “Ninayangojea maneno yako.”

Au “nijifunze.”

Au “mwenendo mpotovu.”

Au “Iendeshe kesi yangu.”

Au “neno lako.”

Au “Hakuna cha kuwakwaza.”

Au “kulingana na neno lako.”

Angalia Kamusi.

Tnn., “Naye atakuongezea nini?”

Au “uyumbe.”

Au “Atailinda nafsi yako.”

Tnn., “unapotoka nje na unapoingia ndani.”

“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “kuta zako zenye ngome.”

Au “Nafsi yetu imechoshwa na dhihaka nyingi za.”

Au “Nafsi yetu.”

Au “wasiielekeze mikono yao kutenda.”

Au “makorongo ya kusini.”

Au “Wana.”

Au “unafuatilia.”

“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Tnn., “Ili uogopwe.”

Au “nimejituliza na kujinyamazisha mwenyewe.” Angalia Kamusi.

Au “Hema tukufu la ibada.”

Au “hema lake tukufu la ibada.”

Tnn., “Usiugeuze nyuma uso wa.”

Tnn., “Mmoja kutoka katika uzao wa tumbo lako.”

Tnn., “nitaifanya pembe ya Daudi ikue.”

Au labda, “mahali patakatifu.”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “Lipigieni muziki.”

Au “mali yake anayothamini sana.”

Au “Huufanya mvuke upande.”

Au labda, “malango.”

Au “jina lako linadumu.” Tnn., “ukumbusho wako unadumu.”

Au “ataamua kesi ya.”

Au “ataghairi kuwahusu.”

Au “kwa uelewaji.”

Tnn., “sehemu sehemu.”

Tnn., “Huipa chakula miili yote.”

Yaani, Babiloni.

Au labda, “unyauke.”

Au labda, “Nitaipinga miungu mingine kwa kukupigia muziki.”

Au “mahali pake patakatifu.”

Au labda, “umelitukuza neno lako juu ya jina lako lote.”

Au “niwe na ujasiri katika nafsi yangu.”

Tnn., “Unanipima.”

Au “ni wa ajabu sana kwangu.”

Au “Umezidi kabisa uelewaji wangu.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au labda, “Ulinifuma pamoja.”

Au “Nafsi yangu inajua.”

Au labda, “nitakuwa bado ninayahesabu.”

Au “wenye hatia ya damu.”

Au “kulingana na mawazo yao.”

Au “yanayonifadhaisha.”

Au “Mashimo yenye umajimaji.”

Au “nchini.”

Au “katika uwepo wako.”

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Au “Usiimwage chini nafsi yangu.”

Angalia Kamusi.

Au “Ninapoishiwa na nguvu.”

Tnn., “anayenitambua.”

Tnn., “Fungu langu.”

Au “Ninaishiwa na nguvu.”

Au “Ninajifunza.”

Tnn., “Roho yangu imefikia.”

Au “kaburini.”

Au “Kwa maana ninakuinulia nafsi yangu.”

Au “katika nchi ya unyoofu.”

Tnn., “wanyamazishe.”

Au “Kilele changu salama.”

Au “kunja.”

Au “udhibiti.”

Tnn., “Na mkono wao wa kulia ni mkono wa kulia wa uwongo.”

Au “Nitakupigia muziki.”

Au “wokovu.”

Au “hawatapasukiwa na mimba.”

Au “hauwezi kueleweka.”

Au “nguvu zako.”

Au “neema.”

Au “kwa unyoofu.”

Tnn., “Miili yote na isifu.”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “Nitampigia muziki.”

Au “viongozi.”

Au “Pumzi.”

Tnn., “mkate.”

Tnn., “waliofungwa.”

Au “huipotosha njia ya waovu.”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “kumpigia muziki.”

Tnn., “mafuta ya ngano.”

Au “Huitupa chini barafu yake.”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Tnn., “mbingu za mbingu.”

Tnn., “mabikira.”

Au “Wakubwa kwa wadogo.”

Tnn., “pembe.”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “wampigie muziki.”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

Au “anga linalotoa ushahidi kuhusu.”

Au “zumari.”

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki